Siwezi amini hichi kitu kinaweza kutokea..(soma kisha hiki)

Huyu jamaa alicheza fyongo mbaya sana,ila ni fundisho kwetu sisi. Nafikiri sasa hivi tekinologia imekuwa kubwa, kuliko kudhalilika, unaenda nairobi hapo wana mbegu wanatunza unachagua nani uzae nae kwa picha, wanakuinsert kuliko kwenda kufedheheka kiasi hicho.

TZ haijafika, ikifika wala hakuna nyumba watalia eti hatuna watoto though ukweli utabaki kuwa uliwekewa mbegu kuliko huyo anayeenda kufanya practical na mkeo live.
 

What use is all that if the woman doesn't love you or respect you any more and non of the children are yours? You will do all the voodoo you want but it won't solve anything. Kwanza, kwa nini umuachie mwanaume mwenzako amzalishe mkeo in the first place?

yaani hiyo ndio hata mimi imeniacha njia panda, unawezaje kumuachia mke wako jamaa mwingine? tena kwa roho safi? huyu jamaa atakuwa anamatatizo makubwa zaidi ya hayo ya kutokuwa na uwezo wa kuzalisha
 
Jamaa akichukua watoto wake mshikaji ataaibika kinoma sasa solution ni kumloga jamaa apotee zake huko manake yeye aliombwa msaada ...msaada wenyewe adimu kama huo halafu anataka kuharibu kila kitu ni kummaliza tu

Hata bila kuwachukua kwani ni aibu tayari mpaka sasa,watu na ndugu wameshatambua kuwa jamaa yule ndio anakula pale na ndio mwenye wale watoto. Bado watoto tu ndio hawajui kwani mkubwa ndio amemaliza darasa la saba kutokana na kisa chenyewe na wanajiuliza kama wawafahamishe watoto baba yao halisi au la.
 
hapo hakuna jinsi jamaa inabidi awe mpole tu, atafute sehemu nyingine.
unadhani mtu na akili zako timamu umeshaonjeshwa utamu halafu uache?, unafanya mapinduzi tu unakamata ngome!.
 
lakini Pia huyo mwanamme hana mamlaka ya kuwachukua watoto wale watoto wamezaliwa ndani ya ndoa

Lakini haya maisha mbona kuna watu wana maamuzi ya ajabu sana
Mtoto ni mapenzi toka kwa mola yeye aliyewapa ndoa ndio atawajaalia mtoto pia kwa wakati autakao

mami ndoa ni nn kama mume na mke walikubaliana wafanya hayo? nadhani anaweza kuchukua wanae tena kilaini kabisa, mana na mke atasema watoto sio wa mumewe na walishapanga iwe hivyo.....nahic huyu mume atajitundika, huyu mme nae ni dhaifu jamani utamwambiaje mkeo alale na frnd wako mpaka watoto wote hao wakazaliwa....huyo frnd ndio kashakuwa mume sasa....
 
The best thing jamaa anaweza kufanya ni kumuacha huyo mke, then aende sehemu nyingine ambayo watu hawamfahamu aanze maisha mapya.

Ameshatenda kosa, hakuna njia anayoweza kulifuta. Inauma ila muda huponya majeraha yote, Mungu hakuletei tatizo kubwa kukuzidi na always atakutengenezea njia ya kutoka kwenye hilo tatizo.
 
Hata bila kuwachukua kwani ni aibu tayari mpaka sasa,watu na ndugu wameshatambua kuwa jamaa yule ndio anakula pale na ndio mwenye wale watoto. Bado watoto tu ndio hawajui kwani mkubwa ndio amemaliza darasa la saba kutokana na kisa chenyewe na wanajiuliza kama wawafahamishe watoto baba yao halisi au la.


uwiii jamani.........
 
The best thing jamaa anaweza kufanya ni kumuacha huyo mke, then aende sehemu nyingine ambayo watu hawamfahamu aanze maisha mapya.

.
Ndio matokeo ya kutenda bila kufikiri kwanza.Wenzetu nchi zilizoendelea kila kitu kinaenda kwa mikataba.Huenda angekua na ueledi basi angeweza kutabiri huko mbeleni itatokea nini.Kumruhusu rafikio akujue undani wako wote kwa kumzalisha mkeo ni kosa kubwa ambalo madhara yake ni makubwa kizazi hadi kizazi.Hata hawa ambao wameamua kugandana na kumpiga kibuti mwenye mke halali hawataishi kwa amani na raha kamwe.Watoto wakikua watakuja kujua ukweli wa kilichotekea hadi wakazaliwa.. itawasumbua sana.
DHAMBI ITAWATAFUNA WOTE KOKOTE WAENDAKO.
 
I agree with you 110% mkuu. Kitu ambacho watu hawaelewi ni kwamba ndoa 1st and for most is husban and wife. Once you are husband and wife then there you already have a family. Children don't build the family but rather add to the family which was initially husband and wife. I think the problem is people not seeing a husband and wife as already a family unit and thinking that only with the presence of children can a family truly be a family. Nadhani kwa wengi tatizo ni definition yao ya what makes a family.



U ril ar MwanaFA, umeongea kitu ambacho wengi hawajui,
Wengi hudhani familia hujengwa in presence of watoto bila kutambua kuwa watoto huongeza familia. Big up mwana))
 
Kweli definition ya family iko na utata - hakuna a general one to cater for all.Kuna watakaosema kuwa familia ni ile nucleus family - baba, mama na huongezea humo na watoto.Kuna watakaosema kama wewe kuwa familia ni baba na mama.Kuna bado watakaosema ni hao pamoja na extended family members - wakwe, shemeji/mawifi, wasaidizi etc.Waafrika wengi hawaoni kama mke na mume ni familia tosha na hivyo hudhani lazima watoto wawepo ndipo ikamilike.



I think in this, we are not talking bout the family but we are talkin bout waanzilishi wa familia ambao ni baba na mama, Quishnei.
 
Mhh mbona utata jamni binafsi siwezi kukubali kabisa kutembea na rafiki wa mume wangu!! Ndoa ni sheria kuzaa na majaliwa jamni!!
..Halafu fikiria jamaa anakula mzigo na wife wako we uko seating room unajifanya kuangalia runinga unasikia jinsi mamsapu anavyolalamikia mambo huko ndani...walahi naweza kuvunja mlango!!!
 
mami ndoa ni nn kama mume na mke walikubaliana wafanya hayo? nadhani anaweza kuchukua wanae tena kilaini kabisa, mana na mke atasema watoto sio wa mumewe na walishapanga iwe hivyo.....nahic huyu mume atajitundika, huyu mme nae ni dhaifu jamani utamwambiaje mkeo alale na frnd wako mpaka watoto wote hao wakazaliwa....huyo frnd ndio kashakuwa mume sasa....

hapo ndo kuna utata kweli tembea uone ..yaani hapa duniani kuna matukio ya hivi?
 
Jamani hii mbona kali sana,hivi huyu mwanaume alikuwa anawaza nini mpaka akafikia hayo maamuzi? Na huyu mke naye napata wasiwasi mwingi sana kwake,hivi inakuwaje mume wako anakwambia utembee na rafiki wa mume wako nawe unakubali? Hapa kuna kitu kimejificha haiingii akilini niambiwe nitembee na rafiki wa mume wangu nami nikubali,hata kama issue ni watoto,jamani si wangeenda hata kwenye vituo vya kulelea watoto wakaomba watoto kuna mtu angewanyima? Au ina maana hata watoto wa ndugu hawakuwepo? Mbona kuna watu hawana watoto na wanaishi na watoto wa ndugu zao na maisha yanaendelea bila shida?

Ila jamani na hawa wazazi wetu pia nadhani wanahitaji kupatiwa ushauri nasaha maana wao wasingewasonga sana wasingefikia kwenye hayo maamuzi,hata wazazi pia lawama lazima ziwaangukie na aibu hii si ya mke na huyo mume wake,hata wazazi pia hapo wanaaibika maana wao ndo wamesababisha tatizo liwe kubwa,wangewaacha wenyewe waendelee na maisha yao kuliko kukaa na kuwaingilia,kwanza ndoa ni makubaliano ya watu wawili sasa wao waliingilia ndoa ya watoto wao ili iweje?
 
I agree with you 110% mkuu. Kitu ambacho watu hawaelewi ni kwamba ndoa 1st and for most is husban and wife. Once you are husband and wife then there you already have a family. Children don't build the family but rather add to the family which was initially husband and wife. I think the problem is people not seeing a husband and wife as already a family unit and thinking that only with the presence of children can a family truly be a family. Nadhani kwa wengi tatizo ni definition yao ya what makes a family.

Thanks for seeing this. hata mimi nashangaa kwa nni waafrica bado tunadhani bila watoto ndoa haiendi? mtu yuko radhi azae tuu hata kama watakuwa machokoraa, vibaka, machangudoa bora tu kazaa.
Acheni hizo ndoa ni mke na mume, watoto majaaliwa, badilikeni.
 
Duuu,huyu jamaa maefanya kosa la maisha.alitakiwa akae na mke wake washauriane kwenda kucheki kwa doctors if kuna any possibilities za kuzaa,na kama hiyo ingeshindikana wangekubaliana either waishi bila watoto au kama mmoja hakuridhika basi ndoa ivunjike,kuliko kujidhalilisha kama alivyofanya yeye!!
 
Duh! Hiyo ni kali sana. Sasa ina maana jamaa alikuwa ha-function kabisa au tatizo ni kukosa kizazi? Nafahamu wanandoa kadhaa wasio na watoto kwa miaka mingi lakini wanaendelea kuheshimiana vizuri huku wakihangaika huku na kule kutafuta tiba ya matatizo yao. Wengine huja kufanikiwa hata baada ya miaka kumi au zaidi. Huyu jamaa ni ****!
 
inategemea dini zao zinasemaje kuhusu hili.....vinginevyo inakuwa haiwezekani kabisa kitu kama hicho kwani inakuwa ni zaidi ya aibu...sijui tusemeje.
 
Story hii kwa kiasi fulani inafanana na moja niliyoisoma (nadhani kutokea Ujerumani). Tofauti ni kwamba jamaa (mwenye familia na watoto) baada ya kujaribu muda mrefu bila mafanikio kumpa mimba mke wa rafiki yake, ikabidi waende kupimwa hospitalini akakutwa yeye ndio matatizo. Hapo sasa mke nyumbani kueleza watoto kawatoa wapi!!!!
 
Back
Top Bottom