Simbachawene ndani ya baraza la Mawaziri!!

Simbachawene ni mchapa kazi na Muadilifu, kwa vyovyote vile akiwa Waziri atalifaa Taifa letu, I hope Mkuu atapepesukia upande wake...

magamba at work....kaka hamisi umechafuka tangu ulipoenda against umma pale rev square muhimbili
 
simbachamwene sio miongoni mwa wajumbe wa kamati waliotuhumiwa na kafulila na spika akazima hilo soo kupewa rushwa mtanisahihisha kama kumbukumbu zangu haziko sahihi
 
Jamaa yuko Udom anaongeza Elimu, kutokana CCM kuwa na Wabunge wengi Vilaza huyu anafaa kupewa Uwaziri, sisemi hivi kwa sababu ya kufahamiana naye ila jamaa ni Gentleman ambaye akipewa fursa anaweza kulitumikia Taifa, nadhani hata akiwaga Mwenyekiti wa Bunge huwa anamzidi hata Spika Makinda kwa kuliendesha Bunge.

Mkuu Matola nadhani jamaa yupo UDOM anasoma mambo ya utawala. Kwa maoni yangu huyu jamaa ana maono. Niliwahi kupata kuongea naye nikaona ana kitu ndani yake. Pia ni mwanasheria na anajua mambo mengi sana si mkurupukaji. Anasema akiwa mwenyekiti huwa anaangalia Taifa kwanza si chama.
 
Last edited by a moderator:
Wilaya moja kuwa na mawaziri wawili haina noma. Mponda na Kombani wanatoka wilaya moja. Ngeleja na Masha. Simbachawene ana uchungu na nchi. Tatizo ni chama alichomo hakina uchungu tena na nchi hii tangu The greatest politician in Africa (Comrade JK Nyerere) atutoke. Simbachawene hamia Airtel ukachape kazi vizuri.
 
Nchi hii unafiki unalipa...nimekua nikimsililiza katika mijadala mbalimbali anavyojifanya kutetea sera za CCM kwa hoja zisizo na mashiko na zinazomfichua kama mtu wa kujipendekeza kwa watawala. Sioni namna mtu kama huyu anavyoweza kuchangia katika kuleta ukombozi wa mwananchi wa tanzania kutoka katika lindi la dhuluma, udhalilishaji, maradhi na ujinga.
 
Huyu huyu kwa kauli yake alisema ni kheri raia wafe kuliko polisi kujeruhiwa au kufa!
Akimaanisha raia kupigwa risasi ni sawa tuu
Nakumbuka aliposema hayo na miwan yake usoni
Huyu huyu leo awe waziri kazi tunayo

Kama alisema hivyo anafaa kuwa waziri wa mambo ya ndani awape heshima waandamanaji
 
Wakuu!

Kweli mna moyo wa chuma. Hivi ni nani msafi ndani ya Chama Cha Mafisadi kiasi kwamba mna matumaini makubwa kiasi hiki?

Huyo mteuaji mwenyewe anashindwa amuweke nani maana akiaangalia wote ni wale wale. Kwamba ana fanana nao!!!!!!!!!!!

Hata mimi nashangazwa sana na hii excitment. It's plainly a misplaced hope!
 
Huyo Kikwete mwenyewe anayechagua baraza hillo saa ingine anashindwa kwa kuwa wote walioko kwa chama chake ni kama yeye tu hawana sifa yeyeto ni wezi wote soo Magamba wanavyosema ooh huyu atafaa hakuna kitu ni kama wale wale tu kina Ngeleja wakati wanachaguliwa mlisema hawa wachapa kazi na kumbe wamekuwa wezi na hata hao wengine watakuwa kama hawa wapya ndani ya Magamba hakuna jipya
 
Nitashindwa kumuelewa Kikwete kama akimsahau Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM, Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde aka Kibajaji!
Tunahitaji wachapakazi.
Pamoja na ugamba wao, wao ndo wana dola.
viva Lusinde for uwaziri!
 
ndio simbachawene mzuri, je atapewa wizara sahihi, hilo tu ndilo la kujiuliza, mimi ningelikuwa nachagua hao mawaziri, kwa kweli magufuli,lissu ama mwakyembe mmoja wapo ningempa mambo ya ndani, jamani amani hakuna tanzania na watu wanafanya mchezo tu. anatakiwa mtu ambaye ni mkali kupindukia katika hii wizara
 
Nchi hii unafiki unalipa...nimekua nikimsililiza katika mijadala mbalimbali anavyojifanya kutetea sera za CCM kwa hoja zisizo na mashiko na zinazomfichua kama mtu wa kujipendekeza kwa watawala. Sioni namna mtu kama huyu anavyoweza kuchangia katika kuleta ukombozi wa mwananchi wa tanzania kutoka katika lindi la dhuluma, udhalilishaji, maradhi na ujinga.
Umenena mkuu jamaa ni mnafiki kwisha kazi huwa anauma na kupuliza kama hauko makini unawezazani ni bonge la mzalendo kumbe ndo walewale chama kwanza.
 
Kikwete na utezi mawaziri wake wapiga debe wa Mabasi. Haya sasa naona sasa atakuwa amejifunza. Askari kakata Mkono. Kwi! Kwi! Kwi!
 
Back
Top Bottom