lameckkawawa
JF-Expert Member
- Sep 13, 2015
- 944
- 665
- Thread starter
- #21
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 16
MTUNZIATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Clara akavuta pumzi ndefu akaenda kukaa kitandani,akainama na kujishika kichwa kwa mikono yake miwili.Sikuelewa alikuwa akiwaza kitu gani lakini ni wazi alikuwa katika hali ya kukata tamaa.Aliumizwa mno na maneno niliyomwambia.Nilimtazama kwa makini huruma ikaniingia.Clara alikuwa akiishi maisha yake kwa raha mustarehe na hakuwa na matatizo .Aliogopa kuingia katika mahusiano tena baada ya kutendwa katika uhusiano wake wa awali.Japokuwa hajawahi kunieleza ni kitu gani kilimtokea hapo kabla kiasi cha kumfanya awachukie wanaume lakini ni wazi kitu alichofanyiwa kilimuumiza sana kiasi cha kumfanya awachukie wanaume wote .Baada ya miaka kadhaa kupita ameamua kumuamini na kumpa mwanaume mwingine nafasi katika moyo wake,mwanaume huyo ni mimi.Siku mbili tu tangu awe na mimi amekutana na mambo ambayo yametonesha donda lililokwisha pona muda mrefu.Clara amejikuta akiuumiza tena moyo wake.Jana nilituhumiwa kumchukua mtoto Baraka bila ridhaa ya wazazi wake kitu kilichopelekea kushikiliwa na polisi kwa masaa kadhaa tukihojiwa.Kutokana na sakata hilo Clara aliahirisha safari yake ya muhimu sana.Leo hii limeibuka tena jambo jingine jipya.Sikuhitaji kumuumiza Clara namna ile lakini sikuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kumueleza ukweli.Sikuona umuhimu wa kumficha kitu kwa sababu hata kama ningeficha ingekuja kufahamika tu.
ENDELEA……………………..
Clara alikuwa akitoa machozi na kwa mbali nilisikia kilio cha chini chini.Nafikiri alikuwa akilia kwa mambo niliyoyafanya kwa sababu ni kinyume kabisa cha maadili ya mfanyakazi wa umma.Niliiba fedha ya serikali ambayo ni kodi za wananchi.Fedha zile nyingi zingeweza kutumika katika miradi ya maendeleo kama zahanati na kununua vifaa vya shule n.k. Kwa mara ya kwanza nilihisi uchungu kwa kuliibia taifa namna ile.Nilisikia uchungu mkubwa moyoni.Kingine nilichohisi kinamliza Clara ni namna jina lake litakavyochafuka.Clara ni mtu mwenye jina na heshima kubwa sana katika jamii kwa hiyo kitendo cha Emmy kulipeka suala lile mbele ya sheria na yeye kuonekana nami ni wazi kingelichafua jina lake zuri lenye heshima kubwa ndani na nje ya nchi.Roho iliniuma nikamuonea huruma mrembo yule aliyekuwa ameketi kitandani akilia kwa kwikwi.
“Kama ni kuchafuka ni bora nichafuke mimi na Clara abaki na heshima yake .Kwa mambo niliyoyafanya sistahili kuwa karibu na mtu kama Clara.Itakuwa vizuri kama nikibaki mwenyewe na kuendelea kuubeba msalaba wangu mwenyewe.” Nikawaza na kuanza kupiga hatua za taratibu na kumsogelea Clara.Nilikuwa na wasi wasi mwingi ni jinsi gani ningeweza kuongea naye .Kwa sasa sikutegemea kama angetaka hata kuzungumza nami.Nikajikaza na kumshika bega.
“Clara “ Nikamuita taratibu akainua uso wake uliokuwa umelowa machozi.Nikamtazama nikasikia uchungu mwingi .Nilimuahidi Clara kwamba sintamliza lakini leo hii uso wake umelowa machozi kwa sababu yangu.
“Clara najua sistahili hata kuongea na wewe tena lakini tafadhali naomba unisikilize japo kwa dakika chache ” Nikasema na kutulia kidogo,nikamtazama Clara aliyekuwa ametulia kimya .
“Clara nakumbuka nilikuahidi kwamba sintathubutu hata siku moja kukutoa chozi na wala kuumiza moyo wako. Ahadi niliyokupa nimeshindwa kuitimiza na tazama sasa hivi uso wako umejaa machozi,na moyo wako umeumia kwa sababu yangu.Nimesikia uchungu sana kukuona ukitoa machozi kwa jambo ulilolisikia.Kwa mara ya kwanza ninajutia kitu nilichokifanya.Chozi lako ulilomwaga limenifanya nisikie uchungu mwingi na kuuona ujinga nilioufanya.Kitu nilichokifanya nitakijutia katika maisha yangu yote yaliyobaki kwa sababu kimenifanya nikampoteza mwanamke niliyempenda kwa moyo wangu wote.”
Clara akaonyesha mstuko baada ya kutamka maneno yale ya mwisho.
“ Clara narudia tena kukiri kwamba nilifanya kosa kubwa sana kuchukua fedha zile za serikali ambazo ni kodi na majasho ya wanachi wanyonge. Fedha ile ingeweza kufanya shughuli mbali mbali za maendeleo .Chozi ulilolimwaga limenifanya nitambue kosa langu.Ninastahili kufikishwa mbele ya sheria na kupata adhabu.Ni kweli ninastahili adhabu kwa kosa hili.Clara wewe ni mtu safi uliyezitumia nguvu na vipaji vyako hadi ukafika hapa ulipo sasa hivi.Jina lako ni kubwa na heshima yako katika jamii ni kubwa sana.Siko tayari kuona jina lako likichafuliwa kwa sababu yangu.Japokuwa inaniuma kusema lakini ni lazima niseme kwamba kutokana na hali halisi ilivyo siko tayari kuyakubali matakwa ya Emmy.Siko tayari kumpatia kiasi hicho cha pesa anachokitaka.Kama alivyokuwa ametishia kwamba endapo nisipotimiza matakwa yake ni lazima atanifikisha katika vyombo vya sheria.Niko tayari kwa hilo..Kwa mambo niliyoyafanya napenda kukiri kwamba sistahili kuwa na mtu kama wewe.Ninaomba uhusiano wetu Clara uishie hapa ili niweze kuyakabili mambo haya mimi mwenyewe bila kumuhusisha mtu yeyote .Hii itakuwa njia pekee ya kukuepusha na aibu hii kubwa na kulilinda jina lako safi.” Nikasema na kutulia kidogo.Clara akafuta machozi na kunitazama kisha akanivuta mkono na kunifanyia ishara niketi kitandani.
“Wayne tafadhali usiseme hivyo.Ukisema hivyo unazidi kunifanya niumie zaidi “Clara akasema
“ Inaniuma kusema hivyo Clara lakini huo ndio ukweli halisi ambao lazima tuukubali siko tayari kuona jina lako likichafuka kwa ufisadi nilioufanya..Ninastahili kuubeba msalaba wangu mwenyewe”
“Wayne naomba unisikilize.” Akasema Clara na kuinama chini kidogo akatafakari.
“Ni kweli nimeumia sana.Siwezi kuelezea ni kwa kiasi gani lakini nimeumia mno.Ni muda mfupi sana tumekuwa pamoja lakini kwa muda huu mfupi yameanza kujitokeza mambo ambayo yamesababisha uhusiano wetu kutetereka.Wayne siku zote nilikuwa nikikwepa kujiingiza katika mahusiano kwa kuogopa kuumiza moyo wangu kwa mara nyingne tena.Pamoja na yote yaliyotokea lakini kuachana si suluhisho.Haya yote ni majaribu ambayo hatuna budi kuyashinda.Mimi siwezi kukuacha hata uniambie kitu gani.Tayari nimekwisha ufungua moyo wangu na kuuruhusu upende tena kwa hiyo siwezi kurudi nyuma.Niko tayari kusimama na wewe katika sakata hili.Sintajali kama jina langu litachafuka ama la.Ninachokijua ni kwamba niko na wewe na moyo wangu unahitaji kuwa na wewe pekee.kwa hiyo sahau suala la kuachana kwa sababu siyo suluhisho la tatizo hili.Nikikuacha leo hii mimi ndiye nitakayeumia zaidi .” Clara akasema na kunivuta kwake ,akanikumbatia halafu akaniachia na kusema
“Pamoja na yote uliyoyafanya Wayne lakini bado hayanizuii mimi kukupenda au kuwa na wewe.Wote tunafanya makosa katika maisha yetu na tujapogundua baadae makosa tuliyoyafanya huwa tayari tumeshachelewa.Wayne nafurahi kama umeligundua kosa lako na kulijutia.Kinachotakiwa kwa sasa ni kuangalia namna tutakavyoweza kulimaliza suala hili” Clara akasema.Nikamtazama mrembo yule na kumwambia
“Kuna jambo nimekuwa nikilifikiria pengine labda linaweza likasaidia ili suala hili libaki kama lilivyo”
“jambo gani hilo Wayne? Clara akauliza
“nafikiria kukubaliana na matakwa ya Emmy.” Nikasema na kumfanya Clara astuke
“Yaani kumpatia Emmy pesa zote kama alivyotaka?
“Ndiyo Clara.Nadhani hii itakuwa njia pekee itakayomfanya anyamaze na asilipeleke suala hili katika vyombo vya usalama”
“Wayne hapana.Huwezi fanya hivyo.Hutakiwi kukubaliana na matakwa ya Emmy.Kukubali anachokitaka kutaonyesha ni jinsi gani ulivyo dhaifu na atautumia udhaifu huo kukufanyia kila aina ya vituko.Leo atataka ufanye hiki,kesho atakuambia ufanye kile.Usikubali kamwe kumpa hiyo nafasi.Unachotakiwa kukifanya ni kumpigia simu na kumtaarfu kwamba hauko tayari kukubaliana na vitisho vyake na kwamba hutampatia hata senti moja katika zile fedha.Muonyeshe kwamba uko imara na hauko tayari kuyumbishwa na kama anataka kupeleka nyaraka hizo katika vyombo vya kisheria mpe ruhusa afanye hivyo.” Clara akasema na kunifanya nizidi kumshangaa.
“Unashangaa nini Wayne? Chukua simu na umpigie sasa hivi na umweleze hayo niliyokwambia halafu nitakueleza nini kitafuata.” Nikachukua simu na kupiga namba zile alizonipigia Emmy.
“hallo Wayne.Mbona umenipigia simu mapema namna hii? Umeshanitumia hizo fedha kama nilivyokuambia? Akasema Emmy baada ya kupokea simu.
“Emmy tafadhali naomba unisikilize” Nikasema huku uso wangu umekasirika.
“Nakusikiliza Wayne” Akasema Emmy
“Nimekupigia simu kukuonya kwamba iwe ni mwanzo na mwisho kunipigia simu na kunipa amri.Naomba ufahamu kwamba siko tayari kuendeshwa na mwanamke mwenye upeo finyu kama wewe.Ninakupa masaa kumi na mbili ,nyaraka zote ulizoziiba hapa nyumbani kwangu ziwe zimerudi na kama hutatekeleza utanitambua mimi ni nani.Nimechoshwa nawe Emmy...” Nikasema kwa ukali.Emmy akacheka na kusema
“Wayne,kumbe kuna nyakati huwa unakuwa jasiri namna hii? Hahahaaa nafurahi kuona huyo mwanamitindo wako anakupa ujasiri wa namna hiyo.Mpe salamu zangu .Na wewe kwa kuwa umeonyesha kiburi basi naomba tupambane mimi na wewe na tuone ni nani atakayechukua ushindi.Bado nakusisitizia kwamba masaa ishirini na manne yakipita bila fedha niliyokwambia kuingia katika akaunti yangu basi ujue kwamba mwisho wako utakuwa ni gerezani na pesa yote nitabaki naimiliki mimi.Kwa hiyo wakati bado una nafasi tafadhali fanya vile nilivyokuamuru.Jambo la mwisho nakuomba usinipigie simu kama huna kitu cha maana cha kuniambia.” Emmy akasema kwa jeuri na kukata simu
Nilipandwa na hasira kasi kwamba kama angekuwa karibu ningemshushia kipigo kikali.Nilikuwa nikihema mfululizo kwa hasira nilizokuwa nazo.Sikuelewa sababu ya Emmy kuwa na uadui mkubwa na mimi kiasi kile.
“You did great” akasema Clara huku akinipiga piga mgongoni
“Kwa sasa hata yeye atakuwa akijiuliza ni kwa nini umekuwa jasiri namna ile.Hata kama alikuwa na wazo la kwenda katika vyombo vya sheria itambidi ajiulize mara mbili.”
“Clara nina wasi wasi baradhuli huyu anaweza akakusababishia matatizo makubwa.”
“Usijali kuhusu hilo Wayne kwa sababu huyu mtalaka wako anaonekana bado ana akili za kitoto na haniwezi mtu kama mimi.Sasa sikiliza Wayne.Mimi nitakusaidia katika kulitatua tatizo hili kwa sababu bado liko ndani ya uwezo wangu kulimaliza.Nitalimaliza suala hili lakini naomba unipe ahadi kwamba baada kumalizika hautajihusisha tena na masuala ya uhujumu wa uchumi wala aina yopyote ya ufujaji wa fedha za umma au kujipatia fedha kwa njia isiyo halali.”
“Clara ninajutia kosa nililolifanya na ninataka kuyabadili maisha yangu na kuishi maisha mazuri ya kujitafutia fedha za halali.” Nikasema na kumfanya Clara atabasamu
“Nafurahi kusikia hivyo.Kwa sababu nakupenda nimeamua kulibeba mimi suala hili.Mpango mzima utasomeka kwamba mimi na wewe ni washirika wa kibiashara toka muda mrefu na una kiasi Fulani cha hisa katika kampuni yangu ya mavazi kwa hiyo fedha zile zilitoka katika kampuni yangu.Nitawasiliana na wahasibu wa kampuni yangu ili waandae nyaraka ambazo zitakuonyesha kwamba wewe ni mshirika wangu kibiashara na kwamba kwa nyakati tofauti ulipokea fedha toka katika kampuni yangu.Vile vile nitawaelekeza waingize leo kiasi fulani cha pesa katika akaunti yako yenye fedha anazozitaka Emmy ili ionekane ni kweli umekuwa unapokea fedha toka kampuni yetu.Kokote atakakokwenda Emmy ataonekana mwongo na tutamtaka athibitishe hilo analolisema na itakuwa ni aibu kubwa kwake.”
“Ouh Clara sijui hata nikushuruje kwa msaada huu mkubwa unaonisaidia.” Nikasema huku nikimkumbatia
“Bado sijamaliza Wayne.Kuna jambo ambalo ninataka kuliweka sawa.Nina uhakika suala hili litamalizika kwa sababu litasimamiwa na wanasheria wangu ambao ni wanasheria wakubwa na wenye uzoefu .Baada ya suala hili kumalizika nitakuwa nimeingia katika dhambi kubwa.Nimeshiriki katika kufunika uovu.Kwa maana hiyo sintakuwa na amani daima.Ninachotaka kukisema hapa ni kwamba fedha ile yote uliyoichukua inabidi tuirudishe kwenye jamii. Sina maana ya kufanya mkutano na waandishi wa habari na kusema kwamba ulichukua fedha za serikali na unataka kuzirudisha bali tutazitumia katika mradi wowote wa maendeleo.Tunaweza tukazitumia fedha hizo kujenga darasa au kuchimba kisima cha maji katika sehemu ambayo kuna shida ya maji au kununua vitabu mashuleni ili mradi tufanye kitu chochote chenye faida kwa jamii kupitia fedha ile.Iwapo utakubaliana nami kuhusu suala hilo nitaamini kwamba ni kweli unajutia kosa lako na kwamba una lengo la dhati la kubadilika na kuanza kuishi maisha mapya kabisa .Je uko tayari kwa hilo? Clara akauliza
Lilikuwa ni swali gumu sana kulijbu kwa haraka. Nikatafakari kwa sekunde chache ili nione nitamjibu nini. Ni kweli nilikuwa na mamilioni ya fedha ambazo zote zilitokana na ufisadi tulioufanya mimi na wenzangu kwa fedha ya walipa kodi wa Tanzania.Swali lile lilikuwa ni mtego wa mimi kuchagua ama fedha ama clara.Kwa sasa Clara ndiye aliyekuwa kila kitu kwangu .Fedha zote nilizokuwa nazo hazitakuwa na maana kama nitaikosa furaha hii ya maisha yangu.Nikakata shauri ni bora nikose fedha lakini niwe na Clara.
“Clara nashukuru sana kwa kukutana nawe kwani ni wewe pekee ambaye umenifanya nifahamu nini nimefanya na nini ninapaswa kufanya .Nimejifunza kitu kikubwa sana toka kwako.Kwa moyo wote nakuahidi kwamba baada ya mambo haya yote kuisha fedha zile zote tutazirudisha kwa wananchi.” Nikasema na kumfanya Clara atabasamu ,akanikumbatia
“Nimefurahi sana kusikia hivyo Wayne.Basi usiumize kichwa tena na huyu kichaa Emmy .Vaa nguo zako tutoke na kuendelea na siku yetu kama tulivyokuwa tumepanga.Wakati ukijiandaa naomba niitumie nafasi hii kuwasiliana na watu wa kampuni yangu pamoja na wanasheria ili waanze kulishughulikia suala hili haraka.” Clara akasema akanibusu na kutoka mle chumbani.Nilibaki nimesimama kwa dakika tatu nikitafakari kisha nikaanza kuvaa nguo tayari kwa kutoka.Baada ya muda Clara akaingia tena chumbani.
“Kuwa na amani mpenzi wangu,usiumizwe kichwa na Emmy.Mimi nimeamua kulisimamia suala hili na litakwisha.Naomba uniamini.” Clara akaniambia huku akilirekebisha shati nililokuwa nimevaa.
“Clara sioni hata nitamke neno gani kukushukuru kwa namna ulivyoamua kunisaidia katika suala hili.Nina deni kubwa ambalo ninahitaji kukulipa” nikasema na kumfanya Clara atabasamu ,akanisogelea karibu zaidi akanibusu.
“Wayne ni kweli una deni kwangu na nitakuomba unilipe kitu kimoja tu”
“Clara niko tayari kukulipa kitu chochote kile utakachoomba.Niambie unahitaji kitu gani na sinta sita kukupatia.Niko tayari kufika hadi pembe ya mwisho wa dunia kwa ajili ya kukutafutia kitu unachokihitaji.Niambie tafadhali unataka nikulipe nini?
Clara akanitazama kwa macho yake mazuri na kunifanya nisisimkwe mwili
“Una uhakika utanipatia ninachokihitaji? Akauliza Clara
“Nina uhakika Clara.Nitakupatia chochote kile unachokihitaji.” Nikajibu kwa kujiamini
“nafurahi kusikia hivyo Wayne.Kitu ninachotaka toka kwako ni kidogo sana na ambacho hakikulazimu kwenda hadi mwisho wa dunia kukipata.Ninachohitaji ni nafasi ndani ya moyo wako.”
Nikamuangalia Clara na kutabasamu baada ya kutamka vile.Nikamvuta karibu yangu zaidi nikamuangalia usoni na kumwambia.
“Clara huna haja ya kuomba nafasi ndani ya moyo wangu.Toka siku nimezaliwa tayari nafasi yako ilikwisha wekwa moyoni mwangu.Moyo wangu umejazwa na sura yako pekee.hakuna tena mwanamke mwingine anayeweza kuipata nafasi hii iliyojazwa nawe.Mapenzi yangu yote yameishia kwako pekee Sina mapenzi tena kwa mwanamke mwingine .” Nikasema na kumbusu Clara ambaye alikilaza kichwa chake kifuani kwangu na kunikumbatia kwa mahaba mazito.
“Wayne naomba uelewe kwamba ninakupenda kuliko kitu chochote katika dunia hii.Wewe ndiye kila kitu kwangu.tafadhali nahitaji nafasi ya kudumu ndani ya moyo wako.Nataka uwe wangu peke yangu.Nahitaji muda wako uliobakia wa kuishi hapa duniani uumalize ukiwa na mimi.Nataka tuishi pamoja,nataka tuzae watoto na kutengeneza familia yenye furaha na upendo.Nnakuhitaji Wayne katika maisha yangu” Mrembo huyu adhimu alikuwa akiongea toka nani kabisa mwa moyo wake.Ni kweli alikuwa akinipenda na hata mimi nilikuwa nikimpenda kupita kiasi.Nilijilaumu sana kwa kupoteza muda mwingi kwa mtu kama Emmy mwanamke asiye na shukrani ambaye katika kipindi cha maisha niliyoishi naye amenisababishai maumivu ambayo naweza kusema ni zaidi ya maumivu ya kawaida.
“Clara my angel.Nakuhakikishia kwamba wewe ni wangu pekee,na mimi niwako pekee.Sijui nitampa nini Mungu kama shukrani zangu kwake kwa kuniletea furaha hii kubwa ya maisha yangu.Amenirudishia furaha ya maisha iliyokwisha toweka.Clara nitakupenda milele na milele na ninakuahidi kwamba hakuna mtu yeyote katika dunia hii atakayeweza kututenganisha.Ni kifo pekee kitakachoweza kututengansiaha mimi na wewe.Nitaishi nawe na kukupenda hadi katika pumzi yangu ya mwisho “ maneno yale yakamfanya Clara ashindwe kujizuia kudondosha machozi.
“tafadhali usilie Clara.Huu ni wakati wa kufurahi na si wakati wa kudondosha machozi” nikamwambia huku nikimfuta machozi
“Wayne ninalia kutokana na furaha niliyonayo.Nimekaa miaka mingi nikijihisi ni mwenye furaha lakini sikuwahi hata mara moja kuipata furaha kubwa kama niipatayo sasa kwa kuwa nawe.Ni wewe ndiye uliyenipa furaha hii kubwa maishani.” Akasema Clara.na kuniangalia usoni.
“Darling twende tukaendelee na ratiba yetu ya siku.Tuna kila sababu ya kufurahi” Tukatoka na kuingia garini tukaelekea eneo la meserani ambako kuna hifadhi ya nyoka.Mimi si mpenzi kabisa wa nyoka na ni moja kati ya vitu ninavyoviogopa sana katika hii dunia lakini niliamua kwenda huko kwa sababu Clara alipenda kwenda kutazama nyoka wa aina mbali mbali wanaofugwa.Amekuwa akisikia hifadhi hii ya nyoka na alipanga siku moja aitembelee na sasa ameipata nafasi hiyo hakutaka kuipoteza.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………….
SEHEMU YA 16
MTUNZIATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Clara akavuta pumzi ndefu akaenda kukaa kitandani,akainama na kujishika kichwa kwa mikono yake miwili.Sikuelewa alikuwa akiwaza kitu gani lakini ni wazi alikuwa katika hali ya kukata tamaa.Aliumizwa mno na maneno niliyomwambia.Nilimtazama kwa makini huruma ikaniingia.Clara alikuwa akiishi maisha yake kwa raha mustarehe na hakuwa na matatizo .Aliogopa kuingia katika mahusiano tena baada ya kutendwa katika uhusiano wake wa awali.Japokuwa hajawahi kunieleza ni kitu gani kilimtokea hapo kabla kiasi cha kumfanya awachukie wanaume lakini ni wazi kitu alichofanyiwa kilimuumiza sana kiasi cha kumfanya awachukie wanaume wote .Baada ya miaka kadhaa kupita ameamua kumuamini na kumpa mwanaume mwingine nafasi katika moyo wake,mwanaume huyo ni mimi.Siku mbili tu tangu awe na mimi amekutana na mambo ambayo yametonesha donda lililokwisha pona muda mrefu.Clara amejikuta akiuumiza tena moyo wake.Jana nilituhumiwa kumchukua mtoto Baraka bila ridhaa ya wazazi wake kitu kilichopelekea kushikiliwa na polisi kwa masaa kadhaa tukihojiwa.Kutokana na sakata hilo Clara aliahirisha safari yake ya muhimu sana.Leo hii limeibuka tena jambo jingine jipya.Sikuhitaji kumuumiza Clara namna ile lakini sikuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kumueleza ukweli.Sikuona umuhimu wa kumficha kitu kwa sababu hata kama ningeficha ingekuja kufahamika tu.
ENDELEA……………………..
Clara alikuwa akitoa machozi na kwa mbali nilisikia kilio cha chini chini.Nafikiri alikuwa akilia kwa mambo niliyoyafanya kwa sababu ni kinyume kabisa cha maadili ya mfanyakazi wa umma.Niliiba fedha ya serikali ambayo ni kodi za wananchi.Fedha zile nyingi zingeweza kutumika katika miradi ya maendeleo kama zahanati na kununua vifaa vya shule n.k. Kwa mara ya kwanza nilihisi uchungu kwa kuliibia taifa namna ile.Nilisikia uchungu mkubwa moyoni.Kingine nilichohisi kinamliza Clara ni namna jina lake litakavyochafuka.Clara ni mtu mwenye jina na heshima kubwa sana katika jamii kwa hiyo kitendo cha Emmy kulipeka suala lile mbele ya sheria na yeye kuonekana nami ni wazi kingelichafua jina lake zuri lenye heshima kubwa ndani na nje ya nchi.Roho iliniuma nikamuonea huruma mrembo yule aliyekuwa ameketi kitandani akilia kwa kwikwi.
“Kama ni kuchafuka ni bora nichafuke mimi na Clara abaki na heshima yake .Kwa mambo niliyoyafanya sistahili kuwa karibu na mtu kama Clara.Itakuwa vizuri kama nikibaki mwenyewe na kuendelea kuubeba msalaba wangu mwenyewe.” Nikawaza na kuanza kupiga hatua za taratibu na kumsogelea Clara.Nilikuwa na wasi wasi mwingi ni jinsi gani ningeweza kuongea naye .Kwa sasa sikutegemea kama angetaka hata kuzungumza nami.Nikajikaza na kumshika bega.
“Clara “ Nikamuita taratibu akainua uso wake uliokuwa umelowa machozi.Nikamtazama nikasikia uchungu mwingi .Nilimuahidi Clara kwamba sintamliza lakini leo hii uso wake umelowa machozi kwa sababu yangu.
“Clara najua sistahili hata kuongea na wewe tena lakini tafadhali naomba unisikilize japo kwa dakika chache ” Nikasema na kutulia kidogo,nikamtazama Clara aliyekuwa ametulia kimya .
“Clara nakumbuka nilikuahidi kwamba sintathubutu hata siku moja kukutoa chozi na wala kuumiza moyo wako. Ahadi niliyokupa nimeshindwa kuitimiza na tazama sasa hivi uso wako umejaa machozi,na moyo wako umeumia kwa sababu yangu.Nimesikia uchungu sana kukuona ukitoa machozi kwa jambo ulilolisikia.Kwa mara ya kwanza ninajutia kitu nilichokifanya.Chozi lako ulilomwaga limenifanya nisikie uchungu mwingi na kuuona ujinga nilioufanya.Kitu nilichokifanya nitakijutia katika maisha yangu yote yaliyobaki kwa sababu kimenifanya nikampoteza mwanamke niliyempenda kwa moyo wangu wote.”
Clara akaonyesha mstuko baada ya kutamka maneno yale ya mwisho.
“ Clara narudia tena kukiri kwamba nilifanya kosa kubwa sana kuchukua fedha zile za serikali ambazo ni kodi na majasho ya wanachi wanyonge. Fedha ile ingeweza kufanya shughuli mbali mbali za maendeleo .Chozi ulilolimwaga limenifanya nitambue kosa langu.Ninastahili kufikishwa mbele ya sheria na kupata adhabu.Ni kweli ninastahili adhabu kwa kosa hili.Clara wewe ni mtu safi uliyezitumia nguvu na vipaji vyako hadi ukafika hapa ulipo sasa hivi.Jina lako ni kubwa na heshima yako katika jamii ni kubwa sana.Siko tayari kuona jina lako likichafuliwa kwa sababu yangu.Japokuwa inaniuma kusema lakini ni lazima niseme kwamba kutokana na hali halisi ilivyo siko tayari kuyakubali matakwa ya Emmy.Siko tayari kumpatia kiasi hicho cha pesa anachokitaka.Kama alivyokuwa ametishia kwamba endapo nisipotimiza matakwa yake ni lazima atanifikisha katika vyombo vya sheria.Niko tayari kwa hilo..Kwa mambo niliyoyafanya napenda kukiri kwamba sistahili kuwa na mtu kama wewe.Ninaomba uhusiano wetu Clara uishie hapa ili niweze kuyakabili mambo haya mimi mwenyewe bila kumuhusisha mtu yeyote .Hii itakuwa njia pekee ya kukuepusha na aibu hii kubwa na kulilinda jina lako safi.” Nikasema na kutulia kidogo.Clara akafuta machozi na kunitazama kisha akanivuta mkono na kunifanyia ishara niketi kitandani.
“Wayne tafadhali usiseme hivyo.Ukisema hivyo unazidi kunifanya niumie zaidi “Clara akasema
“ Inaniuma kusema hivyo Clara lakini huo ndio ukweli halisi ambao lazima tuukubali siko tayari kuona jina lako likichafuka kwa ufisadi nilioufanya..Ninastahili kuubeba msalaba wangu mwenyewe”
“Wayne naomba unisikilize.” Akasema Clara na kuinama chini kidogo akatafakari.
“Ni kweli nimeumia sana.Siwezi kuelezea ni kwa kiasi gani lakini nimeumia mno.Ni muda mfupi sana tumekuwa pamoja lakini kwa muda huu mfupi yameanza kujitokeza mambo ambayo yamesababisha uhusiano wetu kutetereka.Wayne siku zote nilikuwa nikikwepa kujiingiza katika mahusiano kwa kuogopa kuumiza moyo wangu kwa mara nyingne tena.Pamoja na yote yaliyotokea lakini kuachana si suluhisho.Haya yote ni majaribu ambayo hatuna budi kuyashinda.Mimi siwezi kukuacha hata uniambie kitu gani.Tayari nimekwisha ufungua moyo wangu na kuuruhusu upende tena kwa hiyo siwezi kurudi nyuma.Niko tayari kusimama na wewe katika sakata hili.Sintajali kama jina langu litachafuka ama la.Ninachokijua ni kwamba niko na wewe na moyo wangu unahitaji kuwa na wewe pekee.kwa hiyo sahau suala la kuachana kwa sababu siyo suluhisho la tatizo hili.Nikikuacha leo hii mimi ndiye nitakayeumia zaidi .” Clara akasema na kunivuta kwake ,akanikumbatia halafu akaniachia na kusema
“Pamoja na yote uliyoyafanya Wayne lakini bado hayanizuii mimi kukupenda au kuwa na wewe.Wote tunafanya makosa katika maisha yetu na tujapogundua baadae makosa tuliyoyafanya huwa tayari tumeshachelewa.Wayne nafurahi kama umeligundua kosa lako na kulijutia.Kinachotakiwa kwa sasa ni kuangalia namna tutakavyoweza kulimaliza suala hili” Clara akasema.Nikamtazama mrembo yule na kumwambia
“Kuna jambo nimekuwa nikilifikiria pengine labda linaweza likasaidia ili suala hili libaki kama lilivyo”
“jambo gani hilo Wayne? Clara akauliza
“nafikiria kukubaliana na matakwa ya Emmy.” Nikasema na kumfanya Clara astuke
“Yaani kumpatia Emmy pesa zote kama alivyotaka?
“Ndiyo Clara.Nadhani hii itakuwa njia pekee itakayomfanya anyamaze na asilipeleke suala hili katika vyombo vya usalama”
“Wayne hapana.Huwezi fanya hivyo.Hutakiwi kukubaliana na matakwa ya Emmy.Kukubali anachokitaka kutaonyesha ni jinsi gani ulivyo dhaifu na atautumia udhaifu huo kukufanyia kila aina ya vituko.Leo atataka ufanye hiki,kesho atakuambia ufanye kile.Usikubali kamwe kumpa hiyo nafasi.Unachotakiwa kukifanya ni kumpigia simu na kumtaarfu kwamba hauko tayari kukubaliana na vitisho vyake na kwamba hutampatia hata senti moja katika zile fedha.Muonyeshe kwamba uko imara na hauko tayari kuyumbishwa na kama anataka kupeleka nyaraka hizo katika vyombo vya kisheria mpe ruhusa afanye hivyo.” Clara akasema na kunifanya nizidi kumshangaa.
“Unashangaa nini Wayne? Chukua simu na umpigie sasa hivi na umweleze hayo niliyokwambia halafu nitakueleza nini kitafuata.” Nikachukua simu na kupiga namba zile alizonipigia Emmy.
“hallo Wayne.Mbona umenipigia simu mapema namna hii? Umeshanitumia hizo fedha kama nilivyokuambia? Akasema Emmy baada ya kupokea simu.
“Emmy tafadhali naomba unisikilize” Nikasema huku uso wangu umekasirika.
“Nakusikiliza Wayne” Akasema Emmy
“Nimekupigia simu kukuonya kwamba iwe ni mwanzo na mwisho kunipigia simu na kunipa amri.Naomba ufahamu kwamba siko tayari kuendeshwa na mwanamke mwenye upeo finyu kama wewe.Ninakupa masaa kumi na mbili ,nyaraka zote ulizoziiba hapa nyumbani kwangu ziwe zimerudi na kama hutatekeleza utanitambua mimi ni nani.Nimechoshwa nawe Emmy...” Nikasema kwa ukali.Emmy akacheka na kusema
“Wayne,kumbe kuna nyakati huwa unakuwa jasiri namna hii? Hahahaaa nafurahi kuona huyo mwanamitindo wako anakupa ujasiri wa namna hiyo.Mpe salamu zangu .Na wewe kwa kuwa umeonyesha kiburi basi naomba tupambane mimi na wewe na tuone ni nani atakayechukua ushindi.Bado nakusisitizia kwamba masaa ishirini na manne yakipita bila fedha niliyokwambia kuingia katika akaunti yangu basi ujue kwamba mwisho wako utakuwa ni gerezani na pesa yote nitabaki naimiliki mimi.Kwa hiyo wakati bado una nafasi tafadhali fanya vile nilivyokuamuru.Jambo la mwisho nakuomba usinipigie simu kama huna kitu cha maana cha kuniambia.” Emmy akasema kwa jeuri na kukata simu
Nilipandwa na hasira kasi kwamba kama angekuwa karibu ningemshushia kipigo kikali.Nilikuwa nikihema mfululizo kwa hasira nilizokuwa nazo.Sikuelewa sababu ya Emmy kuwa na uadui mkubwa na mimi kiasi kile.
“You did great” akasema Clara huku akinipiga piga mgongoni
“Kwa sasa hata yeye atakuwa akijiuliza ni kwa nini umekuwa jasiri namna ile.Hata kama alikuwa na wazo la kwenda katika vyombo vya sheria itambidi ajiulize mara mbili.”
“Clara nina wasi wasi baradhuli huyu anaweza akakusababishia matatizo makubwa.”
“Usijali kuhusu hilo Wayne kwa sababu huyu mtalaka wako anaonekana bado ana akili za kitoto na haniwezi mtu kama mimi.Sasa sikiliza Wayne.Mimi nitakusaidia katika kulitatua tatizo hili kwa sababu bado liko ndani ya uwezo wangu kulimaliza.Nitalimaliza suala hili lakini naomba unipe ahadi kwamba baada kumalizika hautajihusisha tena na masuala ya uhujumu wa uchumi wala aina yopyote ya ufujaji wa fedha za umma au kujipatia fedha kwa njia isiyo halali.”
“Clara ninajutia kosa nililolifanya na ninataka kuyabadili maisha yangu na kuishi maisha mazuri ya kujitafutia fedha za halali.” Nikasema na kumfanya Clara atabasamu
“Nafurahi kusikia hivyo.Kwa sababu nakupenda nimeamua kulibeba mimi suala hili.Mpango mzima utasomeka kwamba mimi na wewe ni washirika wa kibiashara toka muda mrefu na una kiasi Fulani cha hisa katika kampuni yangu ya mavazi kwa hiyo fedha zile zilitoka katika kampuni yangu.Nitawasiliana na wahasibu wa kampuni yangu ili waandae nyaraka ambazo zitakuonyesha kwamba wewe ni mshirika wangu kibiashara na kwamba kwa nyakati tofauti ulipokea fedha toka katika kampuni yangu.Vile vile nitawaelekeza waingize leo kiasi fulani cha pesa katika akaunti yako yenye fedha anazozitaka Emmy ili ionekane ni kweli umekuwa unapokea fedha toka kampuni yetu.Kokote atakakokwenda Emmy ataonekana mwongo na tutamtaka athibitishe hilo analolisema na itakuwa ni aibu kubwa kwake.”
“Ouh Clara sijui hata nikushuruje kwa msaada huu mkubwa unaonisaidia.” Nikasema huku nikimkumbatia
“Bado sijamaliza Wayne.Kuna jambo ambalo ninataka kuliweka sawa.Nina uhakika suala hili litamalizika kwa sababu litasimamiwa na wanasheria wangu ambao ni wanasheria wakubwa na wenye uzoefu .Baada ya suala hili kumalizika nitakuwa nimeingia katika dhambi kubwa.Nimeshiriki katika kufunika uovu.Kwa maana hiyo sintakuwa na amani daima.Ninachotaka kukisema hapa ni kwamba fedha ile yote uliyoichukua inabidi tuirudishe kwenye jamii. Sina maana ya kufanya mkutano na waandishi wa habari na kusema kwamba ulichukua fedha za serikali na unataka kuzirudisha bali tutazitumia katika mradi wowote wa maendeleo.Tunaweza tukazitumia fedha hizo kujenga darasa au kuchimba kisima cha maji katika sehemu ambayo kuna shida ya maji au kununua vitabu mashuleni ili mradi tufanye kitu chochote chenye faida kwa jamii kupitia fedha ile.Iwapo utakubaliana nami kuhusu suala hilo nitaamini kwamba ni kweli unajutia kosa lako na kwamba una lengo la dhati la kubadilika na kuanza kuishi maisha mapya kabisa .Je uko tayari kwa hilo? Clara akauliza
Lilikuwa ni swali gumu sana kulijbu kwa haraka. Nikatafakari kwa sekunde chache ili nione nitamjibu nini. Ni kweli nilikuwa na mamilioni ya fedha ambazo zote zilitokana na ufisadi tulioufanya mimi na wenzangu kwa fedha ya walipa kodi wa Tanzania.Swali lile lilikuwa ni mtego wa mimi kuchagua ama fedha ama clara.Kwa sasa Clara ndiye aliyekuwa kila kitu kwangu .Fedha zote nilizokuwa nazo hazitakuwa na maana kama nitaikosa furaha hii ya maisha yangu.Nikakata shauri ni bora nikose fedha lakini niwe na Clara.
“Clara nashukuru sana kwa kukutana nawe kwani ni wewe pekee ambaye umenifanya nifahamu nini nimefanya na nini ninapaswa kufanya .Nimejifunza kitu kikubwa sana toka kwako.Kwa moyo wote nakuahidi kwamba baada ya mambo haya yote kuisha fedha zile zote tutazirudisha kwa wananchi.” Nikasema na kumfanya Clara atabasamu ,akanikumbatia
“Nimefurahi sana kusikia hivyo Wayne.Basi usiumize kichwa tena na huyu kichaa Emmy .Vaa nguo zako tutoke na kuendelea na siku yetu kama tulivyokuwa tumepanga.Wakati ukijiandaa naomba niitumie nafasi hii kuwasiliana na watu wa kampuni yangu pamoja na wanasheria ili waanze kulishughulikia suala hili haraka.” Clara akasema akanibusu na kutoka mle chumbani.Nilibaki nimesimama kwa dakika tatu nikitafakari kisha nikaanza kuvaa nguo tayari kwa kutoka.Baada ya muda Clara akaingia tena chumbani.
“Kuwa na amani mpenzi wangu,usiumizwe kichwa na Emmy.Mimi nimeamua kulisimamia suala hili na litakwisha.Naomba uniamini.” Clara akaniambia huku akilirekebisha shati nililokuwa nimevaa.
“Clara sioni hata nitamke neno gani kukushukuru kwa namna ulivyoamua kunisaidia katika suala hili.Nina deni kubwa ambalo ninahitaji kukulipa” nikasema na kumfanya Clara atabasamu ,akanisogelea karibu zaidi akanibusu.
“Wayne ni kweli una deni kwangu na nitakuomba unilipe kitu kimoja tu”
“Clara niko tayari kukulipa kitu chochote kile utakachoomba.Niambie unahitaji kitu gani na sinta sita kukupatia.Niko tayari kufika hadi pembe ya mwisho wa dunia kwa ajili ya kukutafutia kitu unachokihitaji.Niambie tafadhali unataka nikulipe nini?
Clara akanitazama kwa macho yake mazuri na kunifanya nisisimkwe mwili
“Una uhakika utanipatia ninachokihitaji? Akauliza Clara
“Nina uhakika Clara.Nitakupatia chochote kile unachokihitaji.” Nikajibu kwa kujiamini
“nafurahi kusikia hivyo Wayne.Kitu ninachotaka toka kwako ni kidogo sana na ambacho hakikulazimu kwenda hadi mwisho wa dunia kukipata.Ninachohitaji ni nafasi ndani ya moyo wako.”
Nikamuangalia Clara na kutabasamu baada ya kutamka vile.Nikamvuta karibu yangu zaidi nikamuangalia usoni na kumwambia.
“Clara huna haja ya kuomba nafasi ndani ya moyo wangu.Toka siku nimezaliwa tayari nafasi yako ilikwisha wekwa moyoni mwangu.Moyo wangu umejazwa na sura yako pekee.hakuna tena mwanamke mwingine anayeweza kuipata nafasi hii iliyojazwa nawe.Mapenzi yangu yote yameishia kwako pekee Sina mapenzi tena kwa mwanamke mwingine .” Nikasema na kumbusu Clara ambaye alikilaza kichwa chake kifuani kwangu na kunikumbatia kwa mahaba mazito.
“Wayne naomba uelewe kwamba ninakupenda kuliko kitu chochote katika dunia hii.Wewe ndiye kila kitu kwangu.tafadhali nahitaji nafasi ya kudumu ndani ya moyo wako.Nataka uwe wangu peke yangu.Nahitaji muda wako uliobakia wa kuishi hapa duniani uumalize ukiwa na mimi.Nataka tuishi pamoja,nataka tuzae watoto na kutengeneza familia yenye furaha na upendo.Nnakuhitaji Wayne katika maisha yangu” Mrembo huyu adhimu alikuwa akiongea toka nani kabisa mwa moyo wake.Ni kweli alikuwa akinipenda na hata mimi nilikuwa nikimpenda kupita kiasi.Nilijilaumu sana kwa kupoteza muda mwingi kwa mtu kama Emmy mwanamke asiye na shukrani ambaye katika kipindi cha maisha niliyoishi naye amenisababishai maumivu ambayo naweza kusema ni zaidi ya maumivu ya kawaida.
“Clara my angel.Nakuhakikishia kwamba wewe ni wangu pekee,na mimi niwako pekee.Sijui nitampa nini Mungu kama shukrani zangu kwake kwa kuniletea furaha hii kubwa ya maisha yangu.Amenirudishia furaha ya maisha iliyokwisha toweka.Clara nitakupenda milele na milele na ninakuahidi kwamba hakuna mtu yeyote katika dunia hii atakayeweza kututenganisha.Ni kifo pekee kitakachoweza kututengansiaha mimi na wewe.Nitaishi nawe na kukupenda hadi katika pumzi yangu ya mwisho “ maneno yale yakamfanya Clara ashindwe kujizuia kudondosha machozi.
“tafadhali usilie Clara.Huu ni wakati wa kufurahi na si wakati wa kudondosha machozi” nikamwambia huku nikimfuta machozi
“Wayne ninalia kutokana na furaha niliyonayo.Nimekaa miaka mingi nikijihisi ni mwenye furaha lakini sikuwahi hata mara moja kuipata furaha kubwa kama niipatayo sasa kwa kuwa nawe.Ni wewe ndiye uliyenipa furaha hii kubwa maishani.” Akasema Clara.na kuniangalia usoni.
“Darling twende tukaendelee na ratiba yetu ya siku.Tuna kila sababu ya kufurahi” Tukatoka na kuingia garini tukaelekea eneo la meserani ambako kuna hifadhi ya nyoka.Mimi si mpenzi kabisa wa nyoka na ni moja kati ya vitu ninavyoviogopa sana katika hii dunia lakini niliamua kwenda huko kwa sababu Clara alipenda kwenda kutazama nyoka wa aina mbali mbali wanaofugwa.Amekuwa akisikia hifadhi hii ya nyoka na alipanga siku moja aitembelee na sasa ameipata nafasi hiyo hakutaka kuipoteza.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………….