Elections 2010 Slaa Akata Anga Morogoro

Masanilo

Platinum Member
Oct 2, 2007
22,286
4,493
Slaa akata anga Morogoro


LEO Dk. Willlibrod Slaa alikuwa mkoani Morogoro, katika wilaya za Mikumi na Mvomero. Mikutano imefana. Amesisitiza haja ya Morogoro kuwa na wabunge wa upinzani ili kuongeza uwajibikaji katika halmashauri za mkoa huu, na katika nchi nzima kupitia Bunge; na kudhibiti wizi wa fedha za umma.

Akiwa Mikumi, alimlipua mwenyekiti wa kamati ya kampeni za CCM, Abdulahman Kinana, akisema kigogo huyo ana mkono katika biashara chafu za makampuni ya meli; akamtaka ajielekeze katika masuala ya kitaifa badala ya kumwandama yeye (Slaa). Akasisitiza kwamba ana ushahidi wa kauli zake, kwani hana historia ya kukurupuka.

Kauli hiyo ya Dk. Slaa inakuja siku moja baada ya Kinana kujibu mapigo ya makada wa Chadema, hasa Mabere Marando, ambao waliwataja hadharani vigogo wanaohusika na ufisadi mkubwa, huku CCM ikilalamika kwamba chama hicho cha upinzani kinatoa matusi.

Katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za Chadema, Marando alisema vigogo waliohusika na wizi wa EPA ni Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete, Rostam Azizi na Edward Lowassa, akasema waliofikishwa mahakamani kwa tuhuma za ufisadi ni dagaa wanaoonewa ili kuficha madhambi ya wahusika wenyewe wa ufisadi.

Juzi Kinana alijitokeza na kumbeza Dk. Slaa, kwamba anatumia lugha ya matusi kwenye kampeni kinyume cha makubaliano waliyosaini. Dk. Slaa jana alisema mtu akiiba anaitwa mwizi; na kwamba kumwita hivyo si matusi

Source: Ngurumo
 
Rev. Natamani kila mtu ajue hizi habari ila ndio hivyo tena. News ya ch-ten haikuwa na hii kitu nikajua mzee kapumzika. Wao walikuwa na makamba akilalamika eti mtu akimtukana baba ako huwezi muacha! Sasa sijui jk ni baba ake na makamba! Fanyeni mpango mwingine maana naona hali ya hewa sio nzuri radi imeanza na mvua itashuka si mda!
 
Slaa akata anga Morogoro


LEO Dk. Willlibrod Slaa alikuwa mkoani Morogoro, katika wilaya za Mikumi na Mvomero. Mikutano imefana. Amesisitiza haja ya Morogoro kuwa na wabunge wa upinzani ili kuongeza uwajibikaji katika halmashauri za mkoa huu, na katika nchi nzima kupitia Bunge; na kudhibiti wizi wa fedha za umma.

Akiwa Mikumi, alimlipua mwenyekiti wa kamati ya kampeni za CCM, Abdulahman Kinana, akisema kigogo huyo ana mkono katika biashara chafu za makampuni ya meli; akamtaka ajielekeze katika masuala ya kitaifa badala ya kumwandama yeye (Slaa). Akasisitiza kwamba ana ushahidi wa kauli zake, kwani hana historia ya kukurupuka.

Kauli hiyo ya Dk. Slaa inakuja siku moja baada ya Kinana kujibu mapigo ya makada wa Chadema, hasa Mabere Marando, ambao waliwataja hadharani vigogo wanaohusika na ufisadi mkubwa, huku CCM ikilalamika kwamba chama hicho cha upinzani kinatoa matusi.

Katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za Chadema, Marando alisema vigogo waliohusika na wizi wa EPA ni Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete, Rostam Azizi na Edward Lowassa, akasema waliofikishwa mahakamani kwa tuhuma za ufisadi ni dagaa wanaoonewa ili kuficha madhambi ya wahusika wenyewe wa ufisadi.

Juzi Kinana alijitokeza na kumbeza Dk. Slaa, kwamba anatumia lugha ya matusi kwenye kampeni kinyume cha makubaliano waliyosaini. Dk. Slaa jana alisema mtu akiiba anaitwa mwizi; na kwamba kumwita hivyo si matusi

Source: Ngurumo

Nimependa hiyo ya mtu akiiba anaitwa mwizi.
 
unajua CCM sijui wakoje mtu mwizi ni mwizi tu ..au wanataka mwizi tumwite honey and sweetheart
 
Slaa akata anga Morogoro


LEO Dk. Willlibrod Slaa alikuwa mkoani Morogoro, katika wilaya za Mikumi na Mvomero. Mikutano imefana. Amesisitiza haja ya Morogoro kuwa na wabunge wa upinzani ili kuongeza uwajibikaji katika halmashauri za mkoa huu, na katika nchi nzima kupitia Bunge; na kudhibiti wizi wa fedha za umma.

Akiwa Mikumi, alimlipua mwenyekiti wa kamati ya kampeni za CCM, Abdulahman Kinana, akisema kigogo huyo ana mkono katika biashara chafu za makampuni ya meli; akamtaka ajielekeze katika masuala ya kitaifa badala ya kumwandama yeye (Slaa). Akasisitiza kwamba ana ushahidi wa kauli zake, kwani hana historia ya kukurupuka.

Kauli hiyo ya Dk. Slaa inakuja siku moja baada ya Kinana kujibu mapigo ya makada wa Chadema, hasa Mabere Marando, ambao waliwataja hadharani vigogo wanaohusika na ufisadi mkubwa, huku CCM ikilalamika kwamba chama hicho cha upinzani kinatoa matusi.

Katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za Chadema, Marando alisema vigogo waliohusika na wizi wa EPA ni Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete, Rostam Azizi na Edward Lowassa, akasema waliofikishwa mahakamani kwa tuhuma za ufisadi ni dagaa wanaoonewa ili kuficha madhambi ya wahusika wenyewe wa ufisadi.

Juzi Kinana alijitokeza na kumbeza Dk. Slaa, kwamba anatumia lugha ya matusi kwenye kampeni kinyume cha makubaliano waliyosaini. Dk. Slaa jana alisema mtu akiiba anaitwa mwizi; na kwamba kumwita hivyo si matusi

Source: Ngurumo

Kinana ameyataka Mwenyewe! I hope hii ni salamu kwako Mjomba
 
Slaa akata anga Morogoro

Akiwa Mikumi, alimlipua mwenyekiti wa kamati ya kampeni za CCM, Abdulahman Kinana, akisema kigogo huyo ana mkono katika biashara chafu za makampuni ya meli; akamtaka ajielekeze katika masuala ya kitaifa badala ya kumwandama yeye (Slaa). Akasisitiza kwamba ana ushahidi wa kauli zake, kwani hana historia ya kukurupuka.

Source: Ngurumo

Du! Sasa kumekucha . . . . tutasikia mengi . . .
 
Du! Sasa kumekucha . . . . tutasikia mengi . . .

Kweli kumekucha! Kama kinana ndio msafi akaachwa awe mtetezi maana yeye hawezi guswa! Kumbe kanyaga bomu haya limelipuka! Inaitwa Nikanyage bahati mbaya nikulipue makusudi! Dr. endelea kula vichwa!
 
Imagine Komba wa TOT yuko Upinzani na sasa ametunga wimbo kuhusiana na hii issue . . .

Kuna mbunifu yeyote anyeweweza kushusha verses hapa . . .
 
Chadema need to respond ccm smearing machine on time and felociously, chadema ndo wanaongea issue ya ufisadi ccm wanawapaka matope wametoa matusi, that is dirty politics ccm wanayoitumia na chadema inabidi wawe very smart to brash away ccm mud, hizo tricks za smearing campaign ndo bush alizokuwa anatumia in 2000 and 2004 kwa kumtumia spin master wake anaitwa carl rove, kuwapaka matope al-gore and later john kerry, lakini obama alisoma kitabu chao cha dirty politics and smearing campaign ambacho mcain alikuwa atumia vilevile in 2008 but it did not work
kwa sababu obama was responding quickly and setting the record straight na alikuwa na surrogates kibao ambao walikuwa wana flood media, hivyo basi chadema inatakiwa kuwa na strong surrogates kwenye kila kanda wao kazi yao ni kujibu mashambulizi na smears zote ccm wanazozitoa.

Ccm wanatumia kila liwezekanalo chadema wasipate uhalali wa kuzungumzia ufisadi na mbinu chafu waliyokuja nayo ni kuwa label chadema kama radicals na wahuni, kumtuhumu mtu au chama kuwa kimesema matusi na lugha chafu is very wrong, they need to demand serious explaination matusi gani na lugha chafu gani? Wakishindwa kurudia hayo matusi then need to apologize na wananchi wafahamishwe kuwa ccm wana hofu ya kuwa exposed madhambi yao ndo maana wanatumia tricks za kutupaka matope, vyama vya upinzani jukumu lake ni kutafuta udhaifu ya chama kilichopo madarakani na kuutumia kuwanesha na kuwashawishi wananchi kuwa weakness za ccm ni hizi ndo maana hakistahili kurudishwa madarakani, ccm walichotakiwa kufanya ni kujibu hoja kwa hoja kwa vielelezo, this is strugle for power sio kutoa ahadi kibao ambazo ulizotoa nyuma hujatekeleza,
ccm wasijalibu ku set issue za uchaguzi za kuzungumzia kila chama kitakwenda na issue zake and then watanzania tutaamua. Unajua ccm wameishiwa kabisa ndo maana wanaleta sababu zisizo kuwa na msingi wao ndo wamezua kuwa chadema wamesema matusi
 
Slaa akata anga Morogoro
Akiwa Mikumi, alimlipua mwenyekiti wa kamati ya kampeni za CCM, Abdulahman Kinana, akisema kigogo huyo ana mkono katika biashara chafu za makampuni ya meli; akamtaka ajielekeze katika masuala ya kitaifa badala ya kumwandama yeye (Slaa). Akasisitiza kwamba ana ushahidi wa kauli zake, kwani hana historia ya kukurupuka.
Sasa ndiyo naanza kuelewa kwa nini CCM wanasisitiza lugha za ustaarabu wanaogopa kuumbuliwa madhambi yao, Kinana naye kesho aseme katukanwa kwa kuambiwa ukweli kuwa ana mkono kwenye biashara chafu ya meli. Kwani kusema ukweli ni matusi au wanafikiri sisi hatujui matusi ni kitu gani, wao wajibu hoja wasikimbilie kutukanwa au waende mahakamani.
 
Kama namuona vile Kinana!! Amekanyaga bomu.

However, ni vizuri CHADEMA kuweka records staright ili kwenda sawa na wakati. Inabidi Abdulhaman Kinana akose la kusema!!

Go Slaa...
 
Kama namuona vile Kinana!! Amekanyaga bomu.

However, ni vizuri CHADEMA kuweka records staright ili kwenda sawa na wakati. Inabidi Abdulhaman Kinana akose la kusema!!

Go Slaa...
ufisadi au kuitwa wezi sio lugha za matusi jamani wanataka lugha gani zitumike!
 
Nimefurahia sana hili alilosema baba wa taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere.

" Kila nilipokuwa nikitaka kung'atuka, walikuwa wakiniambia Mwalimu andelea tu, hii nchi bado ni changa na umeitoa mbali, nchi haitaendelea bila wewe. Nami niliendelea, hadi pale nilipokuja kugundua kumbe nchi changa wanayoiongelea ni FAMILIA ZAO, na hazitaendelea bila mimi kuwepo madarakani, maana walikuwa hawana uhakika kama RAIS ajae atawaacha katika nafasi walizokuwa nazo" Julius Nyerere
 
Slaa just call a spade a spade and not a spoon.

CCM na kundi lao ni wezi na wanahitaji kuitwa wezi. Hivi wanategemea tuwaite vipi?
 
REV Masanilo nishakula Ndovu sijui kama nitaweza kuweka msisitizo niotaka. Kinana kakiri kuwa meli iliyokamatwa China ikiwa na meno ya Tembo kutoka Tanzania, ni mali yake kwa kumiliki hisa 7,500 kati ya hisa 10,000 za maeli hiyo. Sasa ni kwanini tuansumbuliwa kichwa na huyu mtekaji meli wa Kisomali?

Watanzania kibao wako Keko, Segerea na Ukonga kwa kukutwa na mali za wizi majumbani, ofisini katika magari n.k. Iweje majeshi ya kimataifa yakute mali ya iliyoibiwa Tanzania katika meli ya Ndg Kinana na Jeshi letu la polisi lshindwe kuchukua hatua za kufaa za kumuunganisha katika kesi hiyo kama wanayowafanyia watanzania wanokutwa na mali za wizi? Iweje huyu kikbaka wa Kisomali aliyekutwa na nyara za Tanzania alipopanga asihusishwe katika kesi hiyo? Hivi Mwema kaenda likizo kipindi hiki nini?
 
Jatropha,
Mwema yupo. Lakini kuna watu hawaguswi Bongo. Chenge ni mfano mmojawapo.
 
Back
Top Bottom