Sitta amcharukia Jaji Mkuu

Fundi Mchundo,
Hapa kuna kitu kimoja kinalalamikiwa na kwa kweli nimesoma maelezo ya walio upande wa Spika na walio upande wa Jaji hiki hata mimi kinanichanganya. Hili linahusu hili swala la EWURA. EWURA wamekamata vituo vya mafuta ambavyo vinauza mafuta machafu. Kisheria walizopewa, ni kuwa wanaruhusiwa kuvifungia. Ni sawa na bwana Afya akikuta mtu anahoteli chafu basi anaruhusiwa kuifungia palepale na si kuipeleka mahakamani. Polisi akikuta wewe mhalifu basi anakubeba palepale na si kwenda mahakamani kuomba ruhusa. Sasa Mahakama inapokuja na kusema "vituo vya mafuta endeleeni kuuza mafuta machafu..." hapa hata mie nashindwa kuelewa. Walipokamata bidhaa mbovu za China, walizibeba palepale na baadaye zikachomwa moto. Sasa wenye mali wangelienda mahakamani na kudai warudishiwe mali zao na waendelee kuziuza, na mahakama inakubali hivyo, mie hapa ndipo nachanganyikiwa.
Ila kuna hilo umeandika hapo juu kuhusu mtu kugombea na wanamkatalia kwa gia hajatoka chama cha upinzani. Kwa kweli katika haki za binadamu, hii imekaa ovyo ka maana nyingine Mahakama inatumia uwezo wake KUVUNJA KATIBA BOVU linalotumika hadi leo Tanzania. Hili hata mie niko nao kwa sana. Ila nafikiri Mahakama ilitakiwa kuwatolea UVIVU wabunge na Serikali kwa kuendeleza katiba iliyozeeka na imepitwa na wakati.
 
Fundi Mchundo,
Hapa kuna kitu kimoja kinalalamikiwa na kwa kweli nimesoma maelezo ya walio upande wa Spika na walio upande wa Jaji hiki hata mimi kinanichanganya. Hili linahusu hili swala la EWURA. EWURA wamekamata vituo vya mafuta ambavyo vinauza mafuta machafu. Kisheria walizopewa, ni kuwa wanaruhusiwa kuvifungia. Ni sawa na bwana Afya akikuta mtu anahoteli chafu basi anaruhusiwa kuifungia palepale na si kuipeleka mahakamani. Polisi akikuta wewe mhalifu basi anakubeba palepale na si kwenda mahakamani kuomba ruhusa. Sasa Mahakama inapokuja na kusema "vituo vya mafuta endeleeni kuuza mafuta machafu..." hapa hata mie nashindwa kuelewa. Walipokamata bidhaa mbovu za China, walizibeba palepale na baadaye zikachomwa moto. Sasa wenye mali wangelienda mahakamani na kudai warudishiwe mali zao na waendelee kuziuza, na mahakama inakubali hivyo, mie hapa ndipo nachanganyikiwa.
Ila kuna hilo umeandika hapo juu kuhusu mtu kugombea na wanamkatalia kwa gia hajatoka chama cha upinzani. Kwa kweli katika haki za binadamu, hii imekaa ovyo ka maana nyingine Mahakama inatumia uwezo wake KUVUNJA KATIBA BOVU linalotumika hadi leo Tanzania. Hili hata mie niko nao kwa sana. Ila nafikiri Mahakama ilitakiwa kuwatolea UVIVU wabunge na Serikali kwa kuendeleza katiba iliyozeeka na imepitwa na wakati.

Mimi hii ishu ya Ewura siielewi vizuri. Lakini mara nyingi kinachosababisha mahakama kuamua hivi ni kukiukwa na taratibu na watuhumiwa (hapa ni Ewura). Swali ni jee taratibu zilifuatwa na Ewura katika ufungaji wa vituo hivyo? Nikirudi tena Marekani. Kuna kesi nyingi za wazi watuhumiwa wameshinda kwa sababu polisi walikiuka taratibu katika kuwakamata, kuwasachi n.k. Katika demokrasi ni haki ya msingi ya mtuhumiwa kutendewa haki hata kama wengine tunaona ni wazi kuwa amekosa. Walichopaswa kufanya Ewura ni ku-appeal kwa Mahakama ya juu zaidi ambayo ina uwezo wa kubatilisha maamuzi ya Mahakama ya chini yake. Mahakama haiwezi kusema endelea kuuza MAFUTA MACHAFU maana uwezo wa kutambua kati ya mafuta machafu na masafi haina. Inachoweza kusema ni endeleeni kuuza MAFUTA. Kama kweli wanauza mafuta machafu EWURA wangeweza kuwashitaki kwa kuuza mafuta machafu. Lakini kwa kufanya hivi itabidi wathibitishe mahakamani kuwa kweli mafuta wanayouza ni machafu. Tusisahau kuwa mara nyingi tu wafanyakazi wa mamlaka kama hizi wametumia nguvu zao kujinufaisha! Ukikataa kutoa chochote unaambiwa umekiuka sheria zao na kufungiwa biashara yako.

Amandla.............
 
Ni sahihi kabisa Mkuu FM. Kipengele kinachozua mgombea kushiriki uchaguzi kama kibinafsi, kinamnyima mwananchi haki ya msingi. Ila tujue kuwa kipengele hicho kipo na ni sehemu ya Katiba hiyo hiyo. Kipengele kinachoruhusu mtu yeyote kuchaguliwa kikiungana na kipengele kinachotaka mtu huyo awe ametoka katika chama fulani cha siasa chenye usajili wa kisheria, kinafanya vipengele vyote viwe sahihi na kamilifu. Ila, usawa wa wananchi wote kuchaguliwa bila mipaka unapungua kwa kipengele hicho cha pili (mgombea kutoka chama cha siasa).

Katiba ndio sheria kuu kuliko zote hapa nchini. Mahakama, Bunge, Serikali, Taasisi zote na hata wananchi wa kawaida wanatakiwa kuishi Tanzania kikatiba. Hivyo hakuna chombo chochote kilicho juu ya Katiba. Kumbuka, kuna sheria fulani fulani ambazo hutungwa/hurekebishwa na mahakama. Ila sheria hizo zinatakiwa zitungwe/zirekebishwe kwa kuzingatia Katiba ya nchi (Hii ndio sababu Jaji Mkuu wa JMT hana mamlaka katika mahakama za Zanzibar. Kwakuwa wao pia wana Katiba yao).

Endapo itathibitika kuwa sheria zilizotungwa/kurekebishwa na mahakama zinapingana na Katiba, sheria hizo huwa batili mara moja. Mahakama kote duniani (ambapo Katiba hueshimiwa), hufanya kazi zake kwa mujibu wa Katiba. Katiba ndio iliyounda Mahakama, hivyo ni lazima Mahakama pia ziheshimu Katiba.

Hapa tunatofautiana. Pale ambapo Katiba inajichanganya ni wajibu wa Mahakama kutoa TAFSIRI ya kipi kina uzito zaidi. Tofauti na tunavyofikiri, Katiba sio sacrosant. Inarekebishika pale inapoonekana ina mapungufu. Mahakama kwa kusema walichosema imeweka wazi hiyo contradiction ili wahusika wairekebishe!

Amandla.......
 
............Sasa serikali ikimcharukia jaji mkuu ikisema uamuzi huo wa mahakama uliotolewa na huyo jaji wa kuruhusu wagombea binafsi ulikuwa wa ajabu ajabu kwa kuwa ulikiuka katiba inayotaka watu wagombee kupitia vyama itakuwa ni kuingilia uhuru wa mahakama?.........

.......Spika kwanza inabidi aielewe nafasi yake kwa jamii.......he should know to display himself better than anybody!!.........mtu kama yeye anaposema maamuzi ya mahakama ni ya ajabu ajabu........its a dumb thing kutoka kwa mtu kama yeye..........as if hajui mahakama zinafanyeje kazi........sasa yeye ndio anaonyesha kuwa ni mwanasiasa wa ajabu ajabu.........

.......I assume EWURA walikuwa na kila sababu kushinda kesi ile mahakamani ....au?........yaani mtu kavunja sheria umemkamata........jamaa amekata rufaa amekushinda.........halafu EWURA ukukaa kimya.......ndio maana hizi taasisi za serikali zinatakiwa kuwa na wanasheria makini......otherwise wananchi tutaendelea kutaabika sana na kupoteza billions kutokana na UJINGA wa hizi taasisi za serikali...........

......no wonder watu kama akina Mkono, Tenga wanatafuna pesa za bure.........kwa sababu.........incompetence+ufisadi umeenea sana ndani ya serikali yetu...........halafu mijitu mingine (Spika) inasema upuuzi.....damn!!
 
mihimili yote mitatu ni kama ule wimbo maarufu wa ukutu ukuti wa mnazi wa mnazi! wao wanaimba ukuti x2 mwananchi yupo katikati anaitika bila kufahamu maana ya ukuti wa mnazi, WOTE NIWASANII NA ANAYESANIFIWA NI MWANANCHI MLALAHOI
 
Hapa tunatofautiana. Pale ambapo Katiba inajichanganya ni wajibu wa Mahakama kutoa TAFSIRI ya kipi kina uzito zaidi. Tofauti na tunavyofikiri, Katiba sio sacrosant. Inarekebishika pale inapoonekana ina mapungufu. Mahakama kwa kusema walichosema imeweka wazi hiyo contradiction ili wahusika wairekebishe!

Amandla.......

Unadhani nakukatalia Mkuu FM?

Nadhani unajua kuwa Katiba uhaririwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kuchapishwa na ofisi yake. Mwanasheria Mkuu wa Serikali mara kwa mara huwa ni Mjumbe wa Mahakama Maalum ya Katiba (kwa kuwanusu ya wajumbe wake hutoka Serikali ya JMT).

Hivyo Mahakama Maalum ya Katiba inaijua vyema Katiba, na ndicho chombo kinachoitafsiri. Ila Katiba iko wazi katika suala hili. Haina haja ya uchambuzi wa namna ya kumpata mgombea U-Rais au Ubunge kutokana na Katiba (hasa kipengele cha uwakilishi kichama).
 
Katika Mahakama zetu kuna rushwa za kutisha na ni vyema Bunge likajadili mambo haya ili umma uweze kutambua mapungufu katika waangalizi wa sheria.
Mahakimu , Majai na hata wafanyakazi wa Mahakama wamejiteua kuwa miungu watu, na hata pale ambapo kesi zimeamuliwa bado kupata nakala za hukumu ni shida sana na ni kwa rushwa.Mifano hai ipo.
Wale wasio penda suala hili lijadiliwe wanawalakini katika kuelewa mtiririko wa utekelezaji wa sheria.
Hivyo basi nampongeza sana Spika kwa Ujasiri wa kumshika mbogo huyu wa sheria kwa mapembe yake, tukumbuke Spika Sitta ni mwanasheria.
Wwanaompinga sita ni walarushwa.mahakama zetu hadi mahakama kuu rushwa tupu ndio maana ukihoji kidogo kuhusu hukumu fulani mahakama zinachachamaa eti kuingilia uhuru wa mahakama.kunahaja kuwepo na chombo cha kudhibiti mahakama zet hasa za nchi za kiafrika ambapo mahakimu na majaji njaa tupu
 
Back
Top Bottom