Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Sitta: Nitasema ukweli daima | Send to a friend |
Friday, 22 July 2011 20:16 |
Ramadhan Semtawa WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta, amesema ataendelea kusema ukweli daima kwa wananchi kuhusu kasoro ndani ya CCM na serikali akiamini kuwa huo ndiyo uwajibakaji. Kauli hiyo ya Sitta, inakuja siku moja baada ya Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, kumtuhumu kuwa anataka kuigawa CCM na kuibomoa serikali.Guninita alitoa kauli hizo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano wa wanachama wa CCM wa Tawi la Mbezi, uliojadili matatizo ya chama chao. Katika mazungumzo yake Mwenyekiti huyo alimwelezea waziri huyo,kuwa ni mtu hatari mwenye malengo ya kikitumbukiza chama shimoni.Hata hivyo akizungumzia jijini Dar es Salaam jana na baadhi ya vyombo vya habari, Sitta alisema kuna wafuasi wa mafisadi ndani ya CCM, wanaohofu ukweli kwa kchelea kufahamika wa maovu yao. Sitta alisema serikali makini lazima ikiri upungufu unaotokana na makosa yake."Nilichokisema Mbeya ni kuambia Watanzania ukweli. Na nitaendelea kuwaambia ukweli," alisisitiza spika huyo mstaafu. Alisema serikali makini haiwezi kudanganya wananchi wake na kusisitiza kuwa watanzania wa leo ni watu wenye akili na hawawezi kuwambiwa habari nzuri kuhusu umeme wakati umeme ni tatizo. "Siwezi kuishi katika uongo. Naamini katika ukweli na nitaendelea kusema ukweli. Sasa hivi utamdanganya Mtanzania gani, kuna vijana zaidi ya 100,000 wako katika vyuo vikuu leo uende kwa wananchi ukawadanganye, ebo," alise ma Sitta ambaye ni Mbunge wa Urambo Mashariki. Alisema ni ukweli usiopingika kwamba miundombinu mingi ya umeme ilijengwa tangu serikali ya awamu ya kwanza chini Hayati Mwalimu Julius Nyerere, na kwamba kuwaeleza wananchi upungufu na kasoro za kiutendaji wa serikali katika kuwekeza umeme si tatizo. "Yaani mtu anataka leo uende ukadanganye wananchi. Kwanza unapoeleza wananchi ukweli wa mapungufu ya kiutendaji unaijengea heshima serikali. Serikalia makini ni ile inayokiri mapungufu kwa wananchi na kuwaambia inataka kufanya nini kama nilivyofanya kule Mbeya," alisisitiza. "Kule Mbeya niliueleza ule umati ukweli kuhusu mapungufu yetu serikalini na wananchi walituelewa. Kuna mapungufu tumeyakiri na tunajipanga kuyapatia ufumbuzi. Umeme ni tatizo kubwa huwezi kueleza uongo kwa Watanzania wakakuelewa, waambie wananchi ukweli watakuelewa,"alisema.Alisema miaka ya nyuma kulifanyika utafiti kuhusu uzalishaji umeme katika maporomoko ya maji ya Stiglers, mradi ambao ungeweza kuzalisha megawati zaidi ya 2,000, lakini hadi sasa haujaendelezwa. "Sasa haya ndiyo mapungufu yetu, lakini wanatokea baadhi ya watu wenye upeo mdogo ndani ya CCM wanaoendekeza siasa za ufuasi, wanakaa na kuzungumza mambo ya hovyo," alisisitiza. Akiwa Mbeya, Sitta alisema tatizo la umeme linatokana na mapungufu mbalimbali ya serikali ikiwamo mikataba mibovu na kutaka wahusika washughulikiwe huku serikali ikijipanga kutatua matatizo hayo. |