Simba Mkali
JF-Expert Member
- Jan 31, 2012
- 620
- 239
Wadau kuna kitu kipya kimeingia mjini Kinaitwa Kitchen Mada ambacho kinawahusu wanawake tu, hii jambo nimelishuhudia Wik-end hii wakati nilipoenda kuhudhuria harusi moja maeneo ya Mbezi. Ile harusi ilifungwa kwa imani ya dini ya Kiislamu na kwa kuwa wazazi wa binti walikuwa na maadili ya dini wakaamua kumfanyia Kitchen Mada mtoto wao badala ya Kitchen Party ambayo imezoeleka.
Ndani ya Kitchen Mada kulikuwa na wanawake tu, mwanaume huruhusiwi hata kuchungulia, wanawake wawili walikuwa wakitoa mada mbalimbali za chumbani na huku akina mama wengine wakisikiliza na kuchangia pale panapostahili na kusindikizwa na nyimbo ambazo walikuwa wakiimba wenyewe. Kwa kweli hii nimeipenda kwa kuwa Kitchen Party siku hizi zimekuwa ni uozo wa kukusanya vyombo na vichaka cha matusi. sijui unasemaje mdau?
Ndani ya Kitchen Mada kulikuwa na wanawake tu, mwanaume huruhusiwi hata kuchungulia, wanawake wawili walikuwa wakitoa mada mbalimbali za chumbani na huku akina mama wengine wakisikiliza na kuchangia pale panapostahili na kusindikizwa na nyimbo ambazo walikuwa wakiimba wenyewe. Kwa kweli hii nimeipenda kwa kuwa Kitchen Party siku hizi zimekuwa ni uozo wa kukusanya vyombo na vichaka cha matusi. sijui unasemaje mdau?