CHIMPANZEE
Member
- Mar 30, 2011
- 98
- 10
Story yako nimeikubali mkuu.
Na. M. M. Mwanakijiji
SIYO jukumu la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kukikosoa Chama cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake ili vijirekebishe na hatimaye viweze kutekeleza majukumu yao vizuri. Siyo kazi ya CHADEMA kuwa mkosoaji mkuu wa serikali ili serikali iweze kujisahihisha na kufanya kazi yake vizuri ya kuwahudumia wananchi. Kwa hakika kabisa siyo jukumu la upinzani nchini kuipatia CCM na serikali iliyoko madarakani mawazo mapya ya mambo ya kufanya ili mambo hayo yafanywe na kila mtu awe na furaha. Ni makosa ya kifikra na kutoelewa siasa kudhania au kukubali kuwa upinzani jukumu lake ni "kuikosoa serikali".
.