majata
JF-Expert Member
- Oct 7, 2010
- 431
- 179
Nimeamini kwamba maji yamezidi unga baada ya kushuhudia kile kilichojitokeza katika mkoa wa tanga, Mh Dr slaa alikuwa akihutubia maelfu ya watu waliohudhuria mkutano wake Huku kukiwapo magari kama matatu yaliyojaa polisi waliokaa barabarani mara maandamano ya wanaccm na ngoma zao wakakatiza na kuvuruga uskivu wa watu waliokuwa wanamsikiliza kwa makini Dr, nusura watu waanzishe ugomvi, nimeshindwa kuelewa hawa polisi kazi yao nini kama sio kuepusha uwezekano wa ugomvi? kwani walishindwa kuwaambia ccm wasipite kwenye mkutano wa slaa? HONGERA DR SLAA LEO NIMETHIBITISHA KWA MACHO YANGU JINSI WATU WANAVYOTAKA KULICHAFUA JINA LAKO KWA KISINGIZIO CHA KUMWAGA DAMU WAKATI WAO NDIO CHANZO, ULITUMIA BUSARA SANA KUWAAMBIA WATU WATULIE NA WAWAACHE WATU AMBAO AKILI ZAO NI MBOVU, SERAZAKO TUMEZIKUBALI NA TUNAKUAHIDI KURA ZETU, NASUBIRI KWA HAMU INTERVIEW YAKO LEO JIONI MAANA SICHOKI KUKUSIKILIZA KWA SERA ZAKO ZENYE MATUMAINI MAKUBWA.