SIYO Jukumu la CHADEMA kuikosoa CCM ili ijisahihishe na kutawala Vizuri

Story yako nimeikubali mkuu.
Na. M. M. Mwanakijiji

SIYO jukumu la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kukikosoa Chama cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake ili vijirekebishe na hatimaye viweze kutekeleza majukumu yao vizuri. Siyo kazi ya CHADEMA kuwa mkosoaji mkuu wa serikali ili serikali iweze kujisahihisha na kufanya kazi yake vizuri ya kuwahudumia wananchi. Kwa hakika kabisa siyo jukumu la upinzani nchini kuipatia CCM na serikali iliyoko madarakani mawazo mapya ya mambo ya kufanya ili mambo hayo yafanywe na kila mtu awe na furaha. Ni makosa ya kifikra na kutoelewa siasa kudhania au kukubali kuwa upinzani jukumu lake ni "kuikosoa serikali".

.
 
Hongera kwa kushusha shule ya nguvu kwa wanaopenda kufuatilia maslahi ya taifa letu. ni wakati muafaka kwa vyama vyetu viendeshwe kisayansi. ni jukumu la kila mmoja wetu kufuatilia kwa karibu yanayoendelea, kutathmini na kutoa mchango wake kipi kitatusaidia kwenda mbele ambako ni kwema zaidi kwa kila mmoja wetu. mimi naamini kwamba tutaisaidia nchi yetu kama tutaiweka CCM pembeni walau muhula mmoja tu, ili wajipange upya na kuondoa fikra potovu kwamba wao wana haki ya kutawala nchi hii. wakati tunafanya hivyo, tunaweka mfumo ambao sio rahisi kwa yeyote anayeingia madarakani, kuyahodhi na kufanya anavyotaka. kutumia nguvu za dola kujilinda mwenyewe madarakani, badala ya kulinda na kuendeleza maslahi ya taifa.

Mwisho nakupa hongera kwa kuonesha upuuzi wa fikra za watu kama ZITTO KABWE, ambao wamefikia hatua ya kutofautiana na msimamo wa chama, mfano pale walipoamua kutoka nje ya bunge, kisa ni kubembeleza peremende toka kwa CCM, asionekane mbaya kwa JK. hapo si upinzani kabisa! au tuseme, ni kujitakia upinzani wa kudumu.
 
Ndugu Mwanakijiji,
Ni kweli "Siyo Jukumu la CHADEMA kuikosoa CCM" ila ni jukumu la kila raia wa Nchi hii mwenye mapenzi mema na nchi hii kukikosoa Chama Tawala pale kinapotenda ndivyo sivyo na kukiondolea hadhi ya kutawala nchi hiyo.
Binafsi yale yanayotendeka sasa hata ya kutoa SIRI au CONFIDENTIAL DOCUMENTS kuziweka hapa javini ni ishara ya kudhoofisha Chama tawala na kukifanya kijisahihishe! Kwa hiyo hilo linatakiwa liwe ni jukumu la kila Mtanzania na si Chama cha Upinzani pekee.
 
Mie kwa kweli nachukia siasa na duh story hii ndefu nitaisoma zaidi next time

Ila bado ujue kuna watu watapingana nawe na umecopy wapi point zako

Je wewe ni mwanasiasa

Embu nieleze zaidi labda nitapata hamu ya kusoma story yako mida hii
 
Mie kwa kweli nachukia siasa na duh story hii ndefu nitaisoma zaidi next time

Ila bado ujue kuna watu watapingana nawe na umecopy wapi point zako

Je wewe ni mwanasiasa

Embu nieleze zaidi labda nitapata hamu ya kusoma story yako mida hii

heri upumzike tu huenda wewe si mtanganyika!
 
Kwa hiyo mwanakijiji unaadvocate political manipulation kwa wananchi.
Yaani serikali ikifanya jambo zuri, unataka chadema iseme au itende kinamna fulani hilo jambo lionekane ni baya au "halitoshi?".
Je itakuwaje pale chama tawala kitatenda kwa ufasaha mkubwa baadhi ya mambo yanayosimamiwa na kuaminiwa na chama pinzani ambayo ni ya maslahi kwa taifa?.

Hii hoja ya mwanakijiji inaniconvince tuamini kwamba siasa ni game fulani ya kumanipulate mass.
Kama chama tawala kinafanya kazi vizuri sana, halafu chama pinzani kikaja na hoja ambazo si bora kuliko za chama tawala, halafu kikaconvince mass kwamba hizo ni sera bora zaidi, hii ni suicidal kwa mass yenyewe na chama pinzani chenyewe.
Mimi ninadhani siasa hasa ile inayohusu misingi ya uchumi wa nchi haina budi kujengwa katika misingi ya kisayansi, kwa maana ya kweli za uchumi tunazozijua, na si katika propaganda za kilayman ili mradi tu ueneze fitna mass ikichukie chama tawala na kukiweka madarakani chama pinzani.

Hoja hii ya Mwanakijiji ina pungufu moja kubwa.
pungufu lenyewe ni kujaribu kuonyesha kwamba CHAMA CHA UPINZANI KINA JUKUMU LA KUJIANDAA KUSHIKA DOLA TU, WAKATI HUOHUO INAACHA JUKUMU LA CHAMA CHA UPINZANI KUCHANGIA KATIKA KUTOA MAWAZO MBADALA YA KUSAIDIA NCHI IEEDELEE.

Tatizo la hoja hii ya Mwanakijiji ni kwamba Inajaribu kukita misingi ya "Uchama kwanza", Taifa next. nitaeleza hii pointi.
(1)Chadema au chama fulani kushika dola ni Ishara ya kufaulu kwa Chama Hicho, kufaulu kwa wananchi kutakuja pale ambapo chama fulani kitaunda serikali itakayo deliver. haitamsaidia mwananchi yeyote iwapo CHADEMA Itatimiza lengo lake la kushika dola halafu ikafanya yaleyale kama ya CCM au ikafanya chini ya hapo. sasa je wanasiasa makini wanataka washike dola tu ndo wajione wana nafasi ya kutoa mchango wa Kusaidia Nchi?.

(2) Je ni vipi kama Kusaidia nchi kutajumuisha kutoa mawazo mazuri ambayo yakifanyiwa kazi kutasaidia Kuimprove maisha ya wananchi na hivyo wananchi kuona kwamba kumbe hata Wapinzani wana mawazo mazuri na hivyo wanafaa kupewa dola?.

kiufupi hoja ya mwanakijiji imejaribu kulificha jukumu moja la chama cha upinzani at the expense ya jukumu lingine. KIUFUPI CHAMA CHA UPINZANI KINA JUKUMU KUBWA MUHIMU SANA NALO NI NCHI NA WANANCHI KWANZA, NA KUTIMIZA JUKUMU HILI SI KUSHIKA DOLA PEKE YAKE, BALI INAWEZA KULITIMIZA KWA KUKOSOA NA KUPENDEKEZA NJIA MBADALA, LAKINI WAKATI HUO HUO KIKIJINADI NA KUJIPAMBANUA MBELE YA UMMA KWAMBA KINAWEZA KUSHIKA DOLA.
Kutokikosoa Chama Tawala ni Ubinafsi na Kutokukipa mawazo mbadala kwa ajili ya maslahi ya Umma ni uchoyo usiomithilika kwa wananchi, ni sawa na kuwaadhibu wananchi kwamba Madhali mmeninyima kura, basi na mimi siwaonesheni njia bora za kutatua tatizo kadha wa kadha
 
Naona jina la Zitto lipo kwenye hii post. Namuomba sana sana kama ni yeye na au kama kuna kiongozi/mwanachama wa chama 'rasmi' cha upinzani-CHADEMA waweke BANGO mbele ya office za chama makao makuu DSM na office za mikoa lituongoeze kwenye count-down to siku 90. Tunataka tuone kwa vitendo baada ya hizo siku 90 hii timu ya mpya ya ccm itafanya nini na wanachi wengi kama si wote wakiamka asubuhi wajue zimebakia siku ngapi kabla ya fukuza-fukuza kuanza (kama kweli ipo!).
 
Mimi napingana kabisa na mtoa mada kwani naona ametumia mtindo kiuandishi tunaita amehodhi hoja.

Awali ya yate ni lazima kujua kuwa upinzani sio uadui, lakini vile vile tunapashwa kujua nia na madhumuni ya kuwepo upinzani ni kuleta hali bora kwa jamii husika. Kwa msingi huo upinzani upo pale kuleta hoja mbadala zenye kuweza kukinzana na zile za Serikali kwa nia ya kuchochea maendeleo ya jamii husika kwa haraka.

Siku zote vyama vinakuwa na ILANI zake ambazo zinaeleza bayana vipaumbele na mtazamo wako katika kuiongoza jamii , lakini ikumbukwe kuwa Ilani hizo sio msahafu au Biblia kuwa haiwezekani kuzibadili kulingana na hali halisi na mwelekeo wa maisha.

Kwa kuwa vyama vyote tawala na upnzani wote wana nia ya kuleta maendeleo ya haraka kwa jamii basi chama makini ni kile kinachokubali kukosolewa na kubadili mwelekeo wake kwa nia ile ile ya kuleta maendeleo ya jamii . Kwa msingi huo vyama vya upinzani vina wajibu wa kuikosoa Serikali au chama tawala na hata kuwaeleza njia sahihi ya kuleta maendeleo. Ndio maana ILANI zao zinakuwa sio Siri zinawekwa wazi na mtu yeyote anaweza ku borrow na kuzitumia katika kuendeleza jamii.

Kwa msingi huo tunasema Ni jukumu la wapinzani kuikosoa Chama tawala katika kuhakikisha kuwa wanaleta ustawi wa jamii.
 
Hapana. Nisome vizuri tu. CCM wanayo ILANI yao ya UCHAGUZI. Dr Slaa na wenzake hawaiongelei hiyo. Badala yake wanahangaika na Maghufuli kauza nyumba za serikali. Malecela kaandika vimemo vya EPA na mambo mengine kama hayo ambayo yalipaswa kufanywa na vyombo vya habari za uchunguzi.

Umesema hapo juu na ninakunukuu...."ambayo yalipaswa kufanywa na vyombo vya habari za uchunguzi."

Nami najibu hivi...vyombo vya habari havikufanya uchunguzi na huo ndio ukawa mtaji wa Dr Slaa & co.

Ninaamini mwanzisha thread ana-infer kuwa opposition should be capitalizing on opportunities like this to make CCM look bad....and rightly so!
 
A masterpiece! Thanks for reminding us our core objective ie KUSHIKA DOLA. Lazima tuonekane bila chembe ya shaka kuwa tunajiandaa kushika DOLA na kuongoza. Asante sana for this MUST READ!

Zitto thanks for acknowledging hii article and kama ilivyo emphasize basi CHADEMA has to in the contrary to CCM weaknesses show to the wananchi how different they can be if are to be the ruling party. Mfano viongozi wengi wa CCM hasa hao wakuu ni vigeu geu leo wa kija na hiki kesho wanakuja na kingine kwenye kusema na hata kutenda hapo CHADEMA kinatakiwa kiwe consistent kuonyesha kuwa ni wakuaminiwa zaidi kuliko chama tawala. Mfano mzuri ni kile mlichokifanya kwenye kusitisha maandamano kuwa serikali ikifanya hivi basi sisi hatutafanya coersive measures lakini hamtakiwi kuishia hapo baada ya hilo kutokea ni jukumu lenu kuionyesha jamii how wrong CCM was kuja na kitu ambacho hakina maslahi ya taifa ila selfish interest (Kwakua mliahidi hamtaisema serikali bali kuipongeza basi maandamano yangekuwa kuwapongeza kwa njia ya kuwaponda yaani kueleza how peoples power inaweza kutumiwa kubadili decision za chama tawala so the objective changes badala ya kuweka pressure mna create awereness kwanjia ya kuonyesha how powerfull you are with peoples power tofauti na CCM kwakutumia nguvu ya dola). Hapo mnaonyesha you can do something better and your ideas are also public ideas ndiyo maana CCM ime bow siyo kwasababu ya kitu chochote ila kwasababu CHADEMA iko upande wa public interest na CCM bila public hakina nguvu so is important public i support CHADEMA ili ika implement its correct idea kwakuchukua dola kwani bila dola CHADEMA's idea haziwezi kutekelezwa inavyotakikana maana wao ndiyo wenye hiyo idea na siyo CCM. A good example ni hii issue ya katiba maana CCM imeonyesha kabisa haiwezi kufanya vile public wanavyotaka na CHADEMA inaonyesha wanachokitaka ndiyo public preference so the next step nikuwahamasisha public iwape ninyi nafasi muifanye hiyo kazi vizuri kwani iko kwenye ilani yenu na siyo ilani ya CCM CHADEMA kukubali CCM iifanye wakati wao siyo copy right kwanza ni wizi na pia hawataifanya in a correct way. Kwakuwa nguvu ya umma ipo hapo ndo ingekuwa gate way ya CHADEMA kupata full control katika hilo. Lakini wakati mwingine ku give in kunatakiwa ila siyo kujisahau nakuwaacha sasa wao waendelee kuwa watawala.

Lakini hii ni kwenye siasa kule kwingine kwenye serikali mnatakiwa kutenda kama vile ninyi ni serikali kwakufanya strategic policies formulation and implementation itakayoweza tengeneza system ambayo ni ngumu kuiondoa maana inahold interest za watu. On this naomba nisiweke wazi maana ni silaha ambayo adui akiikamata watatumia kutuangamiza. I being a member haitakuwa sahihi kuiweka hapa.
 
Nadhani tangu mfumo wa vyama vingi ulivyoanzishwa ilimekuwa safari ndefu,Mwanakijiji ukumbuke kama miaka kumi hivi kulikuwa na ombwe nla wanachi kutokuamini wapinzani,kwa hiyo kama ulivyoshauri vyama lazima wawe haswa vya upinzani lazima wafahamu spychology ya wananchi na matakwa ya wananchi ili kukidhi kiu yao.

Kwa kipindi chote hiki vile vile tangu mwaka 1995 bado wanachi wamekuwa hawaaiamini CCM na serikali yake na wala hawaridhiki na mwenendo wa utendaji wao kwa maana nyingine hawana imani na CCM pia,Kwa maana hiyo wanasiasa wanatakiwa wawe mbadala katika kuwaaminisha wanachi kwamba wanafahamu vilio vyao na wanaweza kuongoza na kuwapa ahueni katika maisha yao.

Mwanakijiji katika saikolojia ya binadamu,kuna kitu kinaitwa mawasiliano na mapatano ya kifikra (Mass communication & Ideology)ambayo yanaunganisha vitu vingi ikiwemo uwezo wa kutumia lugha inayoeleweka kwa wananchi ili wakuunge mkono.Kutokana na kwamba kulikuwa na mkanganyiko wa wapinzani kuaminiwa kutokana na ukweli ambao serikali ya CCM na CCM walitumia kuwarbuni wananchi kama vile ( Vyama vya upinzani,ni wa dini,wataleta vita,wakabila,waropokaji,wanahatarisha amani ya nchi )ni vyema vyama vya upinzani kwa mfano Chadema walivyotuia sera ya kuwafahamisha wananchi ukweli wa nini serikali yao inafanya kuwanyima haki zao za msingi na usatawi wa jamii,kwa kutoa mifano halisi ,Kama vile kuanisha wizi wa EPA na ukosefu wa vyumba vya madarasa,ukosefu wa dawa hospitali,barabara mbaya na mengineyo,hili limesaidia wananchi kutambua kwamba kumbe na wao wanawajibika kuhoji matumizi ya rasilimali utaona maandmano,mikutano ya kupinga ufujwaji wa rasilimali unafanyika hata ngazi ya kijiji

Lingine walilofanya vyama vya upinzani ni kujitambulisha kwamba ni sehemu ya wananchi na wananchi kujitambulisha na vyama ni kutokana na kuwa wanazungumza mambo ambayo yanawagusa wananchi

La mwisho ni hilo ulilosema ambalo wanatakiwa watuhakikishie wananchi kwamba wanaweza kutawala ,wanapaswa kuepuka mambo yoyote yatakayorudisha nyuma imani kwa wananchi lazima wawe kifua mbele kusimamia mambo ya wananchi lakini wanatakiwa wafanye kwa uangalifu mkubwa

Hawawezi kusemea kila jambo ni vizuri wapinzani wakawa wanafanya tafiti kila wakati ili kujua wananchi wanataka nini na wao wakaegemea hapo lakini sio yanayojiri kutooka chama tawala
kuna mbinu ya kuudhofisha chama na serikali na zipo nyingi nadhani walichofanya wapinzani kwa sasa ni kuichanganya serikali na chama tawala kupotea dira na kuanza kurukia agenda mbalimbali kwa maneno bila utekelezaji na ndio kifo chao
 
Mimi napingana kabisa na mtoa mada kwani naona ametumia mtindo kiuandishi tunaita amehodhi hoja.

Awali ya yate ni lazima kujua kuwa upinzani sio uadui, lakini vile vile tunapashwa kujua nia na madhumuni ya kuwepo upinzani ni kuleta hali bora kwa jamii husika. Kwa msingi huo upinzani upo pale kuleta hoja mbadala zenye kuweza kukinzana na zile za Serikali kwa nia ya kuchochea maendeleo ya jamii husika kwa haraka.

Siku zote vyama vinakuwa na ILANI zake ambazo zinaeleza bayana vipaumbele na mtazamo wako katika kuiongoza jamii , lakini ikumbukwe kuwa Ilani hizo sio msahafu au Biblia kuwa haiwezekani kuzibadili kulingana na hali halisi na mwelekeo wa maisha.

Kwa kuwa vyama vyote tawala na upnzani wote wana nia ya kuleta maendeleo ya haraka kwa jamii basi chama makini ni kile kinachokubali kukosolewa na kubadili mwelekeo wake kwa nia ile ile ya kuleta maendeleo ya jamii . Kwa msingi huo vyama vya upinzani vina wajibu wa kuikosoa Serikali au chama tawala na hata kuwaeleza njia sahihi ya kuleta maendeleo. Ndio maana ILANI zao zinakuwa sio Siri zinawekwa wazi na mtu yeyote anaweza ku borrow na kuzitumia katika kuendeleza jamii.

Kwa msingi huo tunasema Ni jukumu la wapinzani kuikosoa Chama tawala katika kuhakikisha kuwa wanaleta ustawi wa jamii.

Lakini ilani ni mkataba kati ya watawala na watawaliwa so kama chama hakina watu wakuiwezesha ilani yao iandikwe na kuwa implemented towards public preference basi ndiyo fursa hasa kwa chama pinzani kuchukua dola ili chenyewe ki implement ideas zake through ilani kama wana nchi wanakubaliana na hizo ideas. Ndiyo maana mwandishi kasema hakuna chama chenye haki ya kutawala milele na kingine pinzani cha kudumu. Ila decision factor ni public so kama pinzani kitaisaidia tawala basi inamaana kila chama kita assume a permanent position. Unachokieleza kuhusu welfare then ndo hapo kama ilani yenu ni public preference na mtaiiplement to the expectation ya public then public itaendelea kuwa vote ninyi kuongoza otherwise mtakuwa tu mna dictate na kama kuna true democracy basi hamna budi mfunge virago maana menu yenu haitakiwi na walaji.
 
Ni uchambuzi mzuri sana, ni kweli jukumu la chama cha upinzani si kuishauri serikali wala kuikosoa ili ijirekebishe bali ni kuikosoa(criticize) kwa yale iliyofanya ili kuidhihirishia jamii kuwa serikali haiwezi kutimiza matakwa yao ipasavyo, na kuidhoofisha ili ipoteze ujasiri na ichanganyikiwe. Matokeo yake ni wananchi kupoteza imani kwa chama tawala.
Katika kipindi cha hivi karibuni tumeona serikali ikichanganyikiwa kutokana na kukosolewa na kupewa shinikizo,kiasi kwamba watendaji wa serikali wanajipinga wenyewe, mfano ni suala la katiba(waziri Kombani,Werema V/s Rais),Dowans (Werema V/s Sitta), hii ni dalili kuwa CDM kimekuwa kikifanya kazi yake ya kuidhoofisha serikali vizuri mpaka sasa.
Hili la kujivua gamba linaonekana kuwa ni mbinu ya CCM kurejesha imani ya wananchi iliyopotea, ila niwapongeze CDM maana wameanza vizuri kupambana nalo kwa kutangaza list mpya ya mafisadi, kuonesha kuwa wanaotakiwa kuondolewa si hao watatu tu bali ni wengi akiwamo bwana mkubwa mwenyewe. Hii itawavuruga sana CCM na mpango wao wa kujivua gamba.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Mwanakijiji hiyo article inaonyesha uwezo na ujuzi wako wa kuchambua mambo. Sheba amecomplement vizuri sana. Tukiunganisha hizo postings mbili kila kitu kinakuwa wazi kwa anayetaka kuelewa na kufanikiwa kisiasa.

"Gamba la nyoka" sasa kama utaifa kwanza na chama baadaye basi nawakumbushe CCM kwani hilo walishalisahau siku nyingi mpaka wakaota magamba.
 
Mwanakijiji bwana hata kazi hazifanyiki. Uliyoyasema nikweli tupu na nadhani umewasaidia watu wa type ya Waberoya ( najua kwa busara zako huwezi kumtaja mkuu ila hili tuachie sisi) kuja kupoteza muda wao hapa kila siku chadema haijafanya hiki au kile. Message sent!

IC! alichoandika Mwanakijiji principally ni kilekile ambacho huwa najitahidi kuhubiri kila siku humu. Sina ligha nzuri, tamu na ya kufundisha kama MKJJ, lugha yangu ni kukufanya ujione mjinga na uache mara moja.

Sema asante kwa MKJJ haraka sana! leo amekueleza jukumu lenu na umefurahi meno yote nje! ningeandika mimi ungetukana!! what a joke.

Aibu!! umeshindwa pa kujishika unatokota!

Nadhani kadiri siku zinavyoongezela unagundua kuwa JF ni moto na hapendwi mtu hapa ila hoja tu.

Kataa kubali hoja hii ya MKJJ ndio msimamo wangu, na kwa hili nilichojifunza kwa MKJJ ni uandishi wake maridhawa ambapo Shalo mtoa matusi kwa kutumia biblia leo hii anakubali huku akiona aibu!

Unanikumbusha mbali sana, unanikumbusha utotoni wakati una ulizwa nani kakupiga? unajibu huku ukiangalia chini....unamnyooshea kidole aliyekuchokoza.

Unalia unaninyooshea kidole, waberoya kaingiaje hapa, kama ulishindwa kwenye thread zangu maana yake bado una gubu!!!

Angalia usiote ndoto WABEROYA!!! kama umenikumbuka kwenye darasa hili la MKJJ maana yake hujaelewa RUDIA TENA! amekosoa mwelekeo wenu, Tunataka chadema ichukue nchi.period

Hutalielewa hili kwani unafikiri aliye kinyume na wewe ni adui yako!! Did Jesus teach you that??
 
Na. M. M. Mwanakijiji

SIYO jukumu la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kukikosoa Chama cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake ili vijirekebishe na hatimaye viweze kutekeleza majukumu yao vizuri. Siyo kazi ya CHADEMA kuwa mkosoaji mkuu wa serikali ili serikali iweze kujisahihisha na kufanya kazi yake vizuri ya kuwahudumia wananchi. Kwa hakika kabisa siyo jukumu la upinzani nchini kuipatia CCM na serikali iliyoko madarakani mawazo mapya ya mambo ya kufanya ili mambo hayo yafanywe na kila mtu awe na furaha. Ni makosa ya kifikra na kutoelewa siasa kudhania au kukubali kuwa upinzani jukumu lake ni "kuikosoa serikali".

Salute!!
 
Umeongea vema Mwanakijiji, lakini pia TUTAZAME upande mwingine ni wakuu wa vyama hivi-hivi pinzani ambao wengi wao wanaisaidia CCM kujisafisha na kusafika kwa ushauri wao wanaoutoa (pembezoni *indirect speech) na hilo machoni pa watu wa kawaida halionekani lakini kwa watu wanaofikiria WANALIONA na KUFAHAMU.

Huwezi kuwa unagombea mchumba na adui yako kisha UMWAMBIE "wewe utaendaje UKWENI na tongotongo!!?" kisha ionekane wewe na huyo hamna urafiki...

NAREJEA SEMI ZA AWALI:

MAJI HAYASAHAU BARIDI, WALIOTOKA CCM KWENDA UPINZANI WATABAKI KUWA CCM! WATAISHAURI CCM HUKU WAKIUMALIZA UPINZANI KWA SUMU YA POLEPOLE!

Kwa maana hiyo SITOIPENDA CCM wala KUVIAMINI VYAMA HIVI mpaka pale TAKA zote Zitapokuwa haziko.
 
Back
Top Bottom