Kutokana na message alizoziacha hayati diwani wa kata ya mlangali ludewa, na message hiyo kusomwa na mwendesha mazishi, mh. Huyo aliamua kujinyonga baada ya kutapeliwa sh. Mil 81 na mganga mmoja wa kienyeji mzaliwa wa mlangali (maarufu kama MSABE) anayeishi dar, mganga huyo aligoma kulipa katakata. Sh mil 41 kati ya hizo ni mali ya saccos mlangali na zilizobaki ni mali ya familia. Mazishi ya diwani huyo yalihudhuriwa na maelfu ya watu kutoka sehemu mbalimbali. Hii ni ishara kwamba Kacheche alipendwa na wengi. Hata hivyo imekuwa ni gumzo kwa baadhi ya watu ambao waliweka fedha kwenye saccos hiyo. Diwani huyo alikuwa ni meneja wa saccos hiyo.