Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 68,012
- 95,352
Raha mojawapo ninayofurahia kila siku ni pale mke wangu anapotandika kitanda chetu kwa mkao aupendao. Saa nyingine mtandiko wa kitanda huwa na ujumbe fulani kwangu. Hujui kwamba mtandiko unaweza kukueleza kwamba leo hakuna gwaride ama leo gwaride ni muhimu tena haraka? Hayo ni mawasiliano ya ndani ya wawili hao.
Sasa kama wewe unachukia sijui kama unatafakari. Kama ni mwanaume jifunze hilo, na kamani mwanamke kula nzoke hiyo. Kutandika kitanda could be ni kuvunja kikombe, hasa kama mzee kavimba kutoka alikotoka, akikuta mandhari fulani nyumbani anaelewa kama wewe unamjali au la. Hata jikoni kuna wakati mambo yanabadilika kukuletea ujumbe kwamba jiandae babu! Kwa baya au zuri. Utaendelea kulalamika kama hujui kusoma maandishi ukutani na kitandani. Kalagha baho.
Leka
Binamu nimekugongea senks kule, kaangalie. That means kazi ya kutandika kitanda ni ya mwanamke! FULL STOP!