KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
WanaJF wenzangu natumai hamjambo kabisa.Ni story ndefu sana ila nitajitahidi kuifupisha. Ni mkasa (ugomvi) ulioikumba familia yetu kuanzia mwaka 2000 kati ya mama yangu na baba yangu. Kwa asilimia mia moja ugomvi huo ulisababishwa na mama nasema hivyo kwa sababu vituko alivyoanza kumfanyia baba tulikuwa tunaviona ilipelekea aliwahi kutoka nyumbani na kwenda kuishi Mwanza pasipo baba kujua alipeleleza hadi hapo alipogundua kuwa yuko mwanza ndipo alipochukua jukumu la kumfuata alimsihi sana arudi nyumbani aje kuwalea wadogo zangu akakubali kumbe ilikuwa danganya toto aliporudi hakukaa zaidi ya miezi sita akaondoka tena ila kwa kipindi hiki sasa baba aliamua kutomfuata tena akasema kwa kuwa sii mtoto mdogo siwezi kumlazimisha.
Katika ugomvi huo sikuwahi siku hata moja kumuona baba ameinua mkono wake kumpiga mama yangu.Yote hayo yalisababishwa na mama kuwa na hawara mimi na dada yangu ninayemfuata kwa mara ya pili tulikuwa tunachukizwa sana na vitendo vile ambavyo mama alikuwa anamfanyia baba na hiyo ilisababisha mama kunichukia mimi na dada yangu akidai sisi ndio tunampatia baba taarifa ya yale anayoyafanya.Ninachomshukuru sana baba yangu alitumia sana busara kukabiliana na hali ile kwa sababu ilifikia wakati baba aliingiwa na mawazo ya kutaka kuua kutokana na dharau zile alizokuwa anafanyiwa.
Ilipofika mwaka 2004 mama aliondoka moja kwa moja akimwacha mdogo wetu wa mwisho akiwa darasa la kwanza.Kitendo hicho kilimuumiza baba na hata sisi,pia upande wa kielimu ilituatiri sana kwa kipindi hicho nilikuwa kidato cha tatu. Ilikuwa tukitoka shule ndio tunajiandalia chakula au wadogo zangu waliokuwa wanasoma shule ya msingi tulikuwa tunakuta wamepika halafu wametubakizia chakula wao wamerudi shuleni.Mwaka 2005 Nilihitimu kidato cha nne ila kwa bahati mbaya sikuweza kuchaguliwa kuendelea na masomo sikukata tamaa niliamua kuingia mtaani kujifunza mambo ya ufundi wa umeme na masuala ya IT ambayo kwa kiasi ninayamudu pia mimi ni installer wa hizi dishi za satellite za tv.
Nikiwa na ndoto mbili 1.kuwa na uelewa mkubwa zaidi juu ya masuala ya IT au 2.Kuwa oparetor wa ile mitambo ya kulima barabara.Mwaka 2008 niliamua kuoa nimejaliwa kupata mtoto mmoja.Mwaka 2009 mdogo wangu anayenifuata kwa mara ya pili alihitimu kidato cha nne alikuwa na uwezo mzuri sana shuleni alipatwa na ugonjwa tulimpeleka hospitali tulimuuguza kwa kipindi hicho chote tukiwa na baba ila kabla matokeo hayajatoka ambapo hapo baadae matokeo yalitoka akawa amefaulu kuendelea na kidato cha tano ila kwa mapenzi yake mola alimchukua mdogo wangu alinifia tukiwa naye wodi nakumbuka aliniambia KAKA YANGU SIJUI KAMA NITARUDI NYUMBANI NAOMBA UWASALIMIE WADOGO ZANGU NA MAMA KAMA ATAKUJA KWENYE MAZISHI YANGU kauli hiyo huwa inaniumiza sana kila ninapoikumbuka.
Ilipofika saa kumi jioni mdogo wangu alifariki.Tulishughulikia taratibu za mazishi tulimzika mdogo wetu bila ya mama kuhudhuria mazishi ya mwanae.Baada ya miezi miwili sijui ni nani alimpa taarifa ndio akaja kuliona kaburi la mdogo wetu.Na juzi amekuja amefikia kwangu yaani nampa heshima tu ya mama ila kiukweli simpendi kabisa.
Katika ugomvi huo sikuwahi siku hata moja kumuona baba ameinua mkono wake kumpiga mama yangu.Yote hayo yalisababishwa na mama kuwa na hawara mimi na dada yangu ninayemfuata kwa mara ya pili tulikuwa tunachukizwa sana na vitendo vile ambavyo mama alikuwa anamfanyia baba na hiyo ilisababisha mama kunichukia mimi na dada yangu akidai sisi ndio tunampatia baba taarifa ya yale anayoyafanya.Ninachomshukuru sana baba yangu alitumia sana busara kukabiliana na hali ile kwa sababu ilifikia wakati baba aliingiwa na mawazo ya kutaka kuua kutokana na dharau zile alizokuwa anafanyiwa.
Ilipofika mwaka 2004 mama aliondoka moja kwa moja akimwacha mdogo wetu wa mwisho akiwa darasa la kwanza.Kitendo hicho kilimuumiza baba na hata sisi,pia upande wa kielimu ilituatiri sana kwa kipindi hicho nilikuwa kidato cha tatu. Ilikuwa tukitoka shule ndio tunajiandalia chakula au wadogo zangu waliokuwa wanasoma shule ya msingi tulikuwa tunakuta wamepika halafu wametubakizia chakula wao wamerudi shuleni.Mwaka 2005 Nilihitimu kidato cha nne ila kwa bahati mbaya sikuweza kuchaguliwa kuendelea na masomo sikukata tamaa niliamua kuingia mtaani kujifunza mambo ya ufundi wa umeme na masuala ya IT ambayo kwa kiasi ninayamudu pia mimi ni installer wa hizi dishi za satellite za tv.
Nikiwa na ndoto mbili 1.kuwa na uelewa mkubwa zaidi juu ya masuala ya IT au 2.Kuwa oparetor wa ile mitambo ya kulima barabara.Mwaka 2008 niliamua kuoa nimejaliwa kupata mtoto mmoja.Mwaka 2009 mdogo wangu anayenifuata kwa mara ya pili alihitimu kidato cha nne alikuwa na uwezo mzuri sana shuleni alipatwa na ugonjwa tulimpeleka hospitali tulimuuguza kwa kipindi hicho chote tukiwa na baba ila kabla matokeo hayajatoka ambapo hapo baadae matokeo yalitoka akawa amefaulu kuendelea na kidato cha tano ila kwa mapenzi yake mola alimchukua mdogo wangu alinifia tukiwa naye wodi nakumbuka aliniambia KAKA YANGU SIJUI KAMA NITARUDI NYUMBANI NAOMBA UWASALIMIE WADOGO ZANGU NA MAMA KAMA ATAKUJA KWENYE MAZISHI YANGU kauli hiyo huwa inaniumiza sana kila ninapoikumbuka.
Ilipofika saa kumi jioni mdogo wangu alifariki.Tulishughulikia taratibu za mazishi tulimzika mdogo wetu bila ya mama kuhudhuria mazishi ya mwanae.Baada ya miezi miwili sijui ni nani alimpa taarifa ndio akaja kuliona kaburi la mdogo wetu.Na juzi amekuja amefikia kwangu yaani nampa heshima tu ya mama ila kiukweli simpendi kabisa.