Simba na Nyoso

FILOMBE

Member
Mar 2, 2012
27
0
Habari wana JF, nafuatilia kwa makini kipindi hiki cha usajili wa wachezaji wa timu zetu kuelekea msimu mwingine wa ligi kuu ya Tanzania kwa timu zetu hizi za Bongo. Ukifuatilia kwa kina utaona vyombo vingi vya habari vinatupia macho klabu kubwa za Yanga na Simba na sasa kwa kiasi fulani klabu ya Azam.

Nimesoma na kusikia kwamba klabu ya Simba ina mpango wa kumtupia virago beki wake wa kata Juma Nyoso. Mie, kwa mtizamo wangu naona kama Simba hapo watakuwa wamechemsha kabisa, sababu kubwa wanatoa ni kwamba beki huyu wa kati amekuwa akiigharimu timu. Naomba niseme mie nimekuwa nafuatilia michezo mingi ya klabu ya Simba dhidi ya timu pinzani na sijaona kama Juma Nyoso anastahili kutupiwa vilago.

My take:

Klabu za Simba na Yanga ni chanzo cha kuharibu vipaji kwa wachezaji chipukizi, kumbuka suala la Athuman Idd na sasa Kevin Yondan. Jamani wachezaji muwe makini.

Naomba tujadili.
 
Ni kweli Nyoso ni mzuri ila ni kweli pia Nyoso amekuwa akipata red card rahisi sana na kama viongozi wamepata mbadala mwingine la labda hayupo kwenye mipango ya kocha sioni ubaya wowote wakimalizana naye kwa amani.
 
Mara nyingi issue za aina ya saga la Nyoso na Simba hutokana na falsafa ya Mwalimu husika,inavyoonekana type ya uchezaji wa Nyoso iko tofauti na falsafa ya Mwalimu wa Simba anayoitaka team icheze ndo maana wanaona kama hatawafaa lkn kwa mtazamo wangu kama ni suala la kuigharimu team Nyoso ameisaidia zaidi Simba kuliko kuigharimu,ukichukulia amecheza mechi karibu zote za Simba kwa msimu huu uliomalizika,isitoshe ukichanganya na hili suala la Yondan kuelekea Yanga, Simba watakuwa wamefanya bonge la mistake kama watampoteza Nyoso
 
Mara nyingi issue za aina ya saga la Nyoso na Simba hutokana na falsafa ya Mwalimu husika,inavyoonekana type ya uchezaji wa Nyoso iko tofauti na falsafa ya Mwalimu wa Simba anayoitaka team icheze ndo maana wanaona kama hatawafaa lkn kwa mtazamo wangu kama ni suala la kuigharimu team Nyoso ameisaidia zaidi Simba kuliko kuigharimu,ukichukulia amecheza mechi karibu zote za Simba kwa msimu huu uliomalizika,isitoshe ukichanganya na hili suala la Yondan kuelekea Yanga, Simba watakuwa wamefanya bonge la mistake kama watampoteza Nyoso
Anselm kazi ya ofisa habari wa Simba itakuwa wazi mkataba wa Kimwanga unaelekea kwisha.Ungefaa kwa kazi
hiyo kwani ama upo addicted na Simba au wewe ni Simba in disguise.Nasema haya kwa sababu cheki habari zinazohusu
Simba kwenye posts zako utakuta ni asilimia kubwa sana.
 
Anselm kazi ya ofisa habari wa Simba itakuwa wazi mkataba wa Kimwanga unaelekea kwisha.Ungefaa kwa kazi
hiyo kwani ama upo addicted na Simba au wewe ni Simba in disguise.Nasema haya kwa sababu cheki habari zinazohusu
Simba kwenye posts zako utakuta ni asilimia kubwa sana.

Mkuu Ngarna,
Kama ilivyo kwa Mtanzania yeyote yule,katiba inaniruhusu kutoa maoni yangu kitu ninachokifanya hapa,Simba mimi hawawezi kuniajiri ksbb Mshahara wangu hawatauweza,kama walikuwa wanamlipa Yondani Gross ya Laki 4,mimi wataweza wapi?
 
Mkuu Ngarna,
Kama ilivyo kwa Mtanzania yeyote yule,katiba inaniruhusu kutoa maoni yangu kitu ninachokifanya hapa,Simba mimi hawawezi kuniajiri ksbb Mshahara wangu hawatauweza,kama walikuwa wanamlipa Yondani Gross ya Laki 4,mimi wataweza wapi?
Huendi kuchukua nafasi ya Yondani utachukua nafasi ya Ezekiel Kamwaga.
 
Habari wana JF, nafuatilia kwa makini kipindi hiki cha usajili wa wachezaji wa timu zetu kuelekea msimu mwingine wa ligi kuu ya Tanzania kwa timu zetu hizi za Bongo. Ukifuatilia kwa kina utaona vyombo vingi vya habari vinatupia macho klabu kubwa za Yanga na Simba na sasa kwa kiasi fulani klabu ya Azam.

Nimesoma na kusikia kwamba klabu ya Simba ina mpango wa kumtupia virago beki wake wa kata Juma Nyoso. Mie, kwa mtizamo wangu naona kama Simba hapo watakuwa wamechemsha kabisa, sababu kubwa wanatoa ni kwamba beki huyu wa kati amekuwa akiigharimu timu. Naomba niseme mie nimekuwa nafuatilia michezo mingi ya klabu ya Simba dhidi ya timu pinzani na sijaona kama Juma Nyoso anastahili kutupiwa vilago.

My take:

Klabu za Simba na Yanga ni chanzo cha kuharibu vipaji kwa wachezaji chipukizi, kumbuka suala la Athuman Idd na sasa Kevin Yondan. Jamani wachezaji muwe makini.

Naomba tujadili.


nimefurahi sana kwa uzi wako huu... hata mechi ya shandy nyoso hakuwepo ndio maana simba iko nje, ukweli ndio huo watake wasitake. mimi kama shabiki wa simba huwa nina msimamo wangu na kundi langu... kama nyoso angeachwa ktk usajili tungekaa mechi nne bila kwenda uwanjani kuishangilia simba kama maombolezo ya kuondokewa na Nyoso. habari ndiyo hiyo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom