Leonard Robert
JF-Expert Member
- Apr 22, 2011
- 11,064
- 7,195
ilikua siku ya jumatano, maandamano yakiwa yamepamba moto..wanafunzi wakiwa wamegoma kuingia darasani kushinikiza wanafunzi wenzao waweze kutoka maabusu,maandamano yalianzia eneo la revolution square kuelekea yombo ili kuwaondoa wenzao madarasani hadi utawala kupitia mamalishe,polisi hadi utawala..muda wote huo jamaa mmoja alikua akishtukiwa kuwasaliti wenzao,kwani walianza kumshuku siku mbili kabla,akiwa anaonekana mwenye muonekano tofauti na wana-UDSM. walipofika maeneo ya utawala ndipo jamaa huyo akaamua kutaka kutoloka katika eneo hilo, akiwa amefika maeneo ya CONAS kuelekea COet vijana waliokua wanafatilia nyuma wakamkamata na kuanza kumhoji, alipoonekana kubabaisha ndipo aliposhushiwa kipigo cha mbwa mwizi,kundi hilo lilipotosheka kumpa kipigo wakaamua kumpeleka utawala walikokuwa wanafunzi wengine, wakati wakielekea maeneo ya mdegree ndipo yule jamaa akaanza kujitutumua baada ya kuona walinzi wa chuo. Ugonvi ulianza kati ya walinzi wa chuo(waliokuja kumsaidia huyo jamaa) mara gali la FFU liliingia kwa fujo na kutawanya wanafunzi na kumchukua huyo jamaa.swali ni je hawa wanausalama wa siku hizi sio kama enzi ya mwl nyerere? Nawasilisha.