Sikweli kuwa kila cha Z’bar ni cha Muungano?

abdulahsaf

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
858
130
Wazanzibar ni haki yetu kuulizwa kuwa Muungano tunautaka au vipi.Makubaliano ya Father K nikuwa Muungano ni wamuda mfupi tu. Yani miaka 10 tukiona una faida au hauna faida nilazima tulizwe wananchi wa Zanzibar jee vipi? Lakini hivi sasa ni miaka 49 hatujaulizwa Wzanzibar kuhusu hatima ya Muungano tunaburuzwa tu na chama cha ccm .Nikwa nini wenzetu wa Tanganyika wanajifanya Super Power mbele yetu? Masuwali bila majibu jee mawazo yao wanakumbukumbu zinazosema Zanzibar ilikuwa ni Sehemu yao hapo awali?Au mawazo yao wanahisi sie nikidogo wao ni wengi ndio watuamulie Masuali ya Muungano na Katiba?Katika Masuali ya Katiba ya Muungano inahusu nchi mbili kila nchi ina haki zake zisizo za Muungano na kila nchi inatakikana iwe na katiba yake yakusimamia mambo yake yasio ya Muungano? Kwa nini Tanganyika Haipo na Katiba ya Tanganyika tuambiwavyo haipo Jee mambo yasio ya Muungano yanasimamiwa vipi Tanganyika? Au wanahisi iko siku Wazanzibari watasalimu amri na watakuwa Watanganyika wa Pwani,kama vile Mafya,Tanga,na Bwagamoyo? Au wanahisi historia ya Zanzibar na kizazi cha Wazanzibar kita,disappear kwa vile Watanganyika wote lao moja kuimeza Zanzibar na kujipakaticha kwetu na kujiweka pacha pacha na ilani ya Chama tawala ccm na katiba ya Tanzania Tanganyika ni sera ya Serekali mbili kuelekea moja?.mimi nahisi Muungano sio kitu chakulazimichana au kufosi, nikuulizwa Wzanzibar baado wanataka kuwa ktk Muungano au laa? Sio tuambiwe na Viongozi wa ccm kuwa tulinde na tuuimarishe Muungano wetu walio uwasisi Baba wa Taifa na Mama wa Taifa? Father K alisema bada ya miaka kumi tulizwe wananchi na kabla ya miaka kumi kama Muungano utatubana basi tuvue kama Koti lenye kukukaza. Kwa hio Nyerere kwa Master mind yake akamkataa roho Father K na baada ya hapo makubaliano yote ya Muungano akaanza kuyakanyaga x2 yeye na Wtanganyika wenzake na kubwa la kujuwa kuwa wenzetu nindumi lakuilii nipale walipo iuwa Tanganyika na kuvaa Koti la Tanzania ili tu wapate kujifanya Super power na kuimeza Zanzibar kiimlaa kuwa nchi moja na Zanzibar samani yake mkowa wa Pwani na watu wake tukaanza kuitwa watu wa Pwani na wao wakajita Wtanzania na sisi tukijita Wzanzibar nongwa na ubaguzi. Muungu ibariki Zanzibar na kizazi chake.

Wz'bar tujitahadhari na kutokuja kuwa Kondoo walio potea?

 
Back
Top Bottom