Singo nyingine ya TANESCO!

Waungwana,

Mtaniwia radhi. Hivi kweli kama sisi ni watu makini, kwa nini tunajisumbua kulalamika kuhusu kushindwa kwa TANESCO kumaliza tatizo la mgao wa umeme? Kwani nani alisema kwamba TANESCO peke yao ndio wenye dhamana ya kuzalisha umeme? Kwani nani amekuzuia wewe kuweka mtambo wa wind power, au solar power, nyumbani kwako, ukaachana na huo mgao?

Jamani, kama sisi ni watu makini, tutajua kwamba ni kazi bure kuilalamikia Serikali na TANESCO. Dawa ni (1) funga mtambo wako mwenyewe wa umeme nyumbani, kama ni wind, solar, bioga, etc., kisha (2) ng'oa kabisa service line ya TANESCO, ili uachane na dhana kwamna TANESCO ni kampuni ya kuzalisha na kusambaza umeme, kwani hilo si kweli.

Hata kufikiria mambo madogo kama haya, tunaiachia Serikali? Ujinga huu!

Samahani kwa kuwaambia ukweli lakini TANESCO SIO SOLUTION ya kumaliza mgao wa umeme, na hata Serikali pia, haina nia hiyo.

Umemaliza?
 
nilimsikia huyo badra jana akizungumza ktk kipindi cha jahazi clouds fm, eti panafrica linapotokea tatizo nao watoe matamko kwa linalo wahusu coz ati yeye amechoka kila siku kua ni m2 wa matamko tu na malawama!

aache kazi bas
 
Najitahidi sana kujizuia nisi comment katika hili.............. eee Mungu nisaidie................. nahisi kukosa pumzi....................
 
Imekuwa kawaida kwa serikali yetu kutokuwa na njia mbadala kwenye mambo muhimu kama haya.

kwa serikali yoyote ile inayoongozwa na watu makini na wenye uzalendo na nchi yao huwezi ukasikia au kuona uozo kama huu wa serikali yetu.

tatizo la kutokuwa na umeme wa uhakika halikuanza leo ni la muda mrefu sana. Kwa gharama tulizogharamia kuingia mikataba mbalimbali kwa lengo la kupunguza tatizo hili kama si kulimaliza,ingetosha kabisa kuliwezesha shirika la ugavi wa nishati hii muhimu sana ili kuweza kuendana na teknolojia ya kisasa badala ya kung'ang'ania na teknolojia iliyopitwa na wakati.

viongozi wetu wanapata fursa nyingi sana za kutembelea nchi mbalimbali ndani na nnje ya africa. Napenda kuchukuwa fursa hii kuwashauri wajaribu kuangalia na kujifunza ni jinsi gani wenzao wanafanikiwa kutokomeza matatizo kama haya kisha uwe mfano wa wao kuja kuufanyia kazi wanaporejea.

kupiga picha na kukutana na watu maarufu duniani kutatusaidia nini watanzania tuliochoka na haya maisha yanayosababishwa na porojo zenu?

ufike wakati kwa wa tanzania tujitambue hawa ni viongozi tuliowapa mamlaka ya kuzisimamia na kuziendeleza rasilimali za nchi yetu kwa mikono yetu kwa maslahi ya nchi yetu na watanzania kwa ujumla.

wakati wa kuishi kwa matumaini yasiyokuwepo umekwisha. Ccm pamoja na serikali yake wameshafika kikomo ufahamu wao katika kushugulikia mambo muhimu kama haya tunayokwazikanayo. Kilichobaki sasa ni propaganda tu.

tukiwa na nia thabiti zitokazo ndani ya mioyo yetu haya yote yatakwisha. Lakini kinyume na hapo tutakuwa watu wa kulalamika mpaka mwisho wa ulimwengu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom