Sitta akubali kuhusishwa na CCJ: "Mimi ni mtaji wa Urais"

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Tuesday, 17 May 2011 23:03

Ramadhan Semtawa

SIKU moja baada ya kurushiwa kombora la kutaka kukihama CCM na kuanzisha kilichokuwa Chama Cha Jamii (CCJ), Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amesema yeye ni mtaji wa kisiasa na ndiyo maana amekuwa akifuatwa na vyama mbalimbali vikimhitaji ajiunge navyo kuwania urais.Akizungumza kwa simu jana, Waziri Sitta alisema si CCJ tu, bali alifuatwa na vyama vingine ambavyo kwa ukomavu wa kisiasa hawezi kuvitaja ambavyo baadhi, vilimtaka agombee nafasi hiyo ya urais mwaka jana.

Sitta alisema ni kawaida kwa mwanasiasa mwenye mvuto kufuatwa na vyama vingine vya siasa kwa ajili ya kujiunga navyo na kusema: "Sasa cha ajabu nini kwa CCJ? Mimi ni mtaji wa kisiasa bwana!"

"Katika demokrasia ya vyama vingi mazungumzo ya kisiasa ni kitu cha kawaida sana na hakuna cha ajabu hapo."
"Sasa kuanza kusema huyu fulani alikuwa hivi na mwingine vile kisiasa haipendezi, haya mazungumzo ya kisiasa yanaendelea kila siku hata sasa hivi unaweza kukuta wapo watu wanaendelea na mazungumzo. Sasa hii ya huyu bwana (Mpendazoe) inashangaza na kusikitisha."

Alifafanua kwamba mtu anapofanya mazungumzo ya kisiasa kama kutaka kujiunga na chama kingine na kisha akaghairi, anakuwa ameangalia mambo mengi ya msingi ikiwamo wakati na kuongeza kwamba mazungumzo ya kisiasa na kuanzisha chama ni vitu viwili tofauti.
"Ndiyo maana siwezi kusema kwamba siwezi kufikiria uamuzi huo au la. Haya ni mambo ya kisiasa unaangalia mambo mengi ya msingi, sitakiwi kujifunga kwamba siwezi kufanya hivi au la," alisema Sitta.

Akizungumzia uamuzi wa Mpendazoe kuamua kuwataja majina kwamba alishiriki katika kuanzisha CCJ, Sita alisema: "Huyu bwana amenishangaza sana. Nadhani amekasirishwa na sisi kukataa ushauri wake... Mwanasiasa makini hawezi kupata umaarufu kwa njia hii. Katika siasa watu hawasemi kama alivyosema."
Sitta alisema yeye ni mtaji wa kisiasa hata ndani ya CCM na anajivunia kwamba mabadiliko wanayotaka ndani ya chama hicho sasa yanawezekana.Aliwataka wanasiasa kujadili mambo ya msingi ya maendeleo kuliko kuanza kuzungumza mambo binafsi... "Kama ikiendelea hivyo, tunaweza kuumbuana sana."Alisema alijiunga na TANU Oktoba 3, 1960 hivyo uamuzi wowote wa kuhama CCM anapaswa kuufanya kwa umakini mkubwa.

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCJ anena
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCJ, Renatus Muabhi ameelezea kushangazwa kwake na hatua ya Mpendazoe kuibuka na hoja hiyo sasa wakati chama chenyewe kimeshakufa.

Mbali ya Muabhi, mwanasheria maarufu nchini na kada mwandamizi wa NCCR Mageuzi, Dk Sengondo Mvungi naye ameibeza hoja hiyo ya kada huyo wa zamani wa CCM.

Muabhi alisema jambo la CCJ sasa hivi halipo kwani chama chenyewe kimekufa na kuhoji mantiki ya kuanzisha hoja hiyo katika kipindi hiki huku akisisitiza kamwe hawezi kuanza kuibuka na kuzungumzia kitu kisichokuwapo... "Hicho chama chenyewe hakipo, sasa kuanza kuzungumzia CCJ maana yake nini?

Dk Mvungi na Katiba CCJ
Dk Mvungi ambaye amekuwa akidaiwa kuwa ndiye aliyeandika katiba ya CCJ, alisema kamwe hajawahi kupewa kazi hiyo huku akisisitiza: "Loh! Kama ningepewa kazi hiyo si ningefurahi. Si unajua sisi Watanzania mtu akifanya kitu anaanza kutangaza ni mimi ndiyo nimefanya."
Dk Mvungi alisema kamwe hakuwahi kuandika katiba hiyo ya CCJ huku naye akisisitiza: "Lakini, hivi kweli ni hoja kwa sasa kujadili CCJ ambayo imekufa? Tunapaswa kuangalia mambo ya msingi ya sasa, si yasiyokuwepo," Alisema Watanzania wanapaswa kuangalia jinsi CCM kinavyobomoka sasa hivi na si kuangalia kipindi hicho cha CCJ ambacho chama hicho tawala kiliweza kujipanga na kunusurika na mpasuko huo.
"Sasa hivi CCM ndiyo inabomoka. Hapa ndipo Watanzania walipaswa kupaangalia lakini kuanza kusema huyu alikuwa CCJ, chama chenyewe hakipo, kweli hilo ni jambo la msingi kulizungumzia?" Alihoji Dk Mvungi.

Alisema sasa hivi Rais Jakaya Kikwete, ametangaza chama kujivua gamba kitu ambacho alisema Watanzania wanapaswa kuonyesha mshikamano kwa kuhakikisha kinafanikiwa ili kuona watu wasio na madili wanang'oka.

Nape: Nendeni kwa Msajili
Kwa upande wake, Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa CCM, Nape Nnauye amewaambia wale wanaotaka kujua waanzilishi wa CCJ waende Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye ana rekodi zote.

Juzi, katika mkutano wake alioufanya Njombe, Mpendazoe aliwataja Sitta, Nnauye na makada wengine wa CCM kwamba walikuwa waanzilishi wa CCJ lakini waliwasaliti Watanzania ili wapate vyeo ndani ya Serikali ya Rais Kikwete.
 
Jamaa mmoja kwenye comments za gazeti la Mwananchi kwenye hii habari kasema :
yusuf 2011-05-18 00:41 Mh Sita umekuwa mwungwana kukubali bila ubishi kuwa ulishiriki kuasisi CCJ,maana yake uliwahi kumkana Rais wako ukiwa kiongozi.Unasubiri nini CCM?Kwamba wewe ni mtaji wa CCM na Mh JK, si kweli!Wewe ni mzigo mkubwa CCM.Kumbuka hotuba ya Rais kwenye semina elekezi Dodoma.Umepingana mara nyingi na serikali.Huna uwajibikaji wa pamoja.Unapenda sifa binafsi.Wenye akili wakakutosa kwenye uspika.Enzi zako za uspika ulizima hoja ya RICHMOND kiubabe,sasa imekula kwako.

My take: Ni mtaji au mzigo kwa wa chama cha magamba ? Karibuni tujadili.

Quote
 
Namheshimu sana Sitta, kipindi chake akiwa spika alijitahidi sana kutokuwa bias bungeni. Bunge lilikuwa huru, siyo kama sasa hivi! Anaonyesha ni mtu anayependa mabadiliko, ila chama chake tu ndiyo kinachomwangusha
 
Mara nyingi ukipingana na (wavua magamba mti uleule)kisiasa unakuwa mzigo kinachosubiriwa ni muda tuu wa kutua mzigo wenyewe!
 
Hii sasa ndiyo siasa siyo bwana mdogo Nape naanza ooh ulizeni ilikufaje, mara nenda kwa msajili wa vyama ukitaka kujua waanzilishik ni nani mara ntawajibika...... just endless stories na ndiyo maana hata hao waandishi hawaishi kuuliza jambo hilo Nape need to stand up and just say yes nilishiriki so what? Kuchengesha chengesha kunamfanya aonekana kuna kitu anakwepa au anaogopa life beyond that piece.
 
kwa hili six ameonyesha ukomavu wa kisiasa sio kurukaruka ka anavyofanya Nape, nape anahitaji kujifunza he has a lot to learn isije akawa illeterate
 
Kila nikiziona hizo herufi za CCJ naanza kucheka. Sijui kwa nini tu lol

hahahaha....kuna watu huku walikurupuka nayo...hadi kuishia kuikashifu Chadema! Kumbe wanaingizwa mjini na mchezo wa kuiga!
Anyways....Ilionyesha true colours za watu wengi kweli humu!
 
Tuesday, 17 May 2011 23:03

Ramadhan Semtawa

SIKU moja baada ya kurushiwa kombora la kutaka kukihama CCM na kuanzisha kilichokuwa Chama Cha Jamii (CCJ), Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amesema yeye ni mtaji wa kisiasa na ndiyo maana amekuwa akifuatwa na vyama mbalimbali vikimhitaji ajiunge navyo kuwania urais.Akizungumza kwa simu jana, Waziri Sitta alisema si CCJ tu, bali alifuatwa na vyama vingine ambavyo kwa ukomavu wa kisiasa hawezi kuvitaja ambavyo baadhi, vilimtaka agombee nafasi hiyo ya urais mwaka jana.

Sitta alisema ni kawaida kwa mwanasiasa mwenye mvuto kufuatwa na vyama vingine vya siasa kwa ajili ya kujiunga navyo na kusema: "Sasa cha ajabu nini kwa CCJ? Mimi ni mtaji wa kisiasa bwana!"

"Katika demokrasia ya vyama vingi mazungumzo ya kisiasa ni kitu cha kawaida sana na hakuna cha ajabu hapo."
"Sasa kuanza kusema huyu fulani alikuwa hivi na mwingine vile kisiasa haipendezi, haya mazungumzo ya kisiasa yanaendelea kila siku hata sasa hivi unaweza kukuta wapo watu wanaendelea na mazungumzo. Sasa hii ya huyu bwana (Mpendazoe) inashangaza na kusikitisha."

Alifafanua kwamba mtu anapofanya mazungumzo ya kisiasa kama kutaka kujiunga na chama kingine na kisha akaghairi, anakuwa ameangalia mambo mengi ya msingi ikiwamo wakati na kuongeza kwamba mazungumzo ya kisiasa na kuanzisha chama ni vitu viwili tofauti.
"Ndiyo maana siwezi kusema kwamba siwezi kufikiria uamuzi huo au la. Haya ni mambo ya kisiasa unaangalia mambo mengi ya msingi, sitakiwi kujifunga kwamba siwezi kufanya hivi au la," alisema Sitta.

Akizungumzia uamuzi wa Mpendazoe kuamua kuwataja majina kwamba alishiriki katika kuanzisha CCJ, Sita alisema: "Huyu bwana amenishangaza sana. Nadhani amekasirishwa na sisi kukataa ushauri wake... Mwanasiasa makini hawezi kupata umaarufu kwa njia hii. Katika siasa watu hawasemi kama alivyosema."
Sitta alisema yeye ni mtaji wa kisiasa hata ndani ya CCM na anajivunia kwamba mabadiliko wanayotaka ndani ya chama hicho sasa yanawezekana.Aliwataka wanasiasa kujadili mambo ya msingi ya maendeleo kuliko kuanza kuzungumza mambo binafsi... "Kama ikiendelea hivyo, tunaweza kuumbuana sana."Alisema alijiunga na TANU Oktoba 3, 1960 hivyo uamuzi wowote wa kuhama CCM anapaswa kuufanya kwa umakini mkubwa.

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCJ anena
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCJ, Renatus Muabhi ameelezea kushangazwa kwake na hatua ya Mpendazoe kuibuka na hoja hiyo sasa wakati chama chenyewe kimeshakufa.

Mbali ya Muabhi, mwanasheria maarufu nchini na kada mwandamizi wa NCCR Mageuzi, Dk Sengondo Mvungi naye ameibeza hoja hiyo ya kada huyo wa zamani wa CCM.

Muabhi alisema jambo la CCJ sasa hivi halipo kwani chama chenyewe kimekufa na kuhoji mantiki ya kuanzisha hoja hiyo katika kipindi hiki huku akisisitiza kamwe hawezi kuanza kuibuka na kuzungumzia kitu kisichokuwapo... "Hicho chama chenyewe hakipo, sasa kuanza kuzungumzia CCJ maana yake nini?

Dk Mvungi na Katiba CCJ
Dk Mvungi ambaye amekuwa akidaiwa kuwa ndiye aliyeandika katiba ya CCJ, alisema kamwe hajawahi kupewa kazi hiyo huku akisisitiza: "Loh! Kama ningepewa kazi hiyo si ningefurahi. Si unajua sisi Watanzania mtu akifanya kitu anaanza kutangaza ni mimi ndiyo nimefanya."
Dk Mvungi alisema kamwe hakuwahi kuandika katiba hiyo ya CCJ huku naye akisisitiza: "Lakini, hivi kweli ni hoja kwa sasa kujadili CCJ ambayo imekufa? Tunapaswa kuangalia mambo ya msingi ya sasa, si yasiyokuwepo," Alisema Watanzania wanapaswa kuangalia jinsi CCM kinavyobomoka sasa hivi na si kuangalia kipindi hicho cha CCJ ambacho chama hicho tawala kiliweza kujipanga na kunusurika na mpasuko huo.
"Sasa hivi CCM ndiyo inabomoka. Hapa ndipo Watanzania walipaswa kupaangalia lakini kuanza kusema huyu alikuwa CCJ, chama chenyewe hakipo, kweli hilo ni jambo la msingi kulizungumzia?" Alihoji Dk Mvungi.

Alisema sasa hivi Rais Jakaya Kikwete, ametangaza chama kujivua gamba kitu ambacho alisema Watanzania wanapaswa kuonyesha mshikamano kwa kuhakikisha kinafanikiwa ili kuona watu wasio na madili wanang'oka.

Nape: Nendeni kwa Msajili
Kwa upande wake, Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa CCM, Nape Nnauye amewaambia wale wanaotaka kujua waanzilishi wa CCJ waende Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye ana rekodi zote.

Juzi, katika mkutano wake alioufanya Njombe, Mpendazoe aliwataja Sitta, Nnauye na makada wengine wa CCM kwamba walikuwa waanzilishi wa CCJ lakini waliwasaliti Watanzania ili wapate vyeo ndani ya Serikali ya Rais Kikwete.


Ukisikia upunguani wa akili basi ndio huu. Kwamba CCJ ilishakufa na hakuna umuhimu wa kuijadili sijadhani kama ni sahihi. Julius Kambarage Nyerere, Jomo Kenyata, George Washngton, Osama Bin Laden, DECI, NASACO, UDA nk ni baadhi ya watu na taasisi zilizokufa siku nyingi lakini hadi leo vinajadiliwa kwa sababu vimeleta impact katika historia ya maisha yetu hapa duniani iwe kisasa, kiuchumi na kijamaa.

Hivyo si sahihi tusiijadili CCJ eti kwa sababu ilishakufa. Ni lazima tuijadili kwa sababu ilichukua muda wetu mwingi kuijadili ikituhadaa kwamba yenyewe ndio mkombozi wa kweli kumbe wapi. Tukifumbia macho mambo yaliyopita ndio chanzo ya kujirudia mambo kama hayio..

Nimemaliza..
 
Kazi nzuri aliyoifanya Sita akiwa Spika haina ubishi kwa wapenda uwazi, ukweli na maendeleo. Ametuamsha na matunda yake yanaonekana na anayebisha siyo kwamba hajui bali ni mbinafsi tu, period. Kila binadamu ana mapungufu yake kwani hakuna binadamu mwenye sifa ya Malaika.
 
Tuesday, 17 May 2011 23:03

Ramadhan Semtawa

SIKU moja baada ya kurushiwa kombora la kutaka kukihama CCM na kuanzisha kilichokuwa Chama Cha Jamii (CCJ), Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amesema yeye ni mtaji wa kisiasa na ndiyo maana amekuwa akifuatwa na vyama mbalimbali vikimhitaji ajiunge navyo kuwania urais.Akizungumza kwa simu jana, Waziri Sitta alisema si CCJ tu, bali alifuatwa na vyama vingine ambavyo kwa ukomavu wa kisiasa hawezi kuvitaja ambavyo baadhi, vilimtaka agombee nafasi hiyo ya urais mwaka jana.

Sitta alisema ni kawaida kwa mwanasiasa mwenye mvuto kufuatwa na vyama vingine vya siasa kwa ajili ya kujiunga navyo na kusema: "Sasa cha ajabu nini kwa CCJ? Mimi ni mtaji wa kisiasa bwana!"

"Katika demokrasia ya vyama vingi mazungumzo ya kisiasa ni kitu cha kawaida sana na hakuna cha ajabu hapo."
"Sasa kuanza kusema huyu fulani alikuwa hivi na mwingine vile kisiasa haipendezi, haya mazungumzo ya kisiasa yanaendelea kila siku hata sasa hivi unaweza kukuta wapo watu wanaendelea na mazungumzo. Sasa hii ya huyu bwana (Mpendazoe) inashangaza na kusikitisha."

Alifafanua kwamba mtu anapofanya mazungumzo ya kisiasa kama kutaka kujiunga na chama kingine na kisha akaghairi, anakuwa ameangalia mambo mengi ya msingi ikiwamo wakati na kuongeza kwamba mazungumzo ya kisiasa na kuanzisha chama ni vitu viwili tofauti.
"Ndiyo maana siwezi kusema kwamba siwezi kufikiria uamuzi huo au la. Haya ni mambo ya kisiasa unaangalia mambo mengi ya msingi, sitakiwi kujifunga kwamba siwezi kufanya hivi au la," alisema Sitta.

Akizungumzia uamuzi wa Mpendazoe kuamua kuwataja majina kwamba alishiriki katika kuanzisha CCJ, Sita alisema: "Huyu bwana amenishangaza sana. Nadhani amekasirishwa na sisi kukataa ushauri wake... Mwanasiasa makini hawezi kupata umaarufu kwa njia hii. Katika siasa watu hawasemi kama alivyosema."
Sitta alisema yeye ni mtaji wa kisiasa hata ndani ya CCM na anajivunia kwamba mabadiliko wanayotaka ndani ya chama hicho sasa yanawezekana.Aliwataka wanasiasa kujadili mambo ya msingi ya maendeleo kuliko kuanza kuzungumza mambo binafsi... "Kama ikiendelea hivyo, tunaweza kuumbuana sana."Alisema alijiunga na TANU Oktoba 3, 1960 hivyo uamuzi wowote wa kuhama CCM anapaswa kuufanya kwa umakini mkubwa.

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCJ anena
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCJ, Renatus Muabhi ameelezea kushangazwa kwake na hatua ya Mpendazoe kuibuka na hoja hiyo sasa wakati chama chenyewe kimeshakufa.

Mbali ya Muabhi, mwanasheria maarufu nchini na kada mwandamizi wa NCCR Mageuzi, Dk Sengondo Mvungi naye ameibeza hoja hiyo ya kada huyo wa zamani wa CCM.

Muabhi alisema jambo la CCJ sasa hivi halipo kwani chama chenyewe kimekufa na kuhoji mantiki ya kuanzisha hoja hiyo katika kipindi hiki huku akisisitiza kamwe hawezi kuanza kuibuka na kuzungumzia kitu kisichokuwapo... "Hicho chama chenyewe hakipo, sasa kuanza kuzungumzia CCJ maana yake nini?

Dk Mvungi na Katiba CCJ
Dk Mvungi ambaye amekuwa akidaiwa kuwa ndiye aliyeandika katiba ya CCJ, alisema kamwe hajawahi kupewa kazi hiyo huku akisisitiza: "Loh! Kama ningepewa kazi hiyo si ningefurahi. Si unajua sisi Watanzania mtu akifanya kitu anaanza kutangaza ni mimi ndiyo nimefanya."
Dk Mvungi alisema kamwe hakuwahi kuandika katiba hiyo ya CCJ huku naye akisisitiza: "Lakini, hivi kweli ni hoja kwa sasa kujadili CCJ ambayo imekufa? Tunapaswa kuangalia mambo ya msingi ya sasa, si yasiyokuwepo," Alisema Watanzania wanapaswa kuangalia jinsi CCM kinavyobomoka sasa hivi na si kuangalia kipindi hicho cha CCJ ambacho chama hicho tawala kiliweza kujipanga na kunusurika na mpasuko huo.
"Sasa hivi CCM ndiyo inabomoka. Hapa ndipo Watanzania walipaswa kupaangalia lakini kuanza kusema huyu alikuwa CCJ, chama chenyewe hakipo, kweli hilo ni jambo la msingi kulizungumzia?" Alihoji Dk Mvungi.

Alisema sasa hivi Rais Jakaya Kikwete, ametangaza chama kujivua gamba kitu ambacho alisema Watanzania wanapaswa kuonyesha mshikamano kwa kuhakikisha kinafanikiwa ili kuona watu wasio na madili wanang'oka.

Nape: Nendeni kwa Msajili
Kwa upande wake, Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa CCM, Nape Nnauye amewaambia wale wanaotaka kujua waanzilishi wa CCJ waende Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye ana rekodi zote.

Juzi, katika mkutano wake alioufanya Njombe, Mpendazoe aliwataja Sitta, Nnauye na makada wengine wa CCM kwamba walikuwa waanzilishi wa CCJ lakini waliwasaliti Watanzania ili wapate vyeo ndani ya Serikali ya Rais Kikwete.

CDM mfikirie mara mbili kuhusu Mpendazoe, huyu ni mropokaji ipo siku atakuja kuwaumbua kwani siku yeyote atakimbia CDM na kujiunga na chama kingine. Nawashangaa mnampa kipaza sauti na kuropoka maneno mbovu mbofu jukwaani. Siasa za kusema watu binafsi mzikomeshe muanze kutuambia ni namna gani mtatuondoa watanzania katika lindi la umaskini.
 
Sitta, Mwakyembe kweli kuna michango yenu mmeitoa kwa Taifa lakini kwa jambo hili sina hamu na nyie. Inawezekana kabisa Sitta na Mwakyembe nyie ni wanafiki wakubwa ktk nchi hii yetu. Najua mnataka kuonekana mlionyeshwa na kuendelea kuonyesha kutopendezwa kwenu kuwa ndani ya ccm, ukweli ni kwamba bado mpo ndani ya chungu kinachowaumiza watanzania.

Kuna mambo mengi ya kuwauliza Sitta na Mwakyembe na moja wapo ni hili, kilichowarudisha ndani ya hili gamba la mafisadi na wezi ni nini? Majibu ya Watanzania wengi kuhusu mwelekeo wenu wa kisiasa ni sawa na huo wa Lowassa na Rostam. Ingawa tunajua mnataka sana tuwafahamu kwamba hamtaki kula hadharani bali mnataka kula nyumba ya mlango wa chumbani na kupuliza wakati huo huo. You can't and you will never serve two master, the devil (ccm) and God himself. Uchaguzi wa Sitta na Mwakyembe kubaki au kurudi kundi la kikwete linaonyesha kweli hawa makada wana uroho wa madaraka na njaa za pesa. Kwa haya yote tumewatambua Sitta na Mwakyembe kama Yuda wa Watanzania na sio kama yeye Sitta alivyotaka tumwone kama anavutia vyama vingi. Sidhani kama Watanzania tuliotaka arudishwe kuwa Spika tungejua haya yote tunge-support harakati za Sitta, Sitta is playing kamali na maisha ya Watanzania....

Nape kama tunovyojua this is new coming Rostam kinder, the boy anataka utajiri kwa kutumia tactics za Rostam 2011, Nape hujui kama kesho ccm itakuwa shimo la mita ngapi chini ya udongo... soma harakati za wakati wewe, Ridhiwan na January. Just pimping Tanzanians.

"Change and Revolutions go hand and hand with Sacrifices"
 
Haijaniingia kichwani ni jinsi gani Msomi kama Mvungi anadai hakuna haja ya kuongelea mambo ya CCJ kwa sababu ilishakufa. MMh huyu ni mtaalamu wa sheria anaongea hivyo!! Ingekuwa ni hivyo basi tulikuwa hatuna haja ya kudai pesa za EPA kwani zilishaibwa na mhusika mwingine aliyesimamia wizi huo alishachomoka (Balali). Hakieleweki mpaka wasaliti wote wa demokrasia ya Tanzania wametajwa wote.
 
Sasa nimeamini kweli SITTA alimtoa Lowasa kwa chuki binafsi za kukosa uwaziri mkuu.

Jamaa ni mbinafi huyu ingekuwa enzi ya Mwalimu angeondolewa kwenye chama arudi Tabora akarine asali
 
Hivi na aliyekuwa mwenyekiti wa CCj baada ya kurudia kulivaa gamba kaishia wapi?
 
Tatizo ni kwamba watu hawajmuelewa Mpendazoe, yeye hajasema kuwa tatizo ni kuanzisha CCJ , yeye anasema kuwa hao watu sita walimsaliti. kwa maana nikwamba walifyata mkia baada ya kitu fulani!
 
Sasa nimeamini kweli SITTA alimtoa Lowasa kwa chuki binafsi za kukosa uwaziri mkuu.

Jamaa ni mbinafi huyu ingekuwa enzi ya Mwalimu angeondolewa kwenye chama arudi Tabora akarine asali
Tuonyeshe huo ubinafsi nasi tuuone, la sivyo wewe una chuki binafsi naye, au una mapenzi na EL
 
Back
Top Bottom