Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
• Ashangaa watu kuteseka miaka 50 baada ya uhuru
Na Janet Josiah, Nkasi
MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, juzi alibubujikwa na machozi baada ya kushuhudia umaskini wa kutupwa na nyumba duni zinazotumiwa na wananchi wa eneo la Katanga Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa.
"Nimezunguka sehemu mbalimbali nchini na kushuhudia maisha magumu wanayoishi Watanzania. Lakini leo nimeshindwa kujizuia nisitokwe machozi baada ya kuona nyumba duni wanazoishi wananchi wa Katanga… sasa karibu miaka 50 baada ya taifa hili kupata uhuru, bado kuna Watanzania wanaishi kwenye nyumba za tembe zenye sakafu za udongo zilizojaa mashimo!" alihuzunika Dk. Slaa.
Akihutubia mkutano wa kampeni kwenye uwanja wa Sabasaba katika eneo la Namanyere, Dk. Slaa alisema muda umefika kwa Watanzania kukataa kuendelea kuishi maisha duni ya umaskini wa kutupwa, licha ya taifa kuwa na utajiri wa kupindukia.
"Hatuwezi kuendelea kuishi kwenye hali hii, lazima Watanzania tufanye mabadiliko kwa nguvu ya kura… yapata miaka 50 tangu tupate uhuru tumeendelea kuwa maskini wa kutupwa," alisema Dk. Slaa.
Alisema suala la nyumba duni linamgusa kila Mtanzania bila kujali itikadi za vyama na kuwahimiza wapiga kura kujitokeza kwa wingi Oktoba 31, mwaka huu, kuchagua viongozi wenye uchungu na maisha na wananchi.
Dk. Slaa, alisema wakati wananchi wa mkoa wa Rukwa na mkoa mpya wa Katavi wakiishi kwenye maisha ya dhiki, ndani ya nyumba zao wana mamia ya magunia ya mazao waliyovuna mashambani, lakini wameshindwa kusafirisha kutokana na miundombinu ya barabara kuwa mibovu.
Aliahidi iwapo wananchi watampa ridhaa ya kuingia Ikulu, serikali yake itahakikisha inawawezesha kujenga nyumba bora na za kisasa kwa kuwaondolea kodi kwenye vifaa vya ujenzi, kama bati na simenti ili ziuzwe sh 5,000 kama ilivyokuwa kabla ya uongozi wa awamu ya nne.
"Ukiwa na elimu bora kazi yoyote utaweza kuifanya kwa mafanikio na ubora unaokubalika hata ukiwa mama ntilie… hata kilimo chenye tija kitafanikiwa kwa kuwa na elimu bora. Ndiyo maana (CHADEMA) tunasema Elimu Bora Kwanza na siyo Kilimo Kwanza kama wanavyosema wenzetu wa Chama cha Mapinduzi (CCM)," alisema Dk. Slaa.
Alisema bila kuwawezesha kielimu vijana wa Kitanzania, watageuka kuwa vibarua ndani ya nchi yao, baada ya kufunguliwa Soko la Pamoja la Afrika Mashariki.
Akiwahutubia wananchi wa mji wa Mpanda katika mkutano mwingine, Slaa alisema taifa limepoteza imani na Rais Jakaya Kikwete kwa sababu hana uchungu na nchi na amekuwa akishirikiana na mafisadi kutapanya rasilimali za nchi.
Dk. Slaa ambaye amekuwa akikumbushia jinsi alivyomtaja Kikwete miongoni mwa orodha ya mfisadi iliyotolewa Septemba 15, 2007, Mwembeyanga Dar es Salaam, alisema Kikwete anawalinda mafisadi, huku akijidai mbele ya umma kwamba anapigana na ufisadi.....
Chanzo: Tanzania Daima
Na Janet Josiah, Nkasi
MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, juzi alibubujikwa na machozi baada ya kushuhudia umaskini wa kutupwa na nyumba duni zinazotumiwa na wananchi wa eneo la Katanga Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa.
"Nimezunguka sehemu mbalimbali nchini na kushuhudia maisha magumu wanayoishi Watanzania. Lakini leo nimeshindwa kujizuia nisitokwe machozi baada ya kuona nyumba duni wanazoishi wananchi wa Katanga… sasa karibu miaka 50 baada ya taifa hili kupata uhuru, bado kuna Watanzania wanaishi kwenye nyumba za tembe zenye sakafu za udongo zilizojaa mashimo!" alihuzunika Dk. Slaa.
Akihutubia mkutano wa kampeni kwenye uwanja wa Sabasaba katika eneo la Namanyere, Dk. Slaa alisema muda umefika kwa Watanzania kukataa kuendelea kuishi maisha duni ya umaskini wa kutupwa, licha ya taifa kuwa na utajiri wa kupindukia.
"Hatuwezi kuendelea kuishi kwenye hali hii, lazima Watanzania tufanye mabadiliko kwa nguvu ya kura… yapata miaka 50 tangu tupate uhuru tumeendelea kuwa maskini wa kutupwa," alisema Dk. Slaa.
Alisema suala la nyumba duni linamgusa kila Mtanzania bila kujali itikadi za vyama na kuwahimiza wapiga kura kujitokeza kwa wingi Oktoba 31, mwaka huu, kuchagua viongozi wenye uchungu na maisha na wananchi.
Dk. Slaa, alisema wakati wananchi wa mkoa wa Rukwa na mkoa mpya wa Katavi wakiishi kwenye maisha ya dhiki, ndani ya nyumba zao wana mamia ya magunia ya mazao waliyovuna mashambani, lakini wameshindwa kusafirisha kutokana na miundombinu ya barabara kuwa mibovu.
Aliahidi iwapo wananchi watampa ridhaa ya kuingia Ikulu, serikali yake itahakikisha inawawezesha kujenga nyumba bora na za kisasa kwa kuwaondolea kodi kwenye vifaa vya ujenzi, kama bati na simenti ili ziuzwe sh 5,000 kama ilivyokuwa kabla ya uongozi wa awamu ya nne.
"Ukiwa na elimu bora kazi yoyote utaweza kuifanya kwa mafanikio na ubora unaokubalika hata ukiwa mama ntilie… hata kilimo chenye tija kitafanikiwa kwa kuwa na elimu bora. Ndiyo maana (CHADEMA) tunasema Elimu Bora Kwanza na siyo Kilimo Kwanza kama wanavyosema wenzetu wa Chama cha Mapinduzi (CCM)," alisema Dk. Slaa.
Alisema bila kuwawezesha kielimu vijana wa Kitanzania, watageuka kuwa vibarua ndani ya nchi yao, baada ya kufunguliwa Soko la Pamoja la Afrika Mashariki.
Akiwahutubia wananchi wa mji wa Mpanda katika mkutano mwingine, Slaa alisema taifa limepoteza imani na Rais Jakaya Kikwete kwa sababu hana uchungu na nchi na amekuwa akishirikiana na mafisadi kutapanya rasilimali za nchi.
Dk. Slaa ambaye amekuwa akikumbushia jinsi alivyomtaja Kikwete miongoni mwa orodha ya mfisadi iliyotolewa Septemba 15, 2007, Mwembeyanga Dar es Salaam, alisema Kikwete anawalinda mafisadi, huku akijidai mbele ya umma kwamba anapigana na ufisadi.....
Chanzo: Tanzania Daima