Bitabo
JF-Expert Member
- Sep 27, 2011
- 1,900
- 687
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema anachukizwa na tabia ya baadhi ya watu kukaa na kufikiria urais kila siku huku wakiacha kuutumikia umma.Kauli ya Sitta ambaye alitangaza kwamba kwa sasa hana nia ya kuwania urais 2015, inakuja kipindi ambacho baadhi ya wanasiasa hasa ndani ya CCM wamekuwa wakipigana vikumbo kwa ajili ya mbio za kumrithi Rais Jakaya Kikwete.
Juzi akiwa ziarani jimboni kwake Urambo Mashariki, Sitta alisema urais ni jambo linalokuja lenyewe kwa watu waadilifu hivyo hakuna haja kwa watu kila siku kufanya harakati za urais.
"Urais unakuja wenyewe kwa watu walio waadilifu. Nachukizwa na watu ambao wao kila siku wamekuwa na mawazo ya urais na kuacha mambo ya msingi ya kutumikia wananchi wa Tanzania," alifafanua Sitta.
Sitta ambaye pia alikuwa Spika wa Bunge la Tisa, alisema yeye binafsi anachukizwa pia na kuhusishwa katika harakati za urais wa 2015 na kusema hadi sasa, bado ni mapema na kutaka wanasiasa kutumikia wananchi.
Aliongeza kwamba wapo ambao hata wanajaribu kutengeneza uongo kwamba, amekuwa akienda makinasani na misikitini kwa ajili ya kutaka urais lakini akasema;"Hawa ni wale wale mafisadi wanaoeneza ajenda zao za hovyo kila siku."
Sitta alifafanua kwamba suala la yeye kusaidia shughuli au kujumuika katika Kanisa au Msikiti ni jambo la kawaida na hakuanza kulifanya leo wala jana bali ni muda mrefu.
Alisema wapo watu wanaojaribu kujenga taswira kwa umma kwamba, kujumuika kwake katika baadhi ya shughuli za makanisa au misikiti ni sehemu ya mbinu za kusaka urais kitu alichosema ni upotoshaji kwa kuwa hakuanza leo kujumuika na wana dini.
Waziri huyo mwenye dhamana ya Uhusiano wa Afrika Mashariki, alisema ni vyema wanasiasa wakajikita katika mambo ya msingi ya kusaidia wananchi, kusimamia maadili na kuonyesha uadilifu kuliko kuwaza urais kila kukicha.
Alienda mbali akisema, kama ni urais ameshiriki kusaidia baadhi ya wagombea na baadhi walifanikiwa kushika wadhifa huo hivyo haoni sababu za watu kumhusisha na mbio za urais 2015 pale anapotumikia umma.
"Nimeshashiriki sana kusaidia wagombea urais, baadhi yao walifanikiwa. Hivyo, sina tamaa na urais ninayofanya ni kutumikia umma na taifa langu. Lakini, wapo wanaopitapita na kutaka kuonyesha wananchi kwamba ninavyotumikia umma na msimamo wangu kutetea maslahi ya taifa, kama ni kampeni za urais, lakini hawa ni wale wale maadui wa kila siku," alifafanua Sitta.
Alisema suala la urais siyo la kukimbilia wala kulitafuta kwa nguvu na mbinu chafu, kwani siku zote watu waadilifu wanafahamika na hakuna haja ya kutumia nguvu nyingi kuutafuta madaraka hayo ya juu ya nchi.
"Haya mambo ya urais kila siku hayana maana. Kibaya zaidi watu wanahamisha mambo ya msingi na kuyapeleka katika fikra za ovyo. Hebu ufike wakati tuangalie matatizo ya wananchi kwanza tusifikirie vitu ambavyo havimsaidii mwananchi wala taifa," alisistiza.
Hivi karibuni Sitta amekuwa alitajwa kama mmoja wa watu wanaoutaka urais 2015, lakini mwenyewe hivi karibuni alipozungumza na kituo kimoja cha luninga nchini alisema, "kwa sasa sijafikiria urais."
source: Mwananchi ya leo
Juzi akiwa ziarani jimboni kwake Urambo Mashariki, Sitta alisema urais ni jambo linalokuja lenyewe kwa watu waadilifu hivyo hakuna haja kwa watu kila siku kufanya harakati za urais.
"Urais unakuja wenyewe kwa watu walio waadilifu. Nachukizwa na watu ambao wao kila siku wamekuwa na mawazo ya urais na kuacha mambo ya msingi ya kutumikia wananchi wa Tanzania," alifafanua Sitta.
Sitta ambaye pia alikuwa Spika wa Bunge la Tisa, alisema yeye binafsi anachukizwa pia na kuhusishwa katika harakati za urais wa 2015 na kusema hadi sasa, bado ni mapema na kutaka wanasiasa kutumikia wananchi.
Aliongeza kwamba wapo ambao hata wanajaribu kutengeneza uongo kwamba, amekuwa akienda makinasani na misikitini kwa ajili ya kutaka urais lakini akasema;"Hawa ni wale wale mafisadi wanaoeneza ajenda zao za hovyo kila siku."
Sitta alifafanua kwamba suala la yeye kusaidia shughuli au kujumuika katika Kanisa au Msikiti ni jambo la kawaida na hakuanza kulifanya leo wala jana bali ni muda mrefu.
Alisema wapo watu wanaojaribu kujenga taswira kwa umma kwamba, kujumuika kwake katika baadhi ya shughuli za makanisa au misikiti ni sehemu ya mbinu za kusaka urais kitu alichosema ni upotoshaji kwa kuwa hakuanza leo kujumuika na wana dini.
Waziri huyo mwenye dhamana ya Uhusiano wa Afrika Mashariki, alisema ni vyema wanasiasa wakajikita katika mambo ya msingi ya kusaidia wananchi, kusimamia maadili na kuonyesha uadilifu kuliko kuwaza urais kila kukicha.
Alienda mbali akisema, kama ni urais ameshiriki kusaidia baadhi ya wagombea na baadhi walifanikiwa kushika wadhifa huo hivyo haoni sababu za watu kumhusisha na mbio za urais 2015 pale anapotumikia umma.
"Nimeshashiriki sana kusaidia wagombea urais, baadhi yao walifanikiwa. Hivyo, sina tamaa na urais ninayofanya ni kutumikia umma na taifa langu. Lakini, wapo wanaopitapita na kutaka kuonyesha wananchi kwamba ninavyotumikia umma na msimamo wangu kutetea maslahi ya taifa, kama ni kampeni za urais, lakini hawa ni wale wale maadui wa kila siku," alifafanua Sitta.
Alisema suala la urais siyo la kukimbilia wala kulitafuta kwa nguvu na mbinu chafu, kwani siku zote watu waadilifu wanafahamika na hakuna haja ya kutumia nguvu nyingi kuutafuta madaraka hayo ya juu ya nchi.
"Haya mambo ya urais kila siku hayana maana. Kibaya zaidi watu wanahamisha mambo ya msingi na kuyapeleka katika fikra za ovyo. Hebu ufike wakati tuangalie matatizo ya wananchi kwanza tusifikirie vitu ambavyo havimsaidii mwananchi wala taifa," alisistiza.
Hivi karibuni Sitta amekuwa alitajwa kama mmoja wa watu wanaoutaka urais 2015, lakini mwenyewe hivi karibuni alipozungumza na kituo kimoja cha luninga nchini alisema, "kwa sasa sijafikiria urais."
source: Mwananchi ya leo