SINA JINA1
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 391
- 151
Fikra za mwanadamu zinapotawaliwa na hulka ya ushabiki zaidi ya ukweli ,maamuzi hutolewa pasipo kuzingatia ukweli.Pia maamuzi hayo huambatana na hoja nyepesi zisizo na manufaa katika utatuzi wa tatizo kuu.
Serikali ya Jk tokea imeingia madarakani awamu ya kwanza imegubikwa na vitendo vya rushwa na Ufisadi uliokithiri kupita kiasi.Hii ni kutokana na ukweli kwamba Jk kama Raisi hakuwa na uwezo wa kuongoza nchi. Kongozi yeyote asiye na uwezo wa uongozi ni dhahiri hata team/wasaidizi wake watakuwa ni wabovu.Jk amejaza washkaji zake kwenye nafasi mbalimbali kama wasaidizi wake.Hili limejirudia hata pale bunge lilipomuazibu kwa kumwondoa waziri mkuu EL ili achague team bora bado yamejirudia yale yale.
Kwa nini siungi mkono hoja ya Mh. Zitto?
Sababu nilizotoa hapo kwenye maelezo ni kuwa tatizo kwenye uongozi wa nchi yetu sio mawaziri ama waziri mkuu bali ni mfumo mzima wa uongozi wa Jk.Hapa kilichotakiwa ni kutibu ugonjwa kama sio chanjo/kinga kwa kumwadabisha JK .Kwanini Zitto amekimbilia hoja ya kumwondoa Pinda ili hali kulikuwa na nafasi ya kupeleka hoja ya kutokuwa na imani na Raisi?.
Hapo ndio pale wachambuzi wanapochimba zaidi na kuangalia kwa undani juu ya tuhuma za uswahiba wa Zitto na JK.Hii hoja kwa mtazamo wangu ni kupoteza mantiki ya hoja ya msingi iliyotaka kupelekwa bungeni ya kutaka kumng'oa JK.
Mungu Ibariki Tanzania dhidi ya huu uwizi wa dhahiri dhidi ya mali za walalahoi.
Serikali ya Jk tokea imeingia madarakani awamu ya kwanza imegubikwa na vitendo vya rushwa na Ufisadi uliokithiri kupita kiasi.Hii ni kutokana na ukweli kwamba Jk kama Raisi hakuwa na uwezo wa kuongoza nchi. Kongozi yeyote asiye na uwezo wa uongozi ni dhahiri hata team/wasaidizi wake watakuwa ni wabovu.Jk amejaza washkaji zake kwenye nafasi mbalimbali kama wasaidizi wake.Hili limejirudia hata pale bunge lilipomuazibu kwa kumwondoa waziri mkuu EL ili achague team bora bado yamejirudia yale yale.
Kwa nini siungi mkono hoja ya Mh. Zitto?
Sababu nilizotoa hapo kwenye maelezo ni kuwa tatizo kwenye uongozi wa nchi yetu sio mawaziri ama waziri mkuu bali ni mfumo mzima wa uongozi wa Jk.Hapa kilichotakiwa ni kutibu ugonjwa kama sio chanjo/kinga kwa kumwadabisha JK .Kwanini Zitto amekimbilia hoja ya kumwondoa Pinda ili hali kulikuwa na nafasi ya kupeleka hoja ya kutokuwa na imani na Raisi?.
Hapo ndio pale wachambuzi wanapochimba zaidi na kuangalia kwa undani juu ya tuhuma za uswahiba wa Zitto na JK.Hii hoja kwa mtazamo wangu ni kupoteza mantiki ya hoja ya msingi iliyotaka kupelekwa bungeni ya kutaka kumng'oa JK.
Mungu Ibariki Tanzania dhidi ya huu uwizi wa dhahiri dhidi ya mali za walalahoi.