Hello Wapendwa.
Kuna mahala fulani huwa ninasafiri kwenda mara kwa mara kufuatilia mambo ya kibiashara.Huko mahala ninaposafiri huwa kuna mama yangu mkubwa anaishi huko lakini siku zote huwa nashukia hotelini.Kila nikifika huwa nampigia simu mama mkubwa na pia najitahidi kwenda nyumbani kwake kumsalimia lakini mama mkubwa analalamika kuwa ni vizuri siku nikiwa huko japo siku moja moja nilale nyumbani kwake.
Mama yangu mkubwa nimuathirika wa UKIMWI,sio kwa kumuhisi bali kwa kinywa chake alimweleza mama yangu,pia hataki kutumia hizi dawa za kurefusha maisha hivyo amekonda sana na ana mapele na vidonda na majipu vinamtokea kila mara.
Siku moja nikiwa huko nikaamua kwenda kulala nyumbani kwa mama mkubwa wangu japo ana chumba kimoja,nilipofika nikakuta kidole chake kimoja cha mkononi kimeoza kwa kidonda chenye usaha,mwenyewe akanambia eti kuna mdudu akiingia kwenye kucha kidole ndo kinakua hivyo.
Tulikula kisha tukapiga story hadi usiku mwingi kisha sababu alikua ana magodoro mawili nikamwomba anitandikie godoro mim nilale chini.
Wakati anatandika shuka kwenye hilo godoro kwa bahati mbaya kile kidole chake chenye kidonda kikanichoma mguuni hadi pakakatika hadi damu ikanitoka halafu ule usaha wake ukabakia juu ya hapo aliponikata na kucha yake.Niliogopa sana,cha ajabu yeye hata hakuonesha mshituko,ila mimi niliogopa hadi sikuweza hata kupata usingizi.Kesho yangu nikarudi hotelini kwangu nikiwa na mawazo ya kuwa labda virusi vimenipata.Nilimaliza shughuli zangu huko nikasafiri kurudi nilipotoka lakini wiki mbili tokea aliponikata na kucha nilikuwa na mawazo sana lakini baadae nikasahau.
Kwa kawaida mimi ni mtu mwenye kinga imara,ni kwa miaka mingi sijawahi kuumwa kitu chochote zaidi ya mafua,tena hata mafua yenyewe sio mara kwa mara.Kama baada ya mwezi na nusu hivi tokea nilipokatwa na kucha nikapata mafua makali yaliyoambatana na homa kali na maumivu ya kichwa,nikaanza tena kukumbuka lile tukio,nikaanza kuhisi labda nimeshaathirika,wakati mwingine najipa moyo kuwa ni mafua ya kawaida maana hata kama kuathirika inaweza kuchukua hata miaka mingi bila kuona dalili.
Miezi michache baadae nikasafiri kwenda Ulaya,wiki moja tu tokea nifike nikaanza kupiga chafya mfululizo halafu pua ilikua inawasha ajabu hadi ikawa nyekundu na jicho moja likawa linatoa machozi hasa nikiwa nje natembea,mawazo tena ya kukatwa na kucha yakarudi kwa kasi,safari hii nikawa sina uhakika kabisa kuwa mimi ni muathirika au la maana tokea nizaliwe sijawahi kupatwa na hali kama hii,baada ya kupiga chafya kila dakika kwa wiki nzima mfululizo nikaamua kwenda hospitali,nikaambiwa nina allergy ya polen,daktari akasema kwa vile kilikua kipindi cha summer hewa imechafuka kwa polen inayotokana na maua yaliyopo kila mahala,ila nikashangaa maana home kwangu nina maua ya kila aina na sijawahi kupata hiyo hali,rohoni nikazidi kuogopa kuwa huenda nimeathirika kwa kukatwa na kucha.
Siku nyingine tena ghafla nikaanza kuwashwa na kuvimba mwili,yaani bila kujua sababu nilikuwa nawashwa kuanzia utosini hadi kwenye unyayo halafu nikiamka ngozi imevimba na kuwa nyekundu,kwenda hospitali nikambiwa eti kuna matunda nilikula ambayo nina allergy nayo,kweli kuna vitunda fulani nilikula,lakini nilizidi kuogopa kuwa haya mauza uza labda yanatokana na kukatwa na lile kucha.
Siku nyingine tena nikala viazi na samaki halafu usiku nikaamka tumbo likawa linaniuma sana kisha nikaanza kuendesha,kila dakila nikawa naenda chooni kwa siku mbili kisha likapoa.
Nikaona kukata mzizi wa fitina acha nikapime,kabla ya kukatwa na kucha nilikua nina uhakika kuwa sina ukimwi,niliamini kama mtu hujawahi kusex,wala kuongezewa damu,sindano nilichomwa nikiwa mtoto,wala sishirikiani na mtu vitu vya kukata hivyo chance ya kuwa na UKIMWI ni ndogo.
Kabla ya kwenda kupima nilisali nikamuomba Mungu kuwa kama kuna kirusi chochote kilichojipenyeza mwilini mwangu siku ile nilipokatwa na kucha la muathirika kife kwa jina lake lenye nguvu kupita majina yote.
Majibu yangu yakaja kuwa mim sio muathirika.
Nilichojifunza ni kuwa ukiruhusu ubongo wako uamini unaumwa kweli utakuletea vimagonjwa vya ajabu ajabu kusuport imani yako maana kipindi nilichokua naogopa nilipatwa hadi na vichomi ila nilipoambiwa sina UKIMWI hata sikujua vilipotelea wapi.
Kuna mahala fulani huwa ninasafiri kwenda mara kwa mara kufuatilia mambo ya kibiashara.Huko mahala ninaposafiri huwa kuna mama yangu mkubwa anaishi huko lakini siku zote huwa nashukia hotelini.Kila nikifika huwa nampigia simu mama mkubwa na pia najitahidi kwenda nyumbani kwake kumsalimia lakini mama mkubwa analalamika kuwa ni vizuri siku nikiwa huko japo siku moja moja nilale nyumbani kwake.
Mama yangu mkubwa nimuathirika wa UKIMWI,sio kwa kumuhisi bali kwa kinywa chake alimweleza mama yangu,pia hataki kutumia hizi dawa za kurefusha maisha hivyo amekonda sana na ana mapele na vidonda na majipu vinamtokea kila mara.
Siku moja nikiwa huko nikaamua kwenda kulala nyumbani kwa mama mkubwa wangu japo ana chumba kimoja,nilipofika nikakuta kidole chake kimoja cha mkononi kimeoza kwa kidonda chenye usaha,mwenyewe akanambia eti kuna mdudu akiingia kwenye kucha kidole ndo kinakua hivyo.
Tulikula kisha tukapiga story hadi usiku mwingi kisha sababu alikua ana magodoro mawili nikamwomba anitandikie godoro mim nilale chini.
Wakati anatandika shuka kwenye hilo godoro kwa bahati mbaya kile kidole chake chenye kidonda kikanichoma mguuni hadi pakakatika hadi damu ikanitoka halafu ule usaha wake ukabakia juu ya hapo aliponikata na kucha yake.Niliogopa sana,cha ajabu yeye hata hakuonesha mshituko,ila mimi niliogopa hadi sikuweza hata kupata usingizi.Kesho yangu nikarudi hotelini kwangu nikiwa na mawazo ya kuwa labda virusi vimenipata.Nilimaliza shughuli zangu huko nikasafiri kurudi nilipotoka lakini wiki mbili tokea aliponikata na kucha nilikuwa na mawazo sana lakini baadae nikasahau.
Kwa kawaida mimi ni mtu mwenye kinga imara,ni kwa miaka mingi sijawahi kuumwa kitu chochote zaidi ya mafua,tena hata mafua yenyewe sio mara kwa mara.Kama baada ya mwezi na nusu hivi tokea nilipokatwa na kucha nikapata mafua makali yaliyoambatana na homa kali na maumivu ya kichwa,nikaanza tena kukumbuka lile tukio,nikaanza kuhisi labda nimeshaathirika,wakati mwingine najipa moyo kuwa ni mafua ya kawaida maana hata kama kuathirika inaweza kuchukua hata miaka mingi bila kuona dalili.
Miezi michache baadae nikasafiri kwenda Ulaya,wiki moja tu tokea nifike nikaanza kupiga chafya mfululizo halafu pua ilikua inawasha ajabu hadi ikawa nyekundu na jicho moja likawa linatoa machozi hasa nikiwa nje natembea,mawazo tena ya kukatwa na kucha yakarudi kwa kasi,safari hii nikawa sina uhakika kabisa kuwa mimi ni muathirika au la maana tokea nizaliwe sijawahi kupatwa na hali kama hii,baada ya kupiga chafya kila dakika kwa wiki nzima mfululizo nikaamua kwenda hospitali,nikaambiwa nina allergy ya polen,daktari akasema kwa vile kilikua kipindi cha summer hewa imechafuka kwa polen inayotokana na maua yaliyopo kila mahala,ila nikashangaa maana home kwangu nina maua ya kila aina na sijawahi kupata hiyo hali,rohoni nikazidi kuogopa kuwa huenda nimeathirika kwa kukatwa na kucha.
Siku nyingine tena ghafla nikaanza kuwashwa na kuvimba mwili,yaani bila kujua sababu nilikuwa nawashwa kuanzia utosini hadi kwenye unyayo halafu nikiamka ngozi imevimba na kuwa nyekundu,kwenda hospitali nikambiwa eti kuna matunda nilikula ambayo nina allergy nayo,kweli kuna vitunda fulani nilikula,lakini nilizidi kuogopa kuwa haya mauza uza labda yanatokana na kukatwa na lile kucha.
Siku nyingine tena nikala viazi na samaki halafu usiku nikaamka tumbo likawa linaniuma sana kisha nikaanza kuendesha,kila dakila nikawa naenda chooni kwa siku mbili kisha likapoa.
Nikaona kukata mzizi wa fitina acha nikapime,kabla ya kukatwa na kucha nilikua nina uhakika kuwa sina ukimwi,niliamini kama mtu hujawahi kusex,wala kuongezewa damu,sindano nilichomwa nikiwa mtoto,wala sishirikiani na mtu vitu vya kukata hivyo chance ya kuwa na UKIMWI ni ndogo.
Kabla ya kwenda kupima nilisali nikamuomba Mungu kuwa kama kuna kirusi chochote kilichojipenyeza mwilini mwangu siku ile nilipokatwa na kucha la muathirika kife kwa jina lake lenye nguvu kupita majina yote.
Majibu yangu yakaja kuwa mim sio muathirika.
Nilichojifunza ni kuwa ukiruhusu ubongo wako uamini unaumwa kweli utakuletea vimagonjwa vya ajabu ajabu kusuport imani yako maana kipindi nilichokua naogopa nilipatwa hadi na vichomi ila nilipoambiwa sina UKIMWI hata sikujua vilipotelea wapi.