Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,550
- 19,416
...... Kikwete aliingia madarakani kwa kuwachafua wapinzani wake akina Salim na wengineo. Alipofika madarakani akahodhi CCM kuwa mali ya familia yake na kuendesha nchi kwa mtindo usioona mbele wala nyuma. Ilipofika wakati uchaguzi, akagundua kuwa CCM aliyojenga ya ukoo wake haiwezi kumrudisha tena Ikulu, akaamua kuanza kutumia njia zile zile za kuwachafua wapinzani wake ambazo baada ya kuona hazisaidii, basi ameanza kuingiza njia za mkato za kugawanya wapiga kura kwa msingi wa udini.
Hiyo ni myopic strategy kwa sababu iwapo itafanikiwa kumweka madarakani, basi atatawala nchi isiyotawalika tena, na atakumbukwa katika historia kuwa rais aliyevuruga kabisa amani na utulivu uliojengwa kwa nguvu kubwa sana na mwasisi wa taifa hili.
Hata hivyo nikiangalia nyuma tena, ninadhani kuwa kosa siyo la Kikwete bali ni la bosi wake wa zamani aliyemwachia kiti hicho. Inawezekana ni kwa sababu Mkapa alikuwa na matatizo yake akaogopa asiumbuliwe, lakini Mkapa huyo baada ya kuwa bosi wa Kikwete kwa miaka kumi, alitakiwa ajue fika strengths na weaknesses za Kikwete na kuwasaidia wananchi aliokuwa anaongoza kumfahamu mtu huyo vizuri kabla ya kumpa madaraka mazito namna ile.
Mkapa ana shea yake kubwa sana katika matatizo yanayoletwa na Kikwete.
Hiyo ni myopic strategy kwa sababu iwapo itafanikiwa kumweka madarakani, basi atatawala nchi isiyotawalika tena, na atakumbukwa katika historia kuwa rais aliyevuruga kabisa amani na utulivu uliojengwa kwa nguvu kubwa sana na mwasisi wa taifa hili.
Hata hivyo nikiangalia nyuma tena, ninadhani kuwa kosa siyo la Kikwete bali ni la bosi wake wa zamani aliyemwachia kiti hicho. Inawezekana ni kwa sababu Mkapa alikuwa na matatizo yake akaogopa asiumbuliwe, lakini Mkapa huyo baada ya kuwa bosi wa Kikwete kwa miaka kumi, alitakiwa ajue fika strengths na weaknesses za Kikwete na kuwasaidia wananchi aliokuwa anaongoza kumfahamu mtu huyo vizuri kabla ya kumpa madaraka mazito namna ile.
Mkapa ana shea yake kubwa sana katika matatizo yanayoletwa na Kikwete.