Heheheee nilijua tu huwezi.
Kwamba kuna baadhi ya mambo ambayo watu wengi huwawia vigumu, hiyo ni kweli. Kwa hiyo nimekuelewa.
I say hi too. Nataka nimnunulie personalized sipper cup ya Disney ila nataka kujua favorite Disney character wake...
Naam! Kwani nina wivu kukaa nyumba za kupanga ni hatari na humu ndani ya madaladala michezo ya kupeana namba za simu hupendwa sana!
USIOE kisa dini,hio dini ambayo inaruhusu mwanaume kuwa na wake wengi na si mwanamke kuwa na waume wengi HUONI KAMA HAISMAMII HAKI???? ingekuwa inasimamia haki ingeruhusu pia na mwanamke kuwa na waume wengi!
Upuuzi, haya ni maamuzi yako binafsi ambayo hayatuhusu!
ujue mkuu wangu,kitabu kitakatifu cha Mungu Quran kiliporuhusu ndoa za mke hadi wanne kilikua na malengo mazuri tu mf.kama kuwajali yatima na wajane.Lakini wengi wa kaka zetu mnatumia hii ruhusa kinyume kabisa na mapenzi ya Mungu,mfano mzuri ni wewe hapo kwenye dhambarau,wewe unaoa sbb tamaa zako za kimwili zinakutuma kuona kuwa wako wazuri zaidi ya mkeo wa kwanza.Ni kweli wazuri wako wengi na mzuri kuliko wote bado hajazaliwa,lkn sasa kama wewe unaoa sbb unataka ujijazie wanawake wazuri nyumbani kwako mbona sasa dini inakubana maana mwisho ni wa nne,sasa inaonesha utakapofikia kiwango cha mwisho na wewe ni mwenye uroho kila mwanamke mzuri unamtaka,utaanza kuwa asherati sbb nina hata ukioa wanne bado kuna utakayemuona amewazidi hao wanne.
Sasa je sisi hapa tukikushauri uoe sbb dini anakuruhusu halafu mkeo akakataa kata kata sbb na yeye dini inasema ni lazima aridhie ndio uoe,wakati huo huo wewe ndio umeona kabinti kazuriiiii na kamekubali ukaoa itakuaje hapo na macho yako yanakuonesha kabisa kuwa ni kazuri kumshinda mkeo wa sasa,ukikatizama kana miaka 22 na mkeo ana 44,kana ziwa saa 6 na ya mkeo yamezimia kwa usingizi,uso wa mkeo umejaa wrinkles wa kabinti umenyooka na wenye kuteleza mithili ya hariri,ni kazuri mkeo anaonekana kinyago akisimama mbele yake lkn ndo wife anasema no sitaki mke mwenza,kama watoto naweza kukuzalia idai utakayo,penzi hujawahi kuomba nikakunyima labda nikiwa mgonjwa maana hata ww ukiumwa nakuvumilia,sijawahi kulalamika kuwa kuna kinachonishinda sasa kwanini wataka kuniletea mwenzangu,sitaki.Utafanyaje.Sidhani kama utakaacha kabinti,utaoa kinguvu huku ukipita kifua mbele kuwa dini imeniruhusu kumbe huna hata moja ulilofanya linalikubaliana na dini itakavyo.
Usifikiri watu wote wako sawa na wewe amabe hata maagizo ya Mungu unayatia dosari. Sasa kuna haja gani ya kuolewa si utowe tu kwa unaempenda kwani pana haja ya mkataba maalum kwenye aina ya mapenzi unayotaka wewe?hakuna mwanamke anayependa,wanaridhia baada ya kuona hamna jinsi,kwa mwanaume hamna u turn ndio afanyeje in short wanakubali shingo upande....mtu uliyempenda huwezi kumruhusu awe na mtu mwingine period.
NN mfano dini ingekua inaruhusu na wanawake tuolewe na wanaume wengi.
Mkeo anakujia,"mume wangu Ngabu unajua kiasi gani nakupenda,mpenzi wangu naomba unipe ridhaa yako niongeze mume mwingine,muwe wawili,hana shida ni mtulivu cha msingi umheshimu tu na kumpenda,utapata rafiki wa kushangilia naye mechi za MAN U pia atakusaidia mambo mengi si unajua tena we umeshaanza kuwa mtu mzima na yeye bado ni kijana."
Kama kweli utaridhia kwa moyo wako bila kushurutishwa basi ujue kuna wake wa kwanza wanaoridhia ila kama moyo wako utakataa basi ujue hakuna mwanamke anayeridhia hii kitu.
NN mim nilikuomba wewe ujibu kama wewe.UNGEMKUBALIA?
To be the second/other wife??? Dah..... Lord help me!
Ngabu nilijua huwezi kukubali,hata ungesema ungekubali bado ningejua unadanganya,sbb najua haiwezekani.
Nakuomba utuambie kwanini wewe moyo wako umeona kwamba usingemkubalia.
Ukioa nakushauri wasikae mbali,manake kuna Mdingi namfahamu anao watatu,mmoja anakaa Tanga,mwingineKibaha,mwingine Dar.
Kwa hiyo inabidi karibu kila wiki adrive kutoka Tanga kuja either Dar au Kibaha,ili kuhakikisha anawapa haki yao sa si shughuli hiyo?
Pengine mapenzi yake kwake yamezidi kiasi cha kuwa hawezi kunivunja matakwa yangu.ukiona anaridhia kirahisi ujue hakupendi anasema bora liende
Kwani mmoja hakutoshi???? Au keshachuja kwani miaka 20 mingi ati!
Siwezi kutoka na mandingo hata kama akinambia aliaacha hiyo kazi miaka kumi ilopita.
NN mim pia sipendi generalisation,lkn ukiwa kama binadamu unaweza kujua kitu ambacho ni kigumu binadamu mwingine kufanya,au ukiwa kama mwanamke unaweza kujua ni nini mwanamke mwenzio anaweza kufanya au kutofanya sbb na wewe unafanana nao,japo kila mmoja ana tabia zisizofanana na mwenzie.
Mfano binadamu yeyote wa kawaida anajua kuua binadamu mwingine ni kitu kigumu sana,hata kama sisi sio every human being lkn tunajua kuua binadamu mwingine ni kitu kigumu sana na wengi hatuwezi lkn wapo wachache wetu wanaweza kufanya,na wanapofanya tunawashangaa kuwa wana mioyo ya aina gani mpaka wameweza kufanya hivyo.
hivyo sihitaji kuwa every woman kujua kuwa haiwezekani kwa mwanamke aridhie mpenzi wake ampende mwanamke mwingine.
btw uncle wako anasema hi.
Kwangu mimi kuniongezea mke mwingine au kufanywa mke wa pili ni tusi wala sio mapenzi (samahani kwa wale mtakaokerwa/kukwazwa na maneno yangu)! Siamini katika kupendwa sawa kwa sawa hasa kwa pendo kama hili linalohitaji attention, care na hisia za dhati toka moyoni. Na pia sipendi kupangishwa foleni kwenye penzi langu.....so nikitoa ruhusa basi itakuwa kwa mimi kuachia ngazi coz najua siwezi kuridhia kabisa!!
Omba Mungu yasikukute! Unaonaje wale wanaojitundika?hata mim mtu kunijia eti ananiomba aongeze mwenzangu nitaona kanitukana na nitamkubalia kisha natimua zangu nimuache na ampendae.
Wanawake wanaokubali kuna sababu nyingi zinazofanya wakubali ikiwa ni uoga wa kwenda kupata shida,hawa ni wale wanawake wavivu wasiojiamini wanaoishi hapa duniani kwa support ya mwanaume,bila mwanaume kanga nzuri hawezi kuvaa au bila mwanaume watoto wake watapata shida eti anabaki kwa faida ya watoto wake,au wengine ushirikina unafanya abaki huku akihangaika kwa waganga akidhani iko siku penzi lililohamishiwa kwa bi mdogo litarudi kwake.
Kubaki ktk ndoa ya hivi ni kutojua thamani yako,hata kama sizai siwezi kukuruhusu uoe mke mwingine eti ili upate watoto,je ingekua ni yeye mwanaume ndo hana uzazi angeniruhusu nikazae nje ili aitwe baba.