Sitta amcharukia Jaji Mkuu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Sitta amcharukia Jaji Mkuu

Stella Nyemenohi, Dodoma
Daily News; Monday,February 09, 2009 @20:04
Wakati Bunge likitarajiwa leo kujibu kauli ya Jaji Mkuu Augustino Ramadhan aliyoitoa wiki iliyopita kuwa chombo hicho kimekuwa kikiingilia mahakama, Spika Samuel Sitta amesema malalamiko yaliyotolewa na jaji hayawezi kunyamaziwa. Amesema Bunge kama taasisi, haliwezi kukaa kimya kwa kuwa suala hilo ni la kikatiba.

Akitoa taarifa hiyo bungeni leo mjini hapa, Sitta alionyesha kulaumu baadhi ya uamuzi ambao umekuwa ukitolewa na mahakama na kusema kwamba unatoa fursa kwa mtu mmoja kuliko jamii nzima, jambo linaloumiza. Alisema wao kama wabunge hawana nia mbaya na mahakama, lakini akatahadharisha kwamba chombo hicho cha sheria, hakina budi kuzingatia kwamba jamii inakiangalia.

"Hapa watasema pia naingilia mahakama…potelea mbali," alisema Sitta bungeni hapo. Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa Bunge, tamko la Bunge litatolewa kesho baada ya kipindi cha maswali na majibu. Akifafanua juu ya kile alichosema baadhi ya uamuzi kuegemea kwa mtu mmoja badala ya jamii, Sitta alitoa mfano kuwa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) iliwahi kukifungia kituo kimoja cha mafuta kwa kuzingatia kanuni zake.

Kwa mujibu wake, matajiri walikwenda mahakamani kupinga uamuzi huo ambao ulikubalika mahakamani na ikaamriwa kifunguliwe. Wiki iliyopita, katika maadhimisho ya Siku ya Sheria, Dar es Salaam, Jaji Mkuu licha ya kutaja Bunge kuingilia mahakama, vile vile alivionya vyombo vya habari kwa kile alichosema kwamba vimeshindwa kutofautisha kati ya maoni na ukweli.

Katika hatua nyingine, Bunge leo jioni liliahirisha kikao chake baada ya Naibu Spika Anne Makinda kugundua kuwa hakuna mtu hata mmoja wa serikali.
 
Last edited:
Malumbano ya Mahakama, Bunge ya nini?
Mhariri
Daily News; Monday,February 09, 2009 @19:58​

Leo, Spika wa Bunge Samuel Sitta aliamua kuanzisha mjadala ambao kwetu sisi tunauona hauna maslahi, tija wala manufaa kwa Watanzania ambao kuna mambo mengi ya msingi ambayo si Bunge tu, bali viongozi wanapaswa kuyafanyia kazi.

Spika Sitta aliamua kujibu, tena kwa maneno ya kejeli ya ‘Potelea mbali', hatua ya mhimili mwingine wa Dola, Mahakama, kulalamikia hatua ya mhimili huo wa Bunge unaoongozwa na Sitta, kuingilia kazi za Mahakama.

"Hapa watasema pia naingilia mahakama…potelea mbali," alisema Sitta bungeni Dodoma leo. Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa Bunge, tamko la Bunge litatolewa leo baada ya kipindi cha maswali na majibu.

Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Sheria Tanzania, Ijumaa iliyopita, Jaji Mkuu wa Tanzania Augustino Ramadhani alieleza kuingiliwa kwa chombo hicho cha kutoa haki na mihimili mingine miwili, yaani Serikali na Bunge.

Jaji Mkuu alieleza hayo kwa kutoa mifano, ikiwamo ya Bunge kusikiliza shauri la Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi na Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima na suala la Sitta kuzungumzia uamuzi wa Mahakama juu ya shauri la vituo vya mafuta mkoani Morogoro.

Jaji Mkuu pia alisema serikali imewahi kuingilia uhuru wa mahakama. Lakini pengine kwa kuwa muungwana, Jaji Mkuu alishauri siku moja mihimili hiyo mitatu ikae pamoja na kuzungumza faragha kwa nia ya kuleta mkabala murua baina yao. Bila shaka, huu ulikuwa ushauri wa busara na wa bure.

Lakini cha kushangaza, ni hatua ya leo ya Spika Sitta kuamua kujibu mapigo bungeni kwa kutetea masuala ambayo yanaonyesha dhahiri kuwa Bunge linataka lisikosolewe. Sisi tungefarijika sana kuona Spika Sitta anakubali ushauri wa Jaji Mkuu wa kukutana kwa wakuu wa mihimili hiyo mitatu na kuzungumza kuona kama kuna tofauti na jinsi ya kuzitatua, lakini siyo kwa kuendeleza malumbano.

Na zaidi, ni jambo la kusikitisha kuwa malumbano hayo yanaendelezwa na Sitta, mwanasheria aliyewahi kuwa Waziri wa Sheria, ambaye anajua kwa undani mamlaka na majukumu ya mihimili mitatu ya Dola. Hatumfundishi Sitta wala Jaji Mkuu wajibu wake, lakini tunaamini ni vyema mihimili hii miwili ya Dola ikafanya kazi zake kwa kuheshimiana na kushirikiana kuliko kulumbana hadharani kama inavyotokea sasa.
 
Last edited:
Lakini cha kushangaza, ni hatua ya leo ya Spika Sitta kuamua kujibu mapigo bungeni kwa kutetea masuala ambayo yanaonyesha dhahiri kuwa Bunge linataka lisikosolewe. Sisi tungefarijika sana kuona Spika Sitta anakubali ushauri wa Jaji Mkuu wa kukutana kwa wakuu wa mihimili hiyo mitatu na kuzungumza kuona kama kuna tofauti na jinsi ya kuzitatua, lakini siyo kwa kuendeleza malumbano.

- Very sad, yaani haya ni maoni ya mhariri wa gazeti maarufu sana kwa taifa, masikini ya Mungu haelewi kwamba ili kupata demokrasia ya kweli kinachotakwia ni malumbano kati ya hivi vyombo vitatu vikuu vya taifa, yaaani Executive, Judicial, na Parliament.

- Kwamba ni katika kulumbana kwa vyombo hivi vitatu kisheria ndio unapata ukweli wa kisheria ambao unatakiwa kuongoza siasa ya taifa, masikini jaji mkuu wala hajui power aliyonayo kisheria, kwamba anatakiwa kusubiri mashitaka dhidi ya serikali na kuifundisha adabu kisheria, hajui kuwa bunge likikosa anatakiwa kulisubiri kwenye sheria na kulipa aadhabu kisheria,

- Matokeo yake ndio haya, Jaji Mkuu badala ya kulumbana rasmi kisheria, yeye anaenda kulalamikia kwenye sherehe, badala ya kuwatuma wanasheria wake kuishitaki bunge kwa kuingilia kesi ya Mengi Vs Malima, yeye anakwenda kulia kwa wananchi wasioelewa hata anachosema ni nini kisheria, na kwa bahati mbaya sana ya kutokuelewa kinachotakiwa baadhi yetu tunamuona huyu jaji kuwa ni shujaaa, na Spika naye knowing kwamba huyu Jaji ni nothing but a coward naye anaigeuza ishu ya kisheria kua politics kwa makusudi mazima, na masikini media yetu na sisi wananchi masikini wa habari muhimu za taifa letu, tunakubali na ku-take sides hata bila kuuliza exactly kinachosemwa ni nini?

Mungu Aibariki Tanzania.
 
jaji akituakikishia RUSHWA IMEISHA KWA MAJAJI ZAKE THEN BUNGE LITAWAACHIA NJE YA HAPO BUNGE KULA MENO!!1
 
Katika hii mihimili mitatu, "unaoongoza kwa ufisadi na watendaji wake kuona mali za wananchi hazina mwenyewe na kuzifuja kama mchwa" ni Serikali(Executive branch), "unaoongoza kwa Rushwa za kubaka haki za raia" ni Mahakama na "Unaoongoza kwa uzembe na ubendera fuata upepo bora liende sisi tupate posho" ni Bunge

Sasa hapa ni kwamba mihimili yote au system nzima ni uozo yaani mfu hawezi kulala tanga la mfu mwenzake
.
 
Inasikitisha sana kuona kuwa sasa Bunge linaanzisha malumbano na Mahakama na kuongeza mkanganyiko wa ziada katika nchi yetu, uliopo kati ya Bunge na Serikali. Katika mikanganyiko yote hii, unakuta kuwa Bunge ndio liko kati kati. Ukiangalia kwa makini utakuta kuwa Bunge, chini ya Spika wa sasa, linataka kufanya kazi zote. Lenyewe liendeshe Serikali, (Issue ya Waziri Mwangunga na Vitalu), Liaendeshe Mahakama (Issue ya Malima na Mengi/ Na pia Kumhukumu Masha kabla Mchakato haujamalizika) na litunge sheria. Hii haiwezekani. Sitta ajikite katika kutunga sheria na awaachie wenzake wafanye kazi zao ama sivyo kuna siku naye atakwama.
 
Last edited:
Katika Mahakama zetu kuna rushwa za kutisha na ni vyema Bunge likajadili mambo haya ili umma uweze kutambua mapungufu katika waangalizi wa sheria.
Mahakimu , Majai na hata wafanyakazi wa Mahakama wamejiteua kuwa miungu watu, na hata pale ambapo kesi zimeamuliwa bado kupata nakala za hukumu ni shida sana na ni kwa rushwa.Mifano hai ipo.
Wale wasio penda suala hili lijadiliwe wanawalakini katika kuelewa mtiririko wa utekelezaji wa sheria.
Hivyo basi nampongeza sana Spika kwa Ujasiri wa kumshika mbogo huyu wa sheria kwa mapembe yake, tukumbuke Spika Sitta ni mwanasheria.
 
Lengo la malumbano haya kwa kipindi hiki yana sababu - kuondoa focus ya wadanganyika kupambana na mafisadi na kusililiza kauli ya serikali kuhusu Richmond, TICS, Kiwira na nyumba za serikali.

Ni strategy kali ya mafisadi kupitia mihimili hii ya dola,

Tukiyumbishwa tukaelekezwa kwenye mambo haya yasiyo na umuhimu kwa sasa kumekwisha
 
Na zaidi, ni jambo la kusikitisha kuwa malumbano hayo yanaendelezwa na Sitta, mwanasheria aliyewahi kuwa Waziri wa Sheria, ambaye anajua kwa undani mamlaka na majukumu ya mihimili mitatu ya Dola. Hatumfundishi Sitta wala Jaji Mkuu wajibu wake, lakini tunaamini ni vyema mihimili hii miwili ya Dola ikafanya kazi zake kwa kuheshimiana na kushirikiana kuliko kulumbana hadharani kama inavyotokea sasa.

Hapo Sitta anazidi kuniacha hoi kwani ni mlolongo mrefu kwake kujifagilia kiaina kwa 2010/15-Namfuatilia kwa karibu sana Mh.Spika ni vijimambo vyake kwa wenzie kuwapiga vishoka vya hapa na pale.
Tunajua anauma na kupuliza huku na kule.
Kila la kheri Mh.Spika Kwani janja yako yote tuaifahamu.
 
Kimsingi na kwa akili ya kawaida kabisa mihimili hii mitatu ipo KINADHARIA tu na sio kwa uhalisia wake. Serikali nzima inaundwa na WABUNGE na RAIS mwenyewe ni sehemu muhimu ya BUNGE lenyewe. Makamu wa Rais peke yake ndiye sio mbunge.
Jaji Mkuu na Majaji wote wanateuliwa na kuapishwa na Rais. KATIBA yetu imeichanganya mihimili kiasi kwamba kuitenganisha na ionekane ni HURU ni kazi ngumu sana. RUSHWA na UFISADI ndio imeitafuna mihimili hii mpaka basi.
 
Mimi nadhani alieanzisha malumbano ni Jaji Mkuu. Yeye kama alitaka kukutana kwa mihimili hiyo mitatu kujadili utendaji na mipaka ya kazi zao, angefanya hivyo kwa kuzingatia kanuni na taratibu za kiutendaji ambazo zipo bayana. Hakuwa na haja ya kutangazia umma kupitia kwenye sherehe yao ya siku ya Sheria. Spika Sitta alichofanya ni kuelezea anavyoona mambo yakitendeka katika maamuzi ya Mahakama na kutoa maoni kuwa hali hiyo sio sawa. Spika angedharau suala hilo na kuliachia lielee kama baadhi ya wachangiaji hapa wanavyotaka, asingekuwa tu anadhalilisha chombo hicho cha utungeji wa sheria anachokiongoza, bali pia angekuwa ameshindwa kukitetea, kukilinda na kukiongoza.

Wakuu, Katiba ya nchi hairuhusu kauli yoyote ya Mbunge (iliyotolewa Bungeni) kufunguliwa mashitaka mahakamani. Kwahiyo sulala la Mahakama kuishitaki Bunge haipo.

Mahakama ndicho chombo pekee katika mihimili hii mitatu ambacho hakina control yoyote. Hakuna mahali katika Katiba yetu inapoelezea hatua zozote zinazoweza kuchukuliwa endapo Mahakama itakosea, kama Taasisi. Hivyo nadhani ni jukumu la Bunge ambalo hutunga sheria zitumikazo mahakamani kutetea sheria hizo. Endapo Bunge halitafanya hivyo, ni dhahiri kuwa wananchi wataendelea kununua haki kila wakati. Mahakama ni chombo muhimu sana. Hakiwezi kuachiwa kutenda bila mtu yeyote kuelezea maoni yake, au kukikosoa. Utaratibu huo ndio unaofifisha haki hapa nchini. Bila control, hakuna system inayoweza kufanya kazi.

Bunge pia, inabidi kutenda haki kwa Serikali na Mahakama. Serikali na Bunge vinatakiwa kuzingatia mipaka yao kiutendaji ili kuepusha muingiliano usio wa lazima. Hatua inayoendelea sasa, ni matokeo ya kushindwa kuvumiliana yaliyoanza muda mrefu sana. Sasa umefika wakati wa kusema yote kwa manufaa ya Taifa letu.

Kama Bunge lisiposema, nani atakaesema? Walau wao wana kinga wanapokuwa ndani ya BUNGE.
 
malumbano baina ya taasisi hizi kuu tatu ni muhimu ili kuweza kuweka accountability bora zaidi.
Naamini Samwel Sitta as a good lawyer knows whta he is doing.
Am just looking forward to hearing what they have to say!
 
malumbano baina ya taasisi hizi kuu tatu ni muhimu ili kuweza kuweka accountability bora zaidi.
Naamini Samwel Sitta as a good lawyer knows whta he is doing.
Am just looking forward to hearing what they have to say!

- Walitakiwa wakalumbane kisheria sio mtaani kama wanavyofanya sasa, Jaji Mkuu hajui kuwa politically anacheza mikononi mwa Spika, dawa ni kwa Jaji Mkuu kununua kesi against bunge na kuwafundisha adabu, lakini as long as wanarushiana hizi nyepesi nyepesi mtaaani Spika anakuwa mshindi, na in the end huyu Jaji ataondolewa kwa sababu hapa ameingilia mwenyewe siasa asizozijua,

- Ushauri wa bure kwa Jaji Mkuu, nunua kesi dhidi ya bunge, watwange kama una beef na bunge kisheria, basi tafuta mwananchi wa kulishitaki bunge kwenye sheria then inunue kesi kwa kudai kuwa inahitaji Constitutional explainations kutoka kwako, na watwange kisawa sawa lakini hizi filimbi za mtaani watakutosa tu! kwa sababu kumbuka inapotokea ishus kama hizi zinazotishia mlo wao huungana na kuwa kitu kimoja next thing wanakutosa nje!
 
Muhimili wa Mahakama uonyeshe ubora wake kwa vitendo na si kunung'unika kwani kila Mtanzania anaona yanayotendeka katika Mahakama zetu.Kumekuwa na hukumu nyingi za wazi za kupendelea watu mmoja mmoja wenye uwezo kifedha.Hukumu hizo zimekuwa zikiwanyima haki watu wengi kwa kuwa tu uwezo wao wa kuwalipa mawakili wa kutafuta kupindisha sheria hawana,na uozo huo wa mahakama zetu umesababisha hata mawakili kuwa wafanyabiashara ya sheria badala ya wataomsaada wa kisheria.Rushwa mahakamani imekidhiri pamoja na kuwa wamekuwa wakikamatwa mahakimu wa mahakama za mwanzo lakini papa wa rushwa kubwa yaani baadhi ya majaji na mahakimu wakazi wanaendelea kutamba.Kazi kwako jaji mkuu safisha mahakama badala ya kulalamika.
 
Katika hii mihimili mitatu, "unaoongoza kwa ufisadi na watendaji wake kuona mali za wananchi hazina mwenyewe na kuzifuja kama mchwa" ni Serikali(Executive branch), "unaoongoza kwa Rushwa za kubaka haki za raia" ni Mahakama na "Unaoongoza kwa uzembe na ubendera fuata upepo bora liende sisi tupate posho" ni Bunge

Sasa hapa ni kwamba mihimili yote au system nzima ni uozo yaani mfu hawezi kulala tanga la mfu mwenzake
.

Ni uozo mtupu, lakini bora bunge - humo kuna baadhi ya watu makini.
 
- Very sad, yaani haya ni maoni ya mhariri wa gazeti maarufu sana kwa taifa, masikini ya Mungu haelewi kwamba ili kupata demokrasia ya kweli kinachotakwia ni malumbano kati ya hivi vyombo vitatu vikuu vya taifa, yaaani Executive, Judicial, na Parliament.- Kwamba ni katika kulumbana kwa vyombo hivi vitatu kisheria ndio unapata ukweli wa kisheria ambao unatakiwa kuongoza siasa ya taifa, masikini jaji mkuu wala hajui power aliyonayo kisheria, kwamba anatakiwa kusubiri mashitaka dhidi ya serikali na kuifundisha adabu kisheria, hajui kuwa bunge likikosa anatakiwa kulisubiri kwenye sheria na kulipa aadhabu kisheria,

- Matokeo yake ndio haya, Jaji Mkuu badala ya kulumbana rasmi kisheria, yeye anaenda kulalamikia kwenye sherehe, badala ya kuwatuma wanasheria wake kuishitaki bunge kwa kuingilia kesi ya Mengi Vs Malima, yeye anakwenda kulia kwa wananchi wasioelewa hata anachosema ni nini kisheria, na kwa bahati mbaya sana ya kutokuelewa kinachotakiwa baadhi yetu tunamuona huyu jaji kuwa ni shujaaa, na Spika naye knowing kwamba huyu Jaji ni nothing but a coward naye anaigeuza ishu ya kisheria kua politics kwa makusudi mazima, na masikini media yetu na sisi wananchi masikini wa habari muhimu za taifa letu, tunakubali na ku-take sides hata bila kuuliza exactly kinachosemwa ni nini?

Mungu Aibariki Tanzania.

Mungu ibariki Tanzania na WATU WAKE
Inaonyesha ni tabia yetu Watanzania kuendeleza malumbano yasiyo na maana. Malumbano na majadiliano ni vitu viwili tofauti. Spika wa Bunge analunbana na Jaji Mkuu na gazeti linajadili malumbano badala ya sisi kujadili malumbano tunaanza kulumbana na Gazeti. Mkuu kwa heshima zote naomba kupingana nawe katika kulimbana na yalioandikwa kweye Gazeti kwani nahisi mhariri hakuwa akilumbana na mmojawapo bali akitowa ushauri.
Pengine angetaka kulumbana na Spika angetumia mansno machache tu. 'Kwani hizo sheria anaezitunga ni nani? na mahakama kazi yake ni nini?

Sioni haja ya kudharau ushauri wa mtu bali ni vyema kuujadili ili kuona una faida au la
 
sikutegemea kauli kama hii kutoka kwa spika mwanasheria mbobevu na wakili kuitoa hadharani tena kwa kejeli....nafikiri hii nchi kwa sasa haina utawala wa sheria... POWER CORRUPTS BUT ABSOLUTE POWER CORRUPT absolutely
 
Malumbano ya Mahakama, Bunge ya nini?
Mhariri
Daily News; Monday,February 09, 2009 @19:58

Leo, Spika wa Bunge Samuel Sitta aliamua kuanzisha mjadala ambao kwetu sisi tunauona hauna maslahi, tija wala manufaa kwa Watanzania ambao kuna mambo mengi ya msingi ambayo si Bunge tu, bali viongozi wanapaswa kuyafanyia kazi.

Spika Sitta aliamua kujibu, tena kwa maneno ya kejeli ya ‘Potelea mbali', hatua ya mhimili mwingine wa Dola, Mahakama, kulalamikia hatua ya mhimili huo wa Bunge unaoongozwa na Sitta, kuingilia kazi za Mahakama.

"Hapa watasema pia naingilia mahakama…potelea mbali," alisema Sitta bungeni Dodoma leo. Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa Bunge, tamko la Bunge litatolewa leo baada ya kipindi cha maswali na majibu.




Hapa Mh. Spika tayari amekwisha pre-empty tamko la bunge, maana amelisemea msimamo bunge kabla halijatoa tamko, kazi ipo!
 
Mimi nadhani alieanzisha malumbano ni Jaji Mkuu. Yeye kama alitaka kukutana kwa mihimili hiyo mitatu kujadili utendaji na mipaka ya kazi zao, angefanya hivyo kwa kuzingatia kanuni na taratibu za kiutendaji ambazo zipo bayana. Hakuwa na haja ya kutangazia umma kupitia kwenye sherehe yao ya siku ya Sheria. Spika Sitta alichofanya ni kuelezea anavyoona mambo yakitendeka katika maamuzi ya Mahakama na kutoa maoni kuwa hali hiyo sio sawa. Spika angedharau suala hilo na kuliachia lielee kama baadhi ya wachangiaji hapa wanavyotaka, asingekuwa tu anadhalilisha chombo hicho cha utungeji wa sheria anachokiongoza, bali pia angekuwa ameshindwa kukitetea, kukilinda na kukiongoza.

Wakuu, Katiba ya nchi hairuhusu kauli yoyote ya Mbunge (iliyotolewa Bungeni) kufunguliwa mashitaka mahakamani. Kwahiyo sulala la Mahakama kuishitaki Bunge haipo.

Mahakama ndicho chombo pekee katika mihimili hii mitatu ambacho hakina control yoyote. Hakuna mahali katika Katiba yetu inapoelezea hatua zozote zinazoweza kuchukuliwa endapo Mahakama itakosea, kama Taasisi. Hivyo nadhani ni jukumu la Bunge ambalo hutunga sheria zitumikazo mahakamani kutetea sheria hizo. Endapo Bunge halitafanya hivyo, ni dhahiri kuwa wananchi wataendelea kununua haki kila wakati. Mahakama ni chombo muhimu sana. Hakiwezi kuachiwa kutenda bila mtu yeyote kuelezea maoni yake, au kukikosoa. Utaratibu huo ndio unaofifisha haki hapa nchini. Bila control, hakuna system inayoweza kufanya kazi.

Bunge pia, inabidi kutenda haki kwa Serikali na Mahakama. Serikali na Bunge vinatakiwa kuzingatia mipaka yao kiutendaji ili kuepusha muingiliano usio wa lazima. Hatua inayoendelea sasa, ni matokeo ya kushindwa kuvumiliana yaliyoanza muda mrefu sana. Sasa umefika wakati wa kusema yote kwa manufaa ya Taifa letu.

Kama Bunge lisiposema, nani atakaesema? Walau wao wana kinga wanapokuwa ndani ya BUNGE.

Pamoja na kukubaliana nawe kuwa haikustahili kwa Jaji Mkuu kutumia njia aliyotumia lakini tunavyoelewa kuwa uongozi ni busara na sio jazba na kejeli.
Sawa Spika amemkejeli Jaji Mkuu kwa kutekeleza yale ambayo yeye Sitta na Wenzake wameyatunga na kuyakabidhi kwa Jaji mkuu ayatekeleze nani mkosa hapa. Huyu alieyetekeleza yale aliyoambiwa ayatekeleze au yule aliyoyatunga na kuamrisha yatekelezwe?
Aidha ubabe ndio kigezo cha uongozi? Sitta anakurupika kwa ubabe huku tukijuwa kuwa huyu Bwana ndiye mwenye wajibu wa kututungia sheria zitakazotulinda sisi hana uwezo wa kurekebisha makosa anapokumbushwa,sasa wananchi tukimbilie wapi?
Ninachoona mimi ni kuwa huyu Mzee sasa anaelekea katika udikteta na kujichukulia maamuzi mikonono mwake. Tuangalie mifano kule Zanzibar Wajumbe wa Baraza kutoka upinzani kila wanapofukuzwa Barazani hukimbilia mahakamani na juu ya siasa za kule hawa wajumbe hushinda na Spika hutekeleza maagizo ya mahakama. Sitta hakuwa na haja ya kutumia lugha ya kejeli kwani kwa upande mmoja yeye ana uwezo wa kuzuia au kurekebisha hayo anayoona kuwa ni mapungufu kwa kufuata SHERIA NA KATIBA au anataka tuelewe kwa vile yeye ni kiongozi wa kutunga sheria basi habanwi na sheria? Do we need to read between the lines ili kufahamu nini Jaji Mkuu anakisema?
 
Back
Top Bottom