Mi nadhani ifike mahali tuukubali ukweli kwamba mke/mume wa mtu ndie the first one no matter what, hata ukiwa unatoka naye ujue ana familia na ukweli ulio wazi ni kwamba kwa nyumba ndogo anachofata ni 20% na 80% ziko kwa nyumba kubwa. Na mara zote ni wachache sana wanaokubali kuacha 80% na kufata 20%. So ukiwa unatoka na mume au mke wa tu ujijue we ni mshka pembe so no need to boost. au kwa ufupi kipoozeo. Tafakari na chukua hatua.
Kama mke ndiyo first, naomba tujiulize haya yafuatayo:
1. Kwanini nyumba ndogo anunuliwe usafiri na ilihali mke hana hata bajaji?
2. Kwanini nyumba ndogo awekewe mradi na mke hana shughuli maalum ya kufanya?
3. Kwanini nyumba ndogo ajengewe nyumba na ilihali mke hana hata kiwanja?
4. Kwanini nyumba ndogo ndiyo huwa inapelekwa shopping majuu ama inaambatana Mzee kwenda trip za nje na ilihali mke hajawahi hata kufika Nairobi?
Kama ni kweli huko kwenye nyumba ndogo kuna 20%, je, hiyo asilimia 20 ina justify heavy investment/special treatment kama niliyotaja hapo juu? Kama kwa mke kuna 80%, basi mke angepewa top priority ya kufanyiwa very heavy investment na kupewa special treatment ukilinganisha na nyuma ndogo.
Najua Carmel utauliza kwanini mume hamwachi/hamtaliki mkewe? Wapo ambao wanaogopa dini zao (wakristo) kwamba kilichounganishwa na Mungu binadam hawezi kukitenganisha. Wako wanaoogopa familia zao (wazazi) so wanabaki wanavumiliana ndani ya nyumba hata kama wameishachokana. Wako ambao wanaogopa jamii iliyowazunguka, siku hizi siyo fashion tena kuoa na kuacha, lakini ku-cheat "some how iko acceptable". Kuoa na kuacha wengine wanaichukulia kama failure, lakini ku-cheat kwa siri ama kuwa na nyumba ndogo openly ni kawaida na inakubalika na hakuna mtu anaweza kushangaa.
Nyumba ndogo ikichimba biti, mzee lazima suruali ibane na yuko tayari kwenda kukopa ili amfurahishe nyumba ndogo. Lakini mke hata achimbe biti kali kiasi gani mume wala hashituki. Sasa kwanini suruali ibane wakati kuna 20% tu, na kule kwenye uzito mkubwa mume ndo hajali kabisa?
Mwisho, kuna mentality kwamba waafrika ndo tunaongoza kwa ku-cheat na kwamba wazungu wana afadhali. Ukweli ni kwamba wote ni ngoma droo. US ikifika nyakati za uchaguzi ndo utajua hata magavana na maseneta huwa wana cheat, na wengine wana cheat na wasichana wanaofanya kazi za kampeni. Ndio maana ndoa nyingi za celebs huwa hazidumu kwa kuwa paparazi saa zote wako migongoni. Kuna mtu alijua Tiger Woods alishalamba wanawake zaidi 10 akiwa kwenye ndoa yake? Mume wa Sandra Bullock anasema hata wakijitokeza 1,000,000 ni sawa tu, hoja ni kwamba ka-cheat. Hiyo pekee inaonyesha kwamba alishacheat na wengi sana. Yule Mzee wa Carolina alikuwa anafuata totoz yake Argentina, ameacha mkewe nyumbani. John Edwards kalamba dada wa Kampeni kasingizia kuwa ni gf wa msaidizi wake. Hiyo ni mifano michache tu. Cheating haina rangi wala kabila, labda ni tabia ya wanaume ama ndo asili yetu.
Kwanini wanaume wako radhi kutumia hela nyingi sana na kuingia gharama kubwa sana wanapokuwa wanaenda nje ya ndoa zao? Mwanaume akienda ku-cheat yuko tayari kulipia tiketi ya ndege, na kulala Ngurudoto Lodge, lakini akienda na mkewe wanapanda basi la kawaida na wanalala AM Investment Hotel. Kweli huko kuna 20% ama huwa kuna limbwata?