Sitapangua kikosi tena - Maximo

Sokomoko

JF-Expert Member
Mar 29, 2008
1,915
127
Sitapangua kikosi tena - Maximo




na Dina Zubeiry



KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Mbrazil, Marcio Maximo, amesema kwa sasa hatarajii kupangua tena kikosi cha timu hiyo.

Maximo, aliyasema hayo jana baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wa jijini Dar es Salaam, akitokea nchini Yemen ambako Stars ilikwenda kucheza mechi ya kirafiki.

Ikiwa huko, Stars iliyo katika kampeni ya kusaka tiketi ya kucheza fainali mpya za Afrika kwa nyota wanaocheza ligi za nyumbani zitakazopigwa mwakani nchini Ivory Coast, ilifungwa mabao 2-1 na timu ya taifa ya Yemen.

Mbali ya kampeni hiyo, Stars pia inajipanga kwa kampeni za kusaka tiketi ya fainali za Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini na fainali za Mataifa ya Afrika nchini Angola mwaka 2010.

Mechi iliyo karibu, ni ile ya marudiano dhidi ya Harambee ya Kenya, itakayopigwa Jumapili, katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Maximo alisema, ziara hiyo ya Yemen, ilikuwa ya manufaa kwa timu yake kwani aliitumia kupata nyota wanne watakaoongezwa kwenye kikosi chake kilichopo kambini kwa ajili ya mechi ya Jumapili dhidi ya Harambee Stara.

Maximo alisema ingawa mazingira ya hali ya hewa na staili ya uchezaji wa Yemen, ni tofauti na ule wa Stars, lakini vijana wake wamejifunza mengi.

Alisema, asilimia kubwa ya kikosi kilichokwenda Yemen, kilijaa wachezaji wa kikosi B kwa ajili ya kuwapima ili kuwaongeza kikosi cha kwanza.

Alisema, ukiondoa wachezaji wa Yanga na Simba, wengine wanatarajiwa kuanza mazoezi leo jioni kabla ya kuungana na wenzao.

Kuhusu mechi dhidi ya Kenya, Maximo alisema itakuwa ngumu kwani kila timu inahitaji kushinda ili isonge mbele, hasa Stars ambayo iilipoteza mechi ya kwanza.

Hata hivyo, alisema ana matumaini makubwa ya vijana wake kufanya vema kwani wachezaji walio wengi hususani wa Simba na Yanga, walikuwa na timu zao katika michuano ya kimataifa.

“Mechi ya kwanza tulifungwa na Kenya, hivyo tutatumia siku mbili hizo kuwekana sawa na tuna imani tutashinda mechi yetu hiyo,” alisema Maximo.

Source:Tanzania Daima
 
Makocha wote duniani wanaajiriwa on assignment basis.
Mclaren alishindwa kuwapeleka Euro Waingereza,wamemwondoa na sasa wanaye Cappelo.
Huyu bwana ameshindwa Ghana 2008 assignment yake ya mwisho ni World Cup RSA akishindwa aondoke.
Natofautiana na wale wanaofikiri kuwa tumefika hapa kwa juhudi za Maximo na wachezaji tulionao hawana uwezo.
Tujikumbushe back then 1980 tulipo qualify kwenda Lagos tulikuwa tunarank wa ngapi ktk FIFA?,Maximo hajatutoa shimoni bwana.
Wachezaji wetu ni wazuri sana lakini our very best players HAWASHIRIKISHWI.
TATIZO NI SPORTS ADMNISRATION hususani Kurugenzi ya Ufundi ya TFF.Wachezaji wanaochaguliwa ni wale watakao toa 10% ya mapato yao kwa viongozi waliowachagua,Maximo hachagui wachezaji peke yake kama mlikuwa mnafikiri hivyo hamkuwa sahihi.
Mfano Timu iliyokwenda Rwanda, wale vijana wa Copa Cocacola selection ile ilikuwa aibu tu.Vijana halisi waliachwa wakachukuliwa vijana wa viongozi wa michezo.Tunalijua hilo.Je?,hii ni timu ambayo unasema kesho ndio itakuwa timu ya wakubwa, unatarajia nini? .Mifano ni mingi ufisadi umetawala katika sekta hii ya michezo.
Bado nasema wachezaji wetu ni wazuri. nani amewasahau raha waliokuwa wanatupa akina Eddo Chumila,Hamza maneno,Rajabu Rashid "double R" ,Fumo,Frank Kasanga,OCD Njohole,Danny Muhoja,Issa Athumani,Octavian Mrope, Peter Mhina ,Juma Mgunda,Mwameja,Yassin Abuu Napil,Kassa Mussa,Ali Maumba,Sentahafu Mhando Mdeve,BEki mstaarabu Samli Ayub,je sports academy zilikuwepo kipindi hicho huu ni utapeli mtupu.Kumbuka Said Mrisho "ZICO wa Kilosa",Kitwana Selemani hao ni wachache wa mid and late 90's hatutaki kurudi kwa kina Boniface Mkwasa,"Homa ya Jiji" Makumbi Juma,"Golden Boy" Mogella,Athumani Chama "Jogoo" .
Tuache kuwakashifu na kutukana wachezaji wetu.

"Mwanafunzi mjinga au asiye na uwezo ni reflection ya mwalimu aliyemfundisha".

1.Tuache ufisadi wa kuleta nyasi bandia feki ambazo hazicomply na Specs zinazotakiwa.

2.Tuache kujuana.Kwani soka sasa hivi bwana mihela ipo kedekede ya NMB ,Serengeti.Tufuate vipaji mchangani tulipowatoa akina Chumila then tuwe na serious and REAL SPORTS ACADEMY.
3.Tuwe wazi ktk taratibu za kusource walimu wenye sifa.Tulikuwa na akina Hudson yuje mjerumani.Acha kina Victor.

Huyu Jamaa ni msanii.
Huwezi kwenda Brazil ukacheza mechi 5 huku ukifungwa idadi ndogo ya magoli kila mechi na nyingine utoedraw... then uende dakar upigwe goli 4.Pale kulikuwa na usanii wa hali ya juu.Maximo alitutafutia timu zisizo na uwezo makusudi asijichafulie rekodi yake.Amekuwa anafanya hivyo hata kwenye hizi trial matches zake.

Huyu jamaa ni msanii perse.Binafsi nasema akishindwa assignment yake ya mwisho yakutupeleka RSA, AONDOKE.
 
Nadhani "Fwati" hawawezi kumtoa, ataondoka mwenyewe siku tukimpiga mawe uwanja wa Taifa siku T/stars itakapofungwa
 
Hivi wadau wa soka wanajuaa kiasi gani huyu "msema hovyo na msimamizi wa mazoezi tu...."analipwa kwa mwezi????15,000$ kwa kazi gani anayoifanya?mi nashauri jamani tujaribu makocha wa croatia...maana naona brasil hawatufai na mfumo wao..hautusaidiii kabisa...tubadilishe upepo...sante sana maximo sasa inatoshaaa...go go go
 
awali ya yote napenda kuwaunga mkono watu wooote wanaompinga huyu mbrazil.
nikijaribu kupitia baadhi ya makocha wa soka huko ulaya na hata hapa africa nimegundua kuwa wengi wanawekewa malengo, ambayo kwa namna moja wakishindwa kuyavuka basi hutimuliwa kazi, na timu anapewa mtu mwingine.
binafsi sioni sababu ya huyu jamaa mpaka sasa kwa nini anaendelea kufundisha.
mimi naamini kama ni mafanikio ya ushindi waliyoyapata vijana wetu yalitokana na ahadi na michango iliyokuwa ikimiminika kutoka kila upande wa nchi.
hivyo ninaimani hata timu angepewa kocha yeyote yule angeweza kuifikisha pale ilpokuwa.

watanzania msitumie vichwa kubebea masikio, huyu jamaa akishindwa kuwapeleka south mtadanganywa danganywa kisha atapewa tena mkataba na msipoamka anaweza akapewa ukocha wa milele....waswahili wanasema "usipouanika utautwanga mbichi"
 
Back
Top Bottom