Sintopiga kura yangu 2010

Recta I wish wewe ndie ungekuwa mgombea maana unajua kuchambua fikra na mahitaji ya wananchi wako. Umezungumza jambo moja kubwa na la msingi kuwa kampeni si wakati wa kumtafuta aliye bora ila ubora wa mgombea unatakiwa uonekane toka mwanzo nyakati za nyuma. Kwa hili nakuunga mkono lakini piaukazungumzia kuwa kampeni ni sehemu ya kufanyia ushawishi ili mgombea auzike kwa wapiga kura ni kweli kabisa lakini wasitake tuwanunue kwa uongo wao ila kwa facts zao. Unajua kujua kuongea sio kujua kutenda ingawa kuna maana kubwa sana unapojua kuongea na kujua kutenda pia

Pia nashukuru kwa kujaribu kuona baadhi ya ahadi za wagombea niliowachambua hapo juu kuwa ni za uongo na uzandiki wa hali ya juu.

Mwisho niseme kuwa tunahitaji kiongozi mwanamapinduzi mwenye itikadi ambayo hata wananchi wenyewe wataiona kama kulamba sumu vile lakini matokeo yake baadaye yawe ya kusherehekea na siyo kiongozi ambaye maneno yake na misimamo yake ni kama kulamba asali lakini matokeo yake yawe kilio na kusaga meno.

Kuambiwa elimu bure kila siku sio jambo la kushangilia tunataka serikali ambayo itahahakikisha kuwa wananchi wanaweza kutumia akili zao na rasilimali zilizopo kama vile madini, misitu, ardhi na nyinginezo kujikwamua kimaisha ikiwa ni pamoja na kusomesha watoto wao kwa kulipa karo ya shule. Leo hii siwezi kushangilia elimu ya bure kwa sababu ina maana tutaendelea kuibiwa na viongozi wachache kwa sababu hiyo hiyo.

Nashukuru sana Mokoyo kwa maelezo yako na heshima uliyonipa hadi kudhani kuwa ningefaa kuwa mmoja wa wagombea. Nashukuru kama nilichokiandika kimekushawishi kwa kiasi chochote kuona ukweli wa jinsi ambavyo taifa hili linalosuasua kwenda mbele, linavyohitaji juhudi na maarifa ya kila mmoja wetu kulikwamua katika kisiki ambapo limegota.

Mkuu, naamini kuwa kuwezesha waTanzania mmoja mmoja ni hatua ya juu na ya muhimu kabisa katika kujenga Taifa linalojitegemea. Wananchi wakiweza kushiriki katika kila nyanja ya uchumi wa nchi yao, ni dhahiri kuwa Taifa litanufaika kwa kiasi kikubwa sana, na umasikini wetu utakuwa historia. Ni kweli kabisa hayo unayosema.

Kwa upande mwingine, naamini tuko nyuma sana katika kuondoa ujinga na umasikini nchini (tukiweka pembeni maradhi na rushwa). Hatua ya kwanza ni lazima ichukuliwe ili wananchi waweze kushiriki constructively katika kujiletea maendeleo yao kwa ufanisi mkubwa. Hatua hiyo ndugu yangu ni kuhakikisha kuwa wananchi kwa asilimia kubwa iwezekanavyo wanakuwa na afya njema wakati wote, na wanaepuka magonjwa yanayoweza kuepukwa (kama, Malaria, kipindipindu na mengine ya aibu). Ni aibu kuwa na jamii ambayo watoto wanaozaliwa wanakuwa katika hatari ya kufa wangali wachanga. Ni aibu kuwa asimilia ya wakina mama wanaokufa wakijifungua bado ni kubwa na ya kutisha katika nchi yenye uhuru unaokaribia miaka Hamsini. Hii hali inabidi serikali ipambane nayo kwa kila hali.

Ili tuweze kusimamia na kufaidika vyema na rasilimali zetu, ni lazima tuwe na jamii ambayo imeelimika vya kutosha na hapo ndipo wengine wanaweza kuwategemea wao kuelimika na kuwa huru kiuchumi.
Wachina walifanya hivyo, na ndio siri ya maendeleo yao ya sasa na miaka mingi ijayo. Hatua ya kwanza ya kuhakikisha kuwa jamii ya Tanzania inapata elimu ya kutosha, ni lazima ichukuliwe na serikali kwakuwa uchumi wa nchi kwa sasa uko mikononi mwa serikali inayotawala. Hili likiwezekana, nchi itakuwa salama na yenye heshima na maendeleo zaidi.

Mkuu wangu, nakuomba niendelee kukushawishi upige kura mwaka huu kwa uhuru na haki yako ili uweze kuona mabadiliko au maendeleo unayohitaji. Ni imani yangu kuwa, kama hatutashiriki kwa wingi kupiga kura, uwezekano mkubwa wa kuongozwa na tusiotaka watuongoze.
 
Please! kuwa serious japo kidogo,hatuja test the difference,make it happen! We porojo si umezizoea? Tunataka kuachana nazo sasa.

Mkuu!! kimsingi nishazichoka porojo ya kisiasa kuliko unavyodhani, nchi hii haijawahi kukosa ideas, zipo chungu nzima!! kilichokosekana ni uongozi makini na adilifu utakaoweza kukidhi mahitaji ya sasa kwa maendeleo ya nchi yetu na watu wake, nasikitika kuwa katika uchaguzi wa uraisi wa mwaka huu hatuna "chaguo" hilo.
 

Nashukuru sana Mokoyo kwa maelezo yako na heshima uliyonipa hadi kudhani kuwa ningefaa kuwa mmoja wa wagombea. Nashukuru kama nilichokiandika kimekushawishi kwa kiasi chochote kuona ukweli wa jinsi ambavyo taifa hili linalosuasua kwenda mbele, linavyohitaji juhudi na maarifa ya kila mmoja wetu kulikwamua katika kisiki ambapo limegota.

Mkuu, naamini kuwa kuwezesha waTanzania mmoja mmoja ni hatua ya juu na ya muhimu kabisa katika kujenga Taifa linalojitegemea. Wananchi wakiweza kushiriki katika kila nyanja ya uchumi wa nchi yao, ni dhahiri kuwa Taifa litanufaika kwa kiasi kikubwa sana, na umasikini wetu utakuwa historia. Ni kweli kabisa hayo unayosema.

Kwa upande mwingine, naamini tuko nyuma sana katika kuondoa ujinga na umasikini nchini (tukiweka pembeni maradhi na rushwa). Hatua ya kwanza ni lazima ichukuliwe ili wananchi waweze kushiriki constructively katika kujiletea maendeleo yao kwa ufanisi mkubwa. Hatua hiyo ndugu yangu ni kuhakikisha kuwa wananchi kwa asilimia kubwa iwezekanavyo wanakuwa na afya njema wakati wote, na wanaepuka magonjwa yanayoweza kuepukwa (kama, Malaria, kipindipindu na mengine ya aibu). Ni aibu kuwa na jamii ambayo watoto wanaozaliwa wanakuwa katika hatari ya kufa wangali wachanga. Ni aibu kuwa asimilia ya wakina mama wanaokufa wakijifungua bado ni kubwa na ya kutisha katika nchi yenye uhuru unaokaribia miaka Hamsini. Hii hali inabidi serikali ipambane nayo kwa kila hali.

Ili tuweze kusimamia na kufaidika vyema na rasilimali zetu, ni lazima tuwe na jamii ambayo imeelimika vya kutosha na hapo ndipo wengine wanaweza kuwategemea wao kuelimika na kuwa huru kiuchumi.
Wachina walifanya hivyo, na ndio siri ya maendeleo yao ya sasa na miaka mingi ijayo. Hatua ya kwanza ya kuhakikisha kuwa jamii ya Tanzania inapata elimu ya kutosha, ni lazima ichukuliwe na serikali kwakuwa uchumi wa nchi kwa sasa uko mikononi mwa serikali inayotawala. Hili likiwezekana, nchi itakuwa salama na yenye heshima na maendeleo zaidi.

Mkuu wangu, nakuomba niendelee kukushawishi upige kura mwaka huu kwa uhuru na haki yako ili uweze kuona mabadiliko au maendeleo unayohitaji. Ni imani yangu kuwa, kama hatutashiriki kwa wingi kupiga kura, uwezekano mkubwa wa kuongozwa na tusiotaka watuongoze.
Recta I real appreciate your analysis based on the fact that any member of political party can read this without being annoyed and find him/herself electing the candidate from the opposing party. In real sense you have shown how matured you are in the socio-political arena and this is kind of the people we want in making sure that civil education is there in rural and urban areas for the citizens to to elect their leaders not through corruption rather through the workable policies.

Tunahitaji viongozi wenye kutambua umuhimu wa elimu kiasi cha kuakikisha kuwa wanafunzi wanasoma kwa uwepo wa kutosha wa vitabu na Waalimu wenye kuelewa wanachokifundisha. Ni ukweli usiojificha kuwa msingi wa taifa lolote ni elimu na wala sio maneno na blah blah zisizo na misingi ya utekelezaji. Kilimo ndio mhimili wa maisha ya watanzania takribani 80% lakini bado hakijapata kiongozi mwenye niadhabiti ya kusimamia sera zake.


Nasikitika sana kuwa wananchi wa Watanzania tunasahau kuwa jukumu la kuwapangia masuala ya kufanyia viongozi hawa ni letu na sio viongozi hawa kujipangia nini watafanya jambao ambalo linakuwa gumu kuwawajibisha pale ambapo wakati wa kufanyia hivyo unapofika. Tuache ushabiki na kupiga kura kwa ushabiki tuwape majukumu viongozi hawa ili iwe rahisi kuwasimamia katika kuhakikisha kuwa uchumi wa nchi yetu unakuwa na tunajiendesha wenyewe.

Kura ni haki yangu Recta na sintoitoa kwa misingi ya ushabiki wa ukereketwa wa mtu au chama Fulani ila kwa misingi ya kuikomboa nchi yangu isiangamie kwa kuwa na viongozi mafedhuli na mabradhuli.
 
Hainiingii akilini kusikia mtu mzima kama wewe huoni umuhimu wa kupiga kura. Kutopiga kwako kura ni kuruhusu iongozi wabovu waendelee kuwa madarakani. Piga kura mkubwa kama ulijiandikisha!

I'll mobilize all Tanzanians to vote for CCM. Go JK
 
ulitakiwa usome ILANI .

Pili ulitakiwa huji utekelezaji wa ilani na nia dhahiri za kutekeleza.

Anyway ndio demkrasia ,do whaterver the wacky you wanna do.
 
Kwanza nianze kwa kusema kuwa mimi sio mwanachama wala mkereketwa wa chama chochote kile sio CCM, Chadema, CUF, TLP, NCCR-Mageuzi au chochote kingine.

Baada ya kusema hayo kwa kifupi tu sababu iliyonifanya kuamua kutokupiga kura yangu kwa mwaka huu wa 2010. Kimsingi naipenda nchi yangu na ningetamani siku moja iwe nchi yenye uchumi imara, amani na utulivu madhubuti na zaidi ya yote iwe na viongozi madhubuti ambao ndio chanzo cha hayo yote mema. Siku zote nimekuwa nikiwaza kuwa na viongozi wenye mawazo mbadala wa kubadilisha mwelekeo wa nchi hii.

Kubadilisha kwangu msimamo wa kupiga kura mwaka huu kumetokana na kukosa wagombea wenye nia dhabiti ya kuibadilisha nchi hii itoke katika dimbwi la ufukara. Hakuna hasiyejua kuwa nchi yetu inakabiliwa na matatizo vyungu nzima kwenye kila sekta kuanzia elimu, barabara, kilimo, utalii, madini, afya n.k. Lakini jambo la kushangaza bado wagombea Urais tulio nao mwaka huu wamekuwa wagombea wale wale hapa nikiwa na maana ya wagombea wenye mawazo yaleyale mgando kuwa matatizo ya nchi hii yataondolewa kwa ahadi za kufanyia hiki na kile wakati wanajua kabisa kuwa hawawezi kutekeleza hata theluthi moja ya ahadi zao.

Kama Mtanzania nimekuwa nafuatilia kampeni za kila chama kwa vile vilivyokwishaanza kwa makini sana katika kujua ni kiongozi gani nimchague kwaajili ya uhai wa nchi yangu. Lakini mpaka hapa nilipo tayari kampeni hizi ZIMENIKIFU na KUNIKINAISHA kwa asilimia 100. Sababu kubwa ya kukinaishwa na kampeni hizi ni ahadi wanazotoa wagombea wote wa Urais kwanza na wale wa ubunge. Na kwa bahati mbaya sana wananchi tumekuwa kama vilema wa akili wenye utindio wa ubongo(samahanini kama hapa nimewakwaza ila ndio ukweli) kwani tumekuwa tunashangilia na kufurahia mpaka kusukuma magari ya wagombea hawa kwa nguvu zetu ambazo kwa akili yangu mimi ningezitumia kwenda kutafuta chakula cha watoto wangu wasiokuwa na maisha bora. Nina mifano kama hii hapa chini

Mgombea wa Urais chama cha 1:- Huyu kaahidi kununua meli kubwa za kimataifa kwenye maziwa mawili tofauti. Pia kaahidi kujenga international airport kwenye mikoa miwili. Pia kaahidi mambo mengine kibao kama mishahara, mashule, mahospitali, kusuluhisha migogoro ya ardhi n.k. Ebu tujiulize ni mikakati na mbinu gani zitafanya haya mbona hatupewi mikakati. Je mbona hizi ni ahadi za kawaida na hazishtui masikio ya walio makini katika kufuatilia uhai wa nchi yao. Zitatekelezekaje? Nani atafanya? Kwani hakufanya kipindi kilichopita?

Mgombea wa Urais chama cha 2:- Huyu kwanza kaahidi kuwa yeye sio rafiiki wa mafisadi, yeye atatoa elimu bure kuanzia chekechea hadi vyuo vikuu, rasilimali za nchi zitatumika sawia kwa wananchi wote pasipo ubaguzi, huduma za afya zitaboreshwa hakuna tena kutumia machela kupeleka wagonjwa hospitali. Maswali ya kujiuliza anaoambatana nao ni wasafi kiasi gani mpaka yeye azungumze hivyo? Mbona hata mikakati yake haiku wazi na ina ukungu? Hiyo elimu bure itakujaje? Shule ziko wapi? Vyuo viko wapi? Waalimu wako wapi? Madaktari wako wapi? N.k

Mgombea wa Urais chama cha 3:- Huyu naye kama wengine kaahidi elimu ya bure bure kabisa, kaahidi ajira tele na kupandisha mshahara maradufu, kupunguza kodi kibao ili ziwe affordable, kaahidi umoja na ushirikiano, barabara safi kila mkoa na wilaya pia tarafa na kata. Lakini vile vile serikali ndogo isiyo na gharama kubwa. Huyu naye anatia shaka kwenye kuyatekeleza haya maana mengi ni maneno yasiyo na mikakati inayochambulika.

Ahadi za wabunge ndio kabisa sitaki hata kuzichambua maana ni vichefuchefu vitupu.

MATARAJIO YANGU:- Matarajio yangu yalikuwa ni kuwa na mgombea ambaye hasingekuwa na ahadi za uongo kiasi hiki ila awe mgombea ambaye angetoa mhutasari mzima wa matatizo ya nchi hii toka tumepata uhuru. Vilevile atoea mhutasari wa mafanikio ya nchi hii na mwisho aseme kuwa nipeni nchi nibadilishe mfumo mzima nchi inahitaji mapinduzi katika mifumo yote inahitaji watu wapya waadilifu na wenye kuelewa kuwa ubadhirifu wowote ni kosa la kunyongwa na kutupwa kwenye makaa ya mawe. Nchi yenye msimamo wa mabo yake ya ndani na nje, nchi yenye kuwasafisha kwanza viongozi wote waliowachafu waliokalia nyadhifa kwa kipindi na kujichotea railimali pasipo uhalali wowote. Tunahitaji viongozi wenye akili tofauti zinazowaza tofauti na kutenda tofauti kabisa. Si viongozi ahadi ambazo ukweli ni kuwa mwaka 2015 utafika hata robo yake hazijatekelezwa kwa asilimia 50.

Sipigi kura ingawa hapo awali nilipanga kufanyia hivyo. Sina wa kunishawishi vinginevyo

Mungu ibariki Tanzania

Mokoyo Jr


Una matatizo ya uelewa kwa sababu kuna wagombea wengi sana ambao ni wapya kabisa katika ulingo huo. Wale wale ni wawili tu: Kikwete na Lipumba, wengie wote ni wapya kabisa.


Pili, ahadi za wagombea ndiyo kampeini yenyewe; tofauti ni aina ya ahadi zenyewe. Kuna wanaoahidi kutoa pesa za kuwaletea wananchi ugali mezani kwao na kuna wanaoahidi utawala bora utakaotengeza mazingira ya kuwafanya wananchi wajipatie ugali wao wenyewe. It is clearly black and white: no fuzziness

Kushindwa kupiga kura kwako itakuwa ni uzembe wako wa kuchambua habari, ingawa ninaweza kukuelewa kwa sababu propaganda za kuwazubaisha wananchi kama wewe zimekuwa zinaendeshwa kwa nguvu sana siku hizi.
 
Kwanza nianze kwa kusema kuwa mimi sio mwanachama wala mkereketwa wa chama chochote kile sio CCM, Chadema, CUF, TLP, NCCR-Mageuzi au chochote kingine.

Baada ya kusema hayo kwa kifupi tu sababu iliyonifanya kuamua kutokupiga kura yangu kwa mwaka huu wa 2010. Kimsingi naipenda nchi yangu na ningetamani siku moja iwe nchi yenye uchumi imara, amani na utulivu madhubuti na zaidi ya yote iwe na viongozi madhubuti ambao ndio chanzo cha hayo yote mema. Siku zote nimekuwa nikiwaza kuwa na viongozi wenye mawazo mbadala wa kubadilisha mwelekeo wa nchi hii.

Kubadilisha kwangu msimamo wa kupiga kura mwaka huu kumetokana na kukosa wagombea wenye nia dhabiti ya kuibadilisha nchi hii itoke katika dimbwi la ufukara. Hakuna hasiyejua kuwa nchi yetu inakabiliwa na matatizo vyungu nzima kwenye kila sekta kuanzia elimu, barabara, kilimo, utalii, madini, afya n.k. Lakini jambo la kushangaza bado wagombea Urais tulio nao mwaka huu wamekuwa wagombea wale wale hapa nikiwa na maana ya wagombea wenye mawazo yaleyale mgando kuwa matatizo ya nchi hii yataondolewa kwa ahadi za kufanyia hiki na kile wakati wanajua kabisa kuwa hawawezi kutekeleza hata theluthi moja ya ahadi zao.

Kama Mtanzania nimekuwa nafuatilia kampeni za kila chama kwa vile vilivyokwishaanza kwa makini sana katika kujua ni kiongozi gani nimchague kwaajili ya uhai wa nchi yangu. Lakini mpaka hapa nilipo tayari kampeni hizi ZIMENIKIFU na KUNIKINAISHA kwa asilimia 100. Sababu kubwa ya kukinaishwa na kampeni hizi ni ahadi wanazotoa wagombea wote wa Urais kwanza na wale wa ubunge. Na kwa bahati mbaya sana wananchi tumekuwa kama vilema wa akili wenye utindio wa ubongo(samahanini kama hapa nimewakwaza ila ndio ukweli) kwani tumekuwa tunashangilia na kufurahia mpaka kusukuma magari ya wagombea hawa kwa nguvu zetu ambazo kwa akili yangu mimi ningezitumia kwenda kutafuta chakula cha watoto wangu wasiokuwa na maisha bora. Nina mifano kama hii hapa chini

Mgombea wa Urais chama cha 1:- Huyu kaahidi kununua meli kubwa za kimataifa kwenye maziwa mawili tofauti. Pia kaahidi kujenga international airport kwenye mikoa miwili. Pia kaahidi mambo mengine kibao kama mishahara, mashule, mahospitali, kusuluhisha migogoro ya ardhi n.k. Ebu tujiulize ni mikakati na mbinu gani zitafanya haya mbona hatupewi mikakati. Je mbona hizi ni ahadi za kawaida na hazishtui masikio ya walio makini katika kufuatilia uhai wa nchi yao. Zitatekelezekaje? Nani atafanya? Kwani hakufanya kipindi kilichopita?

Mgombea wa Urais chama cha 2:- Huyu kwanza kaahidi kuwa yeye sio rafiiki wa mafisadi, yeye atatoa elimu bure kuanzia chekechea hadi vyuo vikuu, rasilimali za nchi zitatumika sawia kwa wananchi wote pasipo ubaguzi, huduma za afya zitaboreshwa hakuna tena kutumia machela kupeleka wagonjwa hospitali. Maswali ya kujiuliza anaoambatana nao ni wasafi kiasi gani mpaka yeye azungumze hivyo? Mbona hata mikakati yake haiku wazi na ina ukungu? Hiyo elimu bure itakujaje? Shule ziko wapi? Vyuo viko wapi? Waalimu wako wapi? Madaktari wako wapi? N.k

Mgombea wa Urais chama cha 3:- Huyu naye kama wengine kaahidi elimu ya bure bure kabisa, kaahidi ajira tele na kupandisha mshahara maradufu, kupunguza kodi kibao ili ziwe affordable, kaahidi umoja na ushirikiano, barabara safi kila mkoa na wilaya pia tarafa na kata. Lakini vile vile serikali ndogo isiyo na gharama kubwa. Huyu naye anatia shaka kwenye kuyatekeleza haya maana mengi ni maneno yasiyo na mikakati inayochambulika.

Ahadi za wabunge ndio kabisa sitaki hata kuzichambua maana ni vichefuchefu vitupu.

MATARAJIO YANGU:- Matarajio yangu yalikuwa ni kuwa na mgombea ambaye hasingekuwa na ahadi za uongo kiasi hiki ila awe mgombea ambaye angetoa mhutasari mzima wa matatizo ya nchi hii toka tumepata uhuru. Vilevile atoea mhutasari wa mafanikio ya nchi hii na mwisho aseme kuwa nipeni nchi nibadilishe mfumo mzima nchi inahitaji mapinduzi katika mifumo yote inahitaji watu wapya waadilifu na wenye kuelewa kuwa ubadhirifu wowote ni kosa la kunyongwa na kutupwa kwenye makaa ya mawe. Nchi yenye msimamo wa mabo yake ya ndani na nje, nchi yenye kuwasafisha kwanza viongozi wote waliowachafu waliokalia nyadhifa kwa kipindi na kujichotea railimali pasipo uhalali wowote. Tunahitaji viongozi wenye akili tofauti zinazowaza tofauti na kutenda tofauti kabisa. Si viongozi ahadi ambazo ukweli ni kuwa mwaka 2015 utafika hata robo yake hazijatekelezwa kwa asilimia 50.

Sipigi kura ingawa hapo awali nilipanga kufanyia hivyo. Sina wa kunishawishi vinginevyo

Mungu ibariki Tanzania

Mokoyo Jr

Nilimenya ndizi na nikajua utamu wake, nikakata ndimu nikaonja uchungu wake. nikamung'unya ukwaju nikajua ugwadu wake, nilijiandikisha nataka kuchagua kiongozi bora.
 
Nilimenya ndizi na nikajua utamu wake, nikakata ndimu nikaonja uchungu wake. nikamung'unya ukwaju nikajua ugwadu wake, nilijiandikisha nataka kuchagua kiongozi bora.

Kura ni fimbo ya mnyonge,iwaadhibu viongozi wasiofaa. Kura yako ndio ufunguo wa maisha bora. tumia kura yako kama silaha ya kuleta maisha bora.
 
Kitu kimoja ambacho unaweza kukifanya kibaya ni kukataa kupiga kura huku ukihitaji mabadiliko. kama hahitaji mabadiliko, asipige kura lakini kama anataka mabadiliko, apige kura kwa maana ndiyo njia pekee ya kuwaondoa viongozi wabovu. Strategies baadhi zimewekwa wazi mf. elimu na afya bure inaweza kupatikana kwa kuchukua hatua madhubuti soma gazeti la Nipashe Uk 3 kwenye title Dr. Slaa: Nitafumua mikataba ya madini". hiyo ni njia mojawapo ya kuongeza kipato kuweza kutoa huduma za jamii kama elimu Tsh 700 billion annually to be obtained through that means only. there are many more which have been left by CCM because of what they get from that!!
 
Huyu mokoyo anazuga tu.

Ni CCM dam dam. Anataka kuwakatisha tamaa wanamageuzi waone hakuna tofauti hata wapinzani wakichaguliwa.

He he heee! Tupo macho kama fridge guard.
 
Hizo ni hasira za mkizi. Ukisusa ccm wanaendelea kubugia. Unapenda hilo? Tafakari chukua hatua
 
achana na mjinga makoyo.tuendelee kushawishi watu wapigie chadema na sio kupiga kura tu,tupate mawakala watakaozilinda vyema kura hizo.maana ushindi wa ccm unatokana na wizi wa kura
 
Nakuunga mkono Mokoyo, hata mi nimekata tamaa kwa mda mrefu, hata huyo mgombea no 2 alilazimishwa sana haikuwa nia yake ya dhati, alikuwa anataka zake ubunge.....
 
Hawa wanaokata kupiga kura ninawaelewa kabisa maana kura zitaibiwa tu.:eyeroll2:
 
Nimekuwa nikifanya tathmini toka uchaguzi wa 2010 ulipomalizika na wale waliochaguliwa kuchaguliwa na kukabidhiwa mamlaka ya kuongoza Tanzania. Bila kificho maisha ya watanzania walio wengi ndio yamezidi kuwa katika hatari kuliko au pengine yamekuwa mabaya kuliko huko tulikotoka. Nimefuatilia ahadi zilizotolewa wakati wa kampeni 2010 hasa katika eneo la mgombea Urais nimegundua ni patupu bado. Sidhani kama kura yangu ndio iliyomnyima mgombea bora kukaa madarakani lakini bado nashawishi nafsi yangu kuwa nilikuwa sahihi siku ya uchaguzi kufanya kazi zangu binafsi kuliko kwenda kukaa kwenye foleni. Viva Tanzania
 
Hii ndio inayotokea kila mara kwenye nchi yetu
unanikumbusha maneno ya jenerali:

"Tunachagua kama vipofu, kisha tunalalama kama vichaa. Sasa tuamue: ama tuchague viongozi wetu kwa makini, au tukae kimya wakati wakitunyanyasa. Wachagua hovyo wasiwe wasema hovyo wakitendewa hovyo."

source: Raia Mwema
 
Back
Top Bottom