engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
JUKWAA la Wahariri nchini (TEF) limesema kukamatwa kwa Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Free Media inayochapisha magazeti ya Tanzania Daima na Sayari, Absalom Kibanda, ni utekelezaji wa mpango wa siri wa serikali, unaotokana na chama tawala kuitaka iwashughulikie waandishi wa habari ambao wamekuwa mstari wa mbele kufichua ufisadi wa serikali.
Kibanda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, anakabiliwa na tuhuma za uchochezi, na anatarajiwa kufikishwa mahakamani Kisutu, Dar es Salaam leo kujibu tuhuma hizo.
Katika kuonyesha wahariri wanajua undani wa sakata hilo, jana Jukwaa la Wahariri lilitoa taarifa kwa vyombo vya habari likisema hatua ya serikali kutumia polisi kuwakamata waandishi wa habari na kuwafungulia kesi za jinai kunaihatarisha serikali yenyewe na kuuweka pabaya mustakabali mzima wa taifa.
Tuhuma zinazomkabili Kibanda zinatokana na makala iliyoandikwa na mwanasafu wa wiki katika gazeti hili toleo la Jumatano, Samson Mwigamba, wa Arusha, Novemba 30, 2011.
Katika makala hiyo, Mwigamba anawaasa polisi kutumia uungwana na akili wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao, hasa wanapotumia nguvu kubwa kudhibiti wananchi ambao wanatetea masilahi ya umma yanayowahusu hata wao wenyewe. Polisi wanadai makala hiyo ni ya uchochezi.
Kibanda hakuandika makala hiyo, lakini anashitakiwa kwa mujibu wa wadhifa wake kama mhariri mtendaji wa gazeti lililoichapisha, kwa mujibu wa sheria ya magazeti ya mwaka 1976, ambayo ni miongoni mwa sheria mbaya ambazo Tume ya Nyalali, wanaharakati na wanasiasa, wamekuwa wakishauri zifutwe au zirekebishwe tangu mwaka 1992.
Baada ya kuwa wamemhoji na kumfikisha mahakamani Mwigamba siku kadhaa zilizopita, walimgeukia Kibanda; naye akajisalimisha makao makuu ya Jeshi la Polisi, Dar es Salaam, Desemba 16, mwaka huu; akadhaminiwa kwa sh milioni tano na kuripoti tena polisi makao makuu jana, na kudhaminiwa tena kwa kiasi hicho hicho cha fedha.
Kwa mujibu wa taarifa ya Jukwaa la Wahariri iliyosainiwa na Katibu, Neville Meena, kukamatwa kwa Kibanda na Mwigamba na kufunguliwa mashitaka kumedhihirisha taarifa ambazo zimevuja kutoka kwenye vyanzo kadhaa serikalini na chama tawala (CCM) kwamba kuna mpango wa serikali kunyamazisha ukosoaji kwa kupambana na waandishi na vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikifukua maovu ya watawala.
"Mashitaka haya dhidi ya Kibanda na Mwigamba yanatushawishi kuamini taarifa zisizo rasmi juu ya kuwapo kwa mpango wa kuwashughulikia baadhi ya wahariri na waandishi wa habari ambao wamekuwa msitari wa mbele kukosoa waziwazi mienendo ya watawala," imesema sehemu ya taarifa hiyo.
TEF imesema hatua ya kumkamata Kibanda na Mwigamba imekiuka utaratibu wa siku zote ambao serikali kupitia Idara ya Habari (Maelezo) imekuwa ikiwaita wahusika na kuwahoji sababu za kuandika, kuchapisha ama kutangaza habari ambazo zinadhaniwa kukiuka maadili.
Wahariri hao pamoja na kupinga mpango huo mbovu, wameitaka serikali kuacha mara moja kuwakamata wahariri na waandishi wa habari, kwa kuwa hatua hiyo si tu inaathiri dhana nzima ya utawala bora wa nchi, bali inaliweka taifa katika hatari ya kutumbukia katika uovu uliokithiri, hasa pale wenye dhamana watakapofanya wapendavyo baada ya kuviziba mdomo vyombo vya habari.
"Kwanza makala ambayo ni chimbuko la kukamatwa kwa Mwigamba na baadaye Kibanda haikuwahi kulalamikiwa na Ofisi ya Msajili wa Magazeti kama ambavyo imekuwa ikifanyika kwa taarifa nyingine nyingi, si kwa gazeti la Tanzania Daima tu, bali hata kwa magazeti mengine.
"Kwa maana hiyo, hakuna barua yoyote kutoka Maelezo ambayo iliwasilishwa Tanzania Daima ikimtaka mhariri mtendaji kutoa maelezo ya kimaandishi au kufika kwa msajili kujibu tuhuma za ukiukwaji wa maadili ama sheria katika makala hiyo ya Novemba 30, 2011," imesema taarifa hiyo ambayo imechapishwa katika ukurasa wa tatu wa gazeti hili.
Wakati Jukwaa hilo likitoa tamko, Kibanda anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo, baada ya jana kushindikana kutokana na kile kilichodaiwa na polisi kuendelea kuchukua maelezo ya Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd inayochapa gazeti la Tanzania Daima.
Ijumaa iliyopita, Kibanda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini alijisalimisha polisi ambako baada ya kumhoji kwa zaidi ya saa tatu, aliachiwa kwa dhamana ya sh milioni tano, iliyotolewa na Mkurugenzi wa gazeti la Mwanahalisi, Saed Kubenea, akitakiwa kuripoti tena jana.
Hata hivyo, katika hatua isiyo ya kawaida, huku wakijua kwamba bado ana dhamana, polisi walimzuia tena Kibanda akiwa na mawakili wake Nyaronyo Kicheere na Juma Thomas, wakamlazimisha awe na mdhamini mwingine kwa kiasi cha sh milioni tano. Mhariri Mtendaji wa gazeti la Hoja, Yasin Sadiq, alimdhamini.
Tayari habari zisizothibitishwa zinataja baadhi ya wahariri walio kwenye orodha ya kukamatwa na kushitakiwa katika mkakati wa serikali kutumia polisi kutisha waandishi wa habari na wakosoaji wengine wa serikali.
Hata kabla ya Jukwaa la Wahariri kutoa tamko lao, vyanzo kadhaa vya habari serikalini vililidokeza gazeti hili kwamba polisi wanatekeleza mpango huu kwa amri ya wakubwa wanaokerwa na ukosoaji unaofanya na baadhi ya waandishi, wanasiasa, wanaharakati na vyombo vya habari
na Janet Josiah
Kibanda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, anakabiliwa na tuhuma za uchochezi, na anatarajiwa kufikishwa mahakamani Kisutu, Dar es Salaam leo kujibu tuhuma hizo.
Katika kuonyesha wahariri wanajua undani wa sakata hilo, jana Jukwaa la Wahariri lilitoa taarifa kwa vyombo vya habari likisema hatua ya serikali kutumia polisi kuwakamata waandishi wa habari na kuwafungulia kesi za jinai kunaihatarisha serikali yenyewe na kuuweka pabaya mustakabali mzima wa taifa.
Tuhuma zinazomkabili Kibanda zinatokana na makala iliyoandikwa na mwanasafu wa wiki katika gazeti hili toleo la Jumatano, Samson Mwigamba, wa Arusha, Novemba 30, 2011.
Katika makala hiyo, Mwigamba anawaasa polisi kutumia uungwana na akili wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao, hasa wanapotumia nguvu kubwa kudhibiti wananchi ambao wanatetea masilahi ya umma yanayowahusu hata wao wenyewe. Polisi wanadai makala hiyo ni ya uchochezi.
Kibanda hakuandika makala hiyo, lakini anashitakiwa kwa mujibu wa wadhifa wake kama mhariri mtendaji wa gazeti lililoichapisha, kwa mujibu wa sheria ya magazeti ya mwaka 1976, ambayo ni miongoni mwa sheria mbaya ambazo Tume ya Nyalali, wanaharakati na wanasiasa, wamekuwa wakishauri zifutwe au zirekebishwe tangu mwaka 1992.
Baada ya kuwa wamemhoji na kumfikisha mahakamani Mwigamba siku kadhaa zilizopita, walimgeukia Kibanda; naye akajisalimisha makao makuu ya Jeshi la Polisi, Dar es Salaam, Desemba 16, mwaka huu; akadhaminiwa kwa sh milioni tano na kuripoti tena polisi makao makuu jana, na kudhaminiwa tena kwa kiasi hicho hicho cha fedha.
Kwa mujibu wa taarifa ya Jukwaa la Wahariri iliyosainiwa na Katibu, Neville Meena, kukamatwa kwa Kibanda na Mwigamba na kufunguliwa mashitaka kumedhihirisha taarifa ambazo zimevuja kutoka kwenye vyanzo kadhaa serikalini na chama tawala (CCM) kwamba kuna mpango wa serikali kunyamazisha ukosoaji kwa kupambana na waandishi na vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikifukua maovu ya watawala.
"Mashitaka haya dhidi ya Kibanda na Mwigamba yanatushawishi kuamini taarifa zisizo rasmi juu ya kuwapo kwa mpango wa kuwashughulikia baadhi ya wahariri na waandishi wa habari ambao wamekuwa msitari wa mbele kukosoa waziwazi mienendo ya watawala," imesema sehemu ya taarifa hiyo.
TEF imesema hatua ya kumkamata Kibanda na Mwigamba imekiuka utaratibu wa siku zote ambao serikali kupitia Idara ya Habari (Maelezo) imekuwa ikiwaita wahusika na kuwahoji sababu za kuandika, kuchapisha ama kutangaza habari ambazo zinadhaniwa kukiuka maadili.
Wahariri hao pamoja na kupinga mpango huo mbovu, wameitaka serikali kuacha mara moja kuwakamata wahariri na waandishi wa habari, kwa kuwa hatua hiyo si tu inaathiri dhana nzima ya utawala bora wa nchi, bali inaliweka taifa katika hatari ya kutumbukia katika uovu uliokithiri, hasa pale wenye dhamana watakapofanya wapendavyo baada ya kuviziba mdomo vyombo vya habari.
"Kwanza makala ambayo ni chimbuko la kukamatwa kwa Mwigamba na baadaye Kibanda haikuwahi kulalamikiwa na Ofisi ya Msajili wa Magazeti kama ambavyo imekuwa ikifanyika kwa taarifa nyingine nyingi, si kwa gazeti la Tanzania Daima tu, bali hata kwa magazeti mengine.
"Kwa maana hiyo, hakuna barua yoyote kutoka Maelezo ambayo iliwasilishwa Tanzania Daima ikimtaka mhariri mtendaji kutoa maelezo ya kimaandishi au kufika kwa msajili kujibu tuhuma za ukiukwaji wa maadili ama sheria katika makala hiyo ya Novemba 30, 2011," imesema taarifa hiyo ambayo imechapishwa katika ukurasa wa tatu wa gazeti hili.
Wakati Jukwaa hilo likitoa tamko, Kibanda anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo, baada ya jana kushindikana kutokana na kile kilichodaiwa na polisi kuendelea kuchukua maelezo ya Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd inayochapa gazeti la Tanzania Daima.
Ijumaa iliyopita, Kibanda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini alijisalimisha polisi ambako baada ya kumhoji kwa zaidi ya saa tatu, aliachiwa kwa dhamana ya sh milioni tano, iliyotolewa na Mkurugenzi wa gazeti la Mwanahalisi, Saed Kubenea, akitakiwa kuripoti tena jana.
Hata hivyo, katika hatua isiyo ya kawaida, huku wakijua kwamba bado ana dhamana, polisi walimzuia tena Kibanda akiwa na mawakili wake Nyaronyo Kicheere na Juma Thomas, wakamlazimisha awe na mdhamini mwingine kwa kiasi cha sh milioni tano. Mhariri Mtendaji wa gazeti la Hoja, Yasin Sadiq, alimdhamini.
Tayari habari zisizothibitishwa zinataja baadhi ya wahariri walio kwenye orodha ya kukamatwa na kushitakiwa katika mkakati wa serikali kutumia polisi kutisha waandishi wa habari na wakosoaji wengine wa serikali.
Hata kabla ya Jukwaa la Wahariri kutoa tamko lao, vyanzo kadhaa vya habari serikalini vililidokeza gazeti hili kwamba polisi wanatekeleza mpango huu kwa amri ya wakubwa wanaokerwa na ukosoaji unaofanya na baadhi ya waandishi, wanasiasa, wanaharakati na vyombo vya habari
na Janet Josiah