Sitta: Mtandao CCM mwisho November 2012!

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Imeandikwa tarehe 10 OCTOBER 2012 – NA ARNOLD SWAI, MOSHI

MJUMBE wa Halmashauri kuu y a Taifa ya CC (NEC), Samuel Sitta amesema kwa sasa chama hicho kiko imara zaidi ila alikiri moja ya tatizo kubwa ni mtandao iliyoanza kuundwa kwa ajili ya urais Mwaka 2015.

Hata hivyo, amedai kufkia mwezi ujao, tatizo hilo litakuwa limemalizwa, huku akiwaonya vijana wa Umojawa Vijana wa Chama hicho (UVCCM) kutorubuniwa na watu walioanza kuunda mitandao midogo midogo ya kifisadi ndani ya chama kwa lengo la kugombea urais mwaka 20115.

Sitta ambaya pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, ametoa kauli hiyo leo mjini Moshi wakati alipofika kuwasalimia vijana wa chama hicho Mkoa wa Kilimanjaro walipokuwa wanafanya uchaguzi wa Mwenyekiti na nafasi nyingine mbalimbali kwenye Ukumbi wa CCM Mkoa.

Amesema, mara baada ya kupatia ufumbuzi mitandao hiyo ya kuwania urais 2015, mwezi ujao chmama kitakuja na maamuzi mapya na kuzunguka nchi nzima kueleza mabadiliko na sura mpya ya chama hivyo hakuna mtu wa kukibabaisha chama hicho hata kidogo.

"Sisi sio punguani wa kuangalia vikundi vya kifisadi ili vichukue nchi, hilo hatutalifumbia macho kwa sababu kuna watu wanajaribu kuunda vimitandao tumejipanga ipasavyo na mwezi November tunakuja na maamuzi na tutazunguka nchi nzima kuelezea sura mpya ya chama", alisema Sitta.

Alisema vijana kwa sasa wanatakiwa watumie akili zaidi na si kujali matumbo yao kwa kununuliwa na baadhi ya watu, kwa sababu kiongozi wa aina hiyo hatakuwa na maslahi kwa wananchi na badala yake atakuwa mzigo wa Taifa.

Alisema chama ni imara na hakina haja ya kusumbuliwa na vijana wadogo wanaotaka urais na vyama vinavyotamba vitachukua nchi wakati vyenyewe vikiwa havina hata safu ya viongozi wa kuongoza.
 
Sitta anasema ukweli ingawa kwa njia tofauti. Novemba ya 2015 CCM itakapopigwa chini utakuwa mwisho wa mitandao ya ujambazi inayowafagilia majambazi na mafisadi kugombea urais akiwamo yeye Sitta.
 
Sasa Uongozi Utakuwa MPYA kabisa ??? Nape sio matata kama Miezi iliyopita; yule Mvaa tai sisikii matusi yake sana January alikuwa bado anajiheshimu kwa public DISPLAY; Kale kimama ni kuvaa NJANO n KIJANI tu sisikii suati ake; Katibu Mkuu naona Kofia kama ya SPEAK zaidi ya sura yake...
 
Sitta!! Vyama hivyo visivyo na safu ya uongozi ni mara ngapi umeomba kujiunga navyo na ukakataliwa!!?

Hivyo vyenye safu ya uongozi vimelisaidia vp taifa zaidi kutuongezea Mafisadi na Mafreemasons!?

Very pathetic Sitta!!
 
Huyu mzee anazeeka vibaya..hivi kwa akili zake CCM imezaliwa upya? Yani afahamu kuwa huu uchaguzi ndio umeandaa mazishi ya CCM mwaka 2015?
 
Kila mkubwa kaweka mtoto wake UVCCM, Sitta anaweza kusema with certainty kuwa hao watoto wa vigogo (wa kwake akiwemo) watafanya tofauti na maagizo ya wazazi wao? Na kwa maana hiyo watoto watakuwa wanapalilia mitandao ya wazazi?
 
sitta kasema kweli! Mitandao itakufa baada ya ccm kung'olewa madarakani, wengi niwa chumia tumbo hataweza kuendelea kudumu kuwa kwenye chama kitakacho kuwa kimewakosesha dili za kuuza wanyama na kugawa vitalu, lakini pia wengi watakuwa jela na kawaida ya jela hua hakuna mitandao mule ndani.

Sitta anazeeka vizuri sasa baada ya kukubali kuwa mwisho wa mitandao umefika.
 
Kumbe SITTA nimefungua haraka haraka nilifikiri mnamsema SINTAH
 
Alisema chama ni imara na hakina haja ya kusumbuliwa na vijana wadogo wanaotaka urais na vyama vinavyotamba vitachukua nchi wakati vyenyewe vikiwa havina hata safu ya viongozi wa kuongoza.

TANU 1954-1961, ikiwa ni chama cha siasa chenye umri wa miaka saba tu, kilikuwa na viongozi makini wachache kuliko hata Chadema 1995 - 2012, yenye umri wa miaka 17, lakini kwa sababu hatamu ya chama ni UMMA, hakuna aliyezuia TANU isifanikishe malengo yake;
 
Nafikiri alikuwa anamaanisha November 2015!!

Hata wakati wa Falsafa ya kujivua gamba walikuja na hadithi kama hii, Nape akazunguka nchi nzima, magamba hayakuvuka na mambo yakageuka yakawa ni kuvuana nguo hadharani!!

Rushwa, Ufisadi, Fitna na Usultani ndio ''Operating System'' ya chama cha mapinduzi kwa sasa, halafu unadai unataka kufanya Unstallation!!!! How will the party operate?

Mmasai ameshasema kwa sasa ananguvu maradufu, na Upepo wake ulivuma mpaka ukafika Hanang ukamchinjia porini Sumaye, na sasa upepo wake unavuma kuelekea Msoga, Urambo na Mtama!!
 
sitta kasema kweli! Mitandao itakufa baada ya ccm kung'olewa madarakani, wengi niwa chumia tumbo hataweza kuendelea kudumu kuwa kwenye chama kitakacho kuwa kimewakosesha dili za kuuza wanyama na kugawa vitalu, lakini pia wengi watakuwa jela na kawaida ya jela hua hakuna mitandao mule ndani.

Sitta anazeeka vizuri sasa baada ya kukubali kuwa mwisho wa mitandao umefika.

Mkuu umenena always you have point Kamanda,big up mwisho wao waja si mbali
 
Sasa huyu fisadi mroho wa madaraka anaanzisha mtandao wake peke yake


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Huyu mzee anazeeka vibaya..hivi kwa akili zake CCM imezaliwa upya? Yani afahamu kuwa huu uchaguzi ndio umeandaa mazishi ya CCM mwaka 2015?
Sitta tatizo ni kusahau, amesahau jinsi alivopigwa uspika kiana wakataka kumyanganya kadi alipopiga magoti wakamrudishia? halafu huwa najiuliza vita ya mafisadi anayopigana ni ipi? ikiwa alifunga mjadala wa richmond kihuni na kuwaokoa mafisadi,na pia alishindwa kushimamia maazimio 23 ya bunge yaliyotolewa na kama teule iliyoongozwa na Mwakyembe, ambapo moja wapo ya maazimio ilikuwa ni waliohusika na mkataba huu wa kifisadi wafikishwe kwenye vyombo vya sheria? huyu ni uchu wa madaraka hana lolote ndio maana alianzisha CCJ, mara akarukia chadema, sasa anajikomba ccm, kwanza umri wake anatakiwa astaafu siasa!
 
Nilikuwa na imani sana na Mh. Samwel Sitta na hata maneno anayoongea huwa yanaonyesha hekima fulani lakini utekelezaji wake ni mbovu na hivyo:

-KIGEUGEU/HANA MSIMAMO: Which means hata kwa uongozi tu hafai, ni imara tu awapo mwenyewe(one on one) lakini akirudi kambini, ujanja mfukoni.

-MNAFIKI:Anatoa maneno matamu matamu lakini akienda NEC hakumbuki alichokisema.

Ngoja tusubiri hiyo November(The grand finale) tuone kama watatekeleza.
 
Back
Top Bottom