Watanzania
JF-Expert Member
- Jul 7, 2009
- 727
- 42
Picha sasa inaonyesha wazi kuwa Spika mstaafu Mh. Sitta aliondolewa uspika na CCM ili kujaribu kuruhusu ulipwaji wa Dowans ambayo ilirithi mkataba wa kampuni feki ya Richmond. Kwa vyovyote vile Serikali ya kifisadi ya CCM ilimwona Sitta kama kikwazo kwa sababu angeruhusu bunge kuhoji nyendo zozote za Serikali kujaribu kuwatwisha mzigo wananchi wa Tanzania kuwalipa mafisadi wa Dowans. Kwa vile Richmond ilipata mkataba wa rushwa na kampuni yenyewe kuwa feki, bunge la Sitta lingeshainyoshea kidole Serikali na kuikumbusha kuwa Lowasa, Karamagi na Msabaha walijiuzuru kwa kashfa ya Richmond ambayo imerithiwa na Dowans.
Sasa CCM isuburi tu kuona kwa vitendo jinsi watanzania walivyochoka na utawala mbovu wa CCM Mafisadi maana Spika wa sasa yuko usingizini. Hasemi chochote kupinga mafisadi wa CCM kupitia Dowans wanaotaka kuendeleza utumwa wa watanzania. Sitta endeleza mapambano na mafisadi wa Dowans, sisi watanzania tuko tayari kwa lolote, tumechoka kubeba mizigo ya mafisadi wa CCM.
Sasa CCM isuburi tu kuona kwa vitendo jinsi watanzania walivyochoka na utawala mbovu wa CCM Mafisadi maana Spika wa sasa yuko usingizini. Hasemi chochote kupinga mafisadi wa CCM kupitia Dowans wanaotaka kuendeleza utumwa wa watanzania. Sitta endeleza mapambano na mafisadi wa Dowans, sisi watanzania tuko tayari kwa lolote, tumechoka kubeba mizigo ya mafisadi wa CCM.