Sina upendo kabisa kwa mama yangu mzazi

Pole sana ndugu KIBURUDISHO kwa yaliyowakuta,


Sie tulifundishwa kutoingilia ugomvi wa wazazi....kwa sababu wanayogombania chumbani kwao kamwe huwezi kuyajua!

Kwa sasa umekuwa mkubwa, nakushauri usijitafutie laana ya mama...Kwa hiyo, unatakiwa kumsamehe ili upate nafasi adhimu ya kujua walau mambo kidogo yaliyomfanya akakengeuka kiasi hicho...Naamini unaweza kujikuta mdomo wazi akiamua kukusimulia ugomvi wao na baba yako in her own perspective!!

Mama ni mama na hakuna mwingine.....Uwe mwangalifu sana!

Babu DC!!
hapo kwenye RED tunajiaminisha sana hivyo na ni vizuri tu kuamini hivyo.
kuna siku rafiki yangu mmoja aliniambia aliwahi kumwuliza mama yake kama kweli yeye ni mtoto wake, serious.
kuna rafiki yangu mwingine ana mpango wa kusitisha kumtembelea mama yake sababu hajawahi kwenda kwa mama yake wakakaa na kuongea na kucheka kama akiwa na wengine. ananisimulia kuwa yeye ndo mtu pekee katika familia ambaye anampa kila kitu mama yake (wenzake wote hawana maisha mazuri sana, kwa hiyo aliwaambia maswala yote ya wazazi yeye ndo atahusika, wenzake wajishughulishe na familia zao tu, ingawa hawakatazwi kama wanaamua kupeleka chochote kwa wazazi wao). lakini hasa mama mtu haridhiki kabisa na kila mtoto wake anachofanya. kila akienda kutembea ni malalamiko mwanzo-mwisho; na ni malalamiko ambayo hayana msingi. sasa anawaza kuna faida gani ya mimi kwenda kumtembelea mama wakati kila nikienda narudi depressed?
 
Mdogo wangu Fixed Point,

Watu si wanasema hapa kila siku kuwa mwanamke hawezi kuanza kucheat bila sababu?? Kwa nini huyu tusimpe benefit of doubt kwamba inawezekana kuna kitu kilimtokea na kumharibia her mental soundness??

Babu DC!!
Babu, watu wanasema hivyo, wewe je unakubaliana nao?
mimi binafsi sijawahi kukubaliana na hilo, kuna sababu gani kubwa ya kukufanya u-cheat? mimi naamini ni litabia tu libaya, hakuna sababu ya msingi
 
hapo kwenye RED tunajiaminisha sana hivyo na ni vizuri tu kuamini hivyo.
kuna siku rafiki yangu mmoja aliniambia aliwahi kumwuliza mama yake kama kweli yeye ni mtoto wake, serious.
kuna rafiki yangu mwingine ana mpango wa kusitisha kumtembelea mama yake sababu hajawahi kwenda kwa mama yake wakakaa na kuongea na kucheka kama akiwa na wengine. ananisimulia kuwa yeye ndo mtu pekee katika familia ambaye anampa kila kitu mama yake (wenzake wote hawana maisha mazuri sana, kwa hiyo aliwaambia maswala yote ya wazazi yeye ndo atahusika, wenzake wajishughulishe na familia zao tu, ingawa hawakatazwi kama wanaamua kupeleka chochote kwa wazazi wao). lakini hasa mama mtu haridhiki kabisa na kila mtoto wake anachofanya. kila akienda kutembea ni malalamiko mwanzo-mwisho; na ni malalamiko ambayo hayana msingi. sasa anawaza kuna faida gani ya mimi kwenda kumtembelea mama wakati kila nikienda narudi depressed?


Nakuelewa Fixed Point,

Kama huna amani unapokutana na wazazi au ndugu yeyote, dawa ni kupunguza encounters!! Mie natumia sana hii njia. Ila hilo halifuti ukweli kwamba huyo ni mzazi au ndugu!!

Babu DC!!!
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli kabisa Kaunga, lakini huyu kasema kabisa kuwa mama alipata penzi jipya, akaamua kulimwaga la babake. na kwa vile hakuja na mtoto pale basi akamwachia na wanae, isiwe tabu

Kweli penzi jipya unaacha hata mtoto mdogo? Any way kuna wanaume wanafanya hivyo so l think na wanawake wanaweza pia. Lkn kumbuka penzi jipya bado ni kazi ya shetani ni adultery hiyo!
 
Last edited by a moderator:
Hii story imenifanya nishindwe cha kuandika...............ngoja nifute machozi nirudi kuandika tena maana hapa hata screen siioni

hapa umejitahidi tahidi kuandika ingawa screen huoni. Pole sana mtoa mada, jifunze kusamehe kama ulivyoshauriwa, jifunze kumpenda ili uweze kuishi nae vizuri. Ukishindwa hayo mwambie ukweli kama humpendi na ikibidi akatafute pa kukaa.
 
Baada ya mieze miwili sijui ni nani alimpa taarifa ndio akaja kuliona kaburi la mdogo wetu
Wewe mwenyewe unasema hujui nani alimpa taarifa ya kifo, sasa unalalamika nini wakati nyinyi wenyewe mlificha Mama msiba?

Na unakiri kwamba baadae alipopata taarifa alikuja kuona kaburi, sasa kakosa nini?

Issue kama hii ambayo sijasikia upande wa mwanamke napenda kumpa Mama first benefit of the doubt, because in the preponderant majority of the times wanaume ndio wanaharasha wavuruga mahusiano wa kwanza.
Unasema mama alikuwa na hawara, tutajuaje kama haikuwa reaction yake kwa Baba kuwa na ki-mama mdogo chenu pembeni?
 
Wewe mwenyewe unasema hujui nani alimpa taarifa ya kifo, sasa unalalamika nini wakati nyinyi wenyewe mlificha Mama msiba?

Na unakiri kwamba baadae alipopata taarifa alikuja kuona kaburi, sasa kakosa nini?

Issue kama hii ambayo sijasikia upande wa mwanamke napenda kumpa Mama first benefit of the doubt, because in the preponderant majority of the times wanaume ndio wanaharasha wavuruga mahusiano wa kwanza.
Unasema mama alikuwa na hawara, tutajuaje kama haikuwa reaction yake kwa Baba kuwa na ki-mama mdogo chenu pembeni?

Kwanza nikujulishe kuwa alivyoondoka hakutuachia mawasiliano yoyote yale hivyo ilikuwa vigumu kumpata,pili ili kudhibitisha kuwa sio baba aliyesababisha aondoke bali alituona sisi wanawe tumekuwa mzigo kwake hapati uhuru wa kufanya mambo yake vizuri aliamua kutukimbia sisi na sio baba kama alichukizwa na baba si angelikuwa na mawasiliano na sisi hata mtoto wake wa kike ambaye ni mkubwa wetu? Pia kama baba angelikuwa na kimada tungelijutia kubaki na baba.
 
unajua mkuu Mungu hakunyimi vyote, mshukuru alikupa baba wa aian hiyo, hebu imagine mdingi nae angekuwa legelege labda akawaolea mama wa kambo asiyeeleweka au akaishia kuwa chapombe na kuhama nyumba ingekuwaje,..............

kwa kifupi story yako imeniingia sana moyoni coz mm nampenda sana mama yangu, ila namchukia sana baba yangu coz alikuwa na tabia kama za mama yako, nilimpenda sana my dad nikiwa mdogo, mpaka namaliza a- level nilimpa so many chances kuwa baba yangu but aliishia kunidisappoint tu, namshukuru Mungu alinipa Mama anayejitambua kama si kwa juhud zake God knows kama hata ningekuwa naelewa maana ya JF................

Nashindwa kukwambia msamehe, coz mie mwenyewe huo ni mtihan nilionao mpaka sasa............
pole sana mkuu............big up 4 ua dad.............
 
Pole sana ndugu yangu Muombe sana MUNGU. I am telling you huwezijua nini kilijiri kiasi cha kumfanya mama akabehave alivyobehave please jifunze kusamehe. Wazazi wetu ni mungu wetu wa hapa duniani.
 
She might have not been herself!
Msinitolee mimacho hasa Kongosho na King'asti; nasema hivyo kwanini; real shit do happen. Nimeona far worse things (shuhuda) kuliko hiyo kwenye TV (Emmanuel). Yaani mama anaattempt kuuwa watoto wake mwenyewe, as a result ya evil spirit iliyomuingia at one point of her life; during deriverance lipepo linasema kila kilichokuwa kinatendeka and how, baada ya kuombewa na lispirit kumtoka anakuwa mtu mwingine kabisa.

Sina explaination yoyote ya mama mwenye akili zake timamu kuikimbia familia kwa kiasi hicho, it has to be the work of the devil.

Kaka kama unaamini, jaribuni kusali kwa imani yenu na kumuombea huyo mama yenu hiyo roho imtoke; sio tu mtakuwa mmemsaidia yeye lakini na familia yenu pia.

Saa zingine tunamsingizia shetani hadi basi! Ndo hivi watu wanapata na ukimwi, wakati wanaendelea na maombi wakivumilia. Hata kama alimchukia mumewe, kungekuwa na vivid effeorts za walau kuwaona wanae. Imagine hadi mwanae anakufa hana habari! Hasira zinanishika hapa ntaharibu siku yangu yenye matumaini, uwiii
 
Pole sana ndugu KIBURUDISHO kwa yaliyowakuta,


Sie tulifundishwa kutoingilia ugomvi wa wazazi....kwa sababu wanayogombania chumbani kwao kamwe huwezi kuyajua!

Kwa sasa umekuwa mkubwa, nakushauri usijitafutie laana ya mama...Kwa hiyo, unatakiwa kumsamehe ili upate nafasi adhimu ya kujua walau mambo kidogo yaliyomfanya akakengeuka kiasi hicho...Naamini unaweza kujikuta mdomo wazi akiamua kukusimulia ugomvi wao na baba yako in her own perspective!!

Mama ni mama na hakuna mwingine.....Uwe mwangalifu sana!

Babu DC!!

hapana aisee. mama anatakiwa ajalu ustawi wa wanae; na ndo sababu wahenga wakasema kukea mimba si kazi bali kulea. Hili ni fundisho au onyo kuwa usijitungishe mimba kama huna gut/balls/ commitment ya kulea.

Kuzaa watoto na kuwatelekeza sio uzaxi huo, ni afadhali angetumia uzazi wa mpango asiwapate kuliko kuzaa pasipo kuwajibika na uzazi.
 
Last edited by a moderator:
Pole sana KIBURUDISHO. Usome ushauri wa Kongosho (post no.12) na kuufanyia kazi.
Samehe utapata amani.
 
Last edited by a moderator:
hapana aisee. mama anatakiwa ajalu ustawi wa wanae; na ndo sababu wahenga wakasema kukea mimba si kazi bali kulea. Hili ni fundisho au onyo kuwa usijitungishe mimba kama huna gut/balls/ commitment ya kulea.

Kuzaa watoto na kuwatelekeza sio uzaxi huo, ni afadhali angetumia uzazi wa mpango asiwapate kuliko kuzaa pasipo kuwajibika na uzazi.

Nakubaliana na wewe Freema Agyeman,

Ila unadhani kwamba ukipata nafasi ya kumsikiliza huyo mama unaweza kubaki na mtazamo/msimamo huu??

Nahisi huyo mama na jambo moyoni mwake and I wish we could decode the knots!!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Saa zingine tunamsingizia shetani hadi basi! Ndo hivi watu wanapata na ukimwi, wakati wanaendelea na maombi wakivumilia. Hata kama alimchukia mumewe, kungekuwa na vivid effeorts za walau kuwaona wanae. Imagine hadi mwanae anakufa hana habari! Hasira zinanishika hapa ntaharibu siku yangu yenye matumaini, uwiii

Nakubaliana na wewe, na ndivyo nimekuwa nikiamini siku zote until receently na ikaweza make sense kwangu; this is how:-

Kwa mtu normal ambaye hakuwa na shida ya childhood na amepata malezi, mafundisho na mifano mema; anayejua mema na mabaya ana uwezo wa kuchagua mema au mabaya.

Nani au nini kinamuinfluence mtu kuchagua mema, nafikiri ni Roho nzuri iliyomo ndani yake (tuiite hiyo roho nzuri, roho takatifu/safi au Holy spirit) mtu anachagua kuifuata hiyo roho (ushauri wake au mwongozo wake) hivyo tunaweza kuconclude kuwa aurthor wa vitu vizuri ni hiyo Roho au Mungu chagua kimoja wapo.

Kwa upande mwingine, kwa huyo huyo mtu, kuna sauti au ushauri mwingine anaopata ukimshauri kufanya mabaya (ninaisikia hiyo sauti mara nyingi sana moyoni mwangu), hiyo sauti tuiite roho mbaya/chafu au evil spirit; naweza nikaamua kuifuata hiyo roho chafu au evil spirit na nikatenda mabaya, kama ilivyo kwa mtenda mazuri, ninaweza pia kusema author wa mabaya yote ni hiyo roho chafu/evil spirit au Shetani ukipenda.

Role ya mwanadamu wa kawaida ni kuchagua ipi ya kuifuata, ambayo honestly kwa baadhi ya mambo inakuwa kazi rahisi lakini kwa mengine ni ngumu sana. Mf: kwangu mimi ambaye sijaolewa roho hiyo chafu inakuwa ngumu sana kuishinda hasa inaponishauri nikangonoke, na inanipa sababu nyingi 'za msingi' kwanini si vibaya kungonoka ingawa sina ndoa. Ili kuishinda hii roho, ninahitaji nguvu ya ziada kutoka kwa Mungu ambayo naipata kwa kusali, kufunga na kusoma biblia.

Hiyo ni hali ya kawaida na nimechukulia mfano wa kwangu mie.

Sasa kuna watu ambao, roho hiyo chafu imewakandamiza na kuwatengenezea kama addiction fulani ambayo au hawajui au wamejaribu kwa njia zao wenyewe na kushindwa kuepukana na hiyo kitu. Mfano, waingereza na wataalamu wametoa hata majina na kujaribu kutoa explaination kwa baadhi ya hizo tabia moja wapo ni udokozi (kleptomaniac, nisamehe kama nimekosea spelling), nyingine ni ulevi wa kupindukia na madhara yake, ubakaji n.k

Wanaweza sema ni childhood upbringing, na nani kasema hakuna laana za ukoo (yaani roho chafu iliyoingia kwa familia); wazazi wadhambi, wanaweza changia watoto wawe wadhambi kwa njia ambazo wataalamu wa sociolojia wanaexxplain na watu wa imani wakaexplain pia bila kutofautiana sana kama unaangalia kwa undani zaidi.

Mwisho ninasisitiza kuwa ni kweli mwanadamu ana role kubwa ya kuplay katika kuchagua evil and good; lakini wakati mwingine na kama mtu wa imani ninasema wakati wote unahitaji kuomba msaada wa Mungu ili ushinde, na ukishinda ni vizuri kumrudishia Mungu credit na si kujisifu kwamba mimi sifanyi dhambi hii na hii, kwani siamini wote wanaofanya dhambi wanapenda kufanya dhambi.
 
Nakubaliana na wewe Freema Agyeman,

Ila unadhani kwamba ukipata nafasi ya kumsikiliza huyo mama unaweza kubaki na mtazamo/msimamo huu??

Nahisi huyo mama na jambo moyoni mwake and I wish we could decode the knots!!

Babu DC!!


Akiwa kama mama mwenye watoto, ambaye hakuwahi kuwa mume anayemu abuse physically hakutakiwa kuwaacha watoto kwa sababu binafsi. Na kama ilikuwa lazima kuondoka basi angeondoka n watoto wake; au hata wale wadogo tu. Unapataje usingizi usiku wakati hujui ustawi wa watoto wako
 
Last edited by a moderator:
Akiwa kama mama mwenye watoto, ambaye hakuwahi kuwa mume anayemu abuse physically hakutakiwa kuwaacha watoto kwa sababu binafsi. Na kama ilikuwa lazima kuondoka basi angeondoka n watoto wake; au hata wale wadogo tu. Unapataje usingizi usiku wakati hujui ustawi wa watoto wako

Kweli Freema Agyeman,

Ila sasa huyo mama keshafanya hayo yote....Shida yangu ni kwamba, kwa nini hatutaki kukubali kwamba lazima kuna jambo ambalo lilimfanya afikie hatua hiyo ambayo ki ukweli si ya kawaida. Na je, tukilijua hilo jambo haliwezi kutupa mtamzamo tofauti na huu wa sasa??

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
pole sana mkuu, nadhani wachangiaji wametoa ushauri mzuri sana! jitahidi na watoto wako wasipitie maisha kama mlioishi nyinyi
 
Back
Top Bottom