Kipeperushi
Senior Member
- Aug 17, 2011
- 167
- 33
Habari za leo wanaJF. Naomba msaada/ushauri toka kwenu jamani, computer yangu imegoma kuonyesha Start Menu. Kinachotokea ni kwamba ninapoiwasha, baada ya ku-load katika hatua zile za mwanzo, pale ninapotaka kuingia kwenye program zingine zilizopo kwenye start menu, computer inagoma ku-display start menu. Computer yangu (laptop) ina Microsoft Windows XP ya 2007. Kwenye display nili-opt ku-hide desktop. Mara ya mwisho nili-download Mozilla Fire Fox, na nikaifanya kuwa "default browzer" badala ya internet explorer iliyokuja nayo. Kitu ambacho nakumbuka ni kwamba nilisahau ku-uninstall internet explorer kabla ya ku-install mozilla. Baada ya ku-install mozilla niliendelea ku-surf kutumia mozilla. Tatizo la Start Menu limejitokeza baada ya kuizima computer baada ya kumaliza surffing juzi. Naomba nisaidieni wakuu nifanye nini ili niendelee kutumia computer yangu?