"Sikushinikizwa kumpeleka mwanangu uwanjani"- Baba mzazi wa Ismail

Alfu Lela Ulela

JF-Expert Member
Oct 29, 2010
1,255
77
Baba mzazi wa kijana Ismail aliyepigwa risasi na kuuawa na polisi huko Arusha, katika mapambano kati ya Jeshi la polisi na wafuasi wa CHADEMA amesema kuwa hakukuwa na shinikizo lolote kupeleka mwili wa mwanae viwanja vya NMC kwa ajili ya ibada ya kumuaga.

Mzazi huyo amesema uamuzi wa kupeleka mwili huo viwanjani NMC ulikuwa ni uamuzi wa familia na hakukuwa na shinikizo lolote kutoka nje ya familia kama ilivyodaiwa na baadhi ya vyombo vya habari hapo awali.

"Yalikuwa ni maamuzi ya familia kuwa mwili wa Ismail upelekwe viwanjani kuagwa na hakukuwa na shinikizo lolote kama inavyodaiwa." alisema mzazi huyo na kuongeza
"Tuliamua kufanya hivyo ili kuuonesha ulimwengu ukiukwaji haki uliyofanywa na jeshh la polisi"

Taarifa hii inakuja siku chacie baada ya kuenea uvumi kuwa wazazi wa Ismail walishinikizwa kupeleka mwili wa marehemu viwanja vya NMC kwa ajili ya ibada ya mazishi.

Uvumi huo ulizidi kupaizwa na vyombo vya habari, na kukihusisha chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuhusika kuishinikiza familia kuileta maiti ya Ismail uwanjani NMC.

Kwa maana hiyo taarifa ya mzazi wa Ismail inakisafisha chama cha CHADEMA kutokana na kupakaziwa na kuchafuliwa na taarifa za uvumi zilizotolewa awali.

Vilevile taarifa hii inaonesha wazi namna baadhi ya watu wenye nia mbaya wanavyopika habari na kuzivumisha, huku wakichafua wengine kwa alili ya maslahi yao wenyewe.

Pongezi kwa mzazi wa Ismail aliyeamua kueleza ukweli. Pongezi CHADEMA kwa kuruka kiunzi cha kutaka kuchafuliwa kwenye kazi njema mliyoianza.

SOURCE:Radio One.
 
good, huo ndiyo uanaume mkuu, tufanyeni kazi huku tukijiandaa kumtoa kikwete na makamba, good redio one kwa kuonyesha ukweli wa mambo siyo gazeti la habari leo linalokurupuka tu,
 
Duuu, nambari one imekuwa ziro.... sasa wanatafuta nyia nyingine!!!! Uzuri watanzania tushajua janja yao, aibu kubwa kwa habari leo!!!! :ban:
 
Kuna watu hapa walikuwa wanaongea hadi povu mdomoni kwa kujifanya kuijua dini kuliko mashehe walioswalisha tukawaambia watakuja kuwa wapole siku si nyingi sasa bado polisi nao watasema tu.
 
Walitupa karata ya udini sasa imewageukia, damu ya mtu haimwagiki bure lazima ije kula kwao
 
Walitupa karata ya udini sasa imewageukia, damu ya mtu haimwagiki bure lazima ije kula kwao, mkwere, makamba & co tunawasubiria ni swala la mda tuu you are going down, you have no place to go except down
 
Naomba cdm wanunue muda kwenye main stream waonyeshe mkanda wa maandamano ili dunia ione uhalisia cio ile propaganda ya polisi eti cdm walitaka kuvamia kituo bila silaha
 
dah,kweli siasa ni mchezo mchafu sana

Kwanini mkuu? Mi nadhani siasa si mchezo mchafu bali kuna wanasiasa wachafu, na wengi wao ni CCM. Wanapenda kutumia uongo kupotosha umma, ukweli unapobainika wanaumbuka. ShAME UPON THEIR FACES!!
 
Hii habari itawasumbua sana sisi "M"!!

avatar30595_2.gif



Kitungi habari zako?
 
Back
Top Bottom