Singida yauzwa rasmi kwa mafisadi

Kwani huko wanakohamishiwa wanapelekwa juu ya nguzo za umeme? tena si kuhamishwa ni kusogezwa tu, kama vile inavyopitishwa barabara, watu huhamishwa kusogezwa na si kuhamishwa mji wala wilaya.

Naona hujui kuhamishwa wewe, haukuwepo wakati wa nyerere na vijiji vya ujamaa? basi hata hukuyasoma? kule ndyo kulikuwa kuhamishwa kwa nguvu, ukipenda usipende, unaweza kutolewa wilaya moja ukapelekwa nyingine bila kulipwa wala kujengewa mnatupwa maporini muanze wenyewe kila kitu. Tumetoka mbali kijana, hao wanaletewa neema wanalalamika, ama kweli. Hamsadifiki.

hawakuhamishwa kumpisha mzungu enzi za vijiji vya ujamaa, kusoma kwako hakuna maana kama huoni hii tofauti, naelewa katiba inaelekeza kuheshimu na kulinda hiari yangu ya kuwa popote ndani ya tz kwa kuzingatia sheria, vipi aheshimiwe muwekezaji kwa mimi mwenye nchi kudharauliwa? nani hataki faida? kwanini nisishirikishwe kwenye faida itokanayo na uwekezaji kwenye eneo langu? wakati vijiji vya ujamaa hukuwa pekeyako tumia akili!!
 
Jamani sikilizeni,kwa nini sheria hazifuatwi,Hawa Wind East Africa walishapewa lessen kifisadi na pia kupewa na TIC hati maalumu ya msamaha wa kodi,yenye masharti kua ili upewe shurti uwe na hati miliki ya ardhi,wanaohusika bila kujali sheria waliwapa matapeli Hao hati zote hizo....Swali ....MAFISADI hawa wakikaribishwa itakuwaje?????

Jamani hawa sio watu wa kukaribishwa,lazima wananchi watalzwa......
 
Habari za unwell na uwazi nikua Hao wenye Wind east africa niwale wataalamu waliohusika kwenye kuileta Richmond na wakala mtajwa wa Dowans wakiwa na swahiba wake ambaye ni Mkuu wa Benk ya Raslimali...wananchi hawataponeshwa na ardhii yao,ikumbukwe PIA kua hawa ni wahusika waku kwenye zulma ya Buzwagi...hawa hawafai jamani.....
 
Hakuna ukiukwaji wa sheria hapo, hao watu wanahamisha na wanakuwa "compensated", wanahamishwa bila kulipwa?

Wacheni kulala katafuteni kazi kwenye hizo kampuni, zinalipa vizuri. Mnaletewa maendeleo mnalalamika, hata siwaelewi mu watu wa aina ipi? Sheria za Tanzania hazizuwii maendeleo, yanahamishwa makaburi kwa kufuatwa sheria itakuwa watu walio hai? wacheni chokochoko na ufataani.

Huyo anaeleta ufataani humu mbona hajasema kuhusu barabara ya Dodoma - Singida - Shinyanga na Singida - Dareda - Arusha, wamehamishwa watu wengi sana kupisha barabara mbona alikaa kimya?

Umeme wa upepo unahitaji utafiti wa kina wa kujuwa upepo unapopatikana kwa kasi fulani kwa mwaka mzima unapatikana wapi na hapo sehemu iliyochagiliwa ndio pameonekana panafaa zaidi, mnachotaka ni nini?

Ngojeni na hivi karibuni kuna kampuni zinakuja, moja ya dhahabu, nayo inahitaji eneo kubwa tu na moja ya uranium pale karibu na Manyoni, ndio mseme vizuri.

dearest faiza foxy, wazo lako kweli ni zuri kuhusu uwekezaji na maendeleo kwa ujumla, in most of the world, people get "relocated" from time to time for one reason or another and by doing so receive "fair" compensation, in the US kuna kitu kinaitwa "imminent domain", hii kitu ni sera ya serikali kumiliki eneo lolote linalohitaji for the greater good. Yaani wanachukua kibanda cha mtu kwa manufaa ya jamii, halafu mmiliki wa hicho kibanda analipwa fidia alafu anasanuka. Sijui kama mwenzangu ni mzawa kwani umesikia lini mlalahoi kalipwa fidia yenye haki katika nchi yetu hii tukufu? Its one thing mzungu kumdharau mtu mweusi, ni aibu tupu jinsi mtu mweusi anamtendea mweusi mwenza. Bongo ni kiini macho tu, mipango itapangwa, kamati zitazinduliwa, mada zitazungumziwa, lakini mwisho wa siku ni yale yale, waswazi wanaingizwa chaka. Huu mfumo uliopo sasa haufai kabsaa, hii nchi inakufa slowly but surely and no one will do anything about it but talk.
 
Kampuni iliyotajwa ni WIND EAST AFRICA, Bila kujali ni ya nani? Inaibua maswali mengi. MKuu wa Mkoa wa Singida analazimisha kuwa kampuni ina eneo, Mkurugenzi wa Manispaa husika ambapo hiyo kampuni inatajwa itawekeza anasema haina hata Eneo la Mita Moja. Kampuni hiyo imepewa msamaha wa kodi tangu 2008, ikapewa leseni ya kuwekeza iliyoandikwa majina ya vijiji viwili tu (Unyambwa na Kititimo), lakini wao wametoa ramani yenye vijiji sita, tofauti na vilivyotajwa katika leseni (Unyamikumbi A, Unyamikumbi B, Ughaugha A, Ughaugha B, Kisasida na Kisaki). Hapa kweli hatuoni Tatizo? Leseni Imeandikwa Dodoma, wewe unaleta ramani ya Morogoro, Leseni imeandikwa vijiji viwili, wewe unaleta sita taouti na vilivyotajwa katika leseni, WAKATI HAYO YOTE YANAFANYIKA wananchi wa eno husika hawajui. Wanaona Balozi wa Uingereza analetwa kuonyeshwa vijiji vyao, Sheria ya Ardhi Na. 5 ya mwaka 1999, Inashauri wananchi wapewe fursa ya kushirikishwa ili ardhi itolewe kwa ajili ya maendeleo. Kumbukeni Kisa cha Wakaazi walioko katika maturubai Geita mjini waliotolewa nje ya nyumba zao na Serikali hii hii, Mwekezaji (Geita Gold Mines) akasambaza nyumba zao kwa Greda, hadi leo hawajui mbele wa nyumba. tunaoshabikia maendeleo yasiyofuata sheria tunaangamiza taifa kwa sababu ya Ulafi wa pesa. Madudu mengi yatajulikana tu.
 
Chimbuko la tatizo ni nini hapa? Simply rushwa? Au kuvunjwa kwa sheria na kama ni sheria iliyovunjwa ni sheria ipi? Are we sure kwamba sheria zetu za Ardhi zinajitosheleza kumlinda mwananchi wa kawaida?
 
utaandika mpka server itajaa, karamu zitaisha wino, pencils zitaisha, karatasi reams na reams zitaisha lakini bika KATIBA MPYA ya wananchi wa Tanzania hakuna litakalobadilika hapa!
Kampuni iliyotajwa ni WIND EAST AFRICA, Bila kujali ni ya nani? Inaibua maswali mengi. MKuu wa Mkoa wa Singida analazimisha kuwa kampuni ina eneo, Mkurugenzi wa Manispaa husika ambapo hiyo kampuni inatajwa itawekeza anasema haina hata Eneo la Mita Moja. Kampuni hiyo imepewa msamaha wa kodi tangu 2008, ikapewa leseni ya kuwekeza iliyoandikwa majina ya vijiji viwili tu (Unyambwa na Kititimo), lakini wao wametoa ramani yenye vijiji sita, tofauti na vilivyotajwa katika leseni (Unyamikumbi A, Unyamikumbi B, Ughaugha A, Ughaugha B, Kisasida na Kisaki). Hapa kweli hatuoni Tatizo? Leseni Imeandikwa Dodoma, wewe unaleta ramani ya Morogoro, Leseni imeandikwa vijiji viwili, wewe unaleta sita taouti na vilivyotajwa katika leseni, WAKATI HAYO YOTE YANAFANYIKA wananchi wa eno husika hawajui. Wanaona Balozi wa Uingereza analetwa kuonyeshwa vijiji vyao, Sheria ya Ardhi Na. 5 ya mwaka 1999, Inashauri wananchi wapewe fursa ya kushirikishwa ili ardhi itolewe kwa ajili ya maendeleo. Kumbukeni Kisa cha Wakaazi walioko katika maturubai Geita mjini waliotolewa nje ya nyumba zao na Serikali hii hii, Mwekezaji (Geita Gold Mines) akasambaza nyumba zao kwa Greda, hadi leo hawajui mbele wa nyumba. tunaoshabikia maendeleo yasiyofuata sheria tunaangamiza taifa kwa sababu ya Ulafi wa pesa. Madudu mengi yatajulikana tu.
 
Mkiletewa umeme shida msipoletewa umeme shida.

Kuhamishwa watu kwa ajili ya kuleta maendeleo ni kitu cha kawaida duniani. Unafikiri maendeleo yanakuja kwa kuota kama miti?

Wacheni kulala, amkeni. Mnaletewa umeme, mnaanza ooh Singiga imeuzwa, imeuzwa imepelekwa wapi? kuwa na fikra japo kidogo.
avoid the ignorant." (Qur'an 7:199)
 
Back
Top Bottom