BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
* Asema wamehojiwa bila kufuata taratibu, kanuni
* Shellukindo akiri kuhojiwa, ahusisha na Richmond
* TAKUKURU: Tuko sahihi, hakuna aliye juu ya sheria
Na Edmund Mihale
Majira
26 October 2009
SAKATA la uchunguzi unaofanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) dhidi ya wabunge kupokea posho mara mbili limechukuwa hatua mpya baada ya Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta kusema kitendo hicho kimewadhalilisha wabunge kwani taasisi hiyo haikufuata utaratibu.
Kauli hiyo ya Bw. Sitta imekuja siku moja baada ya TAKUKURU kutoa ufafanuzi kuhusu uchunguzi tuhuma za kuchukua posho katika taasisi mbalimbali wanazotembelea huku wakiwa wameshalipwa na Ofisi ya Bunge.
Katika taarifa yake iliyokaririwa na vyombo vya habari jana, TAKUKURU ilisema Ofisi ya Bunge ndiyo iliomba ufanyike uchunguzi dhidi ya wabunge wanaoomba na kulipwa takrima serikalini na katika mashirika wanayotembelea katika ziara zao za kazi.
Akizungumza na Majira kwa njia ya simu jana, Bw. Sitta alisema hatua iliyofikiwa na TAKUKURU ni udhalilishaji na imekiuka utaratibu na kanuni na sheria za nchi dhidi ya bunge kama taasisi inayojitegemea.
"Mimi sijui kama kuna jambo hilo kwani sijataarifiwa na kama limefanyika bila kunitaarifu, huu utakuwa ni udhalilishaji mkubwa katika ofisi yangu na wabunge pia," alisema Bw. Sitta.
Alisema hata hivyo yeye kama spika hadi sasa hajui ni nini kinachohojiwa na taasisi hiyo kutokana na kutokuwa na taarifa yeyote katika ofisi yake bali anashangaa kuliona jambo hilo katika vyombo vya habari.
Bw. Sitta alisema kimsingi ofisi ya TAKUKURU ilitakiwa kuandika barua katika ofisi yake juu ya tuhuma hizo za wabunge kuwa inahitaji kufanya uchunguzi huo na ilipaswa kuwataarifu wabunge juu ya suala hilo kuliko ilivyolichukuliwa na taasisi hiyo.
"Natoa tahadhari kwa taasisi nyingine za uchunguzi kama TAKUKURU kuwa linapotokea jambo kama hilo ni lazima watoe taarifa kwa maandishi katika ofisi za bunge ili bunge liwe na taarifa ya bunge litoe utaratibu.
"Wabunge wana kinga kama walivyo viongozi wengine wa serikali, ona kitendo kilichofanywa na Polisi Morogoro kwa kumdhalilisha mbunge kwa kumburuza katika pick-up kisa sh 7,000 za bili ya maji tena kilifanywa askari wa ngazi ya chini wasioelewa nini maana ya kinga ya mbunge kuwa ni moja ya udhalilishaji," alisema Bw. Sitta.
Alisema kisheria mbunge anapaswa kukamatwa au kuhojiwa na mtu wa ngazi ya juu wa chombo chochote cha usalma kwa kufuata utaratibu, kanuni na sheria za nchi kwani mbunge hawazi kukimbia, na siyo askari wa ngazi za chini kama ilivyofanya TAKUKURU na Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro.
Lakini Msemaji wa TAKUKURU, Doreen Kapwani alipozungumza na Majira jana alisisitiza kauli ile ile ya juzi kuwa wabunge hawako juu ya sheria, na Katiba ya Nchi inasema hivyo, kwa hiyo walistahili kuhojiwa.
"TAKUKURU inapenda kuujulisha umma kwamba wabunge kama ilivyo kwa mwananchi mwingine yeyote wanawajibika kisheria kuitikia wito katika ofisi za TAKUKURU iwe ni kwa kuhojiwa au kwa kutoa ushahidi kwani hakuna raia yeyote aliye juu ya sheria na Katiba ya Nchi iko wao wazi kwa hili," alisema.
Wakati taarifa ya juzi ya TAKUKURU iliweka bayana kuwa Ofisi ya Bunge iliiomba rasmi taasisi hiyo ifuatilie nyendo za wabunge hao, Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashilillah alikana kufanya hivyo, badala yake akasema ofisi yake iliandikiwa barua na uongozi wa juu wa serikali ikimtaka kutoa ushirikiano.
Bw. Kashililah alisema barua hiyo iliitaka ofisi yake itoe ushirikiano kwa taasisi hiyo pale inapobidi na hivyo aliandika kukubali ombi hilo lakini alitegemea kupata majibu ya utekelezaji wa uchunguzi huo lakini hadi leo hajui nini walichofanyiwa wabunge hao.
Wakati taasisi hizo zikiumana, Mbunge wa Jimbo la Bumbuli, Bw. William Shelukindo ambaye vyanzo vyetu ndani ya TAKUKURU vilidai kuwa amegoma kutoa ushirikiano katika uchunguzi huo, alizungumza na gazeti hili na kukiri kuhojiwa na taasisi hiyo kuhusu tuhuma hizo na kuwa alitoa ushirikiano wa kutosha.
"Hawa watu wananitaka nini mie au kwa kuwa Mkurugenzi wao tunamkaanga wiki ijao ndiyo wanatufanyia visa hivi, nilipigiwa simu na mtu mmoja anaitwa Kigoni mwezi mmoja uliopita nikachoma mafuta yangu kutoka jimboni kwangu hadi Dar es Slaam nikahojiwa na nikatoa ushirikano wa kutosha sasa wanataka ushirikano upi.
"Niliwaambia kuwa kweli nimechukuwa posho hiyo kama takrima na wala si kosa kwani ni taasisi tofauti kama ingekuwa ni ofisi moja hili lingekuwa ni kosa.
"Hapa ninaona kuna kuna jambo linatafutwa hapa, kwanini hoja hii ije wakati huu tunapojadili jambo la Richmond ambapo bosi wao anahusika, naomba niwambie kuwa sitarudi nyuma katika hili, tunaingia bungeni na tutalijadili kwa kina jambo hilo hadi hapo tutakapopata ukweli wasitubabaishe," alisema Bw. Shelukindo.
Alisema kitendo kilichofanywa na TAKUKURU kumhoji bila kutoa taarifa katika ofisi yake ni udhalilishaji mkubwa kwa Bunge.
Alisema kuwa kama inafanya fitina hizo ili kumnusuru bosi wao wamechelewa kwani walitakiwa kufanya hivyo kabla hajatoa uamuzi kuutangazia umma kuwa hakukuwa na rushwa katika kuingia mkataba wa kampuni tata wa Richmond.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughukia Sera, Utaratibu na Bunge. Bw Philip Marmo alisema iwapo wabunge hao wanaona kuwa wamedhalilishwa wanapaswa kwenda katika vyombo vya sheria ili sheria ifuate mkondo wake na sio kukimbilia katika vyombo vya habari.
Kwa miezi mwili TAKUKURU imekuwa ikifanya uchunguzi na kuwahoji wabunge wa wanaotuhumiwa kuchukuwa posho mara mbili katika masharika ya umma wanapoyatembelea katika ziara mablimbalia za kikazi.
* Shellukindo akiri kuhojiwa, ahusisha na Richmond
* TAKUKURU: Tuko sahihi, hakuna aliye juu ya sheria
Na Edmund Mihale
Majira
26 October 2009
SAKATA la uchunguzi unaofanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) dhidi ya wabunge kupokea posho mara mbili limechukuwa hatua mpya baada ya Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta kusema kitendo hicho kimewadhalilisha wabunge kwani taasisi hiyo haikufuata utaratibu.
Kauli hiyo ya Bw. Sitta imekuja siku moja baada ya TAKUKURU kutoa ufafanuzi kuhusu uchunguzi tuhuma za kuchukua posho katika taasisi mbalimbali wanazotembelea huku wakiwa wameshalipwa na Ofisi ya Bunge.
Katika taarifa yake iliyokaririwa na vyombo vya habari jana, TAKUKURU ilisema Ofisi ya Bunge ndiyo iliomba ufanyike uchunguzi dhidi ya wabunge wanaoomba na kulipwa takrima serikalini na katika mashirika wanayotembelea katika ziara zao za kazi.
Akizungumza na Majira kwa njia ya simu jana, Bw. Sitta alisema hatua iliyofikiwa na TAKUKURU ni udhalilishaji na imekiuka utaratibu na kanuni na sheria za nchi dhidi ya bunge kama taasisi inayojitegemea.
"Mimi sijui kama kuna jambo hilo kwani sijataarifiwa na kama limefanyika bila kunitaarifu, huu utakuwa ni udhalilishaji mkubwa katika ofisi yangu na wabunge pia," alisema Bw. Sitta.
Alisema hata hivyo yeye kama spika hadi sasa hajui ni nini kinachohojiwa na taasisi hiyo kutokana na kutokuwa na taarifa yeyote katika ofisi yake bali anashangaa kuliona jambo hilo katika vyombo vya habari.
Bw. Sitta alisema kimsingi ofisi ya TAKUKURU ilitakiwa kuandika barua katika ofisi yake juu ya tuhuma hizo za wabunge kuwa inahitaji kufanya uchunguzi huo na ilipaswa kuwataarifu wabunge juu ya suala hilo kuliko ilivyolichukuliwa na taasisi hiyo.
"Natoa tahadhari kwa taasisi nyingine za uchunguzi kama TAKUKURU kuwa linapotokea jambo kama hilo ni lazima watoe taarifa kwa maandishi katika ofisi za bunge ili bunge liwe na taarifa ya bunge litoe utaratibu.
"Wabunge wana kinga kama walivyo viongozi wengine wa serikali, ona kitendo kilichofanywa na Polisi Morogoro kwa kumdhalilisha mbunge kwa kumburuza katika pick-up kisa sh 7,000 za bili ya maji tena kilifanywa askari wa ngazi ya chini wasioelewa nini maana ya kinga ya mbunge kuwa ni moja ya udhalilishaji," alisema Bw. Sitta.
Alisema kisheria mbunge anapaswa kukamatwa au kuhojiwa na mtu wa ngazi ya juu wa chombo chochote cha usalma kwa kufuata utaratibu, kanuni na sheria za nchi kwani mbunge hawazi kukimbia, na siyo askari wa ngazi za chini kama ilivyofanya TAKUKURU na Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro.
Lakini Msemaji wa TAKUKURU, Doreen Kapwani alipozungumza na Majira jana alisisitiza kauli ile ile ya juzi kuwa wabunge hawako juu ya sheria, na Katiba ya Nchi inasema hivyo, kwa hiyo walistahili kuhojiwa.
"TAKUKURU inapenda kuujulisha umma kwamba wabunge kama ilivyo kwa mwananchi mwingine yeyote wanawajibika kisheria kuitikia wito katika ofisi za TAKUKURU iwe ni kwa kuhojiwa au kwa kutoa ushahidi kwani hakuna raia yeyote aliye juu ya sheria na Katiba ya Nchi iko wao wazi kwa hili," alisema.
Wakati taarifa ya juzi ya TAKUKURU iliweka bayana kuwa Ofisi ya Bunge iliiomba rasmi taasisi hiyo ifuatilie nyendo za wabunge hao, Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashilillah alikana kufanya hivyo, badala yake akasema ofisi yake iliandikiwa barua na uongozi wa juu wa serikali ikimtaka kutoa ushirikiano.
Bw. Kashililah alisema barua hiyo iliitaka ofisi yake itoe ushirikiano kwa taasisi hiyo pale inapobidi na hivyo aliandika kukubali ombi hilo lakini alitegemea kupata majibu ya utekelezaji wa uchunguzi huo lakini hadi leo hajui nini walichofanyiwa wabunge hao.
Wakati taasisi hizo zikiumana, Mbunge wa Jimbo la Bumbuli, Bw. William Shelukindo ambaye vyanzo vyetu ndani ya TAKUKURU vilidai kuwa amegoma kutoa ushirikiano katika uchunguzi huo, alizungumza na gazeti hili na kukiri kuhojiwa na taasisi hiyo kuhusu tuhuma hizo na kuwa alitoa ushirikiano wa kutosha.
"Hawa watu wananitaka nini mie au kwa kuwa Mkurugenzi wao tunamkaanga wiki ijao ndiyo wanatufanyia visa hivi, nilipigiwa simu na mtu mmoja anaitwa Kigoni mwezi mmoja uliopita nikachoma mafuta yangu kutoka jimboni kwangu hadi Dar es Slaam nikahojiwa na nikatoa ushirikano wa kutosha sasa wanataka ushirikano upi.
"Niliwaambia kuwa kweli nimechukuwa posho hiyo kama takrima na wala si kosa kwani ni taasisi tofauti kama ingekuwa ni ofisi moja hili lingekuwa ni kosa.
"Hapa ninaona kuna kuna jambo linatafutwa hapa, kwanini hoja hii ije wakati huu tunapojadili jambo la Richmond ambapo bosi wao anahusika, naomba niwambie kuwa sitarudi nyuma katika hili, tunaingia bungeni na tutalijadili kwa kina jambo hilo hadi hapo tutakapopata ukweli wasitubabaishe," alisema Bw. Shelukindo.
Alisema kitendo kilichofanywa na TAKUKURU kumhoji bila kutoa taarifa katika ofisi yake ni udhalilishaji mkubwa kwa Bunge.
Alisema kuwa kama inafanya fitina hizo ili kumnusuru bosi wao wamechelewa kwani walitakiwa kufanya hivyo kabla hajatoa uamuzi kuutangazia umma kuwa hakukuwa na rushwa katika kuingia mkataba wa kampuni tata wa Richmond.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughukia Sera, Utaratibu na Bunge. Bw Philip Marmo alisema iwapo wabunge hao wanaona kuwa wamedhalilishwa wanapaswa kwenda katika vyombo vya sheria ili sheria ifuate mkondo wake na sio kukimbilia katika vyombo vya habari.
Kwa miezi mwili TAKUKURU imekuwa ikifanya uchunguzi na kuwahoji wabunge wa wanaotuhumiwa kuchukuwa posho mara mbili katika masharika ya umma wanapoyatembelea katika ziara mablimbalia za kikazi.