Sipendi ujinga

Nimejichanga weeeee nikafanikiwa kununua ka Vits kangu cha kunisaidia kwenye misele yangu. Siku moja nipo na baba mkwe wangu nampeleka hospitali, tukiwa tunasubiri kuruhusiwa kwenye mataa pembeni kulikuwa na Range Rover anaendesha kijana kama mimi tu. Baba mkwe wangu akaniuliza, *"mkwe!* *umemuona mwanaume huyo?"* Nilishikwa na hasira nikajikuta nimemjibu *"kuwa na baba mkwe tajiri raha sana, jamaa alipewa hiyo gari kama zawadi na baba mkwe wake siku ya harusi yake"* Basi baba mkwe wangu akanyamaza kimya akawa mdooooooogo.

*Pumbavu!* *huwa sipendi dharau mimi*
 
Mwalimu wa zamu wa kihindi alinituma niende darasani halafu nirudi na Kassim, mi nikaenda nikachukua kasimu ka Mwl. Aliyekua anafundisha nikampelekea mwl. wa zamu, ile na fika tu akaniuliza; wapi iko Kassim , nikamwambia haka hapa.

"Sipendagi ujinga wa kutumwatumwa Mimi"
 
1474821420883.jpg
 
Jinsi ya kuondoa pattern lock kwenye cm ya mumeo/mpnz wako..........!!!

Kwanza muwekee maji ya kuoga akienda kuoga chukua cm yake iweke chaji kwa angalau asilimia 80 kisha muandalie chakula akishakula kaeni angalieni Tv kwa saa 2 mukipiga story za kujenga kisha kaitoe cm mpe mwenyewe cm yake utakuwa umejifunza jinsi ya kumuhudumia mumeo shenzy sana.............

[HASHTAG]#Unataka[/HASHTAG] kuona nini kwenye cm umbea tu utakufa kwa presha cheza nafas yako, michepuko n matokeo ya uzembe wako tu!‼ sipendagi ujinga mm
 
_ *Jamaa kamuaga mkewe anaenda semina Songea kwa wiki nzima kumbe kahamia kwa demu nyumba ya pili toka kwake. Siku ya 1 kalala asubuhi alipoamka kachungulia kwake kukoje, si kamuona jamaa yuko nje ya nyumba yake kavaa taulo lake anapiga mswaki. Akapiga kelele, 'We nani?', Jamaa akajibu, 'Mshikaji mambo ya mjini, mume wa huyu demu kasafiri kaenda Songea mi ndo najivinjari hapa'. Mume kajibu kwa uchungu, Shenzi mkubwa, ngoja nirudi toka Songea nakuua.*_

*Mniache mimi sipendi Ujinga Ujinga
 
Mademu wawil walikua wamekaa disco m1 mbovu mwingine mkali nikawafuata
*MIMI*:mambo vip dada
*DEM MBOVU*:kwa nyodo poaa
*MIMI*:samahani unajua ku dance
*DEM MBOVU*:ndioo huku akitabasamu
*MiMi*:bhas nlikua naomba ukadance nataka niongee na rafik ako

*spendi ujinga mimi*
 
Ishawahi kutokea Pale nilipokutana njiani na Mwalimu aliyenifundisha MATHS secondary afu akaniambia nimuelekeze njia ya kwenda sehemu fulani.
*Nenda mbele kama 2KM hivi kisha kata kushoto,ila hakikisha ANGLE inakuwa ni 30.5 KUSINI MASHARIKI.Kisha tumia PYTHAGORAS na hakikisha una FOUR FIGURE ili kupata thamani ya ANGLE.*

Mwalimu alisonya na kuondoka.

Stakagi ujinga kabisa mimi, wakati ananichapa alifikiri sifa
 
Back
Top Bottom