Sikukuu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Hivi kuna nchi duniani yenye sikukuu nyingi kama Tanzania?

untitled.JPG
 
yakhe,
bado kidogo ! Mie sijalala. Nasubiri watu waje waseme hayo maneno yao, Mnyika sijui ataingia humu ? Namsubiri.
 
Kalenda ya East and cental Africa inanionyeya kuwa
Tanzania ina public holiday 17 mwaka huu, DRC ina 17, Zambia ina 15, Uganda in 14, Kenya in 13, na Ethiopia 12.
my take: sikukuu nyingi zinaleta umasikini tu na wala hazina tija
 
Kalenda ya East and cental Africa inanionyeya kuwa
Tanzania ina public holiday 17 mwaka huu, DRC ina 17, Zambia ina 15, Uganda in 14, Kenya in 13, na Ethiopia 12.
my take: sikukuu nyingi zinaleta umasikini tu na wala hazina tija


Usisahau zile sikukuu za Mwinyi. Ilikuwepo utaratibu wa kama sikukuu ikiangukia weekend basi inalipizwa kwa kupumzika the next working day. Mwaka 1996 mwezi wa nne, nilifanya kazi siku kumi tu kwa mwezi kama sikosei. Mwezi huo tulikuwa na pasaka, ijumaa kuu, sikukuu ya Muungano na siku ya kuilipiza, kulikuwepo na IDD kama sikosei na siku ya kuilipiza, etc. It was one crazy month. Nikifikiria sikukuu za kijinga nakumbuka mwezi huo ambao nililipwa mshahara bila ya kufanya kazi ya maana. I spent more days at home than ever.
 
Nimetafuta online mwezi April 1996 na niliweza kupata information zifuatazo.
April 5 Good Friday
April 7 Easter (sikumbuki kama tulikuwa tunalipiza Easter)
April 8 Easter Monday

April 26 Muungano (it was a Friday)

April 29 Idd-el-Hajj (it was a monday)

Mind you we had Labour day the same week on May 1

Imagine all those days resting at home. Tulifanya kazi mwezi huo siku 16 tu!! Haya unganisha na traditions zetu za kuchelewa kazini, kutokuwa productive, bado udhuru ya kwenda kwenye mazishi, mara watoto wagonjwa mara ya majukumu ya kifamilia. Utapata jibu.

 
Lakini tukumbuke kuwa maendeleo hayaji kwa muda/sikukuu mtu alizonazo/anazopewa........

Issue lazima iwe "Je, kwa ule muda amabo ni wa kazi watu/wafanyakazi wanafanya kazi ipasavyo?"

Mara ya kwanza nilikuwa UAE wakati wa Idd nikakuta kule jamaa wanashereheka na sikukuu kwa wiki nzima, yet kuna sherehe nyingine nyingi tu lakini mambo yao si unayacheki!!??
 
India inaongoza kwa sikukuu duniani. wastani ni sikukuu mbili za kitaifa kila wiki. Zikijumuishwa sikukuu zote za kidini na zile zisizo rasmi za kitaifa zinazidi millioni 20
 
Back
Top Bottom