Siungi mkono kubadili analogue kwenda digital. Toa maoni yako

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,319
Kumekuwa na mchakato huu wa TCRA kutaka kusitisha matumizi ya mfumo wa 'kawaida' tunaotumia sasa kwenda mfumo wa digital.
Japo kuna faida kitaalamu lakini ni wazi kuwa wananchi na wasambaza ving'amuzi wenyewe hawajawa tayari. Wakati madish yanauzwa nchi nzima, ving'amuzi bado haviuzwi nchi nzima. Wakati wapo mafundi wa kufunga na kurekebisha madish nchi nzima, mafundi wa ving'amuzi wanapatikana katika baadhi ya miji tu, tena ni wachache

Hadi sasa na kwa muda mrefu baadae mwaka huu, wapo watanzania kwa maelfu wanaonunua TV sets na kwa kuwa hawana access na ving'amuzi, wananunua madish. Kama TCRA hawaamini waende kwenye maduka ya madish leo, waone mass ya watu wananunua madish

Nadhani inahitajika walau miaka miwili tena, angalau hata kampuni za ving'amuzi zijiimarishe.

Je mwanaJF una maoni gani?
 
madish yataendelea kufanya kazi. Na ving'amuzi ni kama antena tu haitaji utalaam sana kuunganisha. Na mwisho hata usipounga mkono, ndo ishakua.
 
Hii transfer toka analogia kwenda digitali, sio choice au option, ni lazima!. Kama simu zilivyohama toka toka analojia kwenda digitali, did we had a choice?.

Tuko kwenye dunia ya Utandawazi, hivi ni chice sisi Watanzania tuingie kwenye utandawazi?.

No it was not our choice, huu ni uamuzi wa wenyewe, sisi tunaishia kupangiwa tuu na ITU.
 
madish yataendelea kufanya kazi. Na ving'amuzi ni kama antena tu haitaji utalaam sana kuunganisha. Na mwisho hata usipounga mkono, ndo ishakua.

Hii transfer toka analogia kwenda digitali, sio choice au option, ni lazima!. Kama simu zilivyohama toka toka analojia kwenda digitali, did we had a choice?.

Tuko kwenye dunia ya Utandawazi, hivi ni chice sisi Watanzania tuingie kwenye utandawazi?.

No it was not our choice, huu ni uamuzi wa wenyewe, sisi tunaishia kupangiwa tuu na ITU.

Ok,Ok,Ok,,,
Nakubali kuwa lazima tutabadilika. Nisichounga mkono ni kufungwa kwa analogue December 2012. Tunahitaji mda zaidi. At Zagalo, kwa sasa ndio tunatumia both madish na ving'amuzi, but by 2013 madish yatakuwa obsolete...
 
Ok,Ok,Ok,,,
Nakubali kuwa lazima tutabadilika. Nisichounga mkono ni kufungwa kwa analogue December 2012. Tunahitaji mda zaidi. At Zagalo, kwa sasa ndio tunatumia both madish na ving'amuzi, but by 2013 madish yatakuwa obsolete...
Mkuu,
Unaonyesha hujaelewa vema mabadiliko haya!
Hapo kwenye red si kweli, madish hayatakuwa absolete!
Badiliko la kutoka analojia kwenda digitali haliyahusu madishi...labda kwa lugha nyapesi, madish ni sehemu ya teknolojia ya digitali.
Mfumo wa digitali uta'affect terrestrial antennas, yaani hii minara ya aridhini, lakini madishi yenyewe yanapokea signal moja kwa moja toka kwenye sattelite hivyo hayataathirika.
 
Kumekuwa na mchakato huu wa TCRA kutaka kusitisha matumizi ya mfumo wa 'kawaida' tunaotumia sasa kwenda mfumo wa digital.
Japo kuna faida kitaalamu lakini ni wazi kuwa wananchi na wasambaza ving'amuzi wenyewe hawajawa tayari. Wakati madish yanauzwa nchi nzima, ving'amuzi bado haviuzwi nchi nzima. Wakati wapo mafundi wa kufunga na kurekebisha madish nchi nzima, mafundi wa ving'amuzi wanapatikana katika baadhi ya miji tu, tena ni wachache

Hadi sasa na kwa muda mrefu baadae mwaka huu, wapo watanzania kwa maelfu wanaonunua TV sets na kwa kuwa hawana access na ving'amuzi, wananunua madish. Kama TCRA hawaamini waende kwenye maduka ya madish leo, waone mass ya watu wananunua madish

Nadhani inahitajika walau miaka miwili tena, angalau hata kampuni za ving'amuzi zijiimarishe.

Je mwanaJF una maoni gani?

mimi tatizo langu sio muda wala mabadiliko!

kichefuchefu changu ni kuwa hii digital ni ya wazungu, sio yetu.....wahandisi wetu hawana uwezo wa kuifanya digital iwe yetu..eventually electronics and telecommunication engineers wetu wanabadilika na kuwa REPAIR MAN!!

kazi ipo, tunapelekwa pelekwa tu
 
mimi tatizo langu sio muda wala mabadiliko!

kichefuchefu changu ni kuwa hii digital ni ya wazungu, sio yetu.....wahandisi wetu hawana uwezo wa kuifanya digital iwe yetu..eventually electronics and telecommunication engineers wetu wanabadilika na kuwa REPAIR MAN!!
kazi ipo, tunapelekwa pelekwa tu
mKUU,
Sasa kuna geni gani hapo?
Leo hii ndio unaanza kusikitikia na kuona hili kama tatizo?
Kwani ni teknolojia ipi yoyote ya kidunia ambayo ni yetu Watanzania...au zile mashine za kukamua mafuta ya alizeti na Juisi ya Miwa zinazotengenezwa na wahandisi wa Coet pale Mlimani, na wajasiriamali wa SIDO?
 
Mfumo huu ni mzuri ila ni unyonyaji mpya uliokurupukiwa na TCRA, ntarudi baadae nifafanue wizi huo.
 
Siku zote sisi masikini ndo waathirika wakubwa na haya mabadiliko ya teknolojia! Kununua televisheni peke yake ilikuwa kazi, kununua king'amuzi na kukilipia kila mwezi itawezekana kweli! Sidhani kama sisi maskini tutamudu gharama. Kwa wale wenye uwezo wenyewe haitakuwa tatizo sana! Inabidi turudi miaka ya tisini kununua mikanda ya filamu na kuangalia sababu tv channels za bure hazitakuwepo. Umaskini mbaya sana!
 
Siku zote sisi masikini ndo waathirika wakubwa na haya mabadiliko ya teknolojia! Kununua televisheni peke yake ilikuwa kazi, kununua king'amuzi na kukilipia kila mwezi itawezekana kweli! Sidhani kama sisi maskini tutamudu gharama. Kwa wale wenye uwezo wenyewe haitakuwa tatizo sana! Inabidi turudi miaka ya tisini kununua mikanda ya filamu na kuangalia sababu tv channels za bure hazitakuwepo. Umaskini mbaya sana!
Kumbe jambo hili la digitali halijaeleweka na wengi...timu yetu ya elimu kwa jamii inabidi iweke mikakati mizito zaidi pale Morogoro itakapokutana soon mwezi huu!
jAMANI, STATIONS AMBAZO ZINAONEKANA free to Air sasa hivi, bado zitaendelea kuonekana free hata kwa kingamuzi...
Ni mtu yule anayetaka complications za MICHEZO, SINEMA NA MIZIKI YA KILEO ndiye atalazimika kulipia vituo hivyo, yaani ni kama ilivyo sasa!
Gharama atakayoingia mtu ni ndogo tu ya kawaida ya Tshs 59,000 tu, ambapo ni sawa na kumiliki simu ya tochi, ambapo pia kila Mtanzania ana uwezo huo kwa sasa.
Kama kuna maswali ulizeni!
 
Wakuu tunaweza kukaa na kukubaliana kwamba muda uongezwe! Well but others are migrating! Kama Wenzetu wakitangulia hauoni kwamba Tanzania ina hatari ya kugeuzwa Jalala la Vifaa vya Analojia? Think of it Mkuu
 
Hii digital migration ina faida nyingi kuliko hasara, hivi vituo vyetu vya TV vyote vinageuka production houses kwa kuprovide contents tuu!. Ule ukiritimba wa kuitegemea sijui TBC au ITV kutudengulia kurusha vipindi vyetu ndio unamalizika rasmi!.

Mfano Chadema hawahitaji kuwa kituo cha TV kurusha matangazo yake, kinalipia tuu chaneli kwa hao multiplex providers na kwenda hewani!.

Hata mimi na vile vipindi vyangu vya "Wiki ya Utumishi wa Umma na PPR", "Saba Saba na PPR " na " Nane Nane na PPR" sina haja ya kuwanyenyekea tena hao wenye TV zao!, nalipia chaneli nakwenda hewani!.

Mfano kila Jumapili asubuhi karibu kila dhehebu litakuwa hewani kwenye ibada

Chan 1 Katoliki
Chan 2 Kakobe
Chan 3 Rwakatare
Chan 4 Walutheri
Chan 5 Waangalikana
Chan 6 Pentecoste
Chan 7 Menonite
Chan 8 Mzee wa Upako
Chan 9 Mwakasege
etc, etc

Wigo wa chaguo la nini cha kuangalia linakuwa kubwa zaidi

Tatizo kwangu ni moja tuu, nitalazimika kuwa na ving'amuzi vingi zaidi!, saa hizi niko na DSTV kwa ajili ya African Magic, Niko na Star Time kwa ajili ya TBC-1, Agape kwa ajili ya HBO sasa kuna Zuku hicho cha ITV na star kinakuja, hapo sijakihesabu hiki cha Easy TV cha mchina etc!.
 
Mkuu,
Unaonyesha hujaelewa vema mabadiliko haya!
Hapo kwenye red si kweli, madish hayatakuwa absolete!
Badiliko la kutoka analojia kwenda digitali haliyahusu madishi...labda kwa lugha nyapesi, madish ni sehemu ya teknolojia ya digitali.
Mfumo wa digitali uta'affect terrestrial antennas, yaani hii minara ya aridhini, lakini madishi yenyewe yanapokea signal moja kwa moja toka kwenye sattelite hivyo hayataathirika.

Duh.. Mkuu sasa hapa ndo nazidi kuchanganyikiwa, but usichoke kunielimisha. Unaposema madish yataendelea kutumika, najiuliza mambo yafuatayo
a. Kulikuwa na haja gani ya kuleta na kuongelea ving'amuzi?
b. DSTV wana dish, ving'amuzi hawana dish, kuna tofauti gani kati ya technologia inayotumika na DSTV ukilinganisha na hii inayotumika na alina Star times?
c. Kuna watu wanaongelea kurekodi vipindi, kuwa na channels nyingi katika frequency moja, ina maana haya yote yanawezekana katika technologia ya dish?

Ntashukuru ukinijibu hayo machache...
 
Kumbe jambo hili la digitali halijaeleweka na wengi...timu yetu ya elimu kwa jamii inabidi iweke mikakati mizito zaidi pale Morogoro itakapokutana soon mwezi huu!
jAMANI, STATIONS AMBAZO ZINAONEKANA free to Air sasa hivi, bado zitaendelea kuonekana free hata kwa kingamuzi...
Ni mtu yule anayetaka complications za MICHEZO, SINEMA NA MIZIKI YA KILEO ndiye atalazimika kulipia vituo hivyo, yaani ni kama ilivyo sasa!
Gharama atakayoingia mtu ni ndogo tu ya kawaida ya Tshs 59,000 tu, ambapo ni sawa na kumiliki simu ya tochi, ambapo pia kila Mtanzania ana uwezo huo kwa sasa.
Kama kuna maswali ulizeni!

Mkuu PJ ni kweli halijaeleweka kwa wananchi wa kawaida. Wasiwasi wangu ni kuwa complications zake hazijaeleweka hata kwa mamlaka husika ikiwemo TCRA. Naomba unifafanulie mambo yafuatayo
a. Hadi wakati huu ninapoandika hapa, kuna maeneo chungu nzima ya nchi yetu ambapo hivi ving'amuzi havipo. Ni kwa nini?
b. Kwa yale maeneo ambayo kwa sasa hamna dealers wa ving'amuzi, wananchi wananunua TVs za kawaida, kukata shauku yao ya mahitaji ya TV. Je, ni halali imlazimu mtu leo kununua technologia iliyopo maeneo yake, kisha miezi saba baadae unamwambia imepitwa na wakati? Je, haikuwa muafaka kwa serikali kusubiri hadi dealers wa ving'amuzi watakapoenea nchi nzima ndipo waanze kuahmasisha wateja kuhamia huko?
c. Nilimsikia mtaalamu fulani akisema matangazo ya digital yanasambazwa kupitia mkongo wa taifa. Hiyo inamaanisha nini kwa maeneo ambayo mkongo haujafika kwa sasa?

d. Mkuu hii nchi sio Dar na labda Arusha peke yake. Kuunganishiwa king'amuzi cha Ting hapa moro ni Tsh 320,000, Zuku zaidi la laki 2 na hizi ni bei za mawakala wanaotambuliwa...

Ntashukuru ukinijibu baadae...
 
@Pasco.
Hili tatizo la vingamuzi vingi litapungua taratibu! With time teknolojia itaruhusu kuwa na kingamuzi kimoja tu, ambapo kazi yako itakuwa ni kuwa na SmartCards za makampuni mengi utakavyo, na utakaa kwenye kochi ukiwa unahama toka s/card ya Startimes kwenda ya Ting etc, bila kunyenyuka, ukitumia remote ctrl. Hilo liko just on transit, tuwe patient.
 
@Tuko, niko via mobile, na maswali yako ni marefu, nitayajibu nikiwa kwny laptop,
 
Back
Top Bottom