Sisi ni watu wa ajabu duniani?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Date::2/11/2009 (mwananchi)

Waziri Mkuu, wabunge waalikwa tamasha la albino Dar
Na Clara Alphonce

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda kesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tamasha la kupiga vita mauaji ya walemavu wa ngozi (albino) lililoandaliwa na Umoja wa vijana wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam.

Katibu Mwenezi wa UV- CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, Haji Manara alisema kuwa tamasha hilo lililobeba ujumbe wa ' kila kijana ni mlinzi wa albino' litafanyika kesho kwenye Viwanja vya Leaders Jijini Dar es Salaam

Alisema nia ya tamasha hilo ni kuunga mkono hatua ya serikali ya kukemea mauaji ya albino yanayoendelea nchini kote.


Manara alisema mbali na Waziri Mkuu Pinda, pia kutakuwa na wabunge mbalimbali wa Mkoa wa Dar es Salaam,Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, Suleiman Kova ambao watatoa ujumbe wao kuhusu mauaji hayo.

Manara aliwataja wasanii mbalimbali watakao tumbuiza katika tamasha hilo kuwa ni TID, Prof. Jay, Soggy Doggy, Wanaume Halisi na Wanaume TMK wakati bendi zitakazotumbuiza ni Msondo Ngoma, FM Academia, Vibration Sound na kwa muziki wa taarab, East African Melody.

My Take:

what is wrong with this picture? Clue: angalia kauli iliyotiliwa uzito. Yaani bendi zote na viongozi waalikwa watakuwa kwa ajili ya lengo hilo.
 
Last edited:
Matatizo ya nchi yetu na watu wake ukiyafikiria sana..unaweza jistukia unagonga ngumi kwenye screen ya computer yako-Lol!

Raisi analaani, Waziri Mkuu analia, serikali inakemea, Jaji Kiongozi analalamikia Bunge, Spika wa Bunge anashutumu mahakama, CCM, chama tawala, inaandaa tamasha na vijana wake pamoja na wabunge wanaserebuka......masikini nchi yangu, wananchi haooo !! Kweli tu watu wa ajabu.
 
Tu waajabu kweli Mag3 vijana wa chama tawala wanataka kuunga mkono hatua ya serikali ya kukemea mauaji ya albino yanayoendelea nchini kote, ina maana TID prof.Jay Tmk au hau wa taarabu wamejiandaa kuimba single zinazokemea hayo mauaji ni kupeana ulaji tu hapo?!!
 
Tu waajabu kweli Mag3 vijana wa chama tawala wanataka kuunga mkono hatua ya serikali ya kukemea mauaji ya albino yanayoendelea nchini kote, ina maana TID prof.Jay Tmk au hau wa taarabu wamejiandaa kuimba single zinazokemea hayo mauaji ni kupeana ulaji tu hapo?!!

yaani wao wanachounga mkono ni "kukemea" mauaji ya Albino!!
 
Vipi kuhusu kuwatafutia maalbino political asylum mzee?
Kuwaita Maalbino haijakaa vema nionavyo mie......albino uwingi wake ni albino......huwezi kusema "maalbino wameonana na waziri mkuu kayanza"......

naona hii ishu ya albino imeshakuwa deal...
 
Ingekuwa ni njema kama mapato yatakayo tokana na kiingiliio kama ni hivyo kwenye tamasha hilo...yaongezwe kwenye kampeni za kununu simu...na kuwapa albino,kuboresha system ya polisi..ku track walipo via GPS au kingine....lakini hapo najua inaweza kuwa ni watu kunywa na kucheza na speech za hapa na pale...wengine hata nyumbani hawata rudi moja kwa moja kwenye mengine.
 
Last edited:
Kuna baadhi ya maneno inabidi viongozi wetu wayaache, mfano, KUKEMEA, KUONYA, WARSHA, KONGAMANO, UPEMBUZI YAKINIFU, WAFADHILI, TUSUBIRI BAJETI, AMANI NA UMOJA WETU.Maneno haya yanaudhi sana, ukiona moja ya neno hilo limetajwa, ujue hamna kitu kinatendeka hapo, ni porojo tu. Watani wetu wakitucheka sometimes inabidi tujiulize huenda kuna substance ndani yake.
 
Mzee Mwanakijiji, hili suala si dogo kam linavoonekana, nje ya nchi wa Tanzania tunanuka kwa suala hili.Nilikuwa Washington mwezi wa November 2008, actually waafrika wenzetu wanatucheka as if wote tunashiriki suala laushirikina kwa kutumia viungo vya albino.
Suluhisho ni kulipa uzito ili wale wanaolishabikia kiushirikina waache kabisa.
 
Hao ndio CCM ,sidhani kama hizo bendi zote hapo zitakuja kupiga mziki bure na zaidi kama wangeanzisha mfuko maalum ,japo waokwawao wataziiba lakini kilichobaki kingefaa hata kuweka microchip kwenye viungo vya alibino ,pengine microchip ingeliwezekana hata kuwekwa ndani ya mfupa na kuwa sealed.

Sasa wanaenda kushangilia kwa midundo na ulevi wa gongo ,ndio maana yake ,vingunge wote wanahudhuria wakiwemo na washiriki wa vyombo vya dola ambao huwa mstari wa mbele katika kusimamia wizi wa kura ,hivi vyama vya upinzani vikifanya tamasha ,hawa waalikwa toka serikalini watahudhuria ? Wacha polisi aalikwe rasi mwenyewe na mkuu wa majeshi katika kongamano ,wataweza kuhudhuria au watatoa udhuru kuwa wameshikwa na tumbo la kuendesha ? CCM lazima wang'oke. Kule Zanzibar wameshang'olewa wamebaki kujigandisha tu japo wanabanduka lakini palipobaki ambapo watu wake bado hawajawa walevi wa gongo ni hapa Tanganyika lini na wao wataonekana ni walevi wa gongo ?
 
Mzee Mwanakijiji, hili suala si dogo kam linavoonekana, nje ya nchi wa Tanzania tunanuka kwa suala hili.Nilikuwa Washington mwezi wa November 2008, actually waafrika wenzetu wanatucheka as if wote tunashiriki suala laushirikina kwa kutumia viungo vya albino.
Suluhisho ni kulipa uzito ili wale wanaolishabikia kiushirikina waache kabisa.

Hivi kwanini tunaendelea kilijadili...na kwanini mwanakijiji...akabadili heading akaweka yake na sio ya habari yenyewe?
Mzee kuna kitu unafanyia utafiti kujua mawazo?
 
Hivi kwanini tunaendelea kilijadili...na kwanini mwanakijiji...akabadili heading akaweka yake na sio ya habari yenyewe?
Mzee kuna kitu unafanyia utafiti kujua mawazo?

Hapana, nilichotaka kuonesha ni kuwa kongamano hilo ni la kupongeza hatua ya serikali "kukemea" mauaji ya Albino, na siyo kufanikiwa au kupambana na mauaji ya Albino. Ndiyo maana nimesema sisi ni watu wa ajabu, kwamba tunaandaaa tamasha la kupongeza "maneno" kwani kukemea ni maneno tu! Sasa wameanza kukemea toka lini! Mwisho tutajikuta tunaandaa tamasha la kupongeza machozi ya Waziri Mkuu!
 
Back
Top Bottom