Mambo bado magumu kwa Simba kwenye uwanja wa Taifa, ambapo leo inacheza mechi ya kirafiki na Sofapaka, na mpaka muda huu Simba imeshatandikwa magoli 3-0, na kwa hali inayoonekana wanaweza kufungwa zaidi ya hizo! Hali mbaya sana!
jamani, wapeni pole wenzenu
........sijui tumfukuze nani kwenye hii timu: akina Mrwanda na wenzake tulisha watanguliza so who is next! kocha????
Hahaha!mfukuzeni Maha-Rage na makaburi aka Kaburu.Hao ndio wachawi wenu kama hamjui.........sijui tumfukuze nani kwenye hii timu: akina Mrwanda na wenzake tulisha watanguliza so who is next! kocha????
Shangilien sasa, hizi trayo hakuna pointi hapo, subirin ligi ianze ndo mtamjuwa mnyama anafanya nini.
Mkuu team lazima iwe na determination na kujenga winning spirit,mfano ninachokifurahia sasa hivi Yanga hata ibalanganye vp kwenye mchezo inaweza ku'pick 2nd half na kuibuka na ushindi hata wa dakika za lala salama,angalia mechi na Mafunzo, Polisi ya Rwanda na Coastal juzi,mechi zote Yanga ilianza vibaya na kutangulia kufungwa lkn wali'pick na mwisho wa mchezo wakaibuka na ushindi, hivi ndo team ya ushindi inavyotakiwa kuwa... don't read too much from friendlies. lengo ni kujaribu wachezaji na uchezaji wa namna mbalimbali/kutafuta ushindi siyo primary goal hapa. ligi bado...
Yule wa kujifunga na kusababisha Penalt kila siku? yule bomu mbaya bora hata Juma Nyoso wetu,bado nakumbuka tambo za Mzee Zacharia Hans Pop ya kuwa sasa hivi wameamua kujikita kwenye kuchukua wachezaji wa Africa Magharibi ksbb wa ukanda huu wa Africa Mashariki hawajui mpira na si waaminifu,haya sasa kazi wanayo na pazia la usajili ndo lishafungwaduh,aibu sana aise.Nasikia huyo beki wao sijui nani vile!ni bomu hamna kitu,bora ata yule"Lina-Makombo"ni mzuri.
Wana Simba msiwe na hofu, mimi jana nilikuwa uwanjani, ni kweli tumefungwa lakini tuseme tu bahati haikuwa upande wetu hiyo jana, timu ilicheza vizuri na tumefika golini mara kibao ndo maana baada ya mechi bado vijana tuliwapigia makofi kuwapongeza kwa soka waliloonyesha, hakuna shaka Azam lazima wakae hiyo j4 na Yeboyebo nao lazima wakae siku ya tarehe 03/10.
he unanichekesha ya jana yamekushinda ,unayaota yajayo kweli wewe unajipa moyo mimi nakuambia ntakupiga goli moja tuu la uchungu wait for the D DAY.