TIMU ya soka ya Simba imeweza kuendeleza ubabe katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuifunga Prisons ya Mbeya mabao 3-1 katika mchezo uliomalizika dakika chache zilizopita katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kona iliyochongwa na beki Ramadhan Wasso katika dakika ya pili ya mchezo huo iliweza kuunganishwa vyema na Ramadhan Chombo Redondo na kuiandikia Simba bao la kwanza katika mchezo huo.
Baada ya kuingia kwa bao hilo, Prisons walikuja juu na kufanikiwa kupata bao katika dakika ya 27 lililofungwa na Yona Ndabila baada ya kuiwahi pasi ya Osward Morris na kufunga kirahisi.
Simba ilipata penati katika dakika ya 30 iliyofungwa vizuri na Mussa Hassan Mgosi. Bao hilo lilidumu hadi mapumziko.
Simba waliopata bao la tatu katika dakika ya 57 lililosababishwa na raia wa Nigeria Izuchukwu.
kocha wa Simba Patrick Phiri alifurahia ushindi huo kwa kusema; Vijana wangu wameanza kunielewa.
Habari zaidi NIFAHAMISHE dot com
Kona iliyochongwa na beki Ramadhan Wasso katika dakika ya pili ya mchezo huo iliweza kuunganishwa vyema na Ramadhan Chombo Redondo na kuiandikia Simba bao la kwanza katika mchezo huo.
Baada ya kuingia kwa bao hilo, Prisons walikuja juu na kufanikiwa kupata bao katika dakika ya 27 lililofungwa na Yona Ndabila baada ya kuiwahi pasi ya Osward Morris na kufunga kirahisi.
Simba ilipata penati katika dakika ya 30 iliyofungwa vizuri na Mussa Hassan Mgosi. Bao hilo lilidumu hadi mapumziko.
Simba waliopata bao la tatu katika dakika ya 57 lililosababishwa na raia wa Nigeria Izuchukwu.
kocha wa Simba Patrick Phiri alifurahia ushindi huo kwa kusema; Vijana wangu wameanza kunielewa.
Habari zaidi NIFAHAMISHE dot com