buyegiboseba
JF-Expert Member
- Jun 3, 2011
- 535
- 145
Adui yako akiwa na njaa mpe chakula...
Mh S.Sitta akiwa ktk harambee Mjini Arusha.Ameombwa na kutafuta amani ktk mji wa Arusha kwa kuwapatanisha Mbunge Mh Lema na Meya wa Mji wa Arusha,na akachukuwa jukumu hilo kama ambavyo picha inavyojieleza.
Nawasilisha
Hilo pozi la Lemma nimelikubali ile mbaya.
Alafu huyo mayor anatia huruma balaa.
Wamama hawamkubali,
Wacha mungu hawamkubali,
Machalii hawamkubali,
Wazee hawamkubali.
Sijui sasa anan'gan'gania kuwaongoza nani?
Mkuu, kwa hiyo wewe unaangalia pozi la Lema tu, Huna haja ya kujua maendeleo ya wakazi wa Arusha?
Nilitaka kujua kidogo hapa.
Kwani Lema ni nani katika anga za sheria za nchi?
Kwani Meya asipotambuliwa na Lema lakini sheria za nchi zikimtambua inakuwaje?
Tuesday, 06 December 2011 20:44 |
Peter Saramba, Arusha VIONGOZI wa dini mkoani Arusha, wamezitaka pande zinazovutana katika mgogoro wa kisiasa Manispaa ya Arusha, kutafakari kwa kina ili kutafuta njia muafaka na sahihi za kumaliza mgogoro huo uliodumu kwa takriban mwaka mmoja sasa. Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, walisema mgogoro huo haukisaidii chama chochote cha siasa, viongozi wake na hata wakazi wa Mkoa wa Arusha na Watanzania kwa ujumla. Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Arusha, Thomas Laizer na mwenzake wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Arusha, Josephat Lebulu, ambao tangu awali waliweka msimamo wapamoja kutaka viongozi wa vyama vya siasa na Serikali kutumia busara kumaliza mgogoro huo, jana walisema hakuna njia nyingine inayoweza kutumika kumaliza mgogoro huo wa umeya Arusha isipokuwa majadiliano yenye nia njema. Sauti hizo za viongozi hao wa dini, zimekuja siku mbili baada ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta kujitosa katika mgogoro huo akijaribu kutafuta suluhu na kufikia hatua ya kuwakutanisha mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema na meya wa jiji hilo, Gaudence Lyimo. Askofu Laizer Askofu Laizer aliliambia gazeti hili kuwa njia bora ya kupata suluhu ya mgogoro huo, ni muafaka unaopasa kuweka mbele maslahi na faida ya jamii badala ya vyama na makundi ya watu wanaohusika katika mfafaruku huyo. Wapambanapo mafahari wawili, ziumiazo ni nyasi. Nyasi za Arusha ambao ni wananchi wameumia kweli kweli kutokana na mgogoro huu kwani hakuna maendeleo yanayoweza kupatikana penye magomvi, alisema Askofu Laizer. Askofu Laizer alisema tangu kuibuka kwa mgogoro huo yeye na wenzake siku zote, wamekuwa wakifanya maombi maalumu ili suluhu ipatikane. Akaviasa vyama vya CCM na Chadema, kusikia sauti ya wengi wanaopinga vurugu hizo kwa kuwa ni sauti ya Mungu inayolilia amani Arusha. Hata kama wenzangu watapingana na msimamo wangu, mimi na kanisa langu tutaunga mkono juhudi zozote za kutafuta muafaka wa kweli Arusha kwa maslahi, faida na maendeleo ya umma wa Arusha, alisema Askofu Laizer. Askofu Lekulu Kwa upande wake, Askofu Mkuu Lebulu, kupitia kwa msaidizi wake, Padri Simon Tengesi alisema:, "Kama ndugu wawili wamegombana ni busara wakakaa chini kwa pamoja na kufikia makubaliano kwa maslahi na manufaa ya jamii. Pamoja na kupinga utaratibu wa uchaguzi uliowaweka pembeni madiwani wa Chadema, viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali Arusha pia walitangaza kutomtambua meya aliyechaguliwa, kutoka CCM, Lyimo. Bavicha Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la vijana la Chadema(Bavicha), John Heche alisisitiza kuwa njia pekee ya kupatikana kwa muafaka wa kweli na wa kudumu Arusha ni Serikali kukubali kwamba uchaguzi wa meya ulikiuka kanuni, taratibu na sheria na unapaswa kurudiwa upya hata kama meya wa sasa atasimama na kuibuka mshindi. CCM wanaogopa nini kurejea kwenye uchaguzi wakati wana madiwani wengi kuliko Chadema? Serikali iache kutumia mabavu kumngangania meya ambaye hakupatikana kwa njia halali kwani hawezi kutekeleza wajibu na majukumu yake kwa ufanisi kutokana na dhamira yake kumsuta, alisema Heche Heche alisema muafaka wa Arusha hauwezi kupatikana kwa njia ya vitisho vya vyombo vya dola wala hila za baadhi ya watu wachace kuweka mbele maslahi yao binafsi badala ya kujali mahitaji na maoni ya umma. Heche alisistiza kwamba, kamwe chama chake hakiko tayari kufikia muafaka wa kugawana madaraka na CCM kama njia ya kumaliza mgogoro huo kwani hiyo siyo moja ya ajenda zakeo. Alitaja baadhi ya mambo ya msingi yanayostahili kushughlikiwa ili muafaka upatikane kuwa ni pamoja na uchaguzi kurudiwa, askari polisi waliohusika kuua na kujeruhi watu wasio na atia kuchukuliwa hatua za kisheria na kinidhamu na kesi iliyoko mahakamani dhidi ya viongozi wa chama hicho kuhusiana na tukio la Januari 5, mwaka huu kufutwa. UVCCM Mwenyekiti UVCCM Arusha, James Ole Millya alitaka vyama vyote kuepuka mtego wa kutaka kuonekana washindi katika mgogoro huo badala yake washindi wawe wananchi na umma wa Arusha unaoathirika sasa. Baraza la madiwani la Manispaa ya Arusha, liligubikwa na mgogoro baada ya madiwani wa Chadema kupinga zoezi la uchaguzi uliomweka kwenye kiti cha umeya, Lyimo ambaye ni diwani wa Kata ya Olorien. Januari 5, mwaka huu watu watatu walikufa kwa kupigwa risasi na polisi wakati wa maandamano yaliyoitishwa na Chadema kupinga uchaguzi. |
Hivi kambi ya Six na Membe zimeungana ili kupambana na EL??