Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,550
- 6,062
Fundi Mchundo,
Hapa kuna kitu kimoja kinalalamikiwa na kwa kweli nimesoma maelezo ya walio upande wa Spika na walio upande wa Jaji hiki hata mimi kinanichanganya. Hili linahusu hili swala la EWURA. EWURA wamekamata vituo vya mafuta ambavyo vinauza mafuta machafu. Kisheria walizopewa, ni kuwa wanaruhusiwa kuvifungia. Ni sawa na bwana Afya akikuta mtu anahoteli chafu basi anaruhusiwa kuifungia palepale na si kuipeleka mahakamani. Polisi akikuta wewe mhalifu basi anakubeba palepale na si kwenda mahakamani kuomba ruhusa. Sasa Mahakama inapokuja na kusema "vituo vya mafuta endeleeni kuuza mafuta machafu..." hapa hata mie nashindwa kuelewa. Walipokamata bidhaa mbovu za China, walizibeba palepale na baadaye zikachomwa moto. Sasa wenye mali wangelienda mahakamani na kudai warudishiwe mali zao na waendelee kuziuza, na mahakama inakubali hivyo, mie hapa ndipo nachanganyikiwa.
Ila kuna hilo umeandika hapo juu kuhusu mtu kugombea na wanamkatalia kwa gia hajatoka chama cha upinzani. Kwa kweli katika haki za binadamu, hii imekaa ovyo ka maana nyingine Mahakama inatumia uwezo wake KUVUNJA KATIBA BOVU linalotumika hadi leo Tanzania. Hili hata mie niko nao kwa sana. Ila nafikiri Mahakama ilitakiwa kuwatolea UVIVU wabunge na Serikali kwa kuendeleza katiba iliyozeeka na imepitwa na wakati.
Hapa kuna kitu kimoja kinalalamikiwa na kwa kweli nimesoma maelezo ya walio upande wa Spika na walio upande wa Jaji hiki hata mimi kinanichanganya. Hili linahusu hili swala la EWURA. EWURA wamekamata vituo vya mafuta ambavyo vinauza mafuta machafu. Kisheria walizopewa, ni kuwa wanaruhusiwa kuvifungia. Ni sawa na bwana Afya akikuta mtu anahoteli chafu basi anaruhusiwa kuifungia palepale na si kuipeleka mahakamani. Polisi akikuta wewe mhalifu basi anakubeba palepale na si kwenda mahakamani kuomba ruhusa. Sasa Mahakama inapokuja na kusema "vituo vya mafuta endeleeni kuuza mafuta machafu..." hapa hata mie nashindwa kuelewa. Walipokamata bidhaa mbovu za China, walizibeba palepale na baadaye zikachomwa moto. Sasa wenye mali wangelienda mahakamani na kudai warudishiwe mali zao na waendelee kuziuza, na mahakama inakubali hivyo, mie hapa ndipo nachanganyikiwa.
Ila kuna hilo umeandika hapo juu kuhusu mtu kugombea na wanamkatalia kwa gia hajatoka chama cha upinzani. Kwa kweli katika haki za binadamu, hii imekaa ovyo ka maana nyingine Mahakama inatumia uwezo wake KUVUNJA KATIBA BOVU linalotumika hadi leo Tanzania. Hili hata mie niko nao kwa sana. Ila nafikiri Mahakama ilitakiwa kuwatolea UVIVU wabunge na Serikali kwa kuendeleza katiba iliyozeeka na imepitwa na wakati.