mopaozi
JF-Expert Member
- Nov 17, 2010
- 3,301
- 519
Waziri mkuu Bw Pinda amesema kuwa hana nia wala hafikirii kugombea urais mwaka 2015 na kuwataka wanaomtangazia wakae chonjo ameyasema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari juu ya mgomo wa madaktari!!
Huyu baba vp wagonjwa wanakufa kwa mgomo ye anazungimzia urais matokeo yake mantiki nzima ya mkutano wake haijaeleweka na madaktari wamekuja juu kuwa mgomo uko palepale hadi kieleweke!!
Sitaki urais, ni mzigo- Pinda
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, anakuwa Waziri Mkuu wa kwanza nchini tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 kutamka hadharani kwamba hana nia wala hataki kuwania urais mwaka 2015 Rais Jakaya Kikwete atakapomaliza muda wake, kwa kuwa kazi hiyo ni mzigo.
Badala yake amesisitiza kuwa hatajisumbua kuingia katika kinyang'anyiro hicho kwani amejipanga vyema kuanza maisha mapya ya kufuga nyuki baada ya kustaafu.
Aliyasema hayo jana ofisini kwake Magogoni jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na wahariri na waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari kuhusu mwelekeo wa nchi na masuala muhimu ya kitaifa yaliyojitokeza siku za hivi karibuni.
Alisema mwaka 2015 atakuwa mtu mzima sana na haamini kuwa kwa umri huo ataweza kuyamudu majukumu ya nafasi ya urais.
"Niliposema sitawania urais nilimaanisha hivyo na naomba watu wanielewe, urais si kazi ya kukimbilia kama kweli unataka kuwatumikia watu, kwa wale wanaotaka kwenda kuchuma sawa ni pazuri, lakini mimi naona ni mzigo, kuna wakati namwonea huruma Rais Kikwete maana kila kitu kigumu anaangushiwa yeye," alisema.
"Mwaka 2015 nitakuwa na umri wa miaka 67, inamaana nikipata urais baada ya miaka mitano nitakuwa na 72, yanini nifike kote huko kwanini wakati nimeshalitumikia taifa langu muda mrefu sana, nimefanyakazi ya taaluma yangu ya sheria miaka mitatu tu nikaenda Ikulu ambako nimefanyakazi hadi leo hii, nimefanyakazi na Mwalimu Nyerere, nimefanyakazi na Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa na hii awamu ya nne, kama watu hawajaridhika na mchango nilioutoa kwa nchi yangu inamaana hata nikiwa nani hawataridhika. Urais siutaki na wala siwazii wanaotaka waendelee tu," alisema.
"Kuna wakati nikisema sitaki urais watu wananiambia acha kusema hivyo wewe, acha kabisa mzee usiseme hivyo, lakini mimi huwa nawaambia watu hawa kuwa huu ni uamuzi wangu na nataka Watanzania waelewe hivyo, anayetaka haya! Ila mimi sitakuwemo," alisema.
Alisema anataka baada ya kustaafu ajikite zaidi katika ufugaji wa nyuki kwani amebaini kuwa biashara hiyo ina faida sana lakini Watanzania wengi bado hawajabaini fursa hiyo.
Nafasi ya uwaziri mkuu tangu Tanganyika ipate Uhuru mwaka 1961 imeshikiliwa na watu tisa, wa kwanza alikuwa Mwalimu Nyerere aliyekaa kwa mwaka mmoja tu kabla ya kumwachia Rashid Kawawa; akimwachia Kawawa nafasi hiyo naye akaandaa nchi kuwa Jamhuri mwaka 1962.
Mbali na hao mawaziri wakuu wengine ni Edward Sokoine ambaye wengi walitarajia kuwa angemrithi Mwalimu Nyerere, lakini maisha yake yalikatizwa na ajali ya barabarani Aprili 12, 1984.
Wengine ukiacha Kawawa ambaye baada ya kurejea kwa mfumo wa vyama vingi alikuwa amekwisha kuwa mtu mzima mwaka 1992 hivyo kupoteza hamasa ya kuwania kiti hicho, ni Jaji Joseph Warioba ambaye mwaka 1995 alijaribu lakini hakufanikiwa; John Malecela naye mwaka 1995 na mwaka 2005 alijitosa katika kinyang'anyiro hicho lakini chama chake, CCM, kiliondoa jina lake mara mbili kabla ya kupigiwa kura kwenye vikao vya chama vya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).
Wengine waliojaribu karata zao ni David Cleopa Msuya ambaye mwaka 1995 alijitosa kwenye kinyang'anyiro hicho, lakini kura hazikutosha kwenye Mkutano Mkuu wa CCM baada ya kushindwa na Kikwete na Benjamin Mkapa kisha Mkapa akapita katika raundi ya pili ya kura.
Mwaka 2005 Waziri Mkuu Mstaafu ambaye alishikilia wadhifa huo kwa miaka 10 mfululizo chini ya Rais Mkapa, Frederick Sumaye, naye alijitosa katika mbio hizo, lakini aliishia NEC baada kupata kura kidogo akizidiwa na akina Kikwete, Profesa Mark Mwandosya na Dk. Salim Ahmed Salim. Kikwete aliibuka mshindi dhidi ya Dk. Salim na Profesa Mwandosya kwenye mkutano mkuu wa uchaguzi wa mwaka 2005.
Waziri Mkuu pekee ambaye hayatangaza nia ya kuwania nafasi hiyo, ingawa huko nyuma alipata kujaribu nafasi hiyo akiwa waziri wa kawaida ni Edward Lowassa ambaye hadi sasa habari zinasema kuwa anatazamwa kama miongoni mwa wanasiasa wanaoitafuta nafasi hiyo.
Katika mkutano wa jana, Pinda alisema watu wanaokimbilia Ikulu huenda wana jambo lao na si kuwatumikia wananchi kwani kiongozi mzuri ni yule anayependekezwa na watu awatumikie na si yeye kujipendekeza kwa wanachi.
"Watu ndio waseme fulani unafaa tuongoze, lakini wewe kujipeleka wakati kule kuna kazi ngumu lazima kuna jambo utakuwa unafuata maana mimi nimekaa katika nafasi hii zaidi ya kazi ngumu sioni kipya," alisema Pinda maarufu kama mtoto wa mkulima.
NAFASI ZA MADC
Kuhusu wakuu wa wilaya kuchelewa kutangazwa, Pinda alisema sehemu nyingi kulikuwa na migogoro ya ni wapi yawepo makao makuu, lakini kwa sasa wameshamaliza na wiki ya kwanza ya mwezi wa pili watatangazwa.
"Mzee (Rasi Kikwete), amesafiri na wakati nazungumza naye wakati wa kumuaga pale uwanja wa ndege nimemdokeza hilo akasema akirudi tu tutayamaliza, hata mimi hainipendezi suala hili kukaa muda mrefu hivi maana wakuu wa wilaya huko najua kazi haziendi wanamawazo kuhusu nafasi zao," alisema Pinda.
UGONJWA WA MWAKYEMBE
Kuhusu afya ya Naibu Waziri wa Miundombinu, Dk. Harrison Mwakyembe, Pinda alisema hajui anachoumwa, lakini hata kama angekuwa anajua yeye si mtu sahihi wa kutangaza maradhi ya mtu.
Alisema kwa kuwa maradhi ya mtu ni siri yake mwenyewe basi wanaotaka kujua anachoumwa ni vyema wanamwomba mwenyewe awaeleze na si mtu mwingine yeyote.
AMFAGILIA MAGUFULI
Kuhusu bei ya nauli kivuko cha Kigamboni, Pinda alimtetea Waziri wa Ujenzi, John Magufuli kuwa alikuwa sahihi na alifuata sheria, ila kilichomponza ni maneno yake ya utani.
"Magufuli anapenda sana utani na mimi nilimweleza kuwa uko sahihi katika kutekeleza sheria, lakini maneno yako yale ya utani utani ndiyo yamekufikisha hapo, nilimweleza waziwazi kuwa si kila mtu anaelewa utani," alisema.
MAJIBU YA JAIRO ANAYO AG
Kuhusu maazimio ya Bunge juu ya aliyekuwa Katibu Mkuu Nishati na Madini, David Jairo, alisema serikali imeyatolea maelezo maazimio yote na imempelekea Mwanasheria Mkuu wa serikali ili awashauri hatua zaidi wanazoweza kuchukua.
"Katika maazimio yale tumetoa maelezo kila azimio na tumempa AG apitie ili atupe ushauri wa kisheria, kwa sasa anayafanyia kazi na bungeni tutatoa maelezo ya nini kimefanyika," alisema Pinda.
POSHO KITENDAWILI BADO
Akizungumzia posho za wabunge, Pinda alitetea posho hizo akisema kuwa wabunge ni wawakilishi wa wananchi hivyo wakati mwingi wanatumia fedha zao kuwapa watu wenye shida.
Pinda alisema wabunge wengi wamekopa katika taasisi mbalimbali za fedha hivyo mshahara wao wote unaishia kulipa madeni.
"Mshahara wa mbunge ni milioni 2.3 akikatwa mkopo 800,000 anabaki na milioni 1.7 bado unakuta pale nje kuna msururu wa watu wana msubiri. Akifika jimboni hivyo hivyo, sasa kwa kweli posho hizi zinaweza kusaidia kumpunguzia mzigo," alisema.
Alisema mapendekezo yaliyowasilishwa na Bunge kwa Rais Kikwete kwa ajili ya kuwaongezea posho wabunge hayajakubaliwa na badala yake suala hilo limerejeshwa kwake.
"Bunge lilipendekeza suala hilo kwa Rais, na amenipa mimi nilishughulikie kwa hiyo litatolewa uamuzi ila watu wasidhani kuwa wabunge wanaishi maisha ya fahari sana jamani, wanashida kwelikweli," alisema Pinda.
CHANZO: NIPASHE
Huyu baba vp wagonjwa wanakufa kwa mgomo ye anazungimzia urais matokeo yake mantiki nzima ya mkutano wake haijaeleweka na madaktari wamekuja juu kuwa mgomo uko palepale hadi kieleweke!!
Sitaki urais, ni mzigo- Pinda
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, anakuwa Waziri Mkuu wa kwanza nchini tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 kutamka hadharani kwamba hana nia wala hataki kuwania urais mwaka 2015 Rais Jakaya Kikwete atakapomaliza muda wake, kwa kuwa kazi hiyo ni mzigo.
Badala yake amesisitiza kuwa hatajisumbua kuingia katika kinyang'anyiro hicho kwani amejipanga vyema kuanza maisha mapya ya kufuga nyuki baada ya kustaafu.
Aliyasema hayo jana ofisini kwake Magogoni jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na wahariri na waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari kuhusu mwelekeo wa nchi na masuala muhimu ya kitaifa yaliyojitokeza siku za hivi karibuni.
Alisema mwaka 2015 atakuwa mtu mzima sana na haamini kuwa kwa umri huo ataweza kuyamudu majukumu ya nafasi ya urais.
"Niliposema sitawania urais nilimaanisha hivyo na naomba watu wanielewe, urais si kazi ya kukimbilia kama kweli unataka kuwatumikia watu, kwa wale wanaotaka kwenda kuchuma sawa ni pazuri, lakini mimi naona ni mzigo, kuna wakati namwonea huruma Rais Kikwete maana kila kitu kigumu anaangushiwa yeye," alisema.
"Mwaka 2015 nitakuwa na umri wa miaka 67, inamaana nikipata urais baada ya miaka mitano nitakuwa na 72, yanini nifike kote huko kwanini wakati nimeshalitumikia taifa langu muda mrefu sana, nimefanyakazi ya taaluma yangu ya sheria miaka mitatu tu nikaenda Ikulu ambako nimefanyakazi hadi leo hii, nimefanyakazi na Mwalimu Nyerere, nimefanyakazi na Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa na hii awamu ya nne, kama watu hawajaridhika na mchango nilioutoa kwa nchi yangu inamaana hata nikiwa nani hawataridhika. Urais siutaki na wala siwazii wanaotaka waendelee tu," alisema.
"Kuna wakati nikisema sitaki urais watu wananiambia acha kusema hivyo wewe, acha kabisa mzee usiseme hivyo, lakini mimi huwa nawaambia watu hawa kuwa huu ni uamuzi wangu na nataka Watanzania waelewe hivyo, anayetaka haya! Ila mimi sitakuwemo," alisema.
Alisema anataka baada ya kustaafu ajikite zaidi katika ufugaji wa nyuki kwani amebaini kuwa biashara hiyo ina faida sana lakini Watanzania wengi bado hawajabaini fursa hiyo.
Nafasi ya uwaziri mkuu tangu Tanganyika ipate Uhuru mwaka 1961 imeshikiliwa na watu tisa, wa kwanza alikuwa Mwalimu Nyerere aliyekaa kwa mwaka mmoja tu kabla ya kumwachia Rashid Kawawa; akimwachia Kawawa nafasi hiyo naye akaandaa nchi kuwa Jamhuri mwaka 1962.
Mbali na hao mawaziri wakuu wengine ni Edward Sokoine ambaye wengi walitarajia kuwa angemrithi Mwalimu Nyerere, lakini maisha yake yalikatizwa na ajali ya barabarani Aprili 12, 1984.
Wengine ukiacha Kawawa ambaye baada ya kurejea kwa mfumo wa vyama vingi alikuwa amekwisha kuwa mtu mzima mwaka 1992 hivyo kupoteza hamasa ya kuwania kiti hicho, ni Jaji Joseph Warioba ambaye mwaka 1995 alijaribu lakini hakufanikiwa; John Malecela naye mwaka 1995 na mwaka 2005 alijitosa katika kinyang'anyiro hicho lakini chama chake, CCM, kiliondoa jina lake mara mbili kabla ya kupigiwa kura kwenye vikao vya chama vya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).
Wengine waliojaribu karata zao ni David Cleopa Msuya ambaye mwaka 1995 alijitosa kwenye kinyang'anyiro hicho, lakini kura hazikutosha kwenye Mkutano Mkuu wa CCM baada ya kushindwa na Kikwete na Benjamin Mkapa kisha Mkapa akapita katika raundi ya pili ya kura.
Mwaka 2005 Waziri Mkuu Mstaafu ambaye alishikilia wadhifa huo kwa miaka 10 mfululizo chini ya Rais Mkapa, Frederick Sumaye, naye alijitosa katika mbio hizo, lakini aliishia NEC baada kupata kura kidogo akizidiwa na akina Kikwete, Profesa Mark Mwandosya na Dk. Salim Ahmed Salim. Kikwete aliibuka mshindi dhidi ya Dk. Salim na Profesa Mwandosya kwenye mkutano mkuu wa uchaguzi wa mwaka 2005.
Waziri Mkuu pekee ambaye hayatangaza nia ya kuwania nafasi hiyo, ingawa huko nyuma alipata kujaribu nafasi hiyo akiwa waziri wa kawaida ni Edward Lowassa ambaye hadi sasa habari zinasema kuwa anatazamwa kama miongoni mwa wanasiasa wanaoitafuta nafasi hiyo.
Katika mkutano wa jana, Pinda alisema watu wanaokimbilia Ikulu huenda wana jambo lao na si kuwatumikia wananchi kwani kiongozi mzuri ni yule anayependekezwa na watu awatumikie na si yeye kujipendekeza kwa wanachi.
"Watu ndio waseme fulani unafaa tuongoze, lakini wewe kujipeleka wakati kule kuna kazi ngumu lazima kuna jambo utakuwa unafuata maana mimi nimekaa katika nafasi hii zaidi ya kazi ngumu sioni kipya," alisema Pinda maarufu kama mtoto wa mkulima.
NAFASI ZA MADC
Kuhusu wakuu wa wilaya kuchelewa kutangazwa, Pinda alisema sehemu nyingi kulikuwa na migogoro ya ni wapi yawepo makao makuu, lakini kwa sasa wameshamaliza na wiki ya kwanza ya mwezi wa pili watatangazwa.
"Mzee (Rasi Kikwete), amesafiri na wakati nazungumza naye wakati wa kumuaga pale uwanja wa ndege nimemdokeza hilo akasema akirudi tu tutayamaliza, hata mimi hainipendezi suala hili kukaa muda mrefu hivi maana wakuu wa wilaya huko najua kazi haziendi wanamawazo kuhusu nafasi zao," alisema Pinda.
UGONJWA WA MWAKYEMBE
Kuhusu afya ya Naibu Waziri wa Miundombinu, Dk. Harrison Mwakyembe, Pinda alisema hajui anachoumwa, lakini hata kama angekuwa anajua yeye si mtu sahihi wa kutangaza maradhi ya mtu.
Alisema kwa kuwa maradhi ya mtu ni siri yake mwenyewe basi wanaotaka kujua anachoumwa ni vyema wanamwomba mwenyewe awaeleze na si mtu mwingine yeyote.
AMFAGILIA MAGUFULI
Kuhusu bei ya nauli kivuko cha Kigamboni, Pinda alimtetea Waziri wa Ujenzi, John Magufuli kuwa alikuwa sahihi na alifuata sheria, ila kilichomponza ni maneno yake ya utani.
"Magufuli anapenda sana utani na mimi nilimweleza kuwa uko sahihi katika kutekeleza sheria, lakini maneno yako yale ya utani utani ndiyo yamekufikisha hapo, nilimweleza waziwazi kuwa si kila mtu anaelewa utani," alisema.
MAJIBU YA JAIRO ANAYO AG
Kuhusu maazimio ya Bunge juu ya aliyekuwa Katibu Mkuu Nishati na Madini, David Jairo, alisema serikali imeyatolea maelezo maazimio yote na imempelekea Mwanasheria Mkuu wa serikali ili awashauri hatua zaidi wanazoweza kuchukua.
"Katika maazimio yale tumetoa maelezo kila azimio na tumempa AG apitie ili atupe ushauri wa kisheria, kwa sasa anayafanyia kazi na bungeni tutatoa maelezo ya nini kimefanyika," alisema Pinda.
POSHO KITENDAWILI BADO
Akizungumzia posho za wabunge, Pinda alitetea posho hizo akisema kuwa wabunge ni wawakilishi wa wananchi hivyo wakati mwingi wanatumia fedha zao kuwapa watu wenye shida.
Pinda alisema wabunge wengi wamekopa katika taasisi mbalimbali za fedha hivyo mshahara wao wote unaishia kulipa madeni.
"Mshahara wa mbunge ni milioni 2.3 akikatwa mkopo 800,000 anabaki na milioni 1.7 bado unakuta pale nje kuna msururu wa watu wana msubiri. Akifika jimboni hivyo hivyo, sasa kwa kweli posho hizi zinaweza kusaidia kumpunguzia mzigo," alisema.
Alisema mapendekezo yaliyowasilishwa na Bunge kwa Rais Kikwete kwa ajili ya kuwaongezea posho wabunge hayajakubaliwa na badala yake suala hilo limerejeshwa kwake.
"Bunge lilipendekeza suala hilo kwa Rais, na amenipa mimi nilishughulikie kwa hiyo litatolewa uamuzi ila watu wasidhani kuwa wabunge wanaishi maisha ya fahari sana jamani, wanashida kwelikweli," alisema Pinda.
CHANZO: NIPASHE