Japhari Shabani (RIP)
R I P
- Jan 16, 2007
- 721
- 176
Tumekua tukishuhudia maamuzi,kauli na vitendo vingine vingi vya ajabu na aibu kutoka kwa viongozi wa CCM na serikali.Ni kweli kuna wanaotoa kauli,kuunga mkono au kushiriki katika maamuzi bila kujua au kwa upeo mdogo wa kuelewa,mazoae na ushabiki ,hawa tunaweza kuwasamee.Kuna kundi lingine la viongozi katika CCM ambao tunaweza kuwahita wanaupeo na uwezo wa kushauri au kupambanua lipi sawa na lipi sio sawa.Viongozi hawa wanapokaa kimya na kunyamazia yale yote mabaya yanayotendeka katika CCM na serikali ni wa SALITI Kwani wanashiriki katika maamuzi ambayo ni hatari na mzigo kwa taifa.Hawa tunawezakusema wako huko kwa ajiri ya matumbo yao na si kwa manufaa ya Taifa Kilichotokea kwa Mh.Sitta huko Visiwani liwe funzo kwa viongozi wa CCM ambao tunazani bado wanachembe ya uchungu wa Taifa.Niwazi Mh.Sitta alielewa zigo analolibeba(mswaada wa katiba)Kama mwanasheria,linamapungufu makubwa na umeandaliwa kwa makosa lakini akaamua kulibeba.Huku ni kujidhalilisha hivyo onyo kwa viongozi makini kama mpo mliobaki CCM msikubali kubeba madudu ya ajabu.MUNGU IBARIKI TANZANIA.