View attachment 50591Mheshimiwa Edward Lowasa akimnadi mgombea wa ccm,kijana mtanashati na mjenga hoja za nguvu mheshimiwa Sioi Sumari alisema"Nawaahidi, kuwa sasa matatizo yenu yamekwisha, nimekuja kufunga mjadala wa ajenda ya matatizo ya ardhi, maji na umeme, mkimchagua Sioi Aprili 10 saa 3.30 asubuhi ataapishwa na ikifika saa 7.30 mchana mimi Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM wa Mkoa wa Arusha na wabunge wenzangu, tutamwita Waziri wa Ardhi, Mama Tibaijuka (Profesa Anna) ili achukue jalada la suala la ardhi na maji na kulipeleka kwa Rais. Aliendelea kumnadi mbunge mtarajiwa kuwa Sioi "Ni mtu makini na mwenye uwezo. Naomba mumwamini na mumchague, nimekuja kumwombea kura kama mwana CCM mwenzangu. Lakini hata nikimnadi kama mkwe si dhambi. Alimpenda Pamela, watu waache kidomodomo. Ni kijana safi, kwa hivyo nisimsifie kwa vile mimi ni mwanasiasa? Mkimchagua Sioi nawaahidi kuwa mtapata maendeleo makubwa maana tutashirikiana naye nawaahidi hivyo mimi si mtu wa domo ni mtu wa kazi,
MHESHIMIWA EL.NA waziri mkuu staafu tunaomba tumia cheo chako muapisheni siku ya jumapili Tarehe 01.04.itapendeza zaidi.