Wanitakiani
JF-Expert Member
- Apr 18, 2008
- 641
- 135
Serikali ina mpango wa kuagiza Madaktari kutoka nje ya nchi kuziba pengo lililoachwa na Madaktari waliogoma. Tumesikia pia Waalimu nao iwapo hawatatimiziwa madai yao watagoma ktk wiki mbili zijazo,jambo ambalo linawezekana kutokana na ukweli kuwa madai yao hayapishani sana na yale ya Madaktari. Pamoja na raslimali tulizo nazo Tz tunaambiwa nchi hii haina pesa na ni maskini!
Nina maswali yananitatiza katika njia bora za kutatua matatizo yetu, naomba Wanajamvi mnisaidie maswali yafuatayo:
Kwakweli sipati picha! Naogopa!
Nina maswali yananitatiza katika njia bora za kutatua matatizo yetu, naomba Wanajamvi mnisaidie maswali yafuatayo:
- Kuna mikakati gani ya kuhakiki ili kujua Madaktari wanaokuja toka nje ni qualified? Nachojua mimi ukiombwa upunguze manpower yako utatoa wale usiowataka,hutatoa jembe unalolitegemea na badala yake utatoa jembe dhaifu, legelege,lisilo na tija;
- Ni gharama kiasi gani itatumika kuwaagiza, kuwalipa Madaktari hao wa kigeni? Je, watalipwa mishahara kama waliyokuwa wakilipwa Madaktari waliogoma au watalipwa kama Experts (TX?
- Madaktari hao wageni wakija watakuja na dawa? watakuja na vifaa? Wataondoa kero ya wagonjwa kulala chini au watatu watatu vitandani? Watapunguzaje vifo vingi vya akina mama na watoto walio chini ya miaka 5? Wataboresha miundombinu ya hospitali zetu?
- Ikitokea Waalimu nao wakagoma, Serikali itaagiza Waalimu wangaoi na kutoka nchi gani? je, watatosheleza mahitaji hasa ya shule za watoto wetu akina Kayumba?
- Iwapo Waalimu watatoa nje Serikali ina mikakati gani ktk somo la Kiswahili na lile la Civic Education? Au masomo hayo yatafutwa kwenye mitaala ya Elimu?
- Kwa Maswali yote hapo juu Serikali imetenga kiasi gani kutumia manpower ya kutoka nje kwenye sekta hizo hadi hapo itakaposomesha waaalimu na madaktari wa kutosha sijuwi miaka mingapi ijayo? Je, ikitokea Watumishi wa Serikali ktk sekta nyingine nao wakagoma (hatuombi hayo)serikali imejizatiti vipi?
Kwakweli sipati picha! Naogopa!