Siungi Mkono hoja ya Zitto

SINA JINA1

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
391
151
Fikra za mwanadamu zinapotawaliwa na hulka ya ushabiki zaidi ya ukweli ,maamuzi hutolewa pasipo kuzingatia ukweli.Pia maamuzi hayo huambatana na hoja nyepesi zisizo na manufaa katika utatuzi wa tatizo kuu.

Serikali ya Jk tokea imeingia madarakani awamu ya kwanza imegubikwa na vitendo vya rushwa na Ufisadi uliokithiri kupita kiasi.Hii ni kutokana na ukweli kwamba Jk kama Raisi hakuwa na uwezo wa kuongoza nchi. Kongozi yeyote asiye na uwezo wa uongozi ni dhahiri hata team/wasaidizi wake watakuwa ni wabovu.Jk amejaza washkaji zake kwenye nafasi mbalimbali kama wasaidizi wake.Hili limejirudia hata pale bunge lilipomuazibu kwa kumwondoa waziri mkuu EL ili achague team bora bado yamejirudia yale yale.

Kwa nini siungi mkono hoja ya Mh. Zitto?
Sababu nilizotoa hapo kwenye maelezo ni kuwa tatizo kwenye uongozi wa nchi yetu sio mawaziri ama waziri mkuu bali ni mfumo mzima wa uongozi wa Jk.Hapa kilichotakiwa ni kutibu ugonjwa kama sio chanjo/kinga kwa kumwadabisha JK .Kwanini Zitto amekimbilia hoja ya kumwondoa Pinda ili hali kulikuwa na nafasi ya kupeleka hoja ya kutokuwa na imani na Raisi?.

Hapo ndio pale wachambuzi wanapochimba zaidi na kuangalia kwa undani juu ya tuhuma za uswahiba wa Zitto na JK.Hii hoja kwa mtazamo wangu ni kupoteza mantiki ya hoja ya msingi iliyotaka kupelekwa bungeni ya kutaka kumng'oa JK.

Mungu Ibariki Tanzania dhidi ya huu uwizi wa dhahiri dhidi ya mali za walalahoi.
 
Haya mkuu kwa hiyo kama mfumo ni mbovu tusubiri mfumo mpya uletwe na nani? Anyway katiba mpya na je tuwaache waendelee kula hadi mfumo mpya? THINK BIG MKUU!
 
Hujaeleweka Zitto ameomba Mawaziri wabadhirifu wajiuzulu wenyewe wakishindwa waziri Mkuu awawajibishe naye akishindwa awajibishwe yy ili liundwe jipya
 
Kinachotakiwa ni mawaziri wahusika kujitoa. Wakigoma ndo watatolewa kwa njia ya kumtoa PM sababu PM akitoka, cabinet inavunjwa.
 
Hujaeleweka Zitto ameomba Mawaziri wabadhirifu wajiuzulu wenyewe wakishindwa waziri Mkuu awawajibishe naye akishindwa awajibishwe yy ili liundwe jipya

Ameomba uungwaji mkono wa wabunge 70+ ili aweze wasilisha hoja yake ya kumchomoa Pinda
 
Fikra za mwanadamu zinapotawaliwa na hulka ya ushabiki zaidi ya ukweli ,maamuzi hutolewa pasipo kuzingatia ukweli.Pia maamuzi hayo huambatana na hoja nyepesi zisizo na manufaa katika utatuzi wa tatizo kuu.

Serikali ya Jk tokea imeingia madarakani awamu ya kwanza imegubikwa na vitendo vya rushwa na Ufisadi uliokithiri kupita kiasi.Hii ni kutokana na ukweli kwamba Jk kama Raisi hakuwa na uwezo wa kuongoza nchi. Kongozi yeyote asiye na uwezo wa uongozi ni dhahiri hata team/wasaidizi wake watakuwa ni wabovu.Jk amejaza washkaji zake kwenye nafasi mbalimbali kama wasaidizi wake.Hili limejirudia hata pale bunge lilipomuazibu kwa kumwondoa waziri mkuu EL ili achague team bora bado yamejirudia yale yale.

Kwa nini siungi mkono hoja ya Mh. Zitto?
Sababu nilizotoa hapo kwenye maelezo ni kuwa tatizo kwenye uongozi wa nchi yetu sio mawaziri ama waziri mkuu bali ni mfumo mzima wa uongozi wa Jk.Hapa kilichotakiwa ni kutibu ugonjwa kama sio chanjo/kinga kwa kumwadabisha JK .Kwanini Zitto amekimbilia hoja ya kumwondoa Pinda ili hali kulikuwa na nafasi ya kupeleka hoja ya kutokuwa na imani na Raisi?.

Hapo ndio pale wachambuzi wanapochimba zaidi na kuangalia kwa undani juu ya tuhuma za uswahiba wa Zitto na JK.Hii hoja kwa mtazamo wangu ni kupoteza mantiki ya hoja ya msingi iliyotaka kupelekwa bungeni ya kutaka kumng'oa JK.

Mungu Ibariki Tanzania dhidi ya huu uwizi wa dhahiri dhidi ya mali za walalahoi.
Hapo hakuna cha uswahiba huyo janki anajua analolifanya kwani katiba ya sasa inampa rais madaraka makubwa mno,wabunge wa ccm hawako tayari wanahofia madaraka yao,hv rais akivunja bunge na akajiuzulu na uchaguzi ukaitishwa upya sasa hv wabunge wangapi wa ccm watarudi mjengoni?
 
Zitto ameamua kuanza na jambo ambalo linawezekana kutekelezwa na ndo maana ameamua kudeal na waziri.ni vigumu sana kumwajibisha rais moja kwa moja kwani yeye pia anaweza kulivunja bunge kabla halijamng'oa yeye.mkuu hata unapofanya mtihani unashauriwa kuanza na maswali mepesi kwanza!
 
Fikra za mwanadamu zinapotawaliwa na hulka ya ushabiki zaidi ya ukweli ,maamuzi hutolewa pasipo kuzingatia ukweli.Pia maamuzi hayo huambatana na hoja nyepesi zisizo na manufaa katika utatuzi wa tatizo kuu.

Serikali ya Jk tokea imeingia madarakani awamu ya kwanza imegubikwa na vitendo vya rushwa na Ufisadi uliokithiri kupita kiasi.Hii ni kutokana na ukweli kwamba Jk kama Raisi hakuwa na uwezo wa kuongoza nchi. Kongozi yeyote asiye na uwezo wa uongozi ni dhahiri hata team/wasaidizi wake watakuwa ni wabovu.Jk amejaza washkaji zake kwenye nafasi mbalimbali kama wasaidizi wake.Hili limejirudia hata pale bunge lilipomuazibu kwa kumwondoa waziri mkuu EL ili achague team bora bado yamejirudia yale yale.

Kwa nini siungi mkono hoja ya Mh. Zitto?
Sababu nilizotoa hapo kwenye maelezo ni kuwa tatizo kwenye uongozi wa nchi yetu sio mawaziri ama waziri mkuu bali ni mfumo mzima wa uongozi wa Jk.Hapa kilichotakiwa ni kutibu ugonjwa kama sio chanjo/kinga kwa kumwadabisha JK .Kwanini Zitto amekimbilia hoja ya kumwondoa Pinda ili hali kulikuwa na nafasi ya kupeleka hoja ya kutokuwa na imani na Raisi?.

Hapo ndio pale wachambuzi wanapochimba zaidi na kuangalia kwa undani juu ya tuhuma za uswahiba wa Zitto na JK.Hii hoja kwa mtazamo wangu ni kupoteza mantiki ya hoja ya msingi iliyotaka kupelekwa bungeni ya kutaka kumng'oa JK.

Mungu Ibariki Tanzania dhidi ya huu uwizi wa dhahiri dhidi ya mali za walalahoi.

tuna waziri mkuu dhaifu... yeye ndiye mwenye dhamana nambari wani serikalini.... kumbuka pia yeye ndiye mwakilishi wa serikali bungeni, na mshauri mkuu wa rais when it comes to baraza la mawaziri kuanzia uteuzi hadi utendaji na tathmini

naunga mkono hoja ya ZITTO

PS: nahisi unatumika vibaya mkuu
 
Lakini mfumo huo huo mbovu unaweza kuwarudisha mawaziri hao hao wabovu!

Na mimi hapo ndipo napopata wasiwasi kuwa Jk atatafuta maswahiba wakke wengine ambao ataweza kushirikianna nao katika kufanya ufisadi.Hapa ni kwamba watu wanataka kumsafisha JK ili hali imedhihirika hata mwanae anafanya uchafu kama wa hao mawaziri.Kwa minajili hiyo wote watakuwa wanashirikiana naye kama sio yeye anawatuma
 
Fikra za mwanadamu zinapotawaliwa na hulka ya ushabiki zaidi ya ukweli ,maamuzi hutolewa pasipo kuzingatia ukweli.Pia maamuzi hayo huambatana na hoja nyepesi zisizo na manufaa katika utatuzi wa tatizo kuu.

Serikali ya Jk tokea imeingia madarakani awamu ya kwanza imegubikwa na vitendo vya rushwa na Ufisadi uliokithiri kupita kiasi.Hii ni kutokana na ukweli kwamba Jk kama Raisi hakuwa na uwezo wa kuongoza nchi. Kongozi yeyote asiye na uwezo wa uongozi ni dhahiri hata team/wasaidizi wake watakuwa ni wabovu.Jk amejaza washkaji zake kwenye nafasi mbalimbali kama wasaidizi wake.Hili limejirudia hata pale bunge lilipomuazibu kwa kumwondoa waziri mkuu EL ili achague team bora bado yamejirudia yale yale.

Kwa nini siungi mkono hoja ya Mh. Zitto?
Sababu nilizotoa hapo kwenye maelezo ni kuwa tatizo kwenye uongozi wa nchi yetu sio mawaziri ama waziri mkuu bali ni mfumo mzima wa uongozi wa Jk.Hapa kilichotakiwa ni kutibu ugonjwa kama sio chanjo/kinga kwa kumwadabisha JK .Kwanini Zitto amekimbilia hoja ya kumwondoa Pinda ili hali kulikuwa na nafasi ya kupeleka hoja ya kutokuwa na imani na Raisi?.

Hapo ndio pale wachambuzi wanapochimba zaidi na kuangalia kwa undani juu ya tuhuma za uswahiba wa Zitto na JK.Hii hoja kwa mtazamo wangu ni kupoteza mantiki ya hoja ya msingi iliyotaka kupelekwa bungeni ya kutaka kumng'oa JK.

Mungu Ibariki Tanzania dhidi ya huu uwizi wa dhahiri dhidi ya mali za walalahoi.

pinda ndo msimamizi wa shuhuli za serikali bungenii watendaji wa chini yake wameshindwa kuwajibika ivyo basi ni halali yeye kuwajibishwa, thats all, unaishi nchi gani??
 
nimechoka na resolutions zisizozaa matunda, ooh jairo, oooh mkulo, ooooh pinda. no action. ngoja niende jamii jokes nikajiliwaze mie.
 
na mimi nakuunga mkono Rais wetu hana uwezo wa kuongoza,watendaji anaoteua ni dhaifu itakuwa ni kumwonea tu Pinda kwani kila ishu nzito ikitokea rais yupo nje ya nchi kumbukeni mgomo wa madaktari halafu baada ya hapo anakusanya mafisadi kina iddi simba eti anaongea na wazee wa Dar es salaam Tatizo ni mfumo mzima kwani rais hasomi magazeti ,hapewi taarifa na watu wa usalama tusizunguke tukimwachia rais mpaka muda wake uishe tutapata hasara kubwa ni heri aambiwe waziwazi aondoe hizo takataka alizotuwekea
 
Back
Top Bottom