Sitta:Chadema waruhusiwa kumkataa JK......................

Tusiingize mambo ya udini katika hoja zetu. Madrasa yanatoa elimu nzuri kabisa ya Kiislamu kama ambavyo Wakristu wanasoma Mafundisho. Mimi elimu yangu ilianzia mafundisho kwa kuwa wazazi wangu waliona "Chekechea kuwa ni kupoteza muda na kwenda kunywa uji." Nilifundishwa kusoma nyumbani. Kwa sasa sikubaliani na mtazamo wao naamini Chekechea nzuri ni kitu kizuri.

Hoja yangu ni kuwa Madrasa na Mafundisho ni elimu nzuri na si kitu cha kubeza. Kama tunapinga msimamo wa mtu tupinge kwa mawazo yenye mantiki na yanayoweza kumshawishi unayemwambia aweze elimika au muweze kuanzisha majadiliano na si kutumia lugha ambayo inazuia mazungumzo na kuamsha chuki kama ya kupinga dini, kabila au rangi ya mtu. Naomba kutoa hoja.

Huu ndiyo udini anaoulezea Kikwete umeshaanza kuleta ufa nchini!!!Kubeza dini hapa JF sasa ni jambo la kawaida hapa!Mod wapo baridiii nafikiri wanaridhika na hali hii!!!
 
kila mwananchi mwenye mapenzi mema na nchi hii hataona kosa lolote juuu ya chadema kususia hotuba ya rais bali mambumbuna wanaojiita wasomi wa vyeti vya mezani ndio wasiojua matokeo chanya na faida ya watu makini (CHADEMA) kumgomea rais jamani jk sio mungu kuwa ukimpinga utalaaniwa THINK TWICE.

- Well, heshima sana mkuu jaribuni kuwapa nafasi wananchi kutafakari hizi hatua za kawaida katika Demokrasia, ingawa ni mpya sana kwa sisi wananchi wa taifa hili kwa sababu sio kwamba hazikuwepo hapana hatukuwa tu tunazitumia na sasa ndio zimeanza, kwa tabia zetu za ki-conservative lazima zionekane ni za ajabu,

- Infact tumesema toka majuzi kwamba ukubwa na udogo wa hiki kitendo utaamuliwa na response ya CCM, ambao nao to my shock wanaonekana kupigwa na mshangao mkubwa sana na hii yote ni kwa sababu tumekua tukiabudu sana instituion ya Presidency kwa kuilinganisha na almost ufalme, wakati huko kwenye Demokrasia za kweli yaani majuu ambako tunajaribu sana kuiga kila kitu cha siasa huwa ni kawaida sana!

- Kususia au kutomtambua Rais, hakuna tatizo kabisa kikatiba na hata kwenye kisiasa inategemea na nani anajua kucheza karata zake hapa mbele ya umma, haya tumeyasema sana huku CCM kwamba siasa za kisasa bado zinatupa taabu sana kuzielewa na kuzikubali, sasa wakati ni huu. SALUTE kwa Mzee Sitta, kusimama na kusema wazi mbele ya umma kwa maneno mengine kusimama na kuhesabiwa ni ishus kama hizi ndio zinaweza kutuonyesha nani ni nani katika viongozi wetu wa taifa!


William.
 
Yeah, sitta yuko sahihi na ndivyo mwongozo wa nchi (katiba) unavyoeleza, ingawa tunajua fika kuwa maneno yake hayo yanaweza kutafasiriwa isivyo na ndugu zake lakini hata upindishwe vipi siku zote ukweli utabaki kuwa pale pale, tusubiri kusikia bi makinda atasimama upande gani kama ni kumuunga mkono bosi wake wa zamani na kusimamia katiba ama ni kutekeleza matakwa ya waliompeleka

Nenda chadema mzee 6
 
- Kususia au kutomtambua Rais, hakuna tatizo kabisa kikatiba na hata kwenye kisiasa inategemea na nani anajua kucheza karata zake hapa mbele ya umma, haya tumeyasema sana huku CCM kwamba siasa za kisasa bado zinatupa taabu sana kuzielewa na kuzikubali, sasa wakati ni huu. SALUTE kwa Mzee Sitta, kusimama na kusema wazi mbele ya umma kwa maneno mengine kusimama na kuhesabiwa ni ishus kama hizi ndio zinaweza kutuonyesha nani ni nani katika viongozi wetu wa taifa!

William.
Very cogent analysis...................CCM bado wapo kwenye usingizi wa mfumo wa siasa za demokrasia ya chama kimoja......na ndiyo maana hawajui demokrasia ya vyama vingi humu nchini..................................Chadema wametumia haki yao ya kidemokrasia kuonyesha machungu waliyonayo...............................Sasa jamani CCM kitanda usicholala kunguni wake wakuwashia nini?
 
Back
Top Bottom