Siyo kosa la Kikwete, ni la Mkapa

So now Mkapa is good eeh?!. one year ago usingeweza kusema maneno haya kwenye hiki kijiwe watu wakakuacha hivi hivi................lakini siasa ndivyo zilivyo.....majungu kwenda mbele.
 
So now Mkapa is good eeh?!. one year ago usingeweza kusema maneno haya kwenye hiki kijiwe watu wakakuacha hivi hivi................lakini siasa ndivyo zilivyo.....majungu kwenda mbele.
Palipo na shetani wawili, mmoja ana unafuu; sasa kazi ni kuchagua yupi ana unafuu kidogo japo kwa uzito wa sisimizi, kumzidi mwenzie..!!
 
Tatizo ni kwamba,watanzania hawakumjua vizuri tangu mapema!sasa wamemjua vizuri alivyo msanii!!!!!!!!!!!!!!!!
 

Heshima kwako Kichuguu,

Mkuu zipo habari nyingi kwamba Kikwete hakuwa chaguo la Mkapa.Mkapa alipenda Prof mwandosya,Dr Abdallah Kigoda na Brig Gen H Ngwilizi mmoja wapo amwachie kiti cha urais lakini ilishindikana mtandao wa Kikwete ulimzidi nguvu hakuwa na njia ya kukwepa ila kumkabidhi Ikulu shingo upande.
Mkuu,kama ulikuwepo vile,hapo kwenye colour wengi hawaijui hii na naona jamaa kampoteza kiaina.
 
Tatizo ni kwamba,watanzania hawakumjua vizuri tangu mapema!sasa wamemjua vizuri alivyo msanii!!!!!!!!!!!!!!!!

Kwa upande wangu sitapenda kumtupia raisi mstaafu lawama,bali matatizo ya mheshimiwa aliyeko madarakani hata mwalimu Nyerere aliyaona mwaka 1995,ndipo alimwambia asubiri kidogo,lakini kosa liko kwa wananchi ambao walimpa kura za kishindo,tatizo hatuna elimu ya uraia,ya kuona mambo kwa mapana,usishangae wananchi hawa hawa tukampa tena kura za kishindo,utamlaumu Mkapa,"Mkapa did a good work for this country",barabara nzuri tulizo nazo leo,Kiwanja cha kisasa cha mpira, aliendelea kudumisha amani na mshikamano ni juhudi za Mkapa,He played his part anyway.Matatizo ya Kikwete ni yake binafsi,kwa kifupi hawezi kuongoza,acha amalize muda wake,atuachie amani yetu,ambayo ni hazina aliyotuachia muasisi wa taifa letu.

Tukutuku kama alivyosema Elisante Yona

Ni kikwete aliyekuwa kwenye wizara zote mbovu, kama nishati na madini,achilia mbali ya nje.

Ni kikwete aliyeingia mikataba yote haramu nchi hii aliwa waziri.

Kma tungekuwa tunachagua watu based on their previous performance basi hata hiyo 2005 JK was not sipposed to qualify for presidential position.

Tumezoea shida, kuonewa, kunyimwa haki, tumekua hivyo na ujinga huo. wakati wenzetu wanasema wako karne ya 21 , we are far back karne ya 15 mwishoni hivi.

Leo tunavyoongea, CCM wengi na akili zao ndogo, watamchagua JK! uliza what he have done nothing! nothing!

Sisi ndio tuna makosa, ndio wa kulaumiwa, hata strategy zetu za ukombozi zina walakini mwingi sana.Lakini atleast we are somewhere!

cheers
 
Kikwete is a youg Boy... having fun in a state house!

Baada ya kumaliza utasoma kwenye face book yake

... I real enjoyed being there ...and am passing it over to my Boys... if my wife wont make it!!

Kikwete yuko pale kutengeneza rekodi ya kuweka kwenye face book ...hajali chochote kuhusu Taifa na wananchi wake...!

Nashindwa kuelewa na kuamini haya yanatokea kwenye nchi yangu and He is my president!

Na yeyote aliyemuwezasha kufika pale being Mkapa et al ... they should be ashemed!

 
benjamean hausiki kabisa na upuuuzi wa huyu jay kei, jay k ni snitch toka long tym na ndo maana waasisi wanampa cold shoulder.
 
Asante sana mkuu kwa hayo, ila kama ulifuatilia uteuzi wa K'wete mwaka 2005 kwenye ngazi za chama utagundua kuwa Mzee Mkapa was totally against this dude. na K'wete alilifahamu hilo ndoa maana aliamua kuandaa mtandao ambao ndo ulimsaidia kuingia madarakani na kumporomosha kiutendaji. Kimtazamo kwa ile speech ya mwisho siku ya kupiga kura nec Mkapa alimponda kiaina huyu mkwere, alionekana zaidi kumkubali Salim na si kuyu mkwere. But hakuna shida kazi tuanayo kuwa nayo ni kutokubali kufanya makosa tena kwa kuing'oa hii familia ya yeboyebo!
 
inavyo semekana Kikwete na mtandao wake walipojua kwamba hatokuwemo, walimpelekea mzee mkapa faili la madudu alio fanya, mzee ikabidi afanye u-turn, oh kwa kusema tusipo wapa vijana tukaendelea kujipa wazee, tutawakatisha tamaa. naona ra, kikwete walianza kujitayarisha toka 1995 alipo ondolewa na Mwalimu.
So wakulaumiwa ni Mkapa kutokuwa strong enough, nashanga alikuwa strong kumtoa Mzee wa Mtera.
 
Anatumia udini kutawala ni mtu wa ajabu sana,hakika ataenda na dhambi hizi vizazi hata vizazi,kwa kweli ni aibu kuwa Rais mwenye upeo kama huyu bwana dah.
 
Mkapa anahasira na Kikwete saana, anauchungu nae kama mtu aliechanwa na WEMBE KWENYE MBONI YA JICHO.
 
Siamini kama anaweza kushinda lakini kwa vile wote wana nafasi sawa ya kutinga Ikulu niseme itakuwa miaka 5 ya giza JK akirudi Ikulu. Kumbuka ameshindwa kujenga nchi wakati anafikiria kuwania muhula wa pili na piga picha itakuwaje wakati huu ambapo hatakuwa na jambo la kupoteza. Bace for suffering!
 
Mkapa anahasira na Kikwete saana, anauchungu nae kama mtu aliechanwa na WEMBE KWENYE MBONI YA JICHO.

Dah!!, Ndugu Nguvumali, picha yako hiyo ya wembe ndani ya jicho ni graphic sana; je unaweza kuindoa au kuipunguza ukubwa?


Shea ya Mkapa ni kuwa kwa vile alijua kuwa jamaa huyu ana upungufu, na alikuwa akiwania uraisi. Mkapa alikuwa na uwezo wa kuonyesha udhaifu wa jamaa huyu mapema sana kabla hata wakati wa uchaguzi haujafika. Kwa mfano kama angemdemote au kumvua uwaziri na kuelezea wazi sababu za kufanya hivyo, basi JK asingepata nguvu sana za kujenga mtandao kama alizokuwa nazo akiwa waziri aliyeonekana clean.

Of course, kwa kumlaumu Mkapa, haina maana kuwa yeye alikuwa mzuri, ila sasa ukiwaweka katika mizani moja unaona kabisa kuwa Mkapa alikuwa ahueni sana kuliko huyu bradhameni JK
 
Kosa ni la Kikwete mwenyewe, kwani hajijui udhaifu wake?


Sitaki kuaminishwa kuwa Kikwete alidhani anaweza kuongoza. Alijua hawezi, aliamua tu kufanya labda kwa kuridhisha 'ego' yake.

Hii reply haitofautiani na ule mchezo wa Pwagu na Pwaguzi. Jamaa alipigwa jiwe na Pwagu... alipoenda kushtaki mahakamani Pwagu akajitetea: "Ulipoona jiwe linakuja kwa nini hukulikwepa?" Na Gaijin hivyo hivyo anataka kutuaminisha kuwa kabla Kikwete hajagombania urais ilibidi "ajijue udhaifu wake na asigombee".
Back to the topic. Mimi sikubaliani na wanaosema eti Mkapa aliiongoza Tz vizuri. Wakati wa Mkapa yalifanyika mambo mengi sana machafu.. kuanzia mauaji ya Zanzibar mpaka ufisadi wa kila aina. Labda ukimfaninasha na Kikwete ndio unaweza kusema kuwa kuna ka-unafuu kidogo sana. Mwanzilishi wa hii thread amejatoa hoja kwamba kosa ni la Mkapa (kwa kumwachia kilaza kama Kikwete madaraka).... Ukweli ulioje!! Unajua rais wa nchi (hasa Afrika) ambazo "systems" zake bado ni changa anatakiwa kuelewa kwa undani mtu atakayemrithi ni wa aina gani. Ndio maana anakuwa na nyezo nyingi za kumwezesha kupata taarifa na ikiwezekana ku-manipulate mambo pale ambapo anaona kuna hatari ya kurithiwa na mtu mbaya. Sasa mkiniambia Mkapa pamoja na nyenzo zoooooooote alizokuwa nazo alishindwa kumwelewa na kumzuia Kikwete asiwe rais huwa nashangaa sana na kujiuliza: Tulikuwa tumetawaliwa na boga???
 
...... Kikwete aliingia madarakani kwa kuwachafua wapinzani wake akina Salim na wengineo. Alipofika madarakani akahodhi CCM kuwa mali ya familia yake na kuendesha nchi kwa mtindo usioona mbele wala nyuma. Ilipofika wakati uchaguzi, akagundua kuwa CCM aliyojenga ya ukoo wake haiwezi kumrudisha tena Ikulu, akaamua kuanza kutumia njia zile zile za kuwachafua wapinzani wake ambazo baada ya kuona hazisaidii, basi ameanza kuingiza njia za mkato za kugawanya wapiga kura kwa msingi wa udini.

Hiyo ni myopic strategy kwa sababu iwapo itafanikiwa kumweka madarakani, basi atatawala nchi isiyotawalika tena, na atakumbukwa katika historia kuwa rais aliyevuruga kabisa amani na utulivu uliojengwa kwa nguvu kubwa sana na mwasisi wa taifa hili.

Hata hivyo nikiangalia nyuma tena, ninadhani kuwa kosa siyo la Kikwete bali ni la bosi wake wa zamani aliyemwachia kiti hicho. Inawezekana ni kwa sababu Mkapa alikuwa na matatizo yake akaogopa asiumbuliwe, lakini Mkapa huyo baada ya kuwa bosi wa Kikwete kwa miaka kumi, alitakiwa ajue fika strengths na weaknesses za Kikwete na kuwasaidia wananchi aliokuwa anaongoza kumfahamu mtu huyo vizuri kabla ya kumpa madaraka mazito namna ile.

Mkapa ana shea yake kubwa sana katika matatizo yanayoletwa na Kikwete.

Kichuguu:

Toka Mrema ashindwe uchaguzi, nimeweka pembeni siasa za Tanzania. Udhaifu wa Kikwete is probably a blessing in disguise. Mimi ni mshabiki wa political pluralism.

Peformance ya Kikwete ingekuwa kubwa kuliko ya Mkapa, nina uhakika upinzani ungepata kura Pemba tu. Lakini kwa jinsi CCM ilivyoendesha nchi, inawezakana CHADEMA will capitalize this time.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi, bunge lilimfanya waziri mkuu kuachia ngazi LIVE ON TV. Kwa mara ya kwanza, mgombea wa CCM sio entitlement ya ushindi.

Siku zote watanzania tunasema awamu ya kwanza, pili, tatu, nne. Huu ni upuuzi tu. Awamu kamili ni pale rais atakapotoka chama kingine.
 
Kwa na yeye ni msafi?wengineo ie Salim walichafuliwa, ila yeye alikuwa mchafu?Kiwira ilimyima ujasiri?Vipi kuhusu EPA ambayo ilitokea kipindi cha transition?

Wengi tunaweza kukubaliana kuwa Mkapa alikuwa rais mzuri, lakini suala la usafi lina viulizo vingi. Hawezi kuitwa msafi kwenye siasa au mapambano dhidi ya ufisadi, kwa kigezo chochote kile cha mtanzania au mgeni. Lakini for sure alikuwa kiongozi mzuri, aliweza kuonesha leadership na aliweza kuonesha utendaji bora kwa watanzania.

Ni KWELI Mkapa ndiye wa kulaumiwa na matatizo yanayotukabili sasa, sio JK. Alijua kabisa JK anaingia madarakani huku mafisi wanafurahia, Mkapa ndiye superviser wa EPA kwa kuwa EPA ilifanyika akiwa rais na haiwzekani yeye asijue nini kilikuwa kianendelea, amefanya kazi na JK kwa miaka mingi kwa ahiyo alitakiwa ajue wazi udhaifu wa JK angensaidia kuondoa udhaifu wake kwa kumshauri namna ya kuunda cabinet. Even better angekishauri chama namna ya kuhakikisha urais wa JK unakuwa na manufaa kwa Tanzania.

Inawezekana kuwa hakupenda JK awe rais, lakini alitakiwa kusema wazi weakness za JK, kuliko kutuacha watanzania na kusema shauri yenu mtakiona. Sasa kweli tunakiona lakini chanzo cha tatizo ni Mkapa, na yeye akiwa mwenyekiti wa Chama na akiwa rais wa nchi alikuwa na uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi ya kukiokoa chama na nchi, He gave blind eye and said to hell. And that is where we are now.
 
Back
Top Bottom