Siungi mkono mgomo wa madaktari...

ZeMarcopolo: tuko pamoja.
Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na.6/2004 inamuondoa Daktari katika kundi la kugoma. Na zaidi hiyo sheria imeeleza Mfanyakazi yeyote atakaye goma kufanya kazi katika kipindi cha mgomo Mwajiri hatalazimika kumlipa mfanyakazi mshahala. mambo yote ya kazi yana taratibu zake specifically, hivyo ningewashauri ma-Daktari wawatafute wataalamu wa sheria za kazi wawape mwongozo, vinginevyo wataendelea kulalamika tu bila msaada wowote.
 
wakati umefika sasa kwa madaktari kuhamishia mgomo wao maeneo ya wazi kama viwanja vya jangwani na mnazi mmoja ili na sisi wananchi tuwaunge mkono. Ndugu zetu wengi wamekufa kwa huduma mbovu zinazo sababishwa na ama ukosefu wa vifaa au mazingira mabaya mahospitalini. Sasa tumeshamjua mbaya wetu ni nani, wananchi wote tukutane jangwani leo saa saba na wale wa mikoani tukutane katika viwanja vya sabasaba au maeneo ya wazi tuwaunge mkono madaktari ili tupunguze safari za india zisizo za lazima. WANAJESHI, POLISI , FFU NA WAALIMU tunaomba ushirikiano wenu kwani hata ninyi HAMNA NAULI ZA KWENDEA INDIA. FIKENI MAPEMA ILI TUMALIZE KAZI
 
Nimejaribu kukaa kimya lakini nafsi yangu inanisuta. Siwezi kuendelea kukaa kimya. My opinion is unpopular, lakini nitasema.

Nitagusa hoja moja baada ya nyingine kama zilivyotolewa na "jumuiya ya madaktari".

Kuongezwa mshahara: Jumuiya imetoa tarakimu zisizo sahihi kuwa mshahara wa daktari ni sh. laki 7. Hii imeandikwa katika ripoti waliyoipeleka kwa waziri mkuu. Hii inadhihirisha kuwa jumuiya hii haiko serious katika hili swala. Lakini tuangalie uhalisia - jumuiya inataka mshahara uongezwe toka hiyo laki 7 (ambayo si sahihi) mpaka miil. 3.5 with immediate effect. Hivi kweli is it reasonable kudai ongezeko la asilimia 500 la mshahara na uongezwe mara moja la sivyo unagoma? Katika historia, swala hili madaktari hawajafanya jitihada za kujadiliana na serikali kidiplomasia. Ulipotokea mgogoro wa interns wa muhimbili kuhamishwa vituo, basi madaktari wakaibuka na kutaka mshahara wa 3.5 mil na kugoma. Mambo hayafanyiki hivi! Tukiwaambia madaktari waonyeshe barua waliyokwishawahi kuiandikia serikalli kuomba mshahara huo, hakuna atakayetoa barua au ushahidi wowote kwa sababu madaktari wameanza na mgomo moja kwa moja. Siungi mkono mgomo wa namna hii.

Madaktari kupewa nyumba: Mara nyingi adui wa daktari huwa daktari mwenzake. Hili swala la nyumba lilishajadiliwa huko nyuma. Nini kilitokea? Baada ya madaktari wa muhimbili kuthibitishiwwa kuwa wao watalipwa sh laki 4 kila mwezi basi chama cha madaktari ambacho viongozi wake wengi ni madaktari wa muhimbili wakapoteza interest ya kubargain na serikali ili posho hiyo wapate madaktari wa nchi nzima. Chama hicho kilikataa kabisa mara kadhaa kuitisha vikao vya kujadili posho za nyumba huku wakitoa sababu za kuepusha migomo. Sasa hivi inakuja "jumuiya ya madaktari" na kuilazimisha serikali kutoa posho hizo with immediate effect. Siku zote madaktari walikuwa wapi? Je walikuwa wanangoja interns wafukuzwe muhimbili ndio wakumbuke kuwa wanahitaji nyumba? Standing orders za mwaka 1994 zinaeleza kinaga ubaga kuwa daktari anastahili kupewa nyumba, standing orders za mwaka 2009 hazimtaji daktari katika watumishi wanaostahili kupewa nyumba. Maafisa utumishi wote wanatafsiri kuwa standing orders za mwaka 2009 zimemtoa daktari kwenye kundi la watakaopewa nyumba. Ni lini madaktari walienda kujadili hili na wizara ya utumishi? je ni sahihi kuanza na mgomo? Ili madaktari warudishiwe stahili hiyo ni LAZIMA kifungu kwenye standing orders za mwaka 2009 kifanyiwe marekebisho. Je, hilo linaweza kufanyika with immediate effect? Madaktari wamekuwa wavivu kufuatilia mambo yanayowahusu na siwezi kuunga mkono mgomo wa kundi la wavivu wa kubargain na kulobby.

Call allowance: "Jumuiya ya madaktari" inataka call allowance ilipwe kwa half per diem. This is very simple! Kwa nini mnagoma kwenda kazini during working hours? Ni kweli kuwa daktari anastahili kulipwa angalau sh. elfu 40 kwa call lakini solution yake ni rahisi kuliko zote. Madaktari waingie kazini, muda wa kazi ukiisha madaktari warudi nyumbani kama watumishi wengine. Wasikae call mpaka watakapokubaliwa kulipwa kiasi hicho. Kugoma kwenda kazini asubuhi kwa sababu ya malipo madogo ya zamu ya usiku doesn't make sense. lakini again, jitihada gani zimefanyika awali kuhakikisha call inaongezwa? Can doctors provide evidence of their effeorts? HAKUNA.

Mazingira duni ya kazi: Swala la mazingira duni ya kazi ikiwemo wagonjwa kulala chini sio la kulalamikiwa na madaktari. Hili swala waachieni wananchi wenyewe. Daktari unachotakiwa kujua ni capacity ya hospitali yako, beyond that usipokee mgonjwa. Ukishampokea basi unalea ubovu. MV Bukoba, MV spice zilizama kwa sababu ya kubebeshwa mzigo mkubwa kuliko uwezo wake. MV Muhimbili nayo inaingia kwenye hili kundi. Nani alaumiwe? Nahodha lazima awe miongoni mwa watu wa kulaumiwa. Kama madaktarri wataendelea kupekea wagonjwa wengi kuliko idadi ya vitanda it is obvious kuwa wengine watalala chini. hata Ulaya wangekubali kupokea wagonjwa wengi kulikoi uwezo kungekuwa na wagonjwa wanaolala chini. Ila Ulaya swala hilo halipo. Nafasi zikijaa zimejaa, mgonjwa apelekwe wapi, sio swala la daktari. Hata hiyo hospitali unayofanya kazi hujaijenga wewe daktari, ilijengwa kwa sababu mahitaji yalikuwepo. Ukiendelea kupokea wagonjwa wengi kuliko uwezo unaonyesha kuwa mahitaji sio urgent. Wagonjwa wakikosa pa kulazwa ndipo wananchi watashinikiza viongozi wao wawahakikshie facilities za kutosha.

Interns kuhamishiwa hospitali nyingine: Sababu iliyotolewa kuwa hospitali nyingine hazina vifaa inakosa uzito kwa sababu kuna madaktari ambao wapo huko kwenye hizo hospitali nyingine wanafanya intern. Hata hivyo hili swala ni so benign, haliwezi kusababisha mgomo nchi nzima.

Huduma huuzwa na kununuliwa. Bei ya huduma uamuliwa na nguvu za mahitaji na upatikanaji wa huduma. Hakuna daktari aliyelazimishwa kufanya kazi serikali. Kwanini madaktari wanakimbilia kufanya kazi serikalini? Madaktari wawe wakweli na watuambie faida zilizopo serikalini. kwanini madaktari wasitoe notice ya kuacha kazi serikali na kwenda kufanya kazi sehemu bora zaidi. Tanzania kuna soko huria. Kama watu walitumia mamilioni kwenda Loliondo basi hata daktari wanayeamini huduma zake watamfuata popote alipo. Madaktari mnangoja nini kutambua hili?

Mwisho: Mgomo ni risasi ya mwisho. Si sahihi kwa wasomi kutatua changamoto wanazokutana nazo kwa kuanzia na mgomo. Tanzania ni nchi masikini, ili umasikini huo uondoke ni LAZIMA tushirikiane WOTE kuutoa. Ewe daktari, jiulize ni mara ngapi umeingia kazini kwa muda unaostahili na ukafanya kazi mpaka muda wa kazi kuisha? Je, tabia yako ya kila siku kazini inachangia kuondoa umasikini wa nchi yetu? Kila mtu aweke jibu lake moyoni na kujiuliza tena, je mgomo unaoendelea hivi sasa unapaswa kuungwa mkono? Je, kwa siku hizi mlizogoma mshahara mnauchukua wote bila aibu?

Also: Am just curious, nani analipia gharama za kukodi ukumbi wa mikutano wa Starlight Hotel ambao madaktari wamekuwa wakikutania kwa siku kadhaa?!

Mungu Ibariki Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hembu wewe ze marcopolo acha ujinga wako na kujifanya sasa ndiyo unaweza kufanya analysis ya vipato. siku zote ulikuwa wapi kufanya jivyo? Tena wewe inaoneka ndiyo mmoja wa watu wanaonufaika na haya maposho makubwa aliyoyasema Naibu Spika. Acheni ufedhuri na uchoyo wa kiasi hicho, tafuteni balance. Ktk post yangu moja nilisema, hata hao polisi, walimu, mahakimu, magereza na ninyi mliopo serikalini, kama hamtosheki si mgome tu?? Hapa tatizo kubwa ni utawala mbovu, watu wanaendelea kula rushwa za ajabu, matumizi na maposho ya ajabu, hakuna hatua zinazochukuliwa, sasa mnapoona madaktari wanagoma mnajifanya eti usawa upo wapi. Kila kazi ni muhimu, hata yule anayesafisha choo cha ikulu ni muhimu, wakiamua kugoma wale sijui kama humo ikulu mtaingia, acha ujinga wako wa kutetea tumbo lako. Madaktari endeleeni kugoma, Walimu nanyi mkitaka gomeni, askari polisi mkitaka gomeni, magereza pia gomeni, kama mmeridhika basi endeleeni na kazi.
 
Swala la kumuandikia mgonjwa dawa akakosa pesa ya kununua liko dunia nzima, sio kwenye kituo chako cha kazi tu. Na kama umeelewa mafunzo yako shuleni hupaswi kuwa na sympathy, unapaswa kuwa na empathy. Ukigoma humsaidii huyo mgonjwa aliyekosa dawa, kwa sababu the fact is hakuna serikali duniani yenye uwezo wa kuwanunulia dawa wananchi wake wote. Hata hivyo, swala hilo ni la wananchi na viongozi wao.

in red, sijakuelewa hapo unamaanisha madaktari sio wananchi wa hii nchi?
 
Mengi ya madai ya madaktari ni illusion hayawezi kutekelezeka kwa uchumi uliopo...

So kwa madai hayo na kutaka yafanyiwe kazi immediately...inabidi watafute kazi sehemu nyingine..this is free market

Kama unaona muajir wako hawezi kukutimizia maslahi yako kama upendavyo unaweza kwenda kufanya kazi kwa wahindi...au private sector au waanzishe hospitali zao walipane wenyewe kama watakavyoona inafaa..

Mapato ya madaktari ni sawa na ya mwalimu, ni sawa na ya Askari, ni sawa na ya Mkulima????

Natoa hoja.
Ila kwa uchumi uliopo, posho za vikao za wabunge ambazo si halali zinaweza kuongezwa toka 70,000 hadi 200,000/=, safari za nje za rais na viongozi ambazo hazina tija zinazidi kuendelea, magari ya kifahari kwa viongozi yanazidi kununuliwa.
 
Jumuiya imetoa tarakimu zisizo sahihi kuwa mshahara wa daktari ni sh. laki 7. Hii imeandikwa katika ripoti waliyoipeleka kwa waziri mkuu. Hii inadhihirisha kuwa jumuiya hii haiko serious katika hili swala. Lakini tuangalie uhalisia - jumuiya inataka mshahara uongezwe toka hiyo laki 7 (ambayo si sahihi) mpaka miil. 3.5 with immediate effect. Hivi kweli is it reasonable kudai ongezeko la asilimia 500 la mshahara na uongezwe mara moja la sivyo unagoma? Katika historia, swala hili madaktari hawajafanya jitihada za kujadiliana na serikali kidiplomasia
.mkuu inaelekea unaujua mshahara wa daktari anayeanza kazi ni shi ngapi na pia unatambua kikomo cha mshahara wa daktari bingwa ni sh ngapi.kama unatambua hilo basi labda utanijibu kiwango walichoomba ni ongezeko la asilimia ngapi??
Siku zote madaktari walikuwa wapi? Je walikuwa wanangoja interns wafukuzwe muhimbili ndio wakumbuke kuwa wanahitaji nyumba?
siku zote madaktari walivumilia lakini uvumilivu una mwisho.
Madaktari wamekuwa wavivu kufuatilia mambo yanayowahusu na siwezi kuunga mkono mgomo wa kundi la wavivu wa kubargain na kulobby.
ni kweli madaktari sio wazuri katika kulobby,kama mnalijua hilo ni vyema mkaweka sawa mambo yao kabla ya kuwaacha walobby na kubargain haphazardly!!.
Wasikae call mpaka watakapokubaliwa kulipwa kiasi hicho
.
labda huelewi maana ya kuwa call!!kiufupi wakati wa call unalala macho wazi kusubiria kutoa huduma kwa mgonjwa wa dharura kama vile mama mwenye mimba na wale walioko wodini wenye hatari ya kufa.
.kwa hiyo ni bora kutokwenda kazini mchana lakini ukahudhuria call.
Kama madaktarri wataendelea kupekea wagonjwa wengi kuliko idadi ya vitanda it is obvious kuwa wengine watalala chini
.
usifananishe hospitalini na ubungo bus terminal ambapo askari anaweza kukaa getini na kuzuia watu kuingia.wanaofika hospitali na kuhitaji admission ni wagonjwa serious kama vile mama mwenye uchungu anayehitaji upasuaji,mtu aliyepoteza fahamu,mtu aliyevunjika mguu,mlevi aliyezidisha pombe,kichaa anayehitaji sedation n.k ni kawaida sana kusikia muhimbili pamejaa kwa sababu amana hakuna POP,gauze,nyuzi za kushonea n.k
Hata hivyo hili swala ni so benign, haliwezi kusababisha mgomo nchi nzima.
nakubaliana na wewe kwamba swala la interns kufukuzwa muhimbili lilikuwa ni swala dogo sana lakini kwa kuwa mtasiwa,nyoni,nkya,mponda walidharau na kukejeli kama ilivyo kawaida ya wanasiasa basi haya ndio madhara yake.kulikuwa na umuhimu gani kuwafukuza watu wanaodai stahili zao wakati tumekiri tuliwacheleweshea.uamuzi wa kuwafukuza ulilenga kuachieve nini?? "mdharau siafu akiwa mmoja wakiwa wengi usijaribu"

Mgomo ni risasi ya mwisho. Si sahihi kwa wasomi kutatua changamoto wanazokutana nazo kwa kuanzia na mgomo. Tanzania ni nchi masikini, ili umasikini huo uondoke ni LAZIMA tushirikiane WOTE kuutoa
sina uhakika kama umekua ukilifuatilia swala hili la mgomo wa madaktari kuanzia chanzo chake na juhudi walizofanya kina Namala Mkopi(kiongozi wa MAT) kama umefuatilia utaelewa kuwa madaktari walifanya mgomo kuwa silaha yao ya mwisho na walifanya hivyo kwa adabu na heshima ya mtoto mdogo lakini majibu waliyokuwa wakipata yanasikitisha sana.



nihitimishe kwa kusema naunga mkono muendelezo wa vikao endelevu mpaka pale matakwa muhimu ya madaktari yatakaposhughulikiwa mfano kuwafuta kazi viongozi wa wizara ya afya sio jambo la kufikiria kwa sababu wameshindwa kuwahudumia wafanyakazi wa sekta hiyo kwa umakini lakini pia wameshindwa kuzuia mgomo wa madaktari nchi nzima wakati muda na uwezo wa kufanya hivyo walikuwa nao.




Mungu Ibariki Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Very poor argument!

Serikali imetangaza nafasi za kazi madaktari wakaomba wakijua mshahara wa mwajiri wao ni shillingi ngapi?

Kama wanaona hautoshi just QUIT this is free market..waende wakaajiriwe na wahindi au wajenge hospitali zao halafu walipane kama wataweza ..


Waache madai illusions tu..

mbona unakuwa mbogo mkuu.....
umepewa jibu stahiki la swali lako ulilouliza "kwani lazima madaktari wafanya kazi serikalini?????"
ulitaka upewe jibu gani hapo?????
au unamaanisha hata kada zingine mfano wahasibu,waalimu, au wahindisi wanaweza kutoa huduma watoazo madaktari
 
ndiyo, sumgura huyu ni mdogo ma dr. mlitambue hilo uchumi wetu unaweza tu kuakomodeti mahitaji ya wana siasa tu na kwakuwa maisha yamepanda sana hasa huko dodoma, tuna mpango wa kupandisha posho za wabunge hadi laki 4/seat kutokana na sababu tajwa hapo juu. Nyie madaktari,manesi, waalimu, askari wa majeshi yoote ni marufuku kugoma kwani kazi zenu ni za WITO, jamani narudia tena wito,wito wito, vinginevyo mhamie kwenye kazi za siasa!

Dactari kushinda na wagonjwa wa TB ilhali ya kwamba anajua TB ni airborne disease .. dactari huyuhuyu akitoka kazini Ana mtoto wake wa mwaka mmoja nyumbani akifika inabidi amkumbatie just to show some love ..

Hapo unaona dactari amejitoa muhanga yeye na family yake kwa ajili yako . Bado unadai wito hakuna .. labda tuanze hapa NINI MAANA YA WITO ...?
 
@Pasco, naomba mungu wewe usiwe mshauri mkuu wa serikali maana huu mchango ulioandika unatisha! Ndugu ulikuwa umepata serengeti mbili au vipi? Unless unatania lakini kama uko serious na ulichoandika basi ipo hatari kuwa your knowledge about certain issues is overly inflated. Tuanze:

1. "Serikali itoe tamko la kuyakubali madai yao yote na kwamba itayafanyia kazi na kuwalazimisha lazima waripoti kazini by Jumatatu asubuhi, kinyume cha hapo wawe fired without mercy!. Jumanne zitangazwe nafasi za udaktari masharti yawekwe yale yale wanaotaka waje, wasiotaka na wawe huru kujiendea kokote watajakotaka".

Kwenye blue Pasco, kwa nini unafikiri serikali haijafanya kama unavyopendekeza? Na Jummane wakitangaza nafasi za kazi unahakika watapata madaktari? I mean qualified doctors? Inachukuwa muda gani kum-train mtu akawa doctor? Tanzania tuna akiba ya madaktari kiasi kwamba hata ukiwafukuza unaweza kuchota kwenye hiyo akiba?

2. Madaktari ni watu lakini walimu nao watu, wafanyakazi wa serikalini nao watu, polisi nao watu etc, no preferential treatment kwa madaktari huku ni kutengeza classes!. Maadam tayari tunayo supper class ya wabunge, lets make no more classes!.

Hii comment ndiyo imeniacha hoi! Pasco what are you trying to say? Sikiliza ndugu, mtu yeyote anaweza kuwa mbunge lakini sio kila mbunge anaweza kuwa daktari do you know why?

3. madaktari wasijione they are indispensable!.
Madaktari hawajioni kuwa they are indespenble, they are infact indespensable. So get that right Pasco. Sina nia ya kudharau taaluma yoyote ila niseme kuna taaluma ambazo zinaweza kufanywa na watu tofauti. Kwa mfano kazi kama ualimu inaweza kufanywa na watu mbalimbali hata wale ambao hawakusomea ualimu per se as long as wana elimu ya kuridhisha. Ndio maana hata huku mtaani kuna watu wanafundisha tuition vizuri kwenye masomo mbalimbali. Lakini ni vigumu sana kumchukua mtu ambaye hajasomea udaktari, hata kama ana PhD I.e ya Economics na kumwambia aingie wodini kutibu wagonjwa!

Na hapa ndio nataka ku-question your level of understanding wewe Pasco. Labda nikuulize Pasco mwanao akiwa mgonjwa unaweza kumpleka kwa mkuu wa Wilaya ambaye hakusomea udaktari ili amtibu? au unaweza kumuita police yoyote aje kumchoma mwanao sindano hata kama huyo polisi hajawahi kuona darasa la udaktari?
 
Ni jambo la kawaida kabisa kukuta mtu ambaye hajawahi kugusa shule analaani wanafunzi wa vyuo vikuuu kwa kugoma. Wakati wakigoma masaa 2, maji ambayo yalikatika kwa week nzima yanaanza kuflow kwenye mabomba.....Very pathetic in deed!

Uko sahihi Mkuu... ushabiki mwingine ni uzumbukuku! Hawa wanaoona madaktari hawana point, ni ama wanufaika wa mfumo au hawajui tiba maana yake ni nini.Tiba ya hospitali siyo kama kwa mganga wa kienyeji ambapo mganga anapokea kuku na mbuzi karibu kila siku!

Hivi kwa nini madaktari na watumishi wengine kama walimu ndio wafuate utaratibu mrefu kurekebishiwa maslahi yao wakati wanasiasa wanarekebishiwa ndani ya masaa?
Hili nalo neno! Ze Marco atakuwa na jibu zuri kwa hili.


Bado nasikitika sana!!
Tuko pamoja Mkuu wangu DC.

Mengi ya madai ya
madaktari ni illusion hayawezi kutekelezeka kwa uchumi uliopo...
Illusion kwako wewe, ila Watanzania wameamka wanajua kwenye kapu kunaingia nini, nini kinatoka kwenda wapi na kwa vipi.

Kama unaona muajir wako hawezi kukutimizia maslahi yako kama upendavyo unaweza kwenda kufanya kazi kwa wahindi...au private sector au waanzishe hospitali zao walipane wenyewe kama watakavyoona inafaa..

Hii nchi ni yetu sote.Huyo mwajiri angekuwa sekta binafsi labda angekuwa na jeuri hiyo.Kwanini wengine wakikohoa kidogo tu posho zinapanda tena with retrospective effect? Wao ni Watanzania zaidi ya wengine? Sasa huu mgomo utawafundisha kwamba hakuna mtanzania zaidi ya wengine.

Natoa hoja.
Naam!

Sasa baada ya kupata mass support vichwa vimewavimba mpaka sasa wanataka ku ublow huu mgomo out of proportion.
Kumbe ulidhani Mass support maana yake nini? Ina maana ulitoa support bila kujua the snowball effect??Pole jamani kama ulikuwa bendera fuata upepo.Mgomo huu ni shinikizo.Shinikizo litaleta mabadiliko.No one will grant you your right unless u fight for it.Thats what the Drs are doing.Njia za ustaarabu zikishindikana basi zinatumika njia zisizo za kistaarabu kivile.Hili pia ni fundisho kwetu wananchi tusiwe bendera fuata upepo, tusaidie pale watu wanapodai haki zao .Nchi yetu siyo maskini hata kidogo.Ni kujipanga na vipaumbele sahihi tu.Kipi kinatangulia, uhai wa watu au ufahari wa wale waliochaguliwa na wananchi? Tupunguze fahari na anasa!

Nilipendekeza kwenye thread yangu ya jana kuwa serikali itoe tamko la kuyakubali madai yao yote na kwamba itayafanyia kazi na kuwalazimisha lazima waripoti kazini by Jumatatu asubuhi, kinyume cha hapo wawe fired without mercy!. Jumanne zitangazwe nafasi za udaktari masharti yawekwe yale yale wanaotaka waje, wasiotaka na wawe huru kujiendea kokote watajakotaka!.

This is a joke!! Kuyafanyia kazi hakuna chochote kitakachofanywa..hiyo ni lugha ya wanasiasa ikimaanisha - SHUT UP NOW!

Madaktari ni watu lakini walimu nao watu, wafanyakazi wa serikalini nao watu, polisi nao watu etc, no preferential treatment kwa madaktari huku ni kutengeza classes!. Maadam tayari tunayo supper class ya wabunge, lets make no more classes!.

hehehhehe sasa hapo unachemsha kabisaaa! Super class??? is it? Thats where you go wrong in your observations and allussions. Hiki ndicho kinachochochea hii migomo.The Government is making serious mistakes in classifying cadres...... wabunge siyo super class.Hawa tumewaajiri na hawapaswi kujiweka juu ya kila mtu.


Pia nikapandisha thread nyingine kuwa madaktari wasijione they are indispensable!. No body is indispensable hata without them, life goes on the rules of the jungle, wakufa waachwe wajifie wazima waendelee kuishi!.
Kuna cadres ambazo kweli siyo indespensable.Lakini siyo madaktari. Unasema hivyo kwa sababu una pa kuegemea.Ungekuwa mlalahoi muamka hai..hii jeuri usingekuwa nayo hata kidogo.
 

mkuu mi napinga hapo unaposema hospitali ikijaa wagonjwa wasichukuliwe..... imagine mama & mtoto wametoka tuseme kigoma wamekuwa refered muhimbili au temeke wafike pale uwaambie vyumba vimejaa rudini mlipotoka .... yanaingia akili hayo maneno yako...?

1. Huwaambii rudini mlipotoka, hilo siyo kazi yako. Unachofanya ni kuwaambia kuwa vitanda vimejaa. wataenda wapi? thats none of your business. Kimsingi madaktari wanaonyesha udhaifu wa weledi pale ambapo mgoonjwa anapewa referral toka Kigoma to Muhimbili na madaktari hawajadevelop utaratibu wowote wa kuicontact Muhimbili kama ina nafasi ya kumpokea huyo mgonjwa! Jukumu la kubuni utaratibu ambao ni functional ni la wataalam ambao ni madaktari. Usipokee waginjwa wengi kuliko uwezo wako kwa sababu in the end hutampa hata mmoja kati yao huduma anayostahili.

2. Unaposema haiingii akilini kukataa kupokea mgonjwa toka kigoma kwa sababu ya kutokuwepo kwa vitanda inabidi ujiulize je, inaingia akilini kukataa kuwahudumia watu waliotoka nchi zima kwa mgomo? Kwa kifupi hapa umeshasema huungi mkono mgomo.
 
Watu wanatumia zaidi feelings katika hili. Mimi nadhani tutumie facts zaidi. Nakuja na facts soon, stay tuned...
 
Daktari anayeanza kazi just baada ya kusajiriwa na Medical Coucil of Tanganyika anaitwa daktari daraja la II ambaye mshahara wake ni TGHS E ambao ni TSh. 886,800 hadi TSh. 973,110. Kwa hiyo hapa tukubaliane kuwa madaktari kumuandikia waziri mkuu kuwa mshahara wa daktari ni sh laki 7 linadhihirisha kutokuwa serious. Huwezi kumdanganya waziri mkuu kuhusu mshahara wa mtumishi wa umma.

Sasa basi, pamoja na "misquote" hiyo ya madaktari, waje hapa watuambie ni lini walishawahi kuomba serikali iupandishe mshahara huo na kufika 3.5mil? Madaktari hawajawahi kufanya hivyo mpaka wakati wameamua kugoma. Si sahihi kutumia umuhimu wa huduma unayotoa kama bomu la nyuklia. Kila mtu anajua kuwa madaktari ni muhimu na wanastahili kuongezewa mshahara, lakini madaktari nao wako responsible kufuata hatua za kidiplomasia katika kuhakikisha wanapandishiwa mshahara.
 
Pamoja na uhaba wa ajira unaoikabili nchi yetu. Hakuna daktari aliyewahi kuomba kazi serikalini akanyimwa. Watanzania wengine ambao nao wana haki ya kupata ajira kama madaktari wamekuwa wakihaha mitaani kutafuta kazi na vibahasha vya khaki. Wengine wamekaa mtaani zaidi ya miaka miwili kabla ya kupata kazi ingawa wana degree. Badala ya serikali kuongeza nguvu kwenye kuongeza maposho ya wabunge na makundi mengine ya watumishi wa umma, ili kuwa fair ni LAZIMA serikali itoe kipaumbele kwenye kutengeneza ajira mpya ili kila aliyefanya jitihada za kupata ujuzi aweze kupata ajira au kuwezeshwa kujiajiri. Sasa hivi nchi imekutwa na KANSA ya watu wachache waliopata fursa kutaka kufyonza rojorojo yote na wale ambao hata kidogo hawajapata kusahaulika. Kila anayeitaia mema Tanzania hivi sasa anatakiwa atoe kipaumbele kwenye kuhakikisha vijana wetu waliosoma uhasibu, sheria, uhandisi, maendeleo ya jamii na fani nyingine wanapatiwa ajira. Hili ndio jambo ambalo linatakiwa kufanywa MARA MOJA sio kusema wale walioshapata kafursa fulani waongeze fursa hiyo kwa asilimia 500. Watanzania tunaumizana wenyewe kwa wenyewe...
 
Je, kuna daktari yeyote ambaye anayeishi below tanzanian average? Yuko wapi? Wewe binafsi fikiria madaktari unaowafahamu, nani kati yao ana maisha duni?
 
Watu wanatumia zaidi feelings katika hili. Mimi nadhani tutumie facts zaidi. Nakuja na facts soon, stay tuned...
 
madaktri wamegoma kwenda kukutana na PM. Pm anakaribia kutoa tamko la serikali.
 
Daktari mmoja katika ukurasa wa faebook leo ameandika hivi:

GOOD NEWS: Pamoja na mgomo,wauguzi wa Mbeya Referral Hospital wameniwekea tools up na kumsaidia mchumba wangu,kajifungua mtoto wa kiume,kilo 3.1, na APGAR Score 9-10. Mungu awabariki wote walioshiriki katika huduma hii na maombi haya.

Do we learn anything from this?
 
Back
Top Bottom