Brightman Jr
JF-Expert Member
- Mar 22, 2009
- 1,225
- 232
Waheshimiwa kwa wale wanaosumbuliwa na mbu nyakati za usiku, kuna habari njema ya kufurahisha ambayo nimeikuta mtandaoni. Jaribu nawe upitie HAPA.
KAMPUNI ya Samsung Tanzania, imezindua simu ya Samsung Galax Pocket yenye uwezo wa kufukuza mbu usiku, pindi mtumiaji anapowasha.
Hayo yalibainishwa jijini Dar es Salaam na Mwanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Belinda Lawuo ambaye ni miongoni mwa watumiaji watano waliopata fursa ya kutumia simu hiyo siku chache kabla ya uzinduzi uliofanyika juzi.
Lawuo alisema alipopata simu hiyo alifurahishwa na uwezo wake wa kufukuza mbu kupitia programu ya Mosquito Repellant.
Naye Meneja Mkuu wa Samsung Tanzania, Kishor Kumar alisema simu hiyo inampa mnunuzi thamani halisi ya pesa, kwani inauzwa bei nafuu, huku kukiwa na ofa mbalimbali, ikiwemo kutuma ujumbe bure mara 100 kwa mwezi na kifurushi cha intaneti.
KAMPUNI ya Samsung Tanzania, imezindua simu ya Samsung Galax Pocket yenye uwezo wa kufukuza mbu usiku, pindi mtumiaji anapowasha.
Hayo yalibainishwa jijini Dar es Salaam na Mwanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Belinda Lawuo ambaye ni miongoni mwa watumiaji watano waliopata fursa ya kutumia simu hiyo siku chache kabla ya uzinduzi uliofanyika juzi.
Lawuo alisema alipopata simu hiyo alifurahishwa na uwezo wake wa kufukuza mbu kupitia programu ya Mosquito Repellant.
Naye Meneja Mkuu wa Samsung Tanzania, Kishor Kumar alisema simu hiyo inampa mnunuzi thamani halisi ya pesa, kwani inauzwa bei nafuu, huku kukiwa na ofa mbalimbali, ikiwemo kutuma ujumbe bure mara 100 kwa mwezi na kifurushi cha intaneti.